Mawakili Medium Mwale na Loom Ojare ni majambazi?

Kithuku

JF-Expert Member
Nov 19, 2006
1,395
208
Wanabodi,

Naomba tujadili hii mada. Mawakili mabwana Medium Mwale na Loom Ojare ni maarufu sana mjini Arusha hasa katika kutetea majambazi mahakamani, tena wana ujasiri wa kutosha sana wa kuwatetea majambazi wanaokamatwa kwenye tukio. Hawa ndio waliosimamia rufaa ya Bw Nyari hadi akafutiwa hukumu ya kifungo cha miaka 30 jela kufuatia kupatikana na hatia ya ujambazi wa kutumia silaha.

Hawa hawa Ojare na Mwale ndio wanaowatetea wale majambazi wawili waliopambana na polisi kwa masaa 6 katika nyumba ya Bw Chonjo kule Njiro walikokuwa wamejificha baada ya kupora na kuua kwenye benki ya NMB Mwanga. Hawa pia wamewatetea majambazi waliopora sh bil 4 NBC Moshi mwaka 2004. Na katika tukio moja mtuhumiwa mmoja wa ujambazi sugu aliyekuwa anatafutwa na polisi aliwahi kukamatwa akiwa nyumbani kwa mmoja wa mawakili hawa, wakili alipobanwa na polisi akadai ni mpangaji wake.

Na zipo kesi nyingine nyingi tu za watuhumiwa wa ujambazi wa kutumia silaha katika mahakama kuu kanda ya Moshi na katika mahakama za hakimu Mkazi Moshi na Arusha ambazo mawakili hawa wanasimamia. Ukisikia kuna tukio la ujambazi wa kutumia silaha na majambazi wamekamatwa Moshi au Arusha, kama ni majambazi sugu wale wanaofahamika hata na wenyeji, fuatilia utasikia pia kuwa mawakili wao ni Loom Ojare na Medium Mwale.

Ukisikia benki imevamiwa Moshi na kuporwa mabilioni, fuatilia nani wakili wa watuhumiwa mara wakamatwapo; Loom Ojare na Medium Mwale. Sijui kama wana kesi nyingine za wasiotuhumiwa ujambazi. Je kuna uhusiano wowote (zaidi ya umahiri katika sheria) kati ya mawakili hawa na majambazi wauaji? Je hawa jamaa nao pia ni majambazi au washirika wao?

Hebu naomba tujadili hii mada maana kuna watu wameshaanza kupoteza imani si tu na mawakili hawa, bali pia na mfumo wetu wa sheria kwa ujumla. Naelewa katika nchi zilizoendelea kuna mawakili ambao wamejikita katika aina fulani za kesi na kuwa mahiri na wa kutumainiwa kwa mfano katika kesi za murder, fraud, divorce, blasphemy, n.k, ambapo yeyote mwenye kesi ya namna hiyo huwafuata mawakili hao. Je ni hivyo kwa hawa Mwale na Ojare au kuna zaidi?

Nafahamu pia huu usemi: "A bright lawyer knows the law (might be LL.B Hons first class) but a smart lawyer knows the judge" (might have passed his law degree very poorly and by sheer luck, but wins cases by all means!) Hawa jamaa wako upande upi hapa?

Naomba tujadili, mwenye ushahidi wowote hata wa kimazingira atuwekee hapa. Asanteni.
 
Inawezekana wanamegewa kidogo na hayo majambazi, ila siwalaumu sana mbona mkono naye anatetea mafisadi? Hivi sheria inaruhusu kumtetea mtu yeyote hata kama jamaa anarekodi ya ujambazi? Hawa wanasheria watajibu nini kwa Mungu siku ya hukumu?
 
Nadhani katika sheria zetu kila mtuhumiwa ana haki ya kupata uwakilishi wa kisheria kama anakabiliwa na kesi, kwa mantiki hiyo basi hata wanaotuhumiwa ujambazi au ufisadi wana haki hiyo.

Hao mawakili uliowataja pengine wana rekodi nzuri ya kushinda kesi za ujambazi kwa kusambaratisha hoja na madai ya mwendesha mashtaka, hivyo wengi wanaotuhumiwa ujambazi wanapenda kuwatumia kwani wanaona watakuwa na nafasi kubwa zaidi ya kushinda kesi zinazowakabili.
 
Hao mawakili Medium Mwale na Loom Ojare wanajua sana sheria ndo maana hukimbilia kesi za majambazi ili wapate mshiko wa juu, kwa kutetea hao majambazi basi nao wanaingia kwenye ujambazi. Nafikiri kabla majambazi hayajafanyizia bank ama popote huwasiliana na hao jamaa kuona kama kuna kipengere cha sheria kitawalinda iwapo bad get into worst....Kesi ya Nyani mpe ngedere lazima ashinde!!
 
Ni kweli kuwa kila mtuhumiwa ana haki ya kupatiwa uwakilishi kisheria na ndivyo ilivyo kwani hata wale wanaoshitakiwa na serikali kwa kesi za mauaji ambao huwa hawana uwezo wa kuhire wakili hupewa msaada wa bure wa sheria na serikali. Hii hufanyika kwa mawakili kupewa kesi hizo (wao huziita dock briefs).

Lakini linapokuja suala kama hili la kina Ojare hapo ndipo kitu kinachoitwa conscience na/au msimamo binafsi wa kila wakili hujulikana. Kwa mfano Dr. Mvungi yeye alishakataa kabisa kutetea watu wanaotetewa na kina Ojare kwa misingi kwamba dhamira yake itakuwa na conflict. Kwa maana nyingine mtu mwenye dhamira SAFI hawezi kutetea tu kila mtu eti tu kwa vile sheria haibagui!!!

Ndio maana kina Mkono walichukua kesi ya Ditopile "fasta" kwani kwake yeye falsafa yake ni "The End Justifies the Means", ndo sababu mpaka kwenye orodha ya mafisadi yumo. So kwa kina Ojare na mwenzake you knever know ...the world is full of surprises, but time will tell...
 
...i think its unnecessary to doubt or questions hawa wanasheria just kwa sababu wanatetea majambazi,ni kazi yao na sheria inaruhusu na hakuna ubaya wowote na kama kuna foul yeyote wanacheza mwenye kesi apeleke mbele
 
Mtu Aliyekamatwa Live Kwenye Tukio, Tena Akirushiana Risasi Na Polisi, Kwa Nia Ya Kutaka Kuwaua.

Je ingekuwa wewe ni Wakili na ambaye umethibitishiwa hayo, ungeweza kumtetea simply ana haki hiyo kisheria? Hawa jamaa lazima wawe na ubia na hao majambazi, In One Way Or Another. After All Lazima Ueleze Mambo Openly Ili Wakili Aweze Kukusaidia.

Hivyo Hawa Mawakili Huwa Wanaelezwa Kabisa Na Haya Majambazi Kila Kitu, Halafu Ndiyo Wanachukua Hizo Facts And Figures Kwa Ajili Ya Kwenda Kuzitetea Mahakamani. Yaani Hata Ile Collaboration Yao, Kwa Maana Ya Kuwatetea Majambazi, Kunawaqualify 100% Kuwa Ni Majambazi. Hivi Kweli Tutafika?
 
Mtu Aliyekamatwa Live Kwenye Tukio, Tena Akirushiana Risasi Na Polisi, Kwa Nia Ya Kutaka Kuwaua.

Je ingekuwa wewe ni Wakili na ambaye umethibitishiwa hayo, ungeweza kumtetea simply ana haki hiyo kisheria? Hawa jamaa lazima wawe na ubia na hao majambazi, In One Way Or Another. After All Lazima Ueleze Mambo Openly Ili Wakili Aweze Kukusaidia.

Hivyo Hawa Mawakili Huwa Wanaelezwa Kabisa Na Haya Majambazi Kila Kitu, Halafu Ndiyo Wanachukua Hizo Facts And Figures Kwa Ajili Ya Kwenda Kuzitetea Mahakamani. Yaani Hata Ile Collaboration Yao, Kwa Maana Ya Kuwatetea Majambazi, Kunawaqualify 100% Kuwa Ni Majambazi. Hivi Kweli Tutafika?

....well,may be hujui jinsi sheria zinavyofanya kazi...i dont mean to degrade your opinions in any way lakini hapo mzee unaonekana you need some basics kuhusu rights of defendants & advocates
 
Bw. Koba,

Nadhan issue hapa ilikuwa ni kwa wana JF kujaribu ku-establish kama hawa jamaa ni majambazi au la, na si kujaribu kuangalia haki yao kisheria, ...nadhani sheria pia naijua kidoooogo, japo si taaluma yangu.

Mfano: Ukinikopesha hela tukiwa wawili kwa makubaliano ya mdomoni perce, nikikataa kukurudishia, the chances kwamba utanishinda kisheria is almost 0%, ila kidhamira ni 100% wewe ni mshindi.

HAPA TUNAJARIBU KUANGALIA DHAMIRA YA HAWA WATU ZAIDI KULIKO HAKI YAO KISHERIA,... eeh wajameni!
 
Utalii ni biashara ambayo haiwezi kwisha leo wala kesho kama vitega uchumi vingine mfano madini. Serikali inatakiwa kuchukua hatua za makusudi kabisa kuhakikisha usalama wa raia katika kanda hii unatiliwa mkazo na kuweka mikakati ya maana kuona kwamba wale wote wanaoingia na kutaka kuvuruga amani wanachukuliwa hatua mara moja kwa speed kali na kuweza kulinda wageni wanaokuja kutembelea vivutio vyetu.

Kwa sababu hivi sasa Air Tanzania ndiyo imeanza ingawa hii iko kwenye issue ingine ni wajibu wa serikali kuona kwamba njia za usafiri za moja kwa moja kwenda USA zinafanyiwa kazi.

Kuhusu Kampuni kuwa ya majambazi hilo linawezekana lakini kuna Msajili wa makampuni ambapo kama kazi inafanyika vizuri sioni kama wanaweza kupata mwanya.
 
Hili suala nilishawahi kujiuliza sana hapo awali pia.

I know them two lawyers very well. Kuhusu dhamira ya mtu binafsi......................Yes yawezekana mtu kuwa na msimamo kuwa dhamira yangu sitatetea kesi za uhalifu kama ujambazi............fine, kwa upande mwingine Ojare na Mwale kutetea majambazi hakuwafanyi wao kuwa ni majambazi unless they are proven so beyond reasonable doubt......

Tatizo kubwa liko kwa WAENDESHA MASHTAKA WETU..............mfano mzuri hebu angalia kesi ya Braza Ditto jinsi inavyoendeshwa

Wakati ule watoza ushuru walionekana kuwa ni watu wabaya sana, lakinini ukweli ni kuwa walikuwa wakifanya kazi yao effectively. Sikinde waliimba wimbo wa TAXI driver. Nafikri na kwa wanasheria ni hvyo hivyo. Nina uhakika wanazo kesi zingine za kawaida kabisa...........................the difference is hazina publicity kama kesi za ujambazi
 
Wana JF,

Tunaishiwa jamani, sheria inasema everybody is innocent until proven guilty in the court of LAW.

Hata kama umerusha risasi, inawezekana ulikuwa unajitetea, kani polisi nao si ni watu?

Hamkuona wale wananchi wema waliouwawa na ZOMBE? kama wangekuwa na bastola/bunduki wasingejitetea? kwahiyo wangejitetea wangeitwa majambazi na hakuna wakili ambaye angestahili kuwatetea!!!!!!!!!!!!!!!!!!!1

This is very low of US!
 
inawezekana wanamegewa kidogo na hayo majambazi. ila siwalaumu sana mbona Mkono naye anatetea mafisadi? hivi sheria inaruhusu kumtetea mtu yeyote hata kama jamaa anarekodi ya ujambazi? hawa wanasheria watajibu nini kwa Mungu siku ya hukumu?

