Mawaziri wa Dkt. Magufuli waanza kazi kwa kasi

dadoliz

Member
Jul 27, 2015
59
40
Wakati wapenda maneno na siasa za kukosoa wakati wote, wasio ona jema hata moja wakiendelea na uchambuzi wao wa jinsi wanavyoliona baraza la mawaziri la JPM, Askari wa mwavuli wa JPM wameanza kupiga kazi kwa kasi ya ajabu. Jionee mwenyewe hapa.

Baada ya Kuapishwa tu, Kigwangalla afanya ziara ya kushtukiza Hospitali ya Amana


Naibu waziri
wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Khamis Kigwangala akielekea katika hospitali ya Amana leo jijini Dar es Salaa mara baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Joseph Magufuli.
KIGWANGALLA-4.jpg

Naibu waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Khamis Kigwangala akizungumza na wauguzi aliowakuta katika hospitali ya Amana leo alipotembelea katika hospitali hiyo jijini Dar es Salaam.
KIGWANGALLA-1.jpg

Akizungumza na wagonjwa
=============

WAZIRI KITWANGA AKARIBISHWA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI MARA BAADA YA KUAPISHWA IKULU LEO



Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (kushoto) akiteta jambo na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Mbarak Abdulwakil (kulia) na Naibu Katibu Mkuu, John Mngodo mara baada ya kumpongeza Waziri huyo mpya, nje ya Ukumbi wa Mikutano Ikulu, jijini Dar es Salaam. Picha na Felix Mwagara, Kitengo cha Mawasiliano-MOHA
kit2.jpg


kit3.jpg



Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil (kushoto) akimkaribisha Waziri mpya wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga, ndani ya ofisi ya waziri huyo iliyopo Mtaa wa Ohio, jijini Dar es Salaam. Picha na Felix Mwagara, Kitengo cha Mawasiliano-MOHA

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga akisaini kitabu cha wageni kilichopo ndani ya ofisi yake, mara baada ya Waziri huyo mpya kuingia ndani ya ofisi hiyo baada ya kuapishwa Ikulu jijini Dar es Salaam leo. Picha na Felix Mwagara, Kitengo cha Mawasiliano-MOHA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil (wapili kushoto) akimfafanulia Waziri mpya wa Wizara hiyo, Charles Kitwanga (kulia), shughuli mbalimbali zinazofanywa na wizara hiyo. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, John Mngodo. Tukio hilo lilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara hiyo jijini Dar es Salaam, mara baada ya Waziri huyo kuapishwa Ikulu leo. Picha na Felix Mwagara, Kitengo cha Mawasiliano-MOHA


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (kulia) akijadiliana na watendaji wa wizara hiyo kuhusu masuala mbalimbali ya wizara hiyo, mara baada ya Waziri huyo kuapishwa Ikulu jijini Dar es Salaam leo. Wanne kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mbarak Abdulwakil, anayefuata ni Naibu Katibu Mkuu, John Mngodo, Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza (CGP), John Minja, Naibu Mkuu wa Jeshi la Polisi (D/IGP), Abdurahman Kaniki na Kamishina wa Fedha na Utawala wa Idara ya Uhamiaji, Piniel Mgonja (hayupo pichani). Picha zote na Felix Mwagara, Kitengo cha Mawasiliano-MOHA.

SOURCE: FULLSHANGWE BLOG

HAPA KAZI TU
 
Tunaomba kazi ifanyike kwa weledi zaidi, upande wa mambo ya ndani naomba majambazi yashughulikuwe kwa kina
 
Nchi ya kipuuzi hii,maendeleo hayaji kwa ziara za kushtukiza,acheni maigizo
 
Hivi sasa hadi Wana ndoa wanafanya ziara za kustukiza kwa michepuko yao!!..Najiuliza hakuna namna nyingine ya monitoring and Evaluation mpaka kustukiza?..Ni wapi duniani maendeleo yalipatikana kwa ziara za kustukiza?..Je Nape Nnauye akifanya ziara ya kustukiza katika kambi ya Taifa Stars ndio itakwenda World Cup?..
 
Jamaa si kawapa mikataba? wakiboronga, wanafukuzwa then wanafunguliwa mashitaka! sidhani kama wataweza kasi ya magufuri!
 
Waziri wa mambo ya ndani naomba utuondolee hii kero ya askari wa usalama barabarani!! Wengi wamenunuliwa tochi kama kifaa cha kukusanya rushwa!! Hii ni aibu!! Kuthibiti mwendo kwenye vibao vya speed limit 50kph sio kuwa ajali zitapungua!! Huu ni muanya mkubwa wa rushwa!! Imefika wakati polisi hawadai hata overtime wamekuwa kama wameambiwa kuku hula kwa urefu wa kamba yake!!! Wapo road hadi usiku!! Fikiria kutoka dar hadi mlandizi unakutana na polisi 57 wa usalama barabarani siku ya jumapili!! Najiuliza uzalendo huu wameutoa wapi? Ata kama ni overtime hii sasa ni zaidi!!! Kweli ni kero
 
Sikatai uwepo wa check points ambazo ni well planned ili kuwakamata wahalifu na wavunja sharia ila hii ya kukaa kwenye vibao vya 50 kph haina faida yoyote!! Ni muhimu kwa vijiji vilivyopakana na barabara kubwa kupewa elimuzaidi na sio kuanzisha miradi ya overtime kwa polisi
 
Nchi ya kipuuzi hii,maendeleo hayaji kwa ziara za kushtukiza,acheni maigizo

Wewe jinga kweli. mfumo Wa kushtukiza ni bora unapo kuwa unatathmini utendaji Wa watu. Wafanyakazi wetu uvivu umewajaa. Wakifanya huku wanajua kiongozi atawashtukiza muda wowote basi hawawezi zembea hata kidogo.

Inaelekea wewe siyo mtanzania. Upumbavu umekujaa
 
Back
Top Bottom