Mavazi, Mitindo, Mapozi na Sanaa Hizi 'Vimeenda Shule'..unakubali haukubali?!

Steve Dii

JF-Expert Member
Jun 25, 2007
6,402
1,254
irene.jpg

Irene Kiwia, Getting ready to launch 'Face of Tanzania' late 2007. Picture courtesy of IssaMichuzi blog.
 
HappinessMagessa2.jpg


HappinessMagessa1.jpg

Happiness Magese akiwa Jo'burg S.Africa kwenye shughuli zake za modelling.
Picha: hisani ya haki-hakingowi.blogspot.com
 
flav.jpg

Flav Matata akiwakilisha michururizo ya Angelo Elly Mlaki.
Picha: hisani ya issamichuzi.blogspot.com
 
jokate.jpg

Mrembo akiwakilisha chachafya za Haute Couture - Pilipili line by Mustafa Hassanali.
 
richa-bw.jpg

Richa, Miss Tz 2007 akiwa amepose ndani ya Black&White with a tinge of karibu gesture being easily noticeable!!
 
Nancy-Namaste.jpg

Mustafa akiwa na Nancy wakisindikiza Namaste crop. (picture courtesy of issamichuzi blog)
... naona mapozi ya ki-namaste-namaste yamemkubali sana Nancy :)

Je nani ameshaona ile movie ya namaste-namaste (ya kihindi).... movie ndefu hiyo, ina vituko vingi na suspense moment kibao!! Go to your nearest rental store uicheki siku moja, interesting.... lol.
 
vazilataifalakike.jpg

Vazi lililoshinda kwenye shindano la 'vazi la kitaifa la kinamama' mid 2006.
Picha: hisani ya issamichuzi.blogspot.com
 
spotlight.jpg

Stara Thomas, mwimbaji wa zouk akiwa amevalia vazi murua kabisa!
Picha: hisani ya haki-hakingowi blog.
 
Carolinemustafa.jpg


Caroline akiwakilisha mitindo ya Hassanali. (picha kwa hisani ya Haki-Hakingowi blog)

...Vazi hili kwa maoni yangu walifanye mojawapo ya vazi la taifa. 'Have got an eagle eye when it comes to styles, dress codes, and all that jazz... On this one trust me, i'm truly on it. Vazi hili ni kiboko period! Hapo juu Caroline naona angeua na kuzika kama angemalizia na vibangili viwili vilivyo golden au moja pana lililo golden ili kukamilisha mambo... na kwa kuongezea tu, hapo pia kama kuna kaubaridi anaweza akavaa kijambakoti cheupe chenye michiririzi myeusi kwenye mikono, au basi cheusi chenye collar nyeupe.... na kama hatopenda nywele zake zionekane, anaweza kabisa kuvaa kilemba chenye rangi ya dhahabu au kilemba cheupe... The Woow factor is written all over that dress!

....on that note, I wish I can get a picture of her in that dress posing on her own. anyone out there that can help pls...?
 
ZN4K74s.jpg

On the shores of Indian ocean, word is bond, Africa Rocks!!

... and you know what?.......
7.jpg
 
SteveD heri ya pasaka mkuu!

Wengine tumefufuka na Yesu. wewe je?

Nadhani nikipata mchumba itabidi avae vazi moja wapo katika haya uliyoweka humu! au?
 
Hilo lilliloshinda mashindano ya vazi la taifa 2003 (si 2006) lilishonwa na mama mmoja wa Kigoma, lilipotangazwa ukumbini pale Kilimani Dodoma (nilikuwepo) watu wengi walipigwa na butwaa nawengine wakazomea.

Sikujua kwanini! Ila lilitukumbusha wengi picha za magazetini za miaka ya 60 (nadhani wakati ule kulikuwa na aina fulani ya renaisence ya uafrika / uzalendo!
Hilo la Stara lilikuwepo katika shindano lile pia, ni ubunifu wa Ailinda Sawe wa Afrika Sana.

Hili ulilopendelea lingekuwa vazi la taifa si baya, kusema kweli lina elegance ya aina fulani. Ila mie binafsi huwa nasita sana kushabikia hii dhana ya vazi la taifa kwa sababu moja ya msingi: ni vigumu sana watu wote, au wengi kwa asilimia ya kuhalalisha, kukubaliana na aina ya vazi linaloweza kuitwa kwa uhalali la kitaifa.
Napendelea zaidi kuwe na ubunifu wa aina mbalimbali za mavazi ambayo yataunda fungu la mavazi ya kitaifa; na mavazi hayo yakidhi vigezo fulani vilivyokubaliwa na asilimia kubwa ya watanzania.

