Maumivu baada ya kung'oa jino yanapona kwa dawa gani?

MAKOLE

JF-Expert Member
Feb 5, 2012
618
280
Wadau, naomba msaada wenu. Nimengoa jino na leo tar 26/7 nna siku ya nne. Jino lenyewe ni namba 7 kwa sababu nimewasikia madaktari wakilitaja. Lilikatika wakati wakiling'oa na ikasababisha watumie nguvu ya ziada kungoa mizizi. Nilipata maumivu sana kiasi kwamba hadi leo naumwa.

Waliniandikia kumeza Paracetamol, Cloxaxiline na Metronidazole(flagile), Pia wamenishauri nisukutue maji ya uvuguvugu yenye chumvi. Yote nimeyafanya lakini mara kwa mara maumivu yanarudi. Madaktari naomba mnipatie msaada wa dawa ya uhakika kama ipo na pia mnieleze ni mpaka siku ngapi fizi inaweza ikapona?
 
Hadi leo kimya. Pole.
Uzuri haujafa, nimeona last seen yako recently
Hayo maumivu huwa ni matokeo tu ya jino kutoka. Mimi hadi shavu lilivimba kidogo, ila maumivu yake si makali sana na yanapotea kadri siku zinavyoenda. Kama jino lililong'olewa ni kipande basi nguvu iliyotumika kuling'oa ni kubwa kidogo hivyo mwili ndo unarespond kwa hayo maumivu.

Mimi walining'oa mizizi mitatu!!! Yaani hadi damu zilinijaa mdomoni.Ila kesho yake ganzi ilivyoisha na maumivu kuanza niliendelea kutumia hizo hizo dawa za hospitali hadi nikapona.

Ningekuwa nimejiunga jf kipindi hicho ningemsaidia.
 
Back
Top Bottom