Mawaziri 30, manaibu waziri 25, makatibu wakuu 26, Naibu Katibu wakuu 26 ni mzigo mkubwa kwa nchi

Mkurabitambo

JF-Expert Member
Feb 3, 2010
230
57
KAMATI ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala, imesema Baraza la Mawaziri lililoundwa na Rais Jakaya Kikwete ni kubwa linalohitaji kupunguzwa ili kupunguza gharama za uendeshaji wa Serikali.Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Paul Lwanji alisema jana Bungeni kuwa Baraza hilo linapaswa kupunguzwa kwa kuunganisha baadhi ya wizara na idara zinazoshabihiana bila kuathiri utendaji wa shughuli za Serikali.

Akiwasilisha taarifa ya kamati hiyo kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Ofisi ya Rais kwa mwaka wa fedha uliopita na maoni kuhusu makadirio ya matumizi ya mwaka 2012/2013, Lwanji alisema idadi ya mawaziri, manaibu waziri, makatibu wakuu na manaibu wao ni mzigo mkubwa kwa walipa kodi.

Alisema umefika wakati kwa Serikali kukubaliana na ushauri wa wadau mbalimbali na kupunguza Baraza la Mawaziri pamoja na idara zisizo na umuhimu ili kuendana na pato la Taifa.

“Idadi ya mawaziri 30, manaibu waziri 25, makatibu wakuu 26, Naibu Katibu wakuu 26 ni mzigo mkubwa kwa nchi inayoendelea kama yetu. Kamati inashauri kwamba Serikali iangalie uwezekano kupunguzwa kwa kuunganisha baadhi ya Wizara na idara zinazoshabihiana bila kuathiri utendaji wa Serikali,” alisema Lwanji ambaye pia ni Mbunge wa Manyoni Mashariki.

Kamati hiyo ilipendekeza mabadiliko ya mfumo wa kuwateua watumishi wa ngazi za juu serikalini kutokana na wengi kuonekana kutokidhi vigezo vya uongozi.

Alisema umefika wakati wa kuwekwa utaratibu na uwezo wa mtu kumudu majukumu yake na uwezo wa kiakili (IQ), sifa na uzoefu.
 
Back
Top Bottom