OSAM
Member
- May 14, 2011
- 31
- 2
Wadau hivi majuzi nilishikwa na kama kichomi fulani hapa juu ya tumbo yani katikati ya tumbo na kifua sikulala kabisa usiku wake.
Sikuwahi kutokewa na hali hii hiyo ndiyo ilikua mara ya kwanza.
Hata hivyo sikuweza kwenda hospitali kwa sababu nilikua na safari ya muhimu sana. Nilijaribu kuwauliza watu mbali mbali wakawa wananiambia ni chembe ya moyo lakini mimi sijui chochote kuhusu hiyo chembe ya moyo yenyewe.
Naombeni msaada wenu wadau.
=======
w0rM anasema:
Chembe ya moyo(Angina Pectoris) ni tatizo linalowasumbua watu wengi sana kwa sasa na hutokea pale moyo unapopata hewa ya oxygen kidogo tofauti na mahitaje yake
Hali hiyo inaweza kusababishwa na aidha kuziba kwa mishipa ya damu inayopeleka damu moyoni na kusababisha misuli ya moyo isipate damu ya kutosha inayobeba oxygen
Sababu nyingine ni pale moyo unapofanya kazi kubwa sana ya kusukuma damu kiasi kwamba kiwango cha oxygen ambacho moyo huo unapata kinakua hakitoshi
Inaelezwa kuwa Watu waliopo kwenye hatari zaidi ya kupata ugonjwa huo ni; Wanaovuta sigara, Wanene kupita kiasi na wenye ugonjwa wa kisukari
DALILI ZA CHEMBE YA MOYO
Dalili kubwa ni maumivu katikati ya kifua yanayokua kuelekea kwenye mkono wa kushoto
MATIBABU YAKE
Kuna dawa nyingi zinazo weza kutumika kutibu tatizo hili, baadhi ya dawa hizo ni Nitroglycerine(Glyceryl Nitrtrate), Nifedipine na Atenolol
Aidha, ikigundulika mishipa ya damu inayopeleka damu kwenye misuli ya moyo imeziba mgonjwa atakiwa kufanyiwa upasuaji ili kuizibua
Sikuwahi kutokewa na hali hii hiyo ndiyo ilikua mara ya kwanza.
Hata hivyo sikuweza kwenda hospitali kwa sababu nilikua na safari ya muhimu sana. Nilijaribu kuwauliza watu mbali mbali wakawa wananiambia ni chembe ya moyo lakini mimi sijui chochote kuhusu hiyo chembe ya moyo yenyewe.
Naombeni msaada wenu wadau.
=======
w0rM anasema:
Chembe ya moyo(Angina Pectoris) ni tatizo linalowasumbua watu wengi sana kwa sasa na hutokea pale moyo unapopata hewa ya oxygen kidogo tofauti na mahitaje yake
Hali hiyo inaweza kusababishwa na aidha kuziba kwa mishipa ya damu inayopeleka damu moyoni na kusababisha misuli ya moyo isipate damu ya kutosha inayobeba oxygen
Sababu nyingine ni pale moyo unapofanya kazi kubwa sana ya kusukuma damu kiasi kwamba kiwango cha oxygen ambacho moyo huo unapata kinakua hakitoshi
Inaelezwa kuwa Watu waliopo kwenye hatari zaidi ya kupata ugonjwa huo ni; Wanaovuta sigara, Wanene kupita kiasi na wenye ugonjwa wa kisukari
DALILI ZA CHEMBE YA MOYO
Dalili kubwa ni maumivu katikati ya kifua yanayokua kuelekea kwenye mkono wa kushoto
MATIBABU YAKE
Kuna dawa nyingi zinazo weza kutumika kutibu tatizo hili, baadhi ya dawa hizo ni Nitroglycerine(Glyceryl Nitrtrate), Nifedipine na Atenolol
Aidha, ikigundulika mishipa ya damu inayopeleka damu kwenye misuli ya moyo imeziba mgonjwa atakiwa kufanyiwa upasuaji ili kuizibua