Kwamba Ojare na Mwale wanapata kula yao kutokana na kesi za ujambazi haziwaingizi moja kwa moja katika ujambazi. 'They make a living from defending bandits', sawa, ndio kazi waliyochagua, ilimradi hawaunji sheria za nchi. Ikumbukwe kuwa hawa 'majambazi' ni watuhumiwa tu, hawajakutwa na hatia. Hali kadhalika, sheria inaruhusu mtuhuiwa wa ujambazi kutetewa, hata wa mauaji.

Kuhusu hawa watuhumiwa kukutwa eneo la tukio, kwa maana ya kwamba 'red-handed', haiwahalalishii wao kuwa majambazi hadi pale mahakama itakapoamua vinginevyo.

Kwa mantiki hiyo basi, niseme kuwa mawakili hawa huenda wameona kesi za ujambazi 'Zinalipa' kuliko za kugombania mashamba, kwa hiyo 'as businessmen' wanangalia faida, potelea mbali lawama kuwa watetea ujambazi.

Tuendelee kulumbana.
 
Wanabodi,

Naomba tujadili hii mada. Mawakili mabwana Medium Mwale na Loom Ojare ni maarufu sana mjini Arusha hasa katika kutetea majambazi mahakamani, tena wana ujasiri wa kutosha sana wa kuwatetea majambazi wanaokamatwa kwenye tukio. Hawa ndio waliosimamia rufaa ya Bw Nyari hadi akafutiwa hukumu ya kifungo cha miaka 30 jela kufuatia kupatikana na hatia ya ujambazi wa kutumia silaha.

Hawa hawa Ojare na Mwale ndio wanaowatetea wale majambazi wawili waliopambana na polisi kwa masaa 6 katika nyumba ya Bw Chonjo kule Njiro walikokuwa wamejificha baada ya kupora na kuua kwenye benki ya NMB Mwanga. Hawa pia wamewatetea majambazi waliopora sh bil 4 NBC Moshi mwaka 2004. Na katika tukio moja mtuhumiwa mmoja wa ujambazi sugu aliyekuwa anatafutwa na polisi aliwahi kukamatwa akiwa nyumbani kwa mmoja wa mawakili hawa, wakili alipobanwa na polisi akadai ni mpangaji wake.

Na zipo kesi nyingine nyingi tu za watuhumiwa wa ujambazi wa kutumia silaha katika mahakama kuu kanda ya Moshi na katika mahakama za hakimu Mkazi Moshi na Arusha ambazo mawakili hawa wanasimamia. Ukisikia kuna tukio la ujambazi wa kutumia silaha na majambazi wamekamatwa Moshi au Arusha, kama ni majambazi sugu wale wanaofahamika hata na wenyeji, fuatilia utasikia pia kuwa mawakili wao ni Loom Ojare na Medium Mwale.

Ukisikia benki imevamiwa Moshi na kuporwa mabilioni, fuatilia nani wakili wa watuhumiwa mara wakamatwapo; Loom Ojare na Medium Mwale. Sijui kama wana kesi nyingine za wasiotuhumiwa ujambazi. Je kuna uhusiano wowote (zaidi ya umahiri katika sheria) kati ya mawakili hawa na majambazi wauaji? Je hawa jamaa nao pia ni majambazi au washirika wao?

Hebu naomba tujadili hii mada maana kuna watu wameshaanza kupoteza imani si tu na mawakili hawa, bali pia na mfumo wetu wa sheria kwa ujumla. Naelewa katika nchi zilizoendelea kuna mawakili ambao wamejikita katika aina fulani za kesi na kuwa mahiri na wa kutumainiwa kwa mfano katika kesi za murder, fraud, divorce, blasphemy, n.k, ambapo yeyote mwenye kesi ya namna hiyo huwafuata mawakili hao. Je ni hivyo kwa hawa Mwale na Ojare au kuna zaidi?

