moneytalk
JF-Expert Member
- Jan 23, 2017
- 7,636
- 16,225
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
sehemu ya kwanza au ya pili nadhani,ilielekeza kuwa,benjamini ni mwanafunzi wa masomo ya sayansi ya utabibu,yaani udaktari,hii ya leo inasema yeye ni mtaalamu wa kompyuta...marekebisho tafadhaliAsanteni jamani tunaendelea
NYEMO CHILONGANI
MAUAJI YALIYOJAA UTATA
Sehemu ya Ishirini na Saba.
Wanaume watatu wenye uchu wa fedha walikuwa wamekaa sebuleni, chupa kubwa za pombe zilikuwa mezani na walikuwa wakinywa mfululizo, maisha yao yalionekana kubadilika kwani kitu walichokuwa wakikitaka, walikipata na kazi moja tu ndiyo iliyokuwa ikisubiriwa, kumuua mtu ambaye waliambiwa wamuue.
Mbele yao hakukuwa na kazi kubwa, kazi kubwa ambayo walikuwa nayo ni kumtafuta mtu huyo, baada ya kumpata, hakukuwa na kazi nyingine yoyote ile kwani kitendo cha kumuua, wala hakikuwa kazi kubwa, ilikuwa nyepesi sana, kama kumsukuma mlevi katika mteremko wa mlima Kitonga.
Walipokuwa wakiendelea kunywa pombe kali, ndipo waliposikia kelele kutoka katika chumba walichomuhifadhi David, walikumbuka kwamba walimsiba mdomo kwa kutumia gundi hivyo wakajua kwamba kijana huyo alileta ubishi na hatimaye kutoa gundi hiyo mdomoni.
Hilo liliwakasirisha sana, wawili wakamwambia mwenzao achukue bastola na kuelekea huko chumbani ili amtulize David, baada ya kunywa pombe ndipo wamuue kwa kumtumbukiza ndani ya pipa la tindikali.
“Kamtulize, akileta ubishi, mzimishe kwa muda,” alisema Cobra.
“Ila mnanionea sana, tunakunywa na kufurahia maisha, mnaanza kunituma,” alisema jamaa huyo aliyejulikana kwa jina la Amazon.
“Wewe nenda, kwanza wewe si ndiye mdogo, hatumalizi pombe zote,” alisema Cobra huku akimwangalia Amazon kwa jicho lililomtaka kufanya kile alichomwambia.
Huku akionekana kukasirika, Amazon akainuka, akachukua bunduki na tochi kisha kwenda katika chumba kile alichoambiwa aende. David hakunyamaza, aliendelea kuzungumza maneno yaleyale ya kuwatia hasira kwa kudai kwamba waliogopa kumuua.
Alipoufikia mlango ule, akawasha tochi na kuingia ndani, alipomulika, mtu aliyemuona akiwa amelala, hakumuona vizuri, alimuona kwa nyuma tu, kutokana na mavazi aliyokuwa nayo, aliamini kwamba alikuwa David, akaanza kumfuata pale chini.
Alipomfikia na kumwangalia vizuri, nywele nyingi alizokuwa nazo zilimshtua, alipotaka kugeuka tu, akashtukia akipigwa nondo ya kichwa, hapohapo akaanguka chini na kupoteza fahamu.
“Inuka...inuka Vivian,” alisema David huku akimuinua Vivian.
Vivian akainuka, David akachukua bastola ile na kumwambia Vivian amfuate, wakaanza kuelekea sebuleni. Walipofika huko, wakamkuta Cobra na mwenzake wakinywa pombe kali, hapohapo wakawaweka chini ya ulinzi.
“Ukitingishika tu, nakumwaga ubongo,” alisema David huku akionekana kuwa na hasira.
Wote wakatulia, kwa jinsi David alivyoonekana, alionekana kuwa na hasira nyingi ambaye hakutaka kabisa kufanyiwa mchezo. Walibaki wakiwa wametulia na kufanya kile ambacho David alitaka wakifanye.
Alichowaambia ni kwamba wachukue simu na kumpigia mtu ambaye aliwatuma na kumwambia kwamba kazi ilikuwa imekamilika, yaani yeye na Vivian walikuwa wamekufa.
