Mawaziri waanza kuumbuana mchana kweupe!

Kwa maelezo ya Fundi Mchundo hapo juu, inamaanisha kwamba haya malalamiko ya Bw Makufuli hayana msingi wowote. Kwamba NHC imeingia gharama si kwa sababu mawaziri wameshindwa kazi, bali kwa kuwa wanataka nyumba walizojenga ziuzike, ni biashara. Na moja ya gharama ya kuzifanya nyumba hizo ziwe bora ni huko kuweka umeme, maji nk. Wangeweza kusubiri ratiba za wizara hizo za kuweka hizo huduma, lakini wao wenyewe NHC wakaona waingie gharama wenyewe ili mradi wao "usidode". Kwa hiyo ni choice, au siyo? Kumbe pengine Makufuli, licha ya uchapaji kazi wake uliotukuka, hakupaswa "kuwaumbua" mawaziri wenzake mbele ya kadamnasi, kweli au si kweli?


Hapana, Mheshimiwa Kithuku. Nilichokisema ni kuwa ilibidi NHC kama developer (ukiangalia bei ya nyumba zao, hawafanyi charity hawa mabwana) kuingia mikataba na watakaowapatia huduma wanazohitaji katika mradi wao. Si kungoja mpaka hayo mashirika ( si wizara) yatakapopanga kwenye ratiba zao. Hii ni biashara, NHC kwa kufanya hivi anawaletea wateja na ndio maana ilibidi hizo utility companies zichangamkie tenda. Kama NHC akiona wanazembea anaingia nao mkataba wa kuwafanyia yale wanayotakiwa kuyafanya ili mradi watamrudishia gharama zake au atafute njia mbadala za kupata hizo huduma. Unajua mtu unaweza kujenga nyumba ambayo inajitolesha kwa mahitaji yake ya umeme? Unaweza kuvunamvua, kuchimba visima ili uondakane na hao Dawasco. Mipango ya barabara kuu ni ya wizara na manispaa lakini feeder roads si jukumu lao.
Hivi, mkuu, unadhani kipi kingewastua zaidi hao Tanesco na Dawasco kati ya kuletewa barua ya madai na mawakili wa NHC na hili la kutajwa kwenye jukwaa la siasa? Mimi sizungumzii uchapa kazi wa mheshimiwa Waziri, ninachozungumzia ni hili suala ambalo kwa upeo wangu finyu naona lingeshughulikiwa tofauti. Kwa kufanya hivi walivyofanya tunawapatia sababu viongozi wa mashirika yetu kudai kuwa walikuwa wanatimiza maagizo ya waziri. Mimi naamini waziri anatakiwa kusimamia sera na si utendaji wa kila siku wa shirika. Management wapewe full responsibility ya kutekeleza sera na pale wanapozembea washughulikiwe.
 


Hapana, Mheshimiwa Kithuku. Nilichokisema ni kuwa ilibidi NHC kama developer (ukiangalia bei ya nyumba zao, hawafanyi charity hawa mabwana) kuingia mikataba na watakaowapatia huduma wanazohitaji katika mradi wao. Si kungoja mpaka hayo mashirika ( si wizara) yatakapopanga kwenye ratiba zao. Hii ni biashara, NHC kwa kufanya hivi anawaletea wateja na ndio maana ilibidi hizo utility companies zichangamkie tenda. Kama NHC akiona wanazembea anaingia nao mkataba wa kuwafanyia yale wanayotakiwa kuyafanya ili mradi watamrudishia gharama zake au atafute njia mbadala za kupata hizo huduma. Unajua mtu unaweza kujenga nyumba ambayo inajitolesha kwa mahitaji yake ya umeme? Unaweza kuvunamvua, kuchimba visima ili uondakane na hao Dawasco. Mipango ya barabara kuu ni ya wizara na manispaa lakini feeder roads si jukumu lao.
Hivi, mkuu, unadhani kipi kingewastua zaidi hao Tanesco na Dawasco kati ya kuletewa barua ya madai na mawakili wa NHC na hili la kutajwa kwenye jukwaa la siasa? Mimi sizungumzii uchapa kazi wa mheshimiwa Waziri, ninachozungumzia ni hili suala ambalo kwa upeo wangu finyu naona lingeshughulikiwa tofauti. Kwa kufanya hivi walivyofanya tunawapatia sababu viongozi wa mashirika yetu kudai kuwa walikuwa wanatimiza maagizo ya waziri. Mimi naamini waziri anatakiwa kusimamia sera na si utendaji wa kila siku wa shirika. Management wapewe full responsibility ya kutekeleza sera na pale wanapozembea washughulikiwe.

