Mawakili Medium Mwale na Loom Ojare ni majambazi?

Wanafanya kazi zao vizuri,unaweza ukawa refa mzuri wa mpira wa miguu lakini ukawa hujawahi kucheza mpira
 
Mtu Aliyekamatwa Live Kwenye Tukio, Tena Akirushiana Risasi Na Polisi, Kwa Nia Ya Kutaka Kuwaua.

Je ingekuwa wewe ni Wakili na ambaye umethibitishiwa hayo, ungeweza kumtetea simply ana haki hiyo kisheria? Hawa jamaa lazima wawe na ubia na hao majambazi, In One Way Or Another. After All Lazima Ueleze Mambo Openly Ili Wakili Aweze Kukusaidia.

Hivyo Hawa Mawakili Huwa Wanaelezwa Kabisa Na Haya Majambazi Kila Kitu, Halafu Ndiyo Wanachukua Hizo Facts And Figures Kwa Ajili Ya Kwenda Kuzitetea Mahakamani. Yaani Hata Ile Collaboration Yao, Kwa Maana Ya Kuwatetea Majambazi, Kunawaqualify 100% Kuwa Ni Majambazi. Hivi Kweli Tutafika?

Mkuu wewe hujui chochote kuhusu sheria. I doubt your age na uelewa wa mambo haya pia. Ulishawahi ona wapi mtu kaua anafika mahakamani anasema kweli hakimu nimeua.? Mahakama goes with evidences na siyo kusema tu kauaa
 
Mleta Uzi nakushauri ukiwa na kesi au una ndugu yako ana kesi kawatafute hawa jamaa wawili. Hapa umetufumbua macho wengine tuanze kuwatumia hawa watu.

These guys are smart lawyer's.. Huo ujinga wa kusema eti na wao in majambazi unapotoka, kama ni majambazi wangeshakamatwa kitambo. Wanaitumia shule yao ya sheria ipasavyo.

Hongera sana kwao
 
Swali lako halina uhusiano na nilichokiandika! Possibly you qouted the wrong post!
Wewe ni dr? Unajua ethics za u dr? Fanya utafit japo kidogo juu ya nlichokiandika utanielewa tyuu.lakin nakusisitiza ufanye jitihada za kujua valies n ethics za kazi za mawakili .kisha uje uongee hapa
 
Mkuu wewe hujui chochote kuhusu sheria. I doubt your age na uelewa wa mambo haya pia. Ulishawahi ona wapi mtu kaua anafika mahakamani anasema kweli hakimu nimeua.? Mahakama goes with evidences na siyo kusema tu kauaa
Saidi Mwamwindi, ambaye alimtwanga risas Dr Kleruu mbona alifanya hivyo..!?
Zipo case nyingi tu za watu wanaofanya uhalifu na kufika mahakani kisha kueleza jinsi walivyofanya!
 
ndio hadi majambazi yakisakwa na polisi yakutwe nyumbani kwa wakili? yaani majambazi na wauaji wote basi wawe na mawakili wawili tu wanaowatetea? lazima kuwe na jambo na mahusiano ya karibu sio burebure.
Toka umehamia ACT naona hata akili yako imepukutika sasa ndio nini hiki unaandika??? Haitwi jambazi mpaka mahakama ihukumu hivyo kwahyo anapokamatwa kwa mwanasheria watasema amekutwa na MTUHUMIWA!!! na ndio maana ya sheria lazima ziwepo pande mbili na necessarily haimaanishi kwamba lazima atetewe ila huwa wanawapa wanasheria ili na wenyewe wapate haki ya kusikilizwa ili mwisho wa siku hukumu ikitolewa iwe FAIR. we siku ukisingiziwa umefanya ujambazi ndio utaelewa umuhim wa wanasheria kukutetea hata kama utaitwa jambazi sasa unaconclude mtu ni jambazi kisa katetea jambazi!!! Ulitaka sasa afungwe bila kusikilizwa alafu aseme ameonewa??
 
Hao mawakili Medium Mwale na Loom Ojare wanajua sana sheria ndo maana hukimbilia kesi za majambazi ili wapate mshiko wa juu, kwa kutetea hao majambazi basi nao wanaingia kwenye ujambazi. Nafikiri kabla majambazi hayajafanyizia bank ama popote huwasiliana na hao jamaa kuona kama kuna kipengere cha sheria kitawalinda iwapo bad get into worst....Kesi ya Nyani mpe ngedere lazima ashinde!!


