Mawaziri matumbo joto

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,005
Mawaziri matumbo joto

Mwandishi Wetu Novemba 14, 2007
Raia Mwema

MABADILIKO katika Baraza la Mawaziri sasa ni suala la muda tu kwani wakati wowote Rais Jakaya Kikwete atatangaza timu yake mpya, Raia Mwema imefahamishwa.
Habari zilizothibitishwa na vyanzo vya habari ndani ya Serikali zinaeleza kwamba tayari waraka maalumu wa uamuzi huo, “uko mezani kwa Rais Kikwete, kabla ya kuuweka bayana wakati wowote kuanzia leo.”

Habari za hivi karibuni zinataja kuachwa kwa mawaziri saba na manaibu waziri watano huku wakiingizwa wengine ambao wanatokana kwa kiasi kikubwa na matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa CCM uliomalizika karibuni, Kizota, Dodoma.

Hatua hiyo inaelezwa kwenda sambamba na hali ya kisiasa na kiutendaji miongoni mwa wasaidizi hao, ambao amekua akiwapima kwa kipindi chote alichowapa madaraka na kuwapa nguvu ya kufanya maamuzi mazito.

Hata hivyo, wachunguzi wa mambo wanasema huenda Kikwete akapata upinzani mkali kutoka kwa baadhi ya wasaidizi wake ambao wanatajwa kuwa na nguvu kubwa ndani na nje ya mfumo rasmi wa uongozi wa chama na Serikali.

Hata hivyo, matokeo ya mwisho wa uchaguzi ndani ya CCM na hata kitendo cha Kikwete kupinga waziwazi vitendo vya rushwa, vinaelezwa kuwa vinakwenda sawa na haiba yake halisi ya kuwa mtu ambaye asingependa mambo yaendelee kuwa ya hovyo.

“Amekua mkimya mno na alikwisha kutoa muda kwa wala rushwa ambao alisema wazi kwamba anawafahamu, na uamuzi wa kupiga vita rushwa ndani ya CCM ni uamuzi mzito ambao kwa wengi tuliona kama anaongeza maadui zaidi kuliko marafiki ndani ya chama, lakini amefurahisha wengi ndani na nje ya chama,” alisema kiongozi mmoja wa juu wa CCM.

Uteuzi wa Pius Msekwa kuwa Makamu Mwenyekiti wake Bara na kuingiza sura mpya ndani ya Sekretarieti ya chama hicho huku akimuacha Katibu Mkuu, Yussuf Makamba, kwa Bara na kuacha watendaji wote wa Visiwani, kumeelezwa kama “alama za nyakati” ambazo watendaji wa Serikali wanapaswa kuzisoma.

Pamoja na kuwa ni jarida hili pekee lililomtaja Msekwa kuwa mmoja wa waliokuwa wakitajwa kuwa wasaidizi wa Kikwete ndani ya CCM, bado uteuzi wake umekua wa kushitukiza kwa wengi hali ambayo huenda ikajitokeza katika mabadiliko anayotarajia kuyafanya ndani ya Serikali pia.

Ofisa mwandamizi wa Ikulu, ameiambia Raia Mwema kwamba Rais Kikwete amechelewesha mabadiliko hayo ambayo yamekuwa yakisubiriwa sana kutokana na msiba wa Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Salome Mbatia, kinyume cha maelezo ya wengi kwamba msiba huo ndio utakaomsukuma Rais kufanya mabadiliko.

“Ni kweli suala hilo liko mezani kwa Rais lakini aliona si vyema kwa wakati ule kutangaza kutokana na familia ya marehemu Mbatia kuwa katika msiba, lakini sasa nadhani wakati wowote atakaoona unafaa atatangaza anachokusudia kukifanya,” alisema ofisa huyo wa Ikulu, ambaye alisema hana mamlaka ya kutoa taarifa kwa waandishi wa habari.

Wanaotajwa kuwamo katika timu hiyo mpya ni pamoja Mbunge wa Siha, Aggrey Mwanri, ambaye ameondolewa katika nafasi ya ukatibu uenezi wa CCM na Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe.

Wengine ni rafiki wa karibu wa Rais Kikwete na Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, ambaye naye ameondoka kwenye Uweka Hazina wa CCM na nafasi yake kuchukuliwa na aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM, Amos Makala.

