Civilian Coin
JF-Expert Member
- Dec 2, 2012
- 2,305
- 4,334
MAVAZI YA WASANII KWENYE VIDEO SIO TATIZO, TATIZO NI USHAMBA WA VIONGOZI WETU.
Majuzi nimewasikia Naibu Waziri Habari na Rais Magufuli wakikemea kuvaa nguo za utupu kwenye Video. Ukiwa Mshamba ni mshamba tu hata ungekuwa na cheo Ikulu, hata kama ungekuwa Profesa.
Nchini Swaziland kwa King Mswati mavazi wanayovaa ni nusu uchi kabisa tena mbele ya Mfalme wao mpaka matiti yakiwa nje na huo ndio utamaduni wa Mwafrika tangu kale, wazungu wamechukua kwetu na Leo mnafikiri tunawaiga wao. Mwanamke mvuto bila mwanamke kwenye kazi ya Sana'a mambo haya nogi na ndio maana ukiwa na mke unatamani awe mtupu muda wote ule maisha ya mahaba lakini utupu wa kwenye video ni wa maigizo tu kuvuta watazamaji na ndio maana hawaachii kila kitu.
Mziki ni mvuto na inategemea unafanya mziki wa aina gani na una lenga jamii gani, Mziki wa bongofleva ni mziki unaofikisha ujumbe kwa vijana na mavazi lazima yaendane na ujana, kama ni nyimbo za asili nazo zina mavazi yao na aina yake ya watazamaji, na ndio maana kuna vipindi tofauti redioni kulingana na rika, kama tunataka mziki wa kuuza uswahilini basi tusikilize ushamba lakini kama tunataka mziki wa kimataifa basi lazima twende na wakati na mazingira ya Globolaizesheni.
Kazi njema Viongozi wa Awamu ya Tano.
Deogratius Nalimi Kisandu.
25 Desemba 2017.
Majuzi nimewasikia Naibu Waziri Habari na Rais Magufuli wakikemea kuvaa nguo za utupu kwenye Video. Ukiwa Mshamba ni mshamba tu hata ungekuwa na cheo Ikulu, hata kama ungekuwa Profesa.
Nchini Swaziland kwa King Mswati mavazi wanayovaa ni nusu uchi kabisa tena mbele ya Mfalme wao mpaka matiti yakiwa nje na huo ndio utamaduni wa Mwafrika tangu kale, wazungu wamechukua kwetu na Leo mnafikiri tunawaiga wao. Mwanamke mvuto bila mwanamke kwenye kazi ya Sana'a mambo haya nogi na ndio maana ukiwa na mke unatamani awe mtupu muda wote ule maisha ya mahaba lakini utupu wa kwenye video ni wa maigizo tu kuvuta watazamaji na ndio maana hawaachii kila kitu.
Mziki ni mvuto na inategemea unafanya mziki wa aina gani na una lenga jamii gani, Mziki wa bongofleva ni mziki unaofikisha ujumbe kwa vijana na mavazi lazima yaendane na ujana, kama ni nyimbo za asili nazo zina mavazi yao na aina yake ya watazamaji, na ndio maana kuna vipindi tofauti redioni kulingana na rika, kama tunataka mziki wa kuuza uswahilini basi tusikilize ushamba lakini kama tunataka mziki wa kimataifa basi lazima twende na wakati na mazingira ya Globolaizesheni.
Kazi njema Viongozi wa Awamu ya Tano.
Deogratius Nalimi Kisandu.
25 Desemba 2017.