Hakukuwa na aliyeleta ubishi kwani walijua kwamba kijana huyo hakuwa na masihara hata kidogo hivyo wakachukua simu na kumpigia Dracula. Simu iliita kwa muda mchache tu, ikapokelewa.
“Mmekamilisha?” ilisikika sauti ya Dracula kutoka upande wa pili.
“Kila kitu tayari! Tumewaua wote,” alisema Cobra.
“Safi sana! Ngoja niwasiliane na mzee, kiasi kilichobaki kitatumwa katika akaunti zenu,” alisema Dracula kisha Cobra kukata simu.
Hiyo wala haikutosha, alichoagiza David ni kwamba Vivian awafunge kamba na kisha waondoke, hilo wala halikuwa tatizo, Vivvian akarudi chumbani kule ambapo alimkuta Amazon akiwa hoi chini huku damu zikimtoka kichwani, akachukua kamba na kurudi sebuleni ambapo akawafunga vijana hao na wao kuondoka huku wakiufunga mlango kwa nje.
****
Dracula alikuwa akizungumza na Bwana Seppy katika kituo cha polisi, muda wote uso wa mzee huyo ulionyesha tabasamu pana kwani hakuamini kile alichokisikia kwamba mtu aliyekuwa akimsumbua kwa wakati huo alikuwa marehemu.
Hiyo ilimaanisha kwamba hakukuwa na mtu yeyote ambaye angemtisha katika kesi hiyo kwani kama shahidi aliyekuwa akimtegemea Benjamin alikuwa mmoja tu, David ambaye mpaka katika kipindi hicho alipewa taarifa kwamba alikuwa marehemu.
“Una uhakika wamefanikiwa?” aliuliza Bwana Seppy.
“Ndiyo! Wamenipa taarifa, huwa wanafanya hivi kila siku,” alisema Dracula.
“Asante Mungu!”
Hakuwa na cha kufanya zaidi ya kumshukuru Mungu tu, kwake ulionekana kuwa kama muujiza mkubwa kwani kwa kipindi hicho alihitaji sana David auawe kuliko kitu chochote kile.
Alibaki akiiangalia saa yake, aliona muda ukikawia kwenda kwani alitamani kusimama kizimbani na kuiambia mahakama kwamba hakuwa amefanya mauaji na kama wanabisha walete shahidi kitu ambacho ingekuwa ngumu kwa Benjamin na watu wake kufanya hivyo.
Upande wa pili ulikuwa ni kilio tu, taarifa zilianza kusambaa kwamba David alikuwa ameuawa, hakukuwa na siri tena, kwa Benjamin, tayari alikata tamaa, muda wote alionekana kuwa na huzuni tele kwani kwa namna moja au nyingine lazima mahakama ingemhukumu kifo au hata kufungwa kifungo cha maisha gerezani.
Alizungumza na mwanasheria wake, Donald na kumwambia wazi kwamba alikuwa na hofu moyoni mwake, kama ilivyokuwa kwa Benjamin, hata kwa Donald ilikuwa hivyohivyo kwani aliamini kwamba David aliuawa lakini napo ilikuwa ngumu kusema kwamba Bwana Seppy ndiye alikuwa amehusika kwani wangeulizwa kama wana ushahidi kitu ambacho kingewapa wakati mgumu.
“Kwa hiyo tufanye nini?” aliulizaDonald.
“Duh! Yaani siwezi kuamini kama David ameuawa, na FBI wanasemaje?” aliuliza Benjamin huku akionekana kuchanganyikiwa.
“Wamejaribu kumtafuta...”
“Ikawaje?”
“Nao wakamkosa.”
“Hata mwili wake?”
“Nao wameukosa pia,” alijibu Donald.
Benjamin akaona huo ndiyo mwisho wake, alipoambiwa hivyo na Donald, hakutaka kuendelea kuzungumza naye, akaomba kuondoka kwani kichwa chake kilichanganyikiwa mno.
Siku hiyo haikuwa nzuri katika maisha yake, alipagawa kwa sababu mtu pekee ambaye alibaki, aliyekuwa tegemeo lake alikuwa David tu ambaye mpaka muda huo tetesi zilisema kwamba aliuawa kwani hakuwepo nyumbani na wala hakuonekana sehemu yoyote ile.
“Mungu nisaidie!” alisema Benjamin huku akiwa amepiga magoti, alionekana kukata tamaa kwa asilimia mia moja.
****
Siku hazikumsubiri mtu, ziliendelea kukatika, Moyo wa Benjamin ulikuwa kwenye maumivu makali mno hasa baada ya kugundua kwamba mshikaji wake aliyekuwa na ushahirdi wote, David alikuwa amepotea katika mazingira ya kutatanisha.
Hakukaa kimya, aliwaambia wazazi wake juu ya hofu aliyokuwa nayo moyoni mwake, aliwaambia wazi kwamba kila siku alikuwa mtu wa mawazo na hakujua kama ingetokea siku yoyote ile angeweza kupata furaha aliyokuwa nayo kabla kama tu huyo David asingepatikana.
“I don’t know what I should do but the world must know that I killed nobody,” (Sijui ninachotakiwa kufanya lakini lazima dunia ijue sijamuua mtu yeyote yule) alisema Benjamin huku akiwa ameuinamisha uso wake.
“Everybody knows you killed nobody, but we have to look for the evidence to set you free,” (Kila mtu anajua hujamuua mtu yeyote yule lakini ni lazima tuutafute ushahidi) alisema baba yake.
“Nobody knows where David is by now, they killed him, why? When I come back, I’ve to tell the world about what happened although David disappeared” (Hakuna anayejua mahali David alipo kwa sasa, watakuwa wamemuua, kwa nini? Nitakaporudi, nitatakiwa kuiambia dunia kila kitu kilichotokea hata kama David amepotea) alisema Benjamin huku machozi yakianza kumtoka.
Hakukuwa na kilichobadilika, bado Benjamin alitakiwa kukaa jela mpaka pale ambapo angeitwa tena mahakamani. Ushahidi mwingine ukakusanywa na hivyo kilichokuwa kikitakiwa ni siku ya mahakama ifike na kila kitu kuwekwa wazi.
Siku ilipofika, tayari watu wengi walikwishakusanyika ndani ya mahakama hiyo. Hali ilikuwa tofauti na kipindi cha nyuma. Watu walibadilika, hawakutaka tena kuona Benjamin akifungwa bali Bwana Seppy ndiye alitakiwa kufungwa kutokana na kile alichokifanya.
Waandishi wa habari walikuwa ndani ya mahakama hiyo, walitaka kuandika kila kitu kilichokuwa kikiendelea. Mwana huo wa 2011, hakukuwa na kesi iliyovuta hisia za watu wengi kama hiyo.
Kila mtu duniani alitegesha masikio yake kusikiliza kile kilichokuwa kikiendelea katika mahakama hiyo huko nchini Marekani. Jaji yuleyule, McRegan ndiye aliyetakiwa kusikiliza kesi hiyo na kutoa hukumu.
Mahakama ilijaza watu, hakukuwa na nafasi ya watu wengine na hata wale waliokuwa wamechelewa ambao walikuwa ni zaidi ya watu elfu kumi walitakiwa kubaki nje na kufuatilia kesi ile kupitia televisheni kubwa iliyowekwa tayari nje ya mahakama hiyo.
Haukupita muda mrefu, basi kubwa lililobeba watuhumiwa likaanza kuingia ndani ya eneo la mahakama hiyo. Waandishi wa habari ambao walikuwa nje wakalisogelea gari hilo na kuanza kulipiga picha.
Basi liliposimama, mahabusu kadhaa wakaanza kuteremka huku wakiwa na pingu mikononi mwao. Miongoni mwa mahabusu hao alikuwa Benjamin na Bwana Seppy ambaye muda wote uso wake ulikuwa na tabasamu pana.
Alichokuwa akifahamu, David alikuwa ameuawa kama alivyoambiwa na Dracula, alijua kwamba Benjamin hakuwa na ushahidi wowote ule ambao ungemuweka matatani.
Aliwapungia watu mikono, watu wengi walikuwa wakimzomea lakini hakuonekana kujali mpaka alipoingia ndani ya mahakama. Watu walitaka kuisikiliza kesi hiyo na hukumu kutolewa siku hiyohiyo, hakukuwa na mtu aliyefika mahali hapo kwa ajili ya kusikiliza kesi nyingine yoyote ile.
Wakati Jaji McRegan anaingia ndani ya mahakama hiyo, watu wote wakasimama kama ishara ya heshima, jaji akatembea mpaka mbele ambapo akakaa katika kiti chake kisha kuwaruhusu watu kukaa kwa kupiga nyundo yake.
Muda wote Benjamin alikuwa amekiinamisha kichwa chake chini, alionekana kuwa na majonzi mazito na muda wote machozi yalikuwa yakimtoka tu. Wakili wake, Donald ndiye aliyekuwa akimsimamia siku hiyo, mbali na huyo, pia kulikuwa na wakili wa upande wa Bwana Seppy, wakili huyu aliitwa Tedd, mwanaume mrefu ambaye muda wote alivalia miwani.
Zilianza kusikiliza kesi nyingine ambazo zilichukua masaa mawili na ndipo Benjamin akatakiwa kupanda kizimbani. Watu walikuwa wakimwangalia tu, alionekana kuwa na maumivu makali moyoni mwake kiasi kwamba hata watu wengine wote wakaanza kumuonea huruma.
“Unaitwa nani?” aliuliza Donald.
“Naitwa Benjamin Saunders.”
“Unajua kwa nini upo hapa?”
“Ndiyo! Ni kwa sababu mahakama inanihusisha na mauaji yaliyotokea,” alijibu Benjamin.
“Mnamo tarehe ishirini mwezi wa sita mwaka jana, kulikuwa na mauaji yaliyotokea, mwanamuziki, Carter Phillip alikutwa amekufa katika chumba kimoja huko Southampton nchini Uingereza, polisi walifanya kazi yao na kugundua kwamba alama zako za vidole zilikutwa katika mwili wa marehemu, na si kwenye mwili tu bali hata katika sehemu nyingine chumbani humo, unalizungumziaje hilo?” alisema Donald na kuuliza swali.
“Kitu cha kwanza ambacho mahakama hii inatakiwa kufahamu ni kwamba sikuwahi kuua katika maisha yangu. Nilimfahamu Carter kama mwanamuziki chipukizi. Mnamo tarehe tano mwezi wa saba nilipokea simu ya kuhitajika sehemu fulani, huko nilipokwenda, nilikutana na Bwana Seppy ambaye alinipa kazi ya kufanya mauaji ya Carter Phillip. Sikujua sababu ila nilimkatalia kwa kuwa sikuwahi kuua,” alisema Benjamin.
“Unahisi kwa nini alikuchukua wewe?”
“Mimi ni mtaalamu wa kompyuta, aliamini kwamba kama ningeifanya kazi yake ingekuwa nyepesi na hata kugundulika ingekuwa ngumu. Kwa kweli nilikataa kabisa,” alisema.
Huo ulikuwa ni muda wa maswali kutoka kwa wakili wake, maswali yake yalikuwa ya kumpa nafasi ya kuelekezea kile kilichokuwa kimetokea, wakili Donald alichukua dakika kumi, alipomaliza maswali yake, akakaa chini na wakili wa Bwana Seppy kusimama.
Je, nini kitaendelea?
Tukutane Jumamosi.
Ahsante sana safari ilikuwa ndefu lakini tulikuwa na Dereva makini Madame "S" tumefika salama barikiwa sana mama.
Sent using Jamii Forums mobile app
Pia nakupa hongera madam kwa hadithi nzuri. Ukiweka nyengine naomba unitag na Mimi.
Sent using Jamii Forums mobile app
Ahsante
Madam S ndiyo maana nakupenda sana Ahsante kwa kumaliza MAUAJI YALIYOJAA UTATA, kwa kweli wengine waige mfano wako ukianzisha riwaya/Hadithi/Simulizi ni mwanzo mwisho Ubarikiwe sana mama
Asante kwa simuliz nzur sanaAsante sana sana sana jaman nimefarijika mno na comment yako, tubarikiwe sote pia