Fundi Mchundo nakubaliana na wewe kabisa, umejieleza vizuri sana. Mimi nimejiuliza kwamba huyu Magufuli alipokuwa analalamika (sihoji utendaji wake, nakubali anajitahidi na nimeshamsifu kwa hilo), alipolalamika hadharani, alikuwa anamfikishia nani ujumbe huo? Maana kama ni rais, mbona ana nafasi nyingi tu za kumpelekea ripoti za utendaji, tena zilizoandikwa na kuhaririwa? Kama ni hao mawaziri wenzake, mbona anaweza kuwasiliana nao kiofisi, kwa simu, maandishi, mikutano ya ndani, mikutano ya mashauriano (consultative meetings), nk? Kama ni hao DAWASCO na sijui TANESCO, wote anaweza kuwapata moja kwa moja au kupitia kwa mawaziri wao. Kumbe alikuwa anamtaarifu nani basi? Jibu langu: Alikuwa anatoa taarifa hizo kwa wananchi waliohudhuria pale, na kwa wengine popote walipo kwa kupitia kwa waandishi wa habari.

Ni mazingira gani yanayoweza kumfanya waziri atangaze mbele ya umma jambo ambalo angeweza kulishughulikia ndani kwa ndani? Yapo mazingira kadhaa:
1. Labda katumwa hivyo na mkuu wake (Mwungwana mwenyewe kaka yetu JK), ili impe ushahidi ama justification ya kuchukua hatua fulani anayotaka kuchukua. Ametumwa kuuandaa umma kuipokea hatua hiyo. Kabla hujamwua mbwa wako inabidi ukusanye ushahidi wa kuwaonesha wanao (hasa wale wanaompenda mbwa huyo) kwamba huyu mbwa siku hizi ni mdokozi, anauma watu hovyo (pengine ana kichaa), hafai, ni mbaya, nk,nk. Siku ukimvutia trigger ukamlipua watoto watakuwa walishakubali kwamba kweli alikuwa hafai tena, bora kafa!
2.Labda alishachukua hatua zote za kuwasiliana na hao wenzake bado wakagoma kutoa ushirikiano, na hata rais alishaambiwa taarifa zote hizo na bado hakuchukua hatua yoyote. Kwa hiyo hapa waziri anatoa taarifa kwa wananchi kwamba 'oneni nilivyo na bidii miye, lakini wote hawa wananiangusha!'. Hapo JK wala asichekelee, wote wameshitakiwa kwamba hawatimizi wajibu wao!
3.Labda ndio mtindo wa waziri huyo wa kufanya kazi na kushindana na mawaziri wenzake. Hata wanafunzi wa namna hii wapo, nilipokuwa mwalimu niliyaona sana haya. Unatoa kazi wanafunzi waifanye katika kundi, ambako unafahamu mmoja wao ana uwezo sana kiakili. Wanapofanya kazi pamoja kwenye kundi, anachangia kiasi kidogo tu tena cha mwenye uwezo wa kawaida, au anangangania kwenye kundi kwamba kazi igawanywe visehemu, kila mtu chake. Akigawiwa hivyo kweli, kwanza kile kisehemu alichofanya yeye kitaonekana tofauti kabisa unaposoma hiyo kazi, ni kizuri sana! Lakini kwingine kubovu, kwa hiyo kwa ujumla wao wanapata maksi ndogo. Wakati wa kujadili masahihisho ya kazi mbele ya mwalimu, yeye ndio anakuja na resources nyingi zenye majibu mpaka ya yale majukumu ya wenzake! Sasa mwalimu unashangaa, huyu kijana haya anayosema wakati wa kujadili masahihisho mwisho wa kazi (hapo kundi lake limeshapata maksi ndogo za kawaida tu), kwa nini hakuyaweka kwenye kundi wakapata A? Ukimwuliza haya umeyapata wapi? Anakujibu mambo yote haya mwalimu yako kule maktaba, hawa wenzangu hawako makini tu! Kwa hiyo anajionesha alivyo mchapakazi na wenzake walivyo wavivu. Yaani sifa yake ya uchapakazi inatokana na uvivu wa wenzake, kwani wenzake pia wakitia bidii kama yeye, na wote wakawa wachapakazi, basi sifa yake ataikosa! Kwa hiyo kudumu kwa sifa yake kutatokana na wenzake kuendelea kuwa "bongolala!" Ili aonekane na sifa nzuri inabidi ahakikishe sifa mbaya za wenzake zinaendelea kuwepo, na si hivyo tu, ZIJULIKANE, ili watoao sifa waweze kupambanua! Tabia hii alikuwa nayo "Mangi" Lyatonga, hadi ikafikia hatua ya kufanya kazi za mawaziri wenzake kwa mtindo wa kuingilia waziwazi.
 
