Mavazi ya kubana - Athari kwa wanawake

WomanOfSubstance

JF-Expert Member
May 30, 2008
5,458
956
Wanawake wavaao suruali watahadharishwa




na Esther Mbussi



WANAWAKE wanaovaa suruali aina ya jinzi na nguo za kubana, wako kwenye hatari ya kupata magonjwa hatari pamoja na kuharibika maumbo yao ya asili.

Dk. Amos Dadaoh wa Chuo Kikuu Huria Tanzania kinachotoa tiba kwa kutumia mimea, alisema hayo jana alipokuwa akizungumza na Tanzania Daima. Aliongeza kuwa, suruali imetengenezwa kama vazi maalumu kwa wanaume.

“Suruali imetengenezwa likiwa vazi maalumu kwa wanaume na kwamba mwanamke kwa maumbile yake anatakiwa kuvaa mavazi yanayompa nafasi yaani yasiyobana,”alisema Dk. Dadaoh.

Alisema magonjwa wanayoweza kuyapata kutokana na mavazi hayo ni pamoja na kuota mizizi kwenye kizazi, moyo kuwa mkubwa na kushindwa kufanya kazi kama kawaida.

Alisema suruali ya kubana inahamisha mafuta kutoka kiunoni kwenda kwenye moyo na kizazi. Mafuta hayo husababisha mwanamke kushindwa kusukuma mtoto wakati wa kujifungua.

“Mwanamke ambaye amezoea kuvaa suruali hasa aina ya jinzi ya kubana, pia yuko kwenye hatari ya kupoteza uhalisia wa umbo lake na kuwa kama simba - juu kuwa mpana na chini mdogo - kwani anabana mafuta kwenye mapaja ambayo yanaingia moja kwa moja kwenye kizazi na kwenye moyo,” alisema Dk. Dadaoh.

Dk. Dadaoh alisema mwanamke kiasili ni wa pembe tatu na mavazi yake ni ya kuachia na yenye nafasi yasiyobana kwenye kati kati ya mapaja.

“Ukiangalia Wakorea na Wajapani hawana kiuno wala makalio, wako bapa, ni kwa sababu ya tabia ya mazoea ya kuvaa suruali za kubana,” alisema Dk. Dadaoh.

Pia alisema kina dada wenye mazoea ya kubana matiti, tumbo na kiuno pia wako kwenye hatari hii ya kupata magonjwa aliyoyataja hapo awali, kwani mafuta yanaganda kwa kukosa mwelekeo maalumu na ndiyo sababu wasichana wengi siku hizi wana matumbo makubwa (vitambi).

Alitoa ufafanuzi kuwa matatizo hayo yanayosababishwa na mavazi hayo, hayaleti madhara haraka kwa mvaaji kuvaa mara moja na kuathirika baada ya kuvua, bali huja taratibu kutokana na umri na mazoea ya kuvaa mavazi hayo kwa muda mrefu.

Your views please!
 
Utafiti wa huyu mbwana me hata sikubaliane nae. kwani hana points za maana kabisa
 
Ameniacha hoi aliposema "Ukiangalia Wakorea na Wajapani hawana kiuno wala makalio, wako bapa, ni kwa sababu ya tabia ya mazoea ya kuvaa suruali za kubana," alisema Dk. Dadaoh.

Kukosa makalio,kiuno na kuwa bapa nadhani ni genetic zaidi kuliko kuvaa suruali...
ila kwa upande mwingine ni kweli ukivaa nguo ya kubana kiuno utakuwa na kiuno kidogo kuliko ukiwa na kawaida ya kuvaa tank-tops.... athari ndo siwezi kusema.Madaktari walio members humu mtusaidie
 
huyo mtafiti anawaaibisha wenye fani ya kufanya utafiti, kwanza akafanye utafiti kwa nini hao wachina, japan n.k kwa nini wanahizo shepu. natakakukuambia hawataki hiyo mishepu ya kiafrica mitumbo na mimatako mikubwaaa kwani wanafanyishwa mazoezi tangu utotoni, mtafiti ushindwe na ulegee unalako
 
mmh hii ipo katika khali ya kufikirika zaidi kwani hao wakorea hata akiwa mdogo mbona kiuno ni bapa tu na ndo jinsi alivyo zaliwa.
Mbona wazungu wanamakalio na maumbo fresh tu?
 