Baada ya kutangaza Baraza jipya la Mawaziri, Serikali ya Rais Kikwete, imekabiliwa na changamoto kadhaa ikiwa ni pamoja na zile zilizosababishwa na mabadiliko ya hali ya hewa na kudura za Mwenyezi Mungu na changamoto nyingine zilizosababishwa na udhaifu wa watendaji na hali ya kiuchumi.

Ukame ulioikumba nchi ulisababisha tatizo kubwa la nishati ya umeme, hali ambayo ilisababisha Serikali kuingia mkataba wa haraka haraka uliozua utata mkubwa na kampuni ya Richmond Development ya Marekani, kampuni ambayo pamoja na kuuza mkataba wake kwa kampuni nyingine ya Dowans, ilishindwa kuzalisha umeme kwa wakati kulingana na mkataba.

Uamuzi huo ulizua malalamiko na katika mabadiliko yake ya kwanza Kikwete alimuondoa katika Wizara ya Nishati na Madini, Dk. Ibrahim Msabaha aliyehamishiwa Wizara ya Afrika Mashariki, hatua ambayo ilionekana kama “kufunika kombe mwanaharamu apite” kwani mengi yameibuka baada ya hapo.

Changamoto nyingine kwa Rais Kikwete ni sakata la wanafunzi wa elimu ya juu ndani na nje ya nchi, ambao kwa wale wa ndani wamekua wakiandamana kuelekea ofisi za Bodi ya Mikopo na waliko nje ya nchi kuhangaika huku wengine wakirudishwa nyumbani baada ya kudhalilishwa kwa muda mrefu, huku Waziri wake Profesa Peter Msola, akitoa maelezo ya kujikanganya.

Hivi karibuni sekta ya madini imeibua mjadala mkubwa zaidi baada ya kuwapo kwa hoja ya kusainiwa kinyemela kwa mkataba wa mgodi wa dhahabu wa Buzwagi, uliosainiwa London, Uingereza, na Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, huku kukiwa na maswali mengi zaidi yasiyo na majibu.

Changamoto hizo na zile zilizotokana na mchakato wa uchaguzi ndani ya CCM na udhaifu katika maeneo mbalimbali serikalini, yanaelezwa kuwa msingi mkuu wa mabadiliko ambayo wananchi wengi wanatarajia Rais Kikwete atayafanyia marekebisho, pamoja na kuwapo taarifa kwamba maeneo hayo hayataguswa katika mabadiliko ya hivi karibuni.

Katika nafasi ya Salome Mbatia wanatajwa wanawake wengi ambao bado kwa hakika hakuna chanzo kilichokua na angalao hakika ya majina matatu ya wanaoweza kutoka atakayeziba nafasi hiyo.

Pamoja na taarifa za mabadiliko hayo kugusa hisia za Watanzania wengi, bado Rais Kikwete, ana mtihani mgumu wa kufanya uamuzi utakaorudisha imani ya wananchi kwa Serikali yake, ikizingatiwa kwamba baadhi ya wanaoguswa wako karibu yake.
 
Mawaziri matumbo joto

Mwandishi Wetu Novemba 14, 2007
Raia Mwema

MABADILIKO katika Baraza la Mawaziri sasa ni suala la muda tu kwani wakati wowote Rais Jakaya Kikwete atatangaza timu yake mpya, Raia Mwema imefahamishwa.
Habari zilizothibitishwa na vyanzo vya habari ndani ya Serikali zinaeleza kwamba tayari waraka maalumu wa uamuzi huo, “uko mezani kwa Rais Kikwete, kabla ya kuuweka bayana wakati wowote kuanzia leo.”

Habari za hivi karibuni zinataja kuachwa kwa mawaziri saba na manaibu waziri watano huku wakiingizwa wengine ambao wanatokana kwa kiasi kikubwa na matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa CCM uliomalizika karibuni, Kizota, Dodoma.

Hatua hiyo inaelezwa kwenda sambamba na hali ya kisiasa na kiutendaji miongoni mwa wasaidizi hao, ambao amekua akiwapima kwa kipindi chote alichowapa madaraka na kuwapa nguvu ya kufanya maamuzi mazito.

Hata hivyo, wachunguzi wa mambo wanasema huenda Kikwete akapata upinzani mkali kutoka kwa baadhi ya wasaidizi wake ambao wanatajwa kuwa na nguvu kubwa ndani na nje ya mfumo rasmi wa uongozi wa chama na Serikali.

Hata hivyo, matokeo ya mwisho wa uchaguzi ndani ya CCM na hata kitendo cha Kikwete kupinga waziwazi vitendo vya rushwa, vinaelezwa kuwa vinakwenda sawa na haiba yake halisi ya kuwa mtu ambaye asingependa mambo yaendelee kuwa ya hovyo.

“Amekua mkimya mno na alikwisha kutoa muda kwa wala rushwa ambao alisema wazi kwamba anawafahamu, na uamuzi wa kupiga vita rushwa ndani ya CCM ni uamuzi mzito ambao kwa wengi tuliona kama anaongeza maadui zaidi kuliko marafiki ndani ya chama, lakini amefurahisha wengi ndani na nje ya chama,” alisema kiongozi mmoja wa juu wa CCM.

Uteuzi wa Pius Msekwa kuwa Makamu Mwenyekiti wake Bara na kuingiza sura mpya ndani ya Sekretarieti ya chama hicho huku akimuacha Katibu Mkuu, Yussuf Makamba, kwa Bara na kuacha watendaji wote wa Visiwani, kumeelezwa kama “alama za nyakati” ambazo watendaji wa Serikali wanapaswa kuzisoma.

Pamoja na kuwa ni jarida hili pekee lililomtaja Msekwa kuwa mmoja wa waliokuwa wakitajwa kuwa wasaidizi wa Kikwete ndani ya CCM, bado uteuzi wake umekua wa kushitukiza kwa wengi hali ambayo huenda ikajitokeza katika mabadiliko anayotarajia kuyafanya ndani ya Serikali pia.

Ofisa mwandamizi wa Ikulu, ameiambia Raia Mwema kwamba Rais Kikwete amechelewesha mabadiliko hayo ambayo yamekuwa yakisubiriwa sana kutokana na msiba wa Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Salome Mbatia, kinyume cha maelezo ya wengi kwamba msiba huo ndio utakaomsukuma Rais kufanya mabadiliko.

“Ni kweli suala hilo liko mezani kwa Rais lakini aliona si vyema kwa wakati ule kutangaza kutokana na familia ya marehemu Mbatia kuwa katika msiba, lakini sasa nadhani wakati wowote atakaoona unafaa atatangaza anachokusudia kukifanya,” alisema ofisa huyo wa Ikulu, ambaye alisema hana mamlaka ya kutoa taarifa kwa waandishi wa habari.

Wanaotajwa kuwamo katika timu hiyo mpya ni pamoja Mbunge wa Siha, Aggrey Mwanri, ambaye ameondolewa katika nafasi ya ukatibu uenezi wa CCM na Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe.

Wengine ni rafiki wa karibu wa Rais Kikwete na Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, ambaye naye ameondoka kwenye Uweka Hazina wa CCM na nafasi yake kuchukuliwa na aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM, Amos Makala.


Baada ya kutangaza Baraza jipya la Mawaziri, Serikali ya Rais Kikwete, imekabiliwa na changamoto kadhaa ikiwa ni pamoja na zile zilizosababishwa na mabadiliko ya hali ya hewa na kudura za Mwenyezi Mungu na changamoto nyingine zilizosababishwa na udhaifu wa watendaji na hali ya kiuchumi.

Ukame ulioikumba nchi ulisababisha tatizo kubwa la nishati ya umeme, hali ambayo ilisababisha Serikali kuingia mkataba wa haraka haraka uliozua utata mkubwa na kampuni ya Richmond Development ya Marekani, kampuni ambayo pamoja na kuuza mkataba wake kwa kampuni nyingine ya Dowans, ilishindwa kuzalisha umeme kwa wakati kulingana na mkataba.

Uamuzi huo ulizua malalamiko na katika mabadiliko yake ya kwanza Kikwete alimuondoa katika Wizara ya Nishati na Madini, Dk. Ibrahim Msabaha aliyehamishiwa Wizara ya Afrika Mashariki, hatua ambayo ilionekana kama “kufunika kombe mwanaharamu apite” kwani mengi yameibuka baada ya hapo.