Watanzania wenzangu haya ndiyo yaliyotufikisha hapa tulipo. Alichofanya Mh Magufuli ni sawa. Kumbukeni huyu si wa kwanza kufanya hivyi, hat Augustino Lyatonga Mrema alifanya hivyo mwaka 1995 kuhusu issue ya Chavda, lakini yako wapi. Mh Rupia aliendelea kula nchi. Sana sana wananchi wakamuunga mkono Lyatonga kila alicho kifanya, ukiachia inayomuendea hivi sasa.

Hii itasaidia wananchi baadaye kuwajuwa viongozi mizigo na wachapakazi. Wakifuata collectice responsibility tutajua vipi.

Tuache tabia ya kuficha ukweli bali ukweli uanikwe wazi wazi ili wananchi wachekeche pumba na mchele.

Kumbukeni pia haya mambo ya collective responsibility ndiyo yametufikisha hapa kiasi kwa mtu anakuwepo kwenye baraza awamu zote lakini akipata Urais anaanza kukosoa mambo wakati na yeye alishiriki kuamua kwenye Cabinet.

Lakini wakiendelea kuumbuana hivi, wataogopa hata kuchukua form za kuomba nafasi kubwa wakijua tayari tunaujua udhaifu wao.

Bravo Magufuli! Obligado Magufuli! Hongera sana
 
Thanks Kithuku for that exhaustive analysis.

Mimi naamini options 2 or 3, more slanted towards 3.
 
Kithuku, analysis safi sana hiyo. Mfano wako wa mwanafunzi kipanga umenikumbusha mbali sana!
 
nampongeza waziri magufuli..na pamoja na kuwa magufuli ni muwazi na haogopi kusema..KUNA KITU KIMOJA ANAKIJUA KUWA RAIS KIKWETE HAJAPATA KUMUUNGA MKONO WALA KUMPENDA ALIMCHAGUA TU KWA SHINIKIZO..kama alivyomchagua prof mwandosya.

nadhani watu kama mwandosya na magufuli[amabao wamepewa wizara walizopewa ili washindwe] hawatapenda kuwekwa kwenye kundi moja la mawaziri wazembe wa muungwana kama kina chenge..ets al..kama kura za maoni zanavyoonyesha..wapo mawaziri wachapa kazi ila wanaangushwa na rais...kama rais anayo akili amemuelewa.

kuna jambo moja la muhimu ...mawaziri kama mwandosya na magufuli wanayo option ya kujiuzulu uwaziri kama wanahisi baraza ni la VILAZA ...
 
kuna jambo moja la muhimu ...mawaziri kama mwandosya na magufuli wanayo option ya kujiuzulu uwaziri kama wanahisi baraza ni la VILAZA ...
Hapo mzee inabidi nikupinge, mawaziri wachapa kazi wakijiuzulu na kuwaacha vilaza peke yao hapo barazani basi tutakao umia ni sisi wananchi, hao wasiofanya kazi ni kuwaumbua tu, maana mtanzania hata ukimpiga faini hana noma ataendelea tu kuendeleza ujinga, lakini ukimuumbuwa mbele ya watu na kumueleza ukweli wa ujinga wake mbele za watu basi atajirekebisha mara moja, ndio maana hata JK mwenyewe huwa anatishia nitawasema nyie kwa wananchi msipowagawia wakulima miti yao tena mbele ya wananchi. That is a new justice system which works a lot kuliko hata mahakama zetu uchwara.

Ile staili ya kina Slaa na kina Zitto ya kuwaanika watu walivyo inaleta matokeo yaliyokusudiwa kuliko hata kumpeleka mtu mahakamani. Nadhani tuwape hawa watu tuzo la kuivimbua hii staili mpya, kila mtu amefuata mfano wao baada ya kuona makali yake.

Nina uhakika kuwa Magufuli alifuata taratibu zote na hamna matokeo yaliyoonekana kutoka kwa hizo wizara husika, lakini sasa subiri uone jinsi watakavyochakarika baada ya kuumbuliwa.

Mzee Magufuli hongera na endelea kuchapa kazi mze. Hiyo ndio kitu tunaita kuutumikia umma, sio watu wengine huwa wanatamba nimeutumikia umma sijui miaka thelathini, ukimuuliza nini uli-achieve? utasikia ooh, mara hili mara lile, na ukiendelea kudadisi kwa sababu bado hujapata jibu mara anakuwa mkali eti we kijana hauna adabu.
 
Sina matatizo na Mheshimiwa Waziri kuzungumzia adha NHC walizozipata katika kupata hizo huduma. Wasiwasi wangu ni kuwa kama kiongozi kama waziri inabidi asubiri mpaka kwenye mkutano wa hadhara ili aweze kumweleza Mh. Rais kuhusu haya matatizo ni alama ya deeper malaise. Ni kama vile ninaposikia wakuu wakitembelea mikoani wanapokea ripoti za utendaji wa kazi kwenye mikutano ya hadhara! Hivi kweli hakuna taratibu zilizomo serikalini za kuweza kuwasilishwa hizi ripoti, kuchambuliwa na pale zinapoonekana kuna mapungufu mhusika kushughulikiwa? Wasiwasi wangu ni kuwa katika fora kama hizi ni vigumu kupata the true picha maana upande mmoja unakuwa hauna nafasi ya kujieleza! Pengine mimi ni naive!

Sasa ni miaka 46 tangu tupate uhuru wetu mambo ya kuzungumzia mafichoni hadi sasa hatuoni maendeleo yake. Nampongeza sana Mh Magufuli kwani hawa mawaziri watajua nini maana ya kuwajibika kwani wakati mwenzao anajenga nyumba hawakujua kwamba nyumba zile zinahitaji kuwepo maji na barabara na umeme. Hawa mawaziri ni wazembe sana tangu siku nyingi. Inaelekea hata walipokuwa katika shughuli hiyo bado hawakujua nini ilikuwa wajibu wao pale Chalinze hadi Mh Magufuli alipokuwa akitaja wizara zao wakawa wanashituka na kusikiliza nini Magufuli anaongelea na ndiyo maana unakuta Chenge aliduwaa akimuangalia Magufuli wakati akitoa cheche zake kisha akageuka kumwangalia Mh Rais kwamba analipokeeje hilo. Rais alichokizungumza pale ni uungwana tu ili wnanchi wasianze zome zome mbele yake. Kuna haja sasa sisi wenyewe tuwe hivyo ili tuamshane tuijenge Tanzania yetu.
 
There is such a thing as "collective responsibility". Naelewa alichosema ni kweli na kinahitaji kusemwa but not in such a fashion.Serikali lazima i present a united front hata kama kuna tofauti.Hii inaonyesha jinsi tatizo lilivyo kubwa, incompetence mpaka kufikia mawaziri kulumbana hadharani.
Hizi mambo za "fashion" "collective resposibility" etc zinaturudisha nyuma. Wazembe waitwe wazembe full stop! No blah blah. Hizi fasheni ndio zinatufanya mpaka leo mika 46 ya Uhuru watu hawana maji ya kunywa.
 
Many Tanzanians always had a penchant for cheap popular politics, this smells of Mremaism.There has got to be a more efficient way of doing business than this.

Kuna watu wako impressed mpaka na rais kuingia katika huu ujinga wa "nitakusemeeni kwa wananchi"? I mean rais mwenye nguvu zote za dola na fimbo ya appintment naye anahitaji nini zaidi?

Right or wrong, kwa mtu mwenye access na rais na mawaziri kama Magufuli kupayuka kama vile ana lake jambo.Mi nina support theory 3 ya Kithuku which is dangerous indeed.
 
There is such a thing as "collective responsibility". Naelewa alichosema ni kweli na kinahitaji kusemwa but not in such a fashion.Serikali lazima i present a united front hata kama kuna tofauti.Hii inaonyesha jinsi tatizo lilivyo kubwa, incompetence mpaka kufikia mawaziri kulumbana hadharani.

Alikuwa hivyo by then Ben ni Rais kwahiyo si dhambi kufanya hivyo JK akiwa ndiye muhimiri cha muhimu ni nani beneficiary ktk msuguano huo; amini usiamini hawa jamaa huo uwaziri wao under hiyo collective uwabijibikaji ndio chanzo cha matatizo ya nchi,hata JK mwenyewe ni shahidi,muulizeni mradi wa maji kwao alianza lini? Maana mpaka wale wachina walipomletea maji pale ilikuwa ni baada ya kuzungushana hukuhuko tangu enzi ya Mwinyi,u Can imagine JK akiwa waziri Maji,Nishati na Madini aliwahi kukodi mitambo ya kuchimbia malambo ya maji kule kwao toka Stamico-Pugu Kaolin kazi ilifanywa kwa heshima ya Mh. waziri,yeye akaweka kila kitu clear ili Pugu Kaolin walipwe, what happened baada ya yeye kuhamia fedha-then- Foreign,hela ililipwa na yeye akiwa foreign tena kwa mbinde sana na mlipaji akiwa ndg yetu Kigoda. Unaweza kuona huo uwajibikaji ulivyo na unawadhuru wananchi wa Kawaida.

Magufuli yuko sahihi kama alivyosema yeye,kuwa Mh.Rais kwa uwazi yanipasa kuyasema haya mbele ya waheshimiwa wenzangu.............


Tunachoshukuru ni rais ku respond wisely on the issue lakini hoja hii ya Pombe Magufuri isimfanye muhanga wa kimamlaka kama walivyo wengi hapa JF wanavyotaka.
Thank you
 
Hivi kweli alishindwa kuwachongea hao wenzake mpaka kwenye mkutano wa hadhara?
Jibu ni ndiyo.Kafanya vema ili na sisi tujue kwa nani na nani wanafanya nini.JK anasema wakae wajadiliane,wajadiliane nini wakati wapangaji wameanza kuumizwa na gharama za ziada ambazo serikali ilipaswa kugharamia kupitia hizo wizara husika?
Magufuli tumekusikia loud and clear.
 