Ulianza vizuri ila sijaelewa hapo uliposema mawasiliano kabla ya tuhuma , je na watuhumiwa wa uhalifu/maosa mengine km. mauaji, madai nk huwa wanawasliliana na mawakili wao kabla ya kutenda??
Je utasemaje kwa Daktari anayetibu majambazi ?
 
Toka umehamia ACT naona hata akili yako imepukutika sasa ndio nini hiki unaandika??? Haitwi jambazi mpaka mahakama ihukumu hivyo kwahyo anapokamatwa kwa mwanasheria watasema amekutwa na MTUHUMIWA!!! na ndio maana ya sheria lazima ziwepo pande mbili na necessarily haimaanishi kwamba lazima atetewe ila huwa wanawapa wanasheria ili na wenyewe wapate haki ya kusikilizwa ili mwisho wa siku hukumu ikitolewa iwe FAIR. we siku ukisingiziwa umefanya ujambazi ndio utaelewa umuhim wa wanasheria kukutetea hata kama utaitwa jambazi sasa unaconclude mtu ni jambazi kisa katetea jambazi!!! Ulitaka sasa afungwe bila kusikilizwa alafu aseme ameonewa??
tofautisha kati ya kukutwa nyumbani na ofisini kwa wakili, tatizo mkishakariri mnakuwa wapumbavu sana. taarifa haikusema alikutwa ofisini kwa wakili bali nyumbani. mahusiano ya mtu anayekutwa nyumbani kwako ni tofauti na aliyekutwa ofisini. ofisini wanakuja watu wote ila nyumbani ni watu ulio na mahusiano nao ya karibu pekee, jifunze kwa hilo.
 
Wanabodi,

Naomba tujadili hii mada. Mawakili mabwana Medium Mwale na Loom Ojare ni maarufu sana mjini Arusha hasa katika kutetea majambazi mahakamani, tena wana ujasiri wa kutosha sana wa kuwatetea majambazi wanaokamatwa kwenye tukio. Hawa ndio waliosimamia rufaa ya Bw Nyari hadi akafutiwa hukumu ya kifungo cha miaka 30 jela kufuatia kupatikana na hatia ya ujambazi wa kutumia silaha.

Hawa hawa Ojare na Mwale ndio wanaowatetea wale majambazi wawili waliopambana na polisi kwa masaa 6 katika nyumba ya Bw Chonjo kule Njiro walikokuwa wamejificha baada ya kupora na kuua kwenye benki ya NMB Mwanga. Hawa pia wamewatetea majambazi waliopora sh bil 4 NBC Moshi mwaka 2004. Na katika tukio moja mtuhumiwa mmoja wa ujambazi sugu aliyekuwa anatafutwa na polisi aliwahi kukamatwa akiwa nyumbani kwa mmoja wa mawakili hawa, wakili alipobanwa na polisi akadai ni mpangaji wake.

Na zipo kesi nyingine nyingi tu za watuhumiwa wa ujambazi wa kutumia silaha katika mahakama kuu kanda ya Moshi na katika mahakama za hakimu Mkazi Moshi na Arusha ambazo mawakili hawa wanasimamia. Ukisikia kuna tukio la ujambazi wa kutumia silaha na majambazi wamekamatwa Moshi au Arusha, kama ni majambazi sugu wale wanaofahamika hata na wenyeji, fuatilia utasikia pia kuwa mawakili wao ni Loom Ojare na Medium Mwale.

Ukisikia benki imevamiwa Moshi na kuporwa mabilioni, fuatilia nani wakili wa watuhumiwa mara wakamatwapo; Loom Ojare na Medium Mwale. Sijui kama wana kesi nyingine za wasiotuhumiwa ujambazi. Je kuna uhusiano wowote (zaidi ya umahiri katika sheria) kati ya mawakili hawa na majambazi wauaji? Je hawa jamaa nao pia ni majambazi au washirika wao?

Hebu naomba tujadili hii mada maana kuna watu wameshaanza kupoteza imani si tu na mawakili hawa, bali pia na mfumo wetu wa sheria kwa ujumla. Naelewa katika nchi zilizoendelea kuna mawakili ambao wamejikita katika aina fulani za kesi na kuwa mahiri na wa kutumainiwa kwa mfano katika kesi za murder, fraud, divorce, blasphemy, n.k, ambapo yeyote mwenye kesi ya namna hiyo huwafuata mawakili hao. Je ni hivyo kwa hawa Mwale na Ojare au kuna zaidi?