maradhi yatawakuta wanawake wengi siku hizi maana wengi mno wanazivaa .. wengine mpaka wanatia kinyaa mara mpaka mipaka ya nguo za ndani zinaonekana halafu huku mbele ndiyo kabisa umeshamuona ... maana everything is defined ... vaane mashati marefu au tshirts ndefu tafadhali wanawake wenzangu
 
Utafiti wa huyu mbwana me hata sikubaliane nae. kwani hana points za maana kabisa
Je una weza kutuhakikishia vipi kwamba utafiri wa huyu Dr si kweli na hauna maana yoyote. Tupe point zako tafadhali zitakazo tufanya tuone point za Dr Dadaoh si za kweli
 
Why only looking at things you don't agree with? Concern yake kubwa wala sio shepu! Kuna kina dada hapa wana pea nyingi mno za JEANS inaonekana :)



.
 
Kitu muhimu hapa ni akina dada kujihadhari tu kwani wasipovaa hivyo vijeans na vitop kuna shida gani? Tatizo la akina dada wengi wao wanaangalia fulani kavaaje na kama kapendeza nao wanaiga, kwani zamani walipokwa wakivaa mavazi decent walikuwa hawaonekani na kupendeza.

Mimi nadhani hatuna haki ya kumshutumu huyo mtafiti kwa utafiti wake, only time will tell. Kitu muhimu ni kujihadhari tu na kuvaa nguo za kubana ili kama utafiti wake ni kweli dada zetu waepuke athari hizo.
 
maradhi yatawakuta wanawake wengi siku hizi maana wengi mno wanazivaa .. wengine mpaka wanatia kinyaa mara mpaka mipaka ya nguo za ndani zinaonekana halafu huku mbele ndiyo kabisa umeshamuona ... maana everything is defined ... vaane mashati marefu au tshirts ndefu tafadhali wanawake wenzangu


Wanaita "camel toe"!

(Search kwenye googles >> Images)



.
 
Mimemsikia huyu Doctor akihojiwa na Power Breakfast leo. Assound so confident because because of research. Wakinamama mnaweza kuamua lipi bora. Afya au defective elegancy
 
Mimemsikia huyu Doctor akihojiwa na Power Breakfast leo. Assound so confident because because of research. Wakinamama mnaweza kuamua lipi bora. Afya au defective elegancy

Lakini kuna kitu amenifanya nitilie mashaka huo utafiti japo maelezo yake makes a lot os sense.
Kwanini anakazania sana suruali za jeans na coudray ( spelling?)na bra... mbona hazungumzii mikanda, girdles na cossets wanazovaa wanawake au zamani wanawake wa west walikuwa wanakaza matumbo yao kwa mikanda maalumu kupata kiuno kama nyigu wakati wakivaa yale mavazi yao yenye kuchanua kama mwamvuli....je miaka hiyo ( as far as 16th -20th Century)mbona hatujasikia madhara yaliyowapata? Africa... wanawake pia wanakaza matumbo kwa kanga na hata mikanda baada ya kujifungua...madhara ni yapi?
 
Strange thing about this "scientific" explanation by our Mitishamba expert is that people will believe it even the learned one and start demanding for girls and women to stop wearing pants!
 
Kwa mtaji huu basi wanawake wa nchi kama Marekani na kwingineko ambapo wanavaa sana hizo suruali za kubana wangekuwa na matatizo kwa wingi, na hivyo basi jambo hili lingeshaongelewa sana kama tahadhari! Nakubali kuna madhara ya kuvaa Bra inayobana ila sijawahi kusikia suruali inayobana esp. jeans.For some reasons, I don't buy it!
 
Mimi nakubaliana naye on the basis kwamba mwanamke kuvaa jeans inaharibu flow ya foreplay.
 
I just heard this Clouds FM informing last week but the subject was almost at the end. I'm happy to know that this is from Dr. Dadaoh whom I was heard that he is on the process to open a Medical Plant University. Basically, these are good news to ladies and I think this is the right channel to inform them. Despite that they sometimes look extra cute when dressed on tight trousers, let then find alternatives.

Chaooooooo
bm21
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom