Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 152,998
- 453,945
Madame kashushe basi episode zilizobakia ujue ndio nilikua naanza kuisoma kwa hiza ile penzi lenye mautiaya mamii
Madame kashushe basi episode zilizobakia ujue ndio nilikua naanza kuisoma kwa hiza ile penzi lenye mautiaya mamii
dah ngoja nitulie nizitafte humu humuMadame kashushe basi episode zilizobakia ujue ndio nilikua naanza kuisoma kwa hiza ile penzi lenye mauti
n nzuriNYEMO CHILONGANI
MAUAJI YALIYOJAA UTATA
Sehemu ya Pili.
“You are a killer,” (Wewe ni muuaji)
“No! I am not a killer officer, I am not,” (Hapana! Mimi si muuaji ofisa, mimi si muuaji)
“You killed them, why? Why did you kill them? Why?” (Umewaua, kwa nini? Kwa nini umewaua? Kwa nini?)
“I killed nobody officer,” (sijamuua yeyote ofisa)
Yalikuwa ni mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea ndani ya chumba kimoja katika Kituo Kikuu cha Polisi jijini New York. Ndani ya chumba kile, kulikuwa na kijana mmoja, kwa kumwangalia, alikuwa na miaka isiyozidi ishirini na tano, alikuwa mtu mwenye mchanganyiko wa rangi, mama yake alikuwa Mzungu na baba yake alikuwa mtu mweusi.
Polisi wanne waliovalia makoti makubwa ambayo nyuma yaliandikwa NYPD yaani New York Police Department walikuwa wakifanya naye mahojiano kwa sauti kubwa, walimuuliza maswali na kumwambia kwamba yeye alikuwa muuaji lakini alikataa, alikataa katakata lakini polisi hawakuacha, waliendelea kumwambia kwamba alifanya mauaji.
Polisi hao walizungumza naye kwa zaidi ya dakika arobaini, neno lao lilikuwa lilelile kwamba mtu huyo alikuwa muuaji. Kijana huyo aliyeitwa Benjamin Saunders hakukubali, aliwaambia wazi kwamba hakuwa amemuua mtu yeyote na katika maisha yake hakuwahi kuua hata siku moja.
Polisi hawakuridhika, waliendelea kumwambia hivyohivyo mpaka baada ya dakika kadhaa walipotoka ndani ya chumba hicho. Benjamin alikuwa kimya, pingu zilikuwa mikononi mwake, alilia, kila alipokiangalia kile chumba, moyo wake ulimuuma mno, hakuwahi kufikiria kwamba kuna siku angeitwa ndani ya jumba hilo kubwa la polisi na kuambiwa kwamba aliua.
Wakati akiwa humo huku akilia, mara mlango ukafunguliwa, wanaume wawili waliovalia suti nyeusi wakaingia ndani, mmoja alikuwa na begi dogo, wakachukua viti na kukaa mbele yake.
Hawakuzungumza kitu kwanza, walibaki wakimwangalia kwa muda, waliporidhika, wakachukua vitambulisho vyao na kumuonyeshea Benjamini, walikuwa ni maofisa kutoka katika Shirika la Kijasusi la FBI(Federal Bureau of Investigation).
“Naitwa Brett Phillip,” alisema mwanaume mmoja.
“Naitwa Ryan Cashman,” alisema mwingine na kunyamaza.
Benjamin akawaangalia wanaume hao usoni, walionekana kuwa makini na kazi yao. Walipoona kijana huyo ameangalia vitambulisho vyao na kujiridhisha kwamba wao walikuwa maofisa kutoka FBI, wakavirudisha vitambulisho vyao mifukoni.
“Tunajua kwamba hukuua, tunajua hilo Benjamin,” alisema Brett huku akimwangalia Benjamin usoni.
“Ndiyo! Sijaua, sijawahi kuua, na kamwe sitoua,” alisema Benjamin kwa sauti ya chini huku akijifuta machozi.
“Ila alama zote zinaonyesha kwamba uliua,” alisema Brett.
“Sijajua nini kilitokea ila sijamuua mtu yeyote,” alisema Benjamin.
“Kweli?”
“Ndiyo! Sijamuua yeyote yule.”
Alichokifanya Brett ni kuchukua begi lake aliloingia nalo humo ndani, akalifungua na kutoa karatasi fulani kisha kuiweka mezani huku akimtaka Benjamin aichukue na iangalie.
“Mungu wangu!” alisema Benjamin huku akianza kulia.
“Kweli mpaka hapo unasema hujaua?”
Benjamin akabaki kimya, kile alichokiona kwenye karatasi ile hakuamini, hakujua kitu gani