Many Tanzanians always had a penchant for cheap popular politics, this smells of Mremaism.There has got to be a more efficient way of doing business than this.

Kuna watu wako impressed mpaka na rais kuingia katika huu ujinga wa "nitakusemeeni kwa wananchi"? I mean rais mwenye nguvu zote za dola na fimbo ya appintment naye anahitaji nini zaidi?

Right or wrong, kwa mtu mwenye access na rais na mawaziri kama Magufuli kupayuka kama vile ana lake jambo.Mi nina support theory 3 ya Kithuku which is dangerous indeed.

Ndugu Pundit, tunatakiwa tutumie zana zote tulizonazo katika kuwalazimisha watu wafuate wajibu wao.

Hizo njia za kawaida za mawasiliano katika mikutano yao ya baraza la wawaziri au kuandikiana vimemo n.k lazima itumike na wanaitumia, at the same time kuwashitaki hawa watu kwa wananchi ni njia nyingine pia ambayo lazima itumiwe vile vile, isipotumiwa je wananchi tutajuaje nani mzembe? kesho keshokutwa CCM ikimpitisha Chenge kugombea uraisi je wananchi tutajuaje ufanisi wa kazi zake kama hamna mtu wa kutueleza waziwazi?

Mimi binafsi ninaufurahia na kuushabikia sana huu utaratibu mpya wa uwazi, mtu kusema nitakushitaki kwa wananchi ina maana jamaa wameanza kutambua wananchi ndio waajiri wao.

Embu jaribu ku-imagine kama uzembe uliofanyika katika mikataba ya madini ingeelezwa kiuwazi namna hii je Karamagi angethubutu kusign? Je kabla ya Mramba kutoa msamaha wa kodi wa maisha kwa yale makampuni, kama kungekuwa na kiongozi kama Magufuli asiyeogopa kusema wazi wazi angethubutu yule kutoa msamaha ule?

Pundit najua kukulia katika mazingira ya bongo yametu-influence sana, tunaogopa kusema ukweli wazi wazi, tunaogopa kumtaja mtu jina lake wazi kama amefanya ufyoro, uwazi tunauogopa lakini mze wakati umefika tulazimike kusoma alama za nyakati, nyakati za kufichaficha zimekwisha haswa haswa kuficha maovu.

Nchi zilizoendelea hawanaga dogo, viongozi wanapashana wazi wazi, tusiige tu mambo fulani ya kifahari kutoka kwao, hata haya yanayoleta changamoto ya kujirekebisha na kuendelea tuyaige pia jamani.
 
Kwangu mimi mtu ukiwa katika baraza la mawaziri lazima kuwe na collective responsibility.Kama alivyosema Msuya, if you are Catholic you must abide by the papacy, ama sivyo unajitoa katika ukatoliki na kusimama kwa evangelicals na kusema msimamo tofauti.

Baraza la mawaziri must simply speak with one voice.Ama sivyo inakuwa chaos.Ukiona baraza linafanya kinyume na wewe unavyoona ni right platforms mbona nyingi tu? Unaweza kujiuzulu kwenda kuwa backbencher wa CCM, unaweza kuwa columnist wa magazeti, unaweza kuungana na upinzani na kuendelea kuwa moto.

Not to absolve Chenge and Kawambwa, but somehow I get the feeling Magufuli is going for cheap populism.Haya mambo ya "bread and circus" Tanzania tunayapenda sana.Kifupi Waziri Magufuli alikuwa antaka favoritism iwe applied kwenye mradi wake bila kufuata utaratibu uliokuwepo.Kwanza mradi kwenda Chalinze favoritism, na yeye anataka kuweka favoritism juu ya favoritism ili kum-please boss wake Kikwete.The sad thing is that this whole biz is backfiring on him hata Kikwete anamuona jamaa anatafuta sifa.
 
Pundit
nadhani sababu unazotoa hapa bado ni very weak..hiyo collective responsibility ni cover ya weaknesses pamoja na maovu ya watawala.
 
Mfwatiliaji,

My thing is,the government should work in harmony.If you think there is machinations and such, resign and seek another platform. Sasa hivi tunajuaje kwamba bwana Magufuli hana mengi ya kusema ambayo hawezi kwa sababu nu government minister?

Hivi kweli watu wanatetea Magufuli kutumia ugangwe na power ya public opinion kuwa-hoodwink mawaziri wengine waingilie utaratibu wa ratiba za maji na barabara kwa sababu ya project yake?
 
Kwangu mimi mtu ukiwa katika baraza la mawaziri lazima kuwe na collective responsibility.Kama alivyosema Msuya, if you are Catholic you must abide by the papacy, ama sivyo unajitoa katika ukatoliki na kusimama kwa evangelicals na kusema msimamo tofauti.

Baraza la mawaziri must simply speak with one voice.Ama sivyo inakuwa chaos.Ukiona baraza linafanya kinyume na wewe unavyoona ni right platforms mbona nyingi tu? Unaweza kujiuzulu kwenda kuwa backbencher wa CCM, unaweza kuwa columnist wa magazeti, unaweza kuungana na upinzani na kuendelea kuwa moto.

Not to absolve Chenge and Kawambwa, but somehow I get the feeling Magufuli is going for cheap populism.Haya mambo ya "bread and circus" Tanzania tunayapenda sana.Kifupi Waziri Magufuli alikuwa antaka favoritism iwe applied kwenye mradi wake bila kufuata utaratibu uliokuwepo.Kwanza mradi kwenda Chalinze favoritism, na yeye anataka kuweka favoritism juu ya favoritism ili kum-please boss wake Kikwete.The sad thing is that this whole biz is backfiring on him hata Kikwete anamuona jamaa anatafuta sifa.

Pundit:
Just for a moment, lets assume Mh. Magufuli alishafanya kila linalotakiwa, ikiwa ni pamoja na hiyo 'collective responsibility' kufuatilia ili kazi ile ifanyike bila ya mafanikio yoyote. Then the next thing would be just to shut up!

Then wananchi tungejua ni Magufuli ndie mzembe, kazi imemshinda.

Frustrations wanazozipata wananchi wa kawaida, sadly enough, hata vigogo mara nyingine huzipata hivyo hivyo! Pengine the other alternative ingebidi Magufuli aanze mipango ya kutoa chochote kazi ifanyike, ili asionekane kuwa kazi haiwezi.

Magufuli was right to expose these incompetences and irresponsibilities within the government. He must have carefully calculated the risks involved. He is brave. Ndio unafiki tusioutaka - kila siku tunachekeana tuuu, hakuna lolote la maana tunalolifanya. This practice must end.
 
Kwangu mimi mtu ukiwa katika baraza la mawaziri lazima kuwe na collective responsibility...

Hapo nakuunga mkono moja kwa moja, collective responsibility lazima iwepo, mfano tukijenga nyumba wizara ya maji ihakikishe maji yapo, wazara inayoshughulikia umeme ichangie pia, miundo mbinu n.k. Sasa hawa mawaziri wengine wameona hakuna haja ya collective responsibility na kumuacha mzee Magufuli solemba atajiju mwenyewe, ndio maana jamaa akaja juu kwamba jamani mbona tumeacha ku-take responsibility collectively? jamani mambo gani haya kulisukuma gurudumu la maendeleo on the opposite direction?

Wakati umefika watu kuli-define upya neno Responsibility, kuwadai watu fedha za umeme au maji bila kuwapa watu hiyo huduma siyo responsibility hata kidogo hii inaitwa irresponsibility, na watu wanayoitetea hii kitu wakati ni huu wakutambua kuburuzaburuza wananchi sio jambo jema na likemewe hadharani jambo hilo.

