Kichochoro
JF-Expert Member
- Jul 18, 2017
- 1,135
- 1,163
Huu mfumo binafs naufaham sana na hata matapeli walio wengi wanatumia sana wanakuwa na app wanakuambia tuma kwenye namba hii Lakin mda huo namba alishakupa anakuwa na app ambayo anakuwa ameinstall na akaiconnect na namba hyohyo .Wakuu Habari ya Mchana.
Niko Likizo ya Sikuukuu za Mwisho Wa Mwaka Huku Kijijini Kwetu.
Mama yangu Mzazi Anaishi Huku Kwetu Kijijini na Ni Mtu mwenye umri wa takriban miaka 90.
Watoto wake Uwaga tunakawaida ya Kutuma Hela Za Matumizi kwa ajili yake na Matumizi ya Nyumbani Kwa Ujumla.
Hapa Nyumbani Kijijini kwetu anaishi Mama, Mtoto wa Marehemu Kaka ana miaka 12, na Msaidizi wa Ndani.
Mama yetu licha ya Kuwa na umri huo Bado anatembea na anaona Vzr.
Kwa hyo Hapa Kijijini Kuna Kijana anafanya Issue za Mpesa, Airtel Money Nk kwa maana ya Money Transaction.
Kwa hyo Wazee wenye Umri wa Mama wanaenda Hapo Kupata huduma ya Kutoa Fedha so Kwa Umri wake na Hawezi kufanya process ya Kutoa pesa.
So Wazee Wetu wakifika Hapo kibandani kwa hyo mwamba wanatabia ya Kumpa Simu Ili Awasaidie kutoa kiasi wanachokihitaji so huyo Jamaa anajua Namba za Siri Za Kutolea pesa za hawa wazee wetu Hapa Vijijini.
Sasa Juzi Niko Na Mama Tumekaa mida Ya Sa12 jioni Ikaingia Meseji ya Airtel money Kwamba Mama amefanya muamala wa 145000/=kwenda kwa hyo Wakala kwa namba yake binafsi.
Nikamuuliza Mama leo umeenda kutoa pesa kwa hyo Wakala wa hapa kijijini, Mama akaniambia sijaenda huko na hata kama nikienda siwezi kutoa hela yote hyo na natumaje hela kwa namba yake binafsi badala ya kutoa kwenye Till # ya Wakala.
Sasa huyu Mtoto wa Braza akanaMbia kama week hivi ilikuja meseji Kwamba mama amemtumia hyo kijana tena 18500/=
So ikabidi nifuatilie kwa Kupiga Namba ya Huduma kwa Wateja Ya Airtel, Wakaniambia kwamba ni kweli Muamala huo umefanyika na ipo miamala mingine takribani 25 ambayo mama yako ametuma kwa hyo kijana.
Ikabidi nimuulize hyo mtaalamu wa Airtel kwamba inakuwaje anaamisha pesa kutoka kwenye simu ya Mama na Simu wakati anayo Mama?
Wakanijibu Kwamba yawezekana huyo Wakala ana Smartphone ambayo ame download apps ya Airtel money So Ndio anatumia kutoa hyo pesa hata kama hana simu.
Wakaniambia Mtu akiwa na hyo Apps yoyote ya hizi huduma za kifedha na akawa na namba yako ya simu na akawa na namba yako ya Siri anauwezo wa kutoa au kuangalia Salio lako bila ww mwenye simu kujua.
Wakuu niko njia panda naombeni ushauri wenu jinsi ya kudeal na huyu Mtu Kabla Sijarudi mjini maana atakuwa ameshawaumiza Sana Wazee Wetu Hapa Kijijini.
Nawasilisha Wakuu
Sent using Jamii Forums mobile app
Ushauri wewe nenda Hadi kwa hyo kijana ukifika mwambie akuazime smartphone yake baada ya hapo ingia kwenye app Kama ni Airtel money app ama Vodacom then ingia itakuomba namba ya Siri ya mama na baada ya hapo icheki ukishajiridhisha nenda polisi fungua mashitaka dhidi yake then ukishapewa mpelelezi mueleze inshu nzima ilivyo mtaenda naye maana yeye anaauthority wakumuomba simu hyo pamoja na yeye kwa upelelez then mweleze inshu ilivyo na kinachofanyoka.
Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app