Changamoto nyingine kwa Rais Kikwete ni sakata la wanafunzi wa elimu ya juu ndani na nje ya nchi, ambao kwa wale wa ndani wamekua wakiandamana kuelekea ofisi za Bodi ya Mikopo na waliko nje ya nchi kuhangaika huku wengine wakirudishwa nyumbani baada ya kudhalilishwa kwa muda mrefu, huku Waziri wake Profesa Peter Msola, akitoa maelezo ya kujikanganya.

Hivi karibuni sekta ya madini imeibua mjadala mkubwa zaidi baada ya kuwapo kwa hoja ya kusainiwa kinyemela kwa mkataba wa mgodi wa dhahabu wa Buzwagi, uliosainiwa London, Uingereza, na Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, huku kukiwa na maswali mengi zaidi yasiyo na majibu.

Changamoto hizo na zile zilizotokana na mchakato wa uchaguzi ndani ya CCM na udhaifu katika maeneo mbalimbali serikalini, yanaelezwa kuwa msingi mkuu wa mabadiliko ambayo wananchi wengi wanatarajia Rais Kikwete atayafanyia marekebisho, pamoja na kuwapo taarifa kwamba maeneo hayo hayataguswa katika mabadiliko ya hivi karibuni.

Katika nafasi ya Salome Mbatia wanatajwa wanawake wengi ambao bado kwa hakika hakuna chanzo kilichokua na angalao hakika ya majina matatu ya wanaoweza kutoka atakayeziba nafasi hiyo.

Pamoja na taarifa za mabadiliko hayo kugusa hisia za Watanzania wengi, bado Rais Kikwete, ana mtihani mgumu wa kufanya uamuzi utakaorudisha imani ya wananchi kwa Serikali yake, ikizingatiwa kwamba baadhi ya wanaoguswa wako karibu yake.

Mhh Hayo majina yanayotajwa hapa:

Rostam Aziz - Nani alisema Mtandao unapigwa chini?

Mwakyembe - Nani alishangaa huyu kuwekwa kamati zote mbili?

Nani yule alipinga kuwa Kikwete hataongeza ukubwa wa baraza la mawaziri ili liwe kubwa kuliko yote duniani na liongeze matumizi yake kutoka madafu bill 1 kwa mwezi ya sasa kwenda madafu bill 2 au zaidi?

Kazi kweli kweli!
 
Hiyo habari ina siri kubwa,
Msola nje,
Msabaha nje,
Mramba nje,
Mungai nje,
Mwakyusa nje,
Mwandosya nje,
upande wa manaibu..
Buriani nje,
Masha nje,
Mathayo nje,
Nsanzugwako,
 
jamani hizi habari ninazowapa sasa ni za kweli na kama hamniamini tutaona jk atakapopangua baraza,NIMAPATA HABARI ZA KUAMINIKA KUTOKA KATIKA CHANZO CHA KUAMINIKA KUWA ANALIPUNGUZA BARAZA HILO
 
Sawa kwa mbali ninaweza kuamini habari hii ya hawa watu wa gazeti la raia mwema,huenda kweli mawaziri kumi wakaondoka na manaibu watano wakaondoka sasa swali ni wakina nani wanaotwaja kuingia humo ndani?
 
Ninadhani hawa wanaweza wakaingizwa ndani

1 jenista mhagama
2 lucas selelii
3 thomas apson mwangonda
4 peter serukamba
5 ponsiani nyami
6 aggrey mwanri
7 rostam azizi
8 william lukuvi
9 ruth msafiri
kwa nini nimewataja hawa? tukianza na ruth msafiri,kuna tetesi kuwa karamagi huenda akapigwa benchi so kwa mkoa wa kagera mtu ambaye anaweza akapewa nafasi ya kuingia ndani ni huyu mama.TUKUMBUKE JK ALIJITAHIDI SANA KUTOA ATLEAST KILA MKOA MAWAZIRI/NAIBU WAWILI.

2 THOMAS APSON inasemekana kati ya mwandosya hao mwakyusa kuna mmoja atatoka na tu wa kupewa nafasi kwa mkoa huo ni huyu bwana mdogo

3 ROSTAM AZIZ huyu inasemekana atapewa nafasi yoyote ile kutokana na kapuya kuondoka

4 WILLIAM LIKUVI huyu inasemekana atapokezana na mungai namkuu wa mkoa wa dodoma atateuliwa mwengine

PETER SERUKAMBA huyu inasemekana huwenda akachukua kwa mkoa wa kigoma mana nsanzugwanko inasemekana ataondolewa na mbunge anayeonekana kuwepo na nguvu bada ya kutoka nsanzugwako kwa mkoa huo ni huyu bwana
 
Endapo Mwakyembe atawekwa baraza la Mawaziri itabidi ajiengue kwenye hizo Kamati...

Sidhani na siamini kama Mwakyembe atakuwa waziri; huyu bwana si mwana-mtandao; kama ni uwaziri basi mkuu wa mkoa wa Mbeya, Mwakipesile anaweza kuteuliwa kuwa mbunge na kupewa huo uwaziri. Ngoja tusubiri tuone.
 
Hawa raia mwema hii habari wameitoa JF. Rudieni ujumbe wa Mwana siasa unafanana sana na kilichoandikwa hapa.

Si ajabu hawa nao hawana za jikoni, na badala yake jiko lao ni JF
 
ila pia nina wasiwasi kuwa mwakyembe ataingizwa ndani,ni kutokanan na majukumu mengi aliyonayo,endaapo angekuwa hana jukumu lolote ningeweza kupata imani kwa mbali kuwa ataingia
 
wape vidonge vyao hoa raiamwema.mimi napendekeza wafuatao.
1,yusufu makamba
2,poul bomani
3,salim a salim
4,rashid m kawawa
5,daud mwakawago
6,poul kimiti
7,shibuda nangale
8,thomas ngawaiya
9,tambwe hiza
10,seif s hamadi
 
......TUKUMBUKE JK ALIJITAHIDI SANA KUTOA ATLEAST KILA MKOA MAWAZIRI/NAIBU WAWILI.

....

PETER SERUKAMBA huyu inasemekana huwenda akachukua kwa mkoa wa kigoma mana nsanzugwanko inasemekana ataondolewa na mbunge anayeonekana kuwepo na nguvu bada ya kutoka nsanzugwako kwa mkoa huo ni huyu bwana

Mwanasiasa,

asante kwa info ila samahani sana kama nitashangaa sana hiyo sababu iliyowekwa hapo.

Yaani JK ana lundo la mawaziri kwa sababu anataka kila mkoa uwe na waziri na manaibu waziri? What happened kwa Nchi yetu ni moja na haina ukabila na udini?

Yaani kama kila nchi ingekuwa na formula ya Kikwete basi kuna nchi zingekuwa na mawaziri alfu mbili au tatu hivi!

Na hiyo ya chini kuwa somebody apewe uwaziri sio kwa sababu ya utendaji wake bali kwa sababu anatoka Kigoma?

Hii nchi kama kweli mambo ni haya, basi safari ni ndefu sana!
 
PETER SERUKAMBA huyu inasemekana huwenda akachukua kwa mkoa wa kigoma mana nsanzugwanko inasemekana ataondolewa na mbunge anayeonekana kuwepo na nguvu bada ya kutoka nsanzugwako kwa mkoa huo ni huyu bwana

Kama hizi ndiyo sababu za kuwapa watu uwaziri basi any fool can be a Minister in TZ gov.
 
Pole sana ndugu Mtanzania maana najua kwa kuwazia na kumtaja Mwandosya kuondolewa uwaziri imekuwa moto kama vile watu wakimtaja Mzee Malecela na hapo utamsikia jamaa fulani hapa anaibuka kwa kasi zote .Thomas alikuwa apewe uwaziri tangia mwanzo na alipokosa kule kwenye kura za maoni bado aliteuliwa. He played a big role kwenye kugombea kwa Kikwete . Kumbuka Baba yake alikuwa Mkuu pale jikoni na alitoa siri moja nzito ikamsaidia JK kuwapiga chini akina JM na wengineo .
 
sasa mkubwa tz devil tukiangalia vizuri unapomkandia huyu bwana mdogo kwa mkoa wa kigoma,mkoa wa kigoma kuna mawaziri wawili,huyu nzanzugwanko na chizze,inasemekana kuwa huyu nzanzugwanko anaweza akaondolewa,so kwa mkoa huo anabakia peter serukamba, mpologomyi , msambya , na kijiko.
msambya tukumbuke alishakuwaga naibu enzi za mkapa kisha akavurunda akatolewa bada ya kuonyesha udhaifu wake katika utendaji

kijiko, huyu ndo hata kueleweka haeleweki,mana hata kumsikia hatumsikii .shortly yupo kama hayupo

mpologomi huyu kama tujuavyo aliboronga akiwa naibu waziri wa fedha enzi za kina mbilinyi na kumfanya apoteze cr

so nadhani aliyebaki kwa mkoa huo ni serukamba na chizze ambaye hivi sasa yumo ndani ya cabinet ya sasa
 