Nafahamu pia huu usemi: "A bright lawyer knows the law (might be LL.B Hons first class) but a smart lawyer knows the judge" (might have passed his law degree very poorly and by sheer luck, but wins cases by all means!) Hawa jamaa wako upande upi hapa?

Naomba tujadili, mwenye ushahidi wowote hata wa kimazingira atuwekee hapa. Asanteni.

Makubwa ! I pray that kina Chonjooh retires?
 
Nimekukumbusha ethics mkuu. Soma ethics za mawakili kama zinazuia jambazi kutetewa. Ndo mana nikauliza kisa jambazi akienda hospitali asitibiwe?
Hii post ni ya miaka 11 iliyopita, yaani ya mwaka 2007,..., why here today? Nini kimejiri?
 
tofautisha kati ya kukutwa nyumbani na ofisini kwa wakili, tatizo mkishakariri mnakuwa wapumbavu sana. taarifa haikusema alikutwa ofisini kwa wakili bali nyumbani. mahusiano ya mtu anayekutwa nyumbani kwako ni tofauti na aliyekutwa ofisini. ofisini wanakuja watu wote ila nyumbani ni watu ulio na mahusiano nao ya karibu pekee, jifunze kwa hilo.
Kwahiyo sheria inakataza mtuhumiwa kukutana na mwanasheria wake nje ya ofisi??? Kwahyo pale magufuli anapokutana na watu nyumbani kwake chato huwa hakutani nao kama Rais ila kama mwananchi wa kawaida kisa tu hayupo ofisini ikulu ??? Kazi kwelikweli

Huo ni utetezi wa ajabu sana kutoka kwa kijana msomi kama wewe maana hata nikikuuliza sheria gani inasema hivo huna jibu...... Pia pale anakuwa mtuhumiwa au anayehisiwa ila sio jambazi akisha kuwa declared ni jambazi of course hawezi kuwa uraiani unless katimiza kifungo sasa kwanini unaforce eti JAMBAZI kakutwa kwake?? Unaweza thibitisha nani ni jambazi kisheria kabla hajahukumiwa na mahakama ??

Naona toka uambulie kura 300 jimbo zima umeacha kureason kama deo wa mwaka 2013
 
Hao mawakili Medium Mwale na Loom Ojare wanajua sana sheria ndo maana hukimbilia kesi za majambazi ili wapate mshiko wa juu, kwa kutetea hao majambazi basi nao wanaingia kwenye ujambazi. Nafikiri kabla majambazi hayajafanyizia bank ama popote huwasiliana na hao jamaa kuona kama kuna kipengere cha sheria kitawalinda iwapo bad get into worst....Kesi ya Nyani mpe ngedere lazima ashinde!!
Teh teh nimependa kwenye maandishi mekundu
 
Kwahiyo sheria inakataza mtuhumiwa kukutana na mwanasheria wake nje ya ofisi??? Kwahyo pale magufuli anapokutana na watu nyumbani kwake chato huwa hakutani nao kama Rais ila kama mwananchi wa kawaida kisa tu hayupo ofisini ikulu ??? Kazi kwelikweli

Huo ni utetezi wa ajabu sana kutoka kwa kijana msomi kama wewe maana hata nikikuuliza sheria gani inasema hivo huna jibu...... Pia pale anakuwa mtuhumiwa au anayehisiwa ila sio jambazi akisha kuwa declared ni jambazi of course hawezi kuwa uraiani unless katimiza kifungo sasa kwanini unaforce eti JAMBAZI kakutwa kwake?? Unaweza thibitisha nani ni jambazi kisheria kabla hajahukumiwa na mahakama ??

Naona toka uambulie kura 300 jimbo zima umeacha kureason kama deo wa mwaka 2013
leo mwizi akiwa anatafutwa na polisi baada ya kufanya wizi sehemu na akakutwa kajificha kwako, huko unakuchukulia kama kukutana kwa kawaida? iko wazi lema anawatetea hawa maana walikuwa ni watetezi wa majambazi na lema mwenyewe akiwemo maana kazi yake inajulikana alikuwa jambazi, wewe tulia maana hujui lolote.
 
