Mimi si mwanasheria lakini marafiki zangu wengi ni wanasheria na nimeshuhudia mijadala mingi ya wanasheria.
Lakini nilichogundua katika practice (siyo fani) ya wanasheria ni kwamba huwa inafika mahala wanaongea kuhusu tabia ya Jaji fulani, physichology ya Jaji fulani. Kwa maana hiyo ni kama vile unatakiwa kuwajua majaji.
Mfano mtu anasema Jaji fulani hapendi hiki wakati jaji mwingine hana tatizo na hicho anachokataa huyo mwenzake. Nilipogundua hivyo tatizo langu hapa likawa ni hili.
Kwa maana hiyo majadiliano mengi wanajadili hivi vitu. Yaani ukitaka kujua tabia za majaji, siyo katika mambo binafsi au vituko, bali katika uendeshaji wa kesi basi kaa na wanasheria.
Sasa hapa likaja tatizo sijui kama ni ujinga wangu kuhusu sheria au la. Kabla ya urafiki na wanasehria nilikuwa ninadhani kwamba kule University au Law School wanasheria walifundishwa sheria zinavyosema. Nikadhani ukijua provision (vifungu) vya sheria basi utatamba kifua mbele kwamba kesi inayoendana na vifungu hivyo utaishinda maadamu hata utaratibu wa kuifikisha (technicality) mahakamani umeufuata.
Hivyo, hata mjinga wa sheria kama mimi, ukijua vifungu vya jambo fulani na utaratibu wake basi una uhakika wa kushinda hiyo kesi. Na kwa kweli hivyo ndivyo ilitakiwa, tuvijue vifungu, tukiviheshimu hatushindwi kesi na anayetushitaki, tukivikiuka tunashinda kesi tunapowashitaki waliovikuka dhidii yetu.
Niliamini hivyo kwa sababu sheria zinatungwa kwa kwa ajili yetu wote na si kwa ajili ya mawakili au wanasheria ambao siyo lazima uwatumie kama huna hela au huwahitaji.
Na mazoea yangu na wanasheria nilidhani nitaokota mengi kuhusu vifungu kwani nilitarajia wanasheria wabishane vifungu kwamba kifungu hiki kinasema hivi na mwingine anabisha nasema kifungu kile kinasema hivi.
Kumbe sivyo! Ukikaa na wanasheria utasikia wanasema jaji huyu yuko hivi na yule yuko vile. Nilipogundua hilo nikasema hebu nililete humu mitandaoni na ikibidi humu JF.
Kama wanachokifanya wanasheria hawa ni kweli huko mahakamani basi nchi yetu iko katika hatari kubwa na mhimili huu wa mahakama. Tunadhani vifungu vya sheria ulivyosoma chuoni au hata sisi mtaani vinatosha kumbe unatakiwa kumsoma na Jaji jambo ambalo mwanasheria hakulisoma chuoni!
Kama mimi ndiye ninakosea kudhani hivi, basi ninatakiwa nirekebishwe lakini hili nimeliona mara nyingi na ninaiona hatari hii. Wengi wengi tu hufungua kesi zao hawana fedha za kuweka mwanasheria anayejua tabia ya jaji.
Hivyo sisi kazi yetu ni kujua vifungu na kamwe hatutahangaika na kupekenyua tabia za Jaji au Hakimu.
Wasalaam katika mjadala mwema.
Ni mimi MdogoWenu
Lakini nilichogundua katika practice (siyo fani) ya wanasheria ni kwamba huwa inafika mahala wanaongea kuhusu tabia ya Jaji fulani, physichology ya Jaji fulani. Kwa maana hiyo ni kama vile unatakiwa kuwajua majaji.
Mfano mtu anasema Jaji fulani hapendi hiki wakati jaji mwingine hana tatizo na hicho anachokataa huyo mwenzake. Nilipogundua hivyo tatizo langu hapa likawa ni hili.
Kwa maana hiyo majadiliano mengi wanajadili hivi vitu. Yaani ukitaka kujua tabia za majaji, siyo katika mambo binafsi au vituko, bali katika uendeshaji wa kesi basi kaa na wanasheria.
Sasa hapa likaja tatizo sijui kama ni ujinga wangu kuhusu sheria au la. Kabla ya urafiki na wanasehria nilikuwa ninadhani kwamba kule University au Law School wanasheria walifundishwa sheria zinavyosema. Nikadhani ukijua provision (vifungu) vya sheria basi utatamba kifua mbele kwamba kesi inayoendana na vifungu hivyo utaishinda maadamu hata utaratibu wa kuifikisha (technicality) mahakamani umeufuata.
Hivyo, hata mjinga wa sheria kama mimi, ukijua vifungu vya jambo fulani na utaratibu wake basi una uhakika wa kushinda hiyo kesi. Na kwa kweli hivyo ndivyo ilitakiwa, tuvijue vifungu, tukiviheshimu hatushindwi kesi na anayetushitaki, tukivikiuka tunashinda kesi tunapowashitaki waliovikuka dhidii yetu.
Niliamini hivyo kwa sababu sheria zinatungwa kwa kwa ajili yetu wote na si kwa ajili ya mawakili au wanasheria ambao siyo lazima uwatumie kama huna hela au huwahitaji.
Na mazoea yangu na wanasheria nilidhani nitaokota mengi kuhusu vifungu kwani nilitarajia wanasheria wabishane vifungu kwamba kifungu hiki kinasema hivi na mwingine anabisha nasema kifungu kile kinasema hivi.
Kumbe sivyo! Ukikaa na wanasheria utasikia wanasema jaji huyu yuko hivi na yule yuko vile. Nilipogundua hilo nikasema hebu nililete humu mitandaoni na ikibidi humu JF.
Kama wanachokifanya wanasheria hawa ni kweli huko mahakamani basi nchi yetu iko katika hatari kubwa na mhimili huu wa mahakama. Tunadhani vifungu vya sheria ulivyosoma chuoni au hata sisi mtaani vinatosha kumbe unatakiwa kumsoma na Jaji jambo ambalo mwanasheria hakulisoma chuoni!
Kama mimi ndiye ninakosea kudhani hivi, basi ninatakiwa nirekebishwe lakini hili nimeliona mara nyingi na ninaiona hatari hii. Wengi wengi tu hufungua kesi zao hawana fedha za kuweka mwanasheria anayejua tabia ya jaji.
Hivyo sisi kazi yetu ni kujua vifungu na kamwe hatutahangaika na kupekenyua tabia za Jaji au Hakimu.
Wasalaam katika mjadala mwema.
Ni mimi MdogoWenu