Pole sana ndugu Mtanzania maana najua kwa kuwazia na kumtaja Mwandosya kuondolewa uwaziri imekuwa moto kama vile watu wakimtaja Mzee Malecela na hapo utamsikia jamaa fulani hapa anaibuka kwa kasi zote .Thomas alikuwa apewe uwaziri tangia mwanzo na alipokosa kule kwenye kura za maoni bado aliteuliwa. He played a big role kwenye kugombea kwa Kikwete . Kumbuka Baba yake alikuwa Mkuu pale jikoni na alitoa siri moja nzito ikamsaidia JK kuwapiga chini akina JM na wengineo .

Kwi kwi kwi!!!! labda na mimi ni ...... JF bwana ina mambo, yaani kumtetea Prof. hapo juzi tayari imeshakuwa nongwa?
 
Alichoandika Mwana Siasa, kinakaribiana sana na walichoandika raia mwema, Soma alichoandika Mwana siasa:

Wana jf nimepata fununu kutoka kwenye vyombo vyangu vya habari nimepata tetesi kuwa huenda mabadiliko ya cabinet yakawa jumatano ya wiki ianzayo kesho,kisha nikaendelea kudadisi nikaja kupata tetesi kuwa mabadiliko hayo yatawakumba wengi ikiwemo mawaziri waandamizi,na katika kutafuta habari hapa na pale nikaja kupata TETESI akuwa huenda hawa wafuatao wanaweza kupumzika kwa sasa,(kumbuka ni tetesi);
1-Capt john chiligati-ni kwa sababu ana majukumu mengine makubwa ndani ya chama so itakuwa vigumu kufanya mambo mengi kwa mpigo
2-joseph mungai
3-prof juma kapuya
4-magufuli
5-dr Nchimbi
6-masha
7-dr mathayo
8 ngeleja
9-hawa ghasia
10-prof mwandosya
11-prof mssola
12-mramba

pia katika pita pita yangu ya hapa nakule nimeweza kupata tetesi kuwa wafiatao HUENDA wakawa ndani,
1-aggrey mwanri
2-jaka mwambi
3-harrison mwakyembe
4-makamba(inasemekana kwa yeye kupitishwa tena ukatibu ilikuwa si pendekezo na pia habari ya kutolewa ukatibu ilikuwa imezagaa mno) la wakubwa,so kitakachotokea huenda akaachia ngazi ya ukatibu ili nae aingie barazani
5-rostam azizi
6-na pia katika nafasi ya mpendwa wetu marehemu salome mbatia(rip)inasemekana nafasi yake inaweza ikachukuliwa na wafuatao;
tatu ntimizi
frolence kyendesya
mama shelukindo
jenista mhagama

hizi ndo tetesi nilizoweza kupata,kama kuna mwengine ana lolote basi jamvi liko wazi
 
Bado napinga kwa wabunge kuwa mawaziri, hiyo iliwezekana kipindi cha chama kushika hatamu ila sasa inabidi kuwepo na uwiano na uwajibikaji kisiasa maana maamuzi mengi ya kukatisha tamaa yametokana na kukosa haiba ya kiuwajibikaji.

Akilipunguza baraza itakuwa mchicha sana lakini asirudishe watuhumiwa wa ufisadi, sijui kaka yangu cgenge kama atacgenga tena safari hii. Akimrudisha Karamagi ahesabu maumivu 2010
 
3-prof juma kapuya
5-dr Nchimbi
7-dr mathayo
10-prof mwandosya
11-prof mssola

Hawa Madaktari na Maprofessor nilitegemea wawe vinara kweli kweli sasa inaonekana wameover-perform au nini?

JK anataka kutwambia tuchunguze vyeti vyao au nini kinaendelea hapa.

Anyway amefungua vyuo vingi Tanzania, Dodoma University, MUCHs University, Mzumbe University, SUA nk wataweza kujipatia ajira bila matatizo.

Hila kuna mtu mmoja sina uhakika kama atakubaliwa.
 
Back
Top Bottom