Wanabodi,

Naomba tujadili hii mada. Mawakili mabwana Medium Mwale na Loom Ojare ni maarufu sana mjini Arusha hasa katika kutetea majambazi mahakamani, tena wana ujasiri wa kutosha sana wa kuwatetea majambazi wanaokamatwa kwenye tukio. Hawa ndio waliosimamia rufaa ya Bw Nyari hadi akafutiwa hukumu ya kifungo cha miaka 30 jela kufuatia kupatikana na hatia ya ujambazi wa kutumia silaha.

Hawa hawa Ojare na Mwale ndio wanaowatetea wale majambazi wawili waliopambana na polisi kwa masaa 6 katika nyumba ya Bw Chonjo kule Njiro walikokuwa wamejificha baada ya kupora na kuua kwenye benki ya NMB Mwanga. Hawa pia wamewatetea majambazi waliopora sh bil 4 NBC Moshi mwaka 2004. Na katika tukio moja mtuhumiwa mmoja wa ujambazi sugu aliyekuwa anatafutwa na polisi aliwahi kukamatwa akiwa nyumbani kwa mmoja wa mawakili hawa, wakili alipobanwa na polisi akadai ni mpangaji wake.

Na zipo kesi nyingine nyingi tu za watuhumiwa wa ujambazi wa kutumia silaha katika mahakama kuu kanda ya Moshi na katika mahakama za hakimu Mkazi Moshi na Arusha ambazo mawakili hawa wanasimamia. Ukisikia kuna tukio la ujambazi wa kutumia silaha na majambazi wamekamatwa Moshi au Arusha, kama ni majambazi sugu wale wanaofahamika hata na wenyeji, fuatilia utasikia pia kuwa mawakili wao ni Loom Ojare na Medium Mwale.

Ukisikia benki imevamiwa Moshi na kuporwa mabilioni, fuatilia nani wakili wa watuhumiwa mara wakamatwapo; Loom Ojare na Medium Mwale. Sijui kama wana kesi nyingine za wasiotuhumiwa ujambazi. Je kuna uhusiano wowote (zaidi ya umahiri katika sheria) kati ya mawakili hawa na majambazi wauaji? Je hawa jamaa nao pia ni majambazi au washirika wao?

Hebu naomba tujadili hii mada maana kuna watu wameshaanza kupoteza imani si tu na mawakili hawa, bali pia na mfumo wetu wa sheria kwa ujumla. Naelewa katika nchi zilizoendelea kuna mawakili ambao wamejikita katika aina fulani za kesi na kuwa mahiri na wa kutumainiwa kwa mfano katika kesi za murder, fraud, divorce, blasphemy, n.k, ambapo yeyote mwenye kesi ya namna hiyo huwafuata mawakili hao. Je ni hivyo kwa hawa Mwale na Ojare au kuna zaidi?

Nafahamu pia huu usemi: "A bright lawyer knows the law (might be LL.B Hons first class) but a smart lawyer knows the judge" (might have passed his law degree very poorly and by sheer luck, but wins cases by all means!) Hawa jamaa wako upande upi hapa?

Naomba tujadili, mwenye ushahidi wowote hata wa kimazingira atuwekee hapa. Asanteni.
Katika moja ya maelezo ya wakili, aliwahi kusema eti hawatetei waharifu, bali huwatafutia haki yao. Lakini, mara zote mawakili hujisifu pale mteja wao anapoachiwa.

Wapo mawakili wengi ambao kazi zao ni kutetea watu wapuuzi wa aina hiyo. Kuna tatizo la moral sanity kwa watu hawa. wengine makuzi yao ni ya uharifu, leo hii akiwa wakili hataacha tabia hiyo. Immorality imemponza PLO pale Kenya sasa hivi hata zile mbwembwe zake za kiingereza zimekwisha. Huyu ana nafuu, anaona haya. wapo wale wasiokuwa na haya hata kidogo!!!
 
KUMBE HAWA MAWAKILI WALIO KUWA WATETEZI WA MAJAMBAZI NDIO LEMA ANAWATETEA WATOKE? KWELI ONCE JAMBAZI UNABAKI JAMBAZI MILELE. MTANDAO ULEULE.

Hivi hawa mawakili bado wapo gerezani kisongo?? Wakitoka hawata watetea tena majambazi...ila watu walikuwa wanawatilia shaka...
 
Back
Top Bottom