Maumivu katika mwili hasa nyuma ya mabega

Ngozi Joram

JF-Expert Member
Sep 9, 2016
659
543
Salaam ndg zangu na heri ya mwaka mpya. Nimekua napata maumivu mwilini ambayo sielewi sababu yake. Hasa misuli iliyopo nyuma ya bega au niseme sehemu ya juu ya mgongo inayounganisha mabega na shingo.

Je kuna mwenye kujua jambo hili?
 
Niliwahi kuwa na Maumivu kama hayo, nlipoenda hosp wakanambia kuwa huwa ni dalili za Vidonda vya tumbo. Nikapima kipimo kinachoitwa H-pillory. Wakakuta negative. Ikaonekana kuwa nakula sana. Vyakula vyenye gesi.
 
Niliwahi kuwa na Maumivu kama hayo, nlipoenda hosp wakanambia kuwa huwa ni dalili za Vidonda vya tumbo. Nikapima kipimo kinachoitwa H-pillory. Wakakuta negative. Ikaonekana kuwa nakula sana. Vyakula vyenye gesi.
Sasa tiba ikawa ni nini?yaani ukafanyaje?
 
Walinipa anti biotics na dawa za kuondoa gesi. Na nikawa vizuri. Nilitibiwa Tumaini hospital.
 
Salaam ndg zangu na heri ya mwaka mpya. Nimekua napata maumivu mwilini ambayo sielewi sababu yake. Hasa misuli iliyopo nyuma ya bega au niseme sehemu ya juu ya mgongo inayounganisha mabega na shingo.

Je kuna mwenye kujua jambo hili?
Ukiwa na Shida yoyote ile
Usipo pona kwa Dawa za Hospitali nitafute mimi nipate kukutibia upate kupona ukihitaji matibabu yangu
Unaweza kunitafuta kwa Mawasiliano Herbalist Dr. MziziMkavu Email barua ya pepe. fewgoodman@hotmail.com What's App na Viber +905344508169
 
Salaam ndg zangu na heri ya mwaka mpya. Nimekua napata maumivu mwilini ambayo sielewi sababu yake. Hasa misuli iliyopo nyuma ya bega au niseme sehemu ya juu ya mgongo inayounganisha mabega na shingo.

Je kuna mwenye kujua jambo hili?
Hiyo hali kwa sisi tunao ishi ulaya tunaielewa sana kupita kiasi. Ugonjwa kama ukitaka tuuite hivo ila mimi naweza pendelea kuita hali, unaitwa "stress" au hali ya stress. Huu Ugonjwa mara nyingi Africa hatuujuwi na unawafanya ma Dr. wa kienyeji kupata riziki zao kwa wingi. Mabadiliko ya mfumo wa maisha Africa kwa sasa wenye hali ngumu na hali mtu, hapa kazi tu unapelekeya hii hali kuwa ya kawaida. Stress ni Ugonjwa wenye dalili nyingi mno. Yaani sio tu mgongo au bega, unasababisha hata kuharisha. Unakumbuka wanaposema mtu kaharisha kwa uoga, au kwa mshituko? Basi kazi ya stress. Inaleta majipu, maupele, chunusi ... inategemeya na mwili wako uta react vipi. Sasa tiba yake kubwa: punguza mawazo, zunguukwa na watu wanaokufurahisha, fanya kile unacho kipenda(kazi), fanya mazoezi, kisha usisahau massage. Kama hujaoa basi kuoa ni dawa kubwa manaake licha ya kupata massage ya kila unapoitaji, utapata rafiki wa karibu wa kuongea nae matatizo na furaha yako. Tiba ya haraka haraka ni hapo palipo na unundu, tafuta mtu apakande kweli kwa mafuta yoyote yale au vicksi hadi nundu ipotee kabisa. Vumiliya maumivu, ila baadae utahisi umeutuwa mzigo wa kilo 50 za mchele ulizo bebeshwa na shangazi yako kuleta kijijini kipindi kile ulienda waona.
Uongo mtupu, hujarogwa wala nini. Unaumwa stress. Kwa lugha nyingine Unaumwa MAISHA. Pole sana.
 
Salaam ndg zangu na heri ya mwaka mpya. Nimekua napata maumivu mwilini ambayo sielewi sababu yake. Hasa misuli iliyopo nyuma ya bega au niseme sehemu ya juu ya mgongo inayounganisha mabega na shingo.

Je kuna mwenye kujua jambo hili?
Huu ugonjwa ninao piaa unanisunbua toka mwez wa 03/2016 nilienda Hospital hapa Dar nikapewa dawa na nikapiga X_ray nikakutwa niko poaa wakanipa dawa za kumeza ikapoaa week ila toka hapo bado tu hadi leo
 
Back
Top Bottom