Msongoru
JF-Expert Member
- Apr 16, 2008
- 306
- 24
TUKIO la mawaziri wawili ambao ni Stephen Wassira, Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, na Ezekiel Maige, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii kuungana na wadau mbalimbali kupinga muswada wa madini limepokelewa kwa hisia tofauti.
Tunasema kwamba hatua ya mawaziri hawa kuukataa muswada huo ni katika hali isiyo kawaida kwa kuwa tunaamini muswada wa sheria ya madini tayari ulikwishajadiliwa na Baraza la Mawaziri na kwamba kile kilichomo ndani ndicho walikubaliana.
Kwa upande mwingine, tunaona hatua ya mawaziri hao kuupinga kasoro zilizoko kwenye muswada huo hadharani ni hatua muhimu katika kukuza demokrasia ambapo kila mtu anakuwa huru kutoa maoni kwa mujibu wa sheria.
Kwa mantiki hiyo tunaweza kusema ukomavu wa demokrasia nchini umefikia hatua ya mawaziri kuweka kando ule utaratibu wao wa uwajibikaji wa pamoja na kutetea maslahi ya Watanzania. Kwa hatua hiyo tunaweza kuwapongeza.
Kutokana na mawaziri hawa na wadau wengine wa sekta ya madini kugundua katika muswada wa sheria ya madini kuna kasoro, ni vema wabunge ambao ndio wana jukumu la kuichambua na kisha kuipitisha sheria hiyo wakawa waangalifu kwa maslahi ya Watanzania wote.
Tunasema hivyo kwa sababu hoja nyingine ambazo zimejadiliwa katika mkutano wa wadau wa madini na Waziri mwenye dhamana, William Ngeleja zinadai kuwa muswada huo umejaa mapungufu makubwa na unalenga kunufaisha wachimbaji wakubwa na kuacha wadogo wakitaabika.
Ndio maana nasi wa Mwananchi tunaungana na wadau ambao walishauri muswada huo ufanyiwe marekebisho kabla ya kuwasilishwa bungeni kwa mjadala ili ulenge kumsaidia mchimbaji mdogo.
Tunatambua umuhimu wa muswada huu, lakini vilevile tusingependa upitishwe alafu kasoro hizi zije kuleta dosari siku zijazo
Mwananchi.
Tunasema kwamba hatua ya mawaziri hawa kuukataa muswada huo ni katika hali isiyo kawaida kwa kuwa tunaamini muswada wa sheria ya madini tayari ulikwishajadiliwa na Baraza la Mawaziri na kwamba kile kilichomo ndani ndicho walikubaliana.
Kwa upande mwingine, tunaona hatua ya mawaziri hao kuupinga kasoro zilizoko kwenye muswada huo hadharani ni hatua muhimu katika kukuza demokrasia ambapo kila mtu anakuwa huru kutoa maoni kwa mujibu wa sheria.
Kwa mantiki hiyo tunaweza kusema ukomavu wa demokrasia nchini umefikia hatua ya mawaziri kuweka kando ule utaratibu wao wa uwajibikaji wa pamoja na kutetea maslahi ya Watanzania. Kwa hatua hiyo tunaweza kuwapongeza.
Kutokana na mawaziri hawa na wadau wengine wa sekta ya madini kugundua katika muswada wa sheria ya madini kuna kasoro, ni vema wabunge ambao ndio wana jukumu la kuichambua na kisha kuipitisha sheria hiyo wakawa waangalifu kwa maslahi ya Watanzania wote.
Tunasema hivyo kwa sababu hoja nyingine ambazo zimejadiliwa katika mkutano wa wadau wa madini na Waziri mwenye dhamana, William Ngeleja zinadai kuwa muswada huo umejaa mapungufu makubwa na unalenga kunufaisha wachimbaji wakubwa na kuacha wadogo wakitaabika.
Ndio maana nasi wa Mwananchi tunaungana na wadau ambao walishauri muswada huo ufanyiwe marekebisho kabla ya kuwasilishwa bungeni kwa mjadala ili ulenge kumsaidia mchimbaji mdogo.
Tunatambua umuhimu wa muswada huu, lakini vilevile tusingependa upitishwe alafu kasoro hizi zije kuleta dosari siku zijazo
Mwananchi.