Sasa kama kulikemea hilo jambo waziwazi na kutetea haki za wananchi ni kutafuta sifa basi viongozi wetu sharti moja wawe watu wa kutafuta sifa.Na kama kuuminyia uovu huo ndio sio kutafuta sifa basi viongozi wa namna hiyo hatuwahitaji unless tuwe watu tunaopenda shida, mimi binafsi sipendi shida na ninachukia dhuluma na shida tunazoletewa bila hiari yetu na nina uhakika watanzania wengi hawapendi dhuluma vilevile.
 
Katika hafla ya jana, Bw. Magufuli, alianza kuishutumu Wizara ya Miundombinu, inayoongozwa na Bw. Chenge, kuwa imeshindwa kuboresha miundombinu inayoelekea katika maeneo yaliyotumika kwa ujenzi wa nyumba za NHC.

``Mheshimiwa Rais, Shirika la Nyumba la Taifa limejikuta linaingia gharama kubwa katika kuboresha miundombinu, iliyopaswa kushughulikiwa na wizara husika, lakini wameshindwa kutekelea wajibu wao huo,`` alisema.

Wakati akisema hayo, Bw. Chenge aliyehudhuria mkutano huo, alikuwa akimtazama Bw. Magufuli na baadaye kuelekeza macho yake kwa Rais Kikwete.

Bw. Magufuli, aliyeonekana kujiamini katika kutoa madai hayo, alitoa mfano wa miundombinu iliyogharamiwa na NHC, ni barabara, njia za maji na nguzo za umeme.

Aidha, alisema Wizara ya Maji inayoongozwa na Dk. Kawambwa, ambaye pia alikuwapo mkutanoni hapo, imeshindwa kufikisha huduma ya maji katika maeneo yenye nyumba hizo

What Magufuli does not say, and due to his fiery delivery one suspects he is being modest as Churchill would have it "because he has much to be modest about" is whether there was any agreement for the respective ministries to give preferential treatment to this project.Kama kulikuwa na mkataba au makubaliano mahsusi, basi Magufuli anafanya dhambi ya ku-under report the problem.Kama kulikuwa na makubaliano hayo, na kajaribu kupata msaada wa ikulu na mawaziri bila mafanikio then anaweza kusema hivyo kwa frustration akiripoti kwa wananchi kama point ya mwisho kabla ya kujiuzulu kutokana na fundamental differences kati yake na cabinet in work ethics.

Lakini maneno yake (direct quote) hayaonyeshi kama kulikuwa na makubaliano hayo.In that case kila mbunge wa sehemu isiyo na maji Tanzania anaweza kusema huvyo na anapoteza mantiki ya kulalamika kwa sababu inabidi kila mtu asimame kwenye mstari. Ssasa yeye alitaka kukatisha msitari na mambo ya favoritism kwa sababu ya kujikomba kwa Kikwete kwamba mradi wa nyumba unahusika kwao ama vipi? Kama ratiba ilisema watu wa Pugu wapewe maji je na wizara ilikuwa ina concentrate huko?

We have to see further than these cheap political shots.Huyu Magufuli hana tofauti na Mrema, the only difference ni kuwa yeye hana guts za kujiuzulu lakini he is just another attention craving Mrema in the making.
 
Pundit, am sorry,
Sikuabaliani nawewe na collective responsibility ya kuficha uozo ulio tufikisha tulipo!
Ni haya haya mambo ya collective resp, yameletelezea u mwenzetu, kulindana, mtu anavuruga hapa anahamishiwa pale!
hata akikosea mambo yanafunikwa

Tanzania sasa inakaribia kuuzwa na kwisha kabisa kwa hizo fasheni za collective resp.

Mpaka lini?? tumewachoka, tunahitaji kina magufuri 7 mara 70, wanao sema kweli kweli tupu, Mungu awasaidie tufikie ukombozi wa kweli siyo ukombozi wa jina kama tulio nao sasa!
 
Back
Top Bottom