Ila nakubali kweli baadhi ya haya mavazi "yameenda shule" (whatever that may mean!) Bila shaka yamemzingua Sveve D. Lakini Sveve D ujue si kila likuzingualo weye litanzingua mie. Kama usanii wa kuyasanifu, naam ni kweli wasanifu wamejitahidi. Lakini hata yangekuwa na uzuri gani, kuna tamaduni kama za kiunguja,baadhi ya haya yangepata taabu kidogo kukubalika, au yasikubalike kabisa! Leta nyingine!
 
Duh! Halafu nilikuwa sijaliona hilo la kanga alilovaa huyo mtoto akawa kama nguva aliyesimama juu ya mwamba baharini!Aminia babaake! Msanii kajitahidi kuchanganya matambala, japo katika ubunifu hakuna jipya! Ni mtindo unaoshonwa asubuhi na jioni kwa miaka au miongo mingi!
 
Caroline akiwakilisha mitindo ya Hassanali. (picha kwa hisani ya Haki-Hakingowi blog)

...Vazi hili kwa maoni yangu walifanye mojawapo ya vazi la taifa. 'Have got an eagle eye when it comes to styles, dress codes, and all that jazz... On this one trust me, i'm truly on it. Vazi hili ni kiboko period! Hapo juu Caroline naona angeua na kuzika kama angemalizia na vibangili viwili vilivyo golden au moja pana lililo golden ili kukamilisha mambo... na kwa kuongezea tu, hapo pia kama kuna kaubaridi anaweza akavaa kijambakoti cheupe chenye michiririzi myeusi kwenye mikono, au basi cheusi chenye collar nyeupe.... na kama hatopenda nywele zake zionekane, anaweza kabisa kuvaa kilemba chenye rangi ya dhahabu au kilemba cheupe... The Woow factor is written all over that dress!

....on that note, I wish I can get a picture of her in that dress posing on her own. anyone out there that can help pls...?


Yap! Hilo vazi rangi yake na mshono super sana, isipokuwa, kama lingeshonwa kwa namna fulani ya kufunika mabega na kifua naamini wanawake asilimia 80% au zaidi watalipenda. Kwanzan, kwa design, style na staha ya hilo vasi itawavutia akina mama wengi.

Unajua sio wanawake wote wanapenda nguo zenye kuacha magega na Kifua nje! Labda ziwepo design za aina mbili kwa mshono wa aina hii, moja full (yenye kufunika mabega na kifua) na nyingine kama inavyoonekana katika picha.
 
Will be back, asanteni nyote kwa comments zenu. Tanzania lazima tutafute mbinu ya kutangaza sanaa zetu, mambo ya mpaka kutegemea watalii watembelee jumba la sanaa Dar au kwenda kwenye showrooms za vinyago na mambo ya utalii kwenye mahoteli tusiyaendekeze....

Utalii, ujuzi na sanaa zetu tuwapelekee wazione na wazifate!! Tuwaonjeshe so they can come back for more!! :)
 
Je na mimi naweza kuweka picha za ma models wengine?

mkinipa ruksa sawa
Sawa BRAZAMENI, preferably kutoka Africa, (ukishindwa hata huko kwingineko) muhimu- hisia zako katika hayo mavazi au sanaa. Shukrani... anyway, i know u have gobs of da stuff, tunakusubiria.... lol!
 
Mnamo August 2008 Tanzania ilipata mwakilishi kwenye moja ya mizunguko inayothaminika sana katika ulimwengu wa mitindo. Thamani hiyo ni kule kushiriki London Fashion Week. Mwakilishi wetu alikuwa Ally Rhemtullah. Off course nadhani alienda huko kama mtu binafsi, mwanamitindo binafsi. Hata hivyo kwa uwepo wake tu kule ni sababu tosha ya kumpongeza na kuweza kusema kuwa yeye alikuwa mwakilishi wetu. Maonesho yalinoga sana. Picha mbalimbali kwenye ma-blog zilitundikwa. Wenye kukosoa walikosoa, wenye kukerwa walikerwa na kuziponda na wenye kuzipenda walionesha mapenzi yao.

Moja ya picha niliyokutana nayo sana ni hii hapa:

steved-albums-mh_pinda-picture174-londonfashionwk-allyrhemtullah.jpg

Tukiweka pembeni mambo ya maadili na tamaduni, mitindo hii "imeenda shule kwa maoni yangu." Hapa naongelea jinsi vile mbunifu alivyochanganya rangi, vitambaa, (vitenge, kanga na batiki) ambavyo vinapatikana hapa nyumbani na kuweza kutengeneza vitu maridhawa kabisa ambako maadili kama hayo yanakubalika kwa namna moja au nyingine ndani ya ulimwengu madoido hayo yalipofanyika.

 
Back
Top Bottom