Nafahamu pia huu usemi: "A bright lawyer knows the law (might be LL.B Hons first class) but a smart lawyer knows the judge" (might have passed his law degree very poorly and by sheer luck, but wins cases by all means!) Hawa jamaa wako upande upi hapa?

Naomba tujadili, mwenye ushahidi wowote hata wa kimazingira atuwekee hapa. Asanteni.

Not guilty until proven Innocent. Huu ndio muongozo. Sasa kama kuna mawakili wame-specialize katika kutetea kesi za ujambazi, that is their speciality. Nakumbumbuka Marehemu Johnie Cochran (if it doesnt fit, acquit) who successifuly defended OJ Simposon. Huyu bwana was the undisputed criminal 'trial' lawyer of his time, highly respected by his peers.. Almost 'wakubwa' wote waliokuwa wanakabiliwa na mashtaka ya mauaji walikuwa wanakimbilia kwake kwanza as a matter of 'first choice'.

Sheria zetu zinaruhusu 'watuhumiwa wa mauaji' kutetewa na mwanasheria regardless of concience. sheria za nchi haziongozwi na 'personal concience'. Sioni kama kuna haja ya kuwachunguza hawa mawakili, that will be a waste of time and energy.

uendeshaji wa kesi unategemea mambo mengi. kuna ushahidi, kuna namna ushahidi unavyotolewa, uendeshaji wa mashtaka, hakimu/jaji, halafu kuna utetezi. inawezekana kabisa kwamba kuna 'udhaifu' katika utekelezaji wa hizi taratibu, but definately kuwachunguza mawakili sounds like a witch hunt to me.
 
Wana JF,

Tunaishiwa jamani, sheria inasema everybody is innocent until proven guilty in the court of LAW.

Hata kama umerusha risasi, inawezekana ulikuwa unajitetea, kani polisi nao si ni watu?

Hamkuona wale wananchi wema waliouwawa na ZOMBE? kama wangekuwa na bastola/bunduki wasingejitetea? kwahiyo wangejitetea wangeitwa majambazi na hakuna wakili ambaye angestahili kuwatetea!!!!!!!!!!!!!!!!!!!1

This is very low of US!


Sasa wewe unatetea nini? Mbona unajichanganya? Unasema "Tunaishiwa jamani, sheria inasema everybody is innocent until proven guilty in the court of LAW" halafu unasema "Hamkuona wale wananchi wema waliouwawa na ZOMBE? kama wangekuwa na bastola/bunduki wasingejitetea?" Kwani imethibitika kuwa Zombe ndio kawaua?
 
yawezekana nao wapo na gang ya majambazi yawatumia meaning wakubwa so wanajua kila kesi ikianza wanawasiliana na ma lawyer wao kama jinsi family flani inavyoweza sema ngoja wawasiliane na lawyer wa...ila yawezekana ni katika kutafuta mkate wa kila siku..ndio maana mwaambiwa ma lawyer mlango wa mbinguni kwao utakua mdogo saaana
 
Wanabodi,

Naomba tujadili hii mada. Mawakili mabwana Medium Mwale na Loom Ojare ni maarufu sana mjini Arusha hasa katika kutetea majambazi mahakamani, tena wana ujasiri wa kutosha sana wa kuwatetea majambazi wanaokamatwa kwenye tukio. Hawa ndio waliosimamia rufaa ya Bw Nyari hadi akafutiwa hukumu ya kifungo cha miaka 30 jela kufuatia kupatikana na hatia ya ujambazi wa kutumia silaha.

Hawa hawa Ojare na Mwale ndio wanaowatetea wale majambazi wawili waliopambana na polisi kwa masaa 6 katika nyumba ya Bw Chonjo kule Njiro walikokuwa wamejificha baada ya kupora na kuua kwenye benki ya NMB Mwanga. Hawa pia wamewatetea majambazi waliopora sh bil 4 NBC Moshi mwaka 2004. Na katika tukio moja mtuhumiwa mmoja wa ujambazi sugu aliyekuwa anatafutwa na polisi aliwahi kukamatwa akiwa nyumbani kwa mmoja wa mawakili hawa, wakili alipobanwa na polisi akadai ni mpangaji wake.

Na zipo kesi nyingine nyingi tu za watuhumiwa wa ujambazi wa kutumia silaha katika mahakama kuu kanda ya Moshi na katika mahakama za hakimu Mkazi Moshi na Arusha ambazo mawakili hawa wanasimamia. Ukisikia kuna tukio la ujambazi wa kutumia silaha na majambazi wamekamatwa Moshi au Arusha, kama ni majambazi sugu wale wanaofahamika hata na wenyeji, fuatilia utasikia pia kuwa mawakili wao ni Loom Ojare na Medium Mwale.

Ukisikia benki imevamiwa Moshi na kuporwa mabilioni, fuatilia nani wakili wa watuhumiwa mara wakamatwapo; Loom Ojare na Medium Mwale. Sijui kama wana kesi nyingine za wasiotuhumiwa ujambazi. Je kuna uhusiano wowote (zaidi ya umahiri katika sheria) kati ya mawakili hawa na majambazi wauaji? Je hawa jamaa nao pia ni majambazi au washirika wao?

Hebu naomba tujadili hii mada maana kuna watu wameshaanza kupoteza imani si tu na mawakili hawa, bali pia na mfumo wetu wa sheria kwa ujumla. Naelewa katika nchi zilizoendelea kuna mawakili ambao wamejikita katika aina fulani za kesi na kuwa mahiri na wa kutumainiwa kwa mfano katika kesi za murder, fraud, divorce, blasphemy, n.k, ambapo yeyote mwenye kesi ya namna hiyo huwafuata mawakili hao. Je ni hivyo kwa hawa Mwale na Ojare au kuna zaidi?

Nafahamu pia huu usemi: "A bright lawyer knows the law (might be LL.B Hons first class) but a smart lawyer knows the judge" (might have passed his law degree very poorly and by sheer luck, but wins cases by all means!) Hawa jamaa wako upande upi hapa?

Naomba tujadili, mwenye ushahidi wowote hata wa kimazingira atuwekee hapa. Asanteni.
Kwenye mada ile ya Jeuri ya Mkapa uliandika haya:
... Mzee Mkapa kula pini hivyo hivyo, ulishastaafu, achana na malumbano yasiyo na msingi. Tulia, ule pensheni yako. Mwenye wivu ajinyonge, na yule mwenye suala la msingi la kulalamikiwa aende mahakamani au kwenye vyombo vingine stahili. Watu mnakalia majungu tu. Ovyoo!

Unawambia watu wamekalia majungu wakati wewe ndio inaonekana ndiye hasa mtaalamu wa kuyatengeneza. Kama ulivyoshauri kwenye ile thread nyingine; kama una suala la msingi la kulalamika nenda mahakamani au kwenye vyombo vingine stahili vinginevyo haya ndiyo majungu classic
 
Kwenye mada ile ya Jeuri ya Mkapa uliandika haya:


Unawambia watu wamekalia majungu wakati wewe ndio inaonekana ndiye hasa mtaalamu wa kuyatengeneza. Kama ulivyoshauri kwenye ile thread nyingine; kama una suala la msingi la kulalamika nenda mahakamani au kwenye vyombo vingine stahili vinginevyo haya ndiyo majungu classic

Eh! yamekuwa hayo tena? Siku ukivamiwa na majambazi utatamani usingeandika hivi hapa. Ni wabaya hao watu, na wanakuathiri mtu binafsi moja kwa moja. Hailinganishiki hata kidogo na suala la Chez Nkapa kula pensheni yake.
 
14 Reactions
Reply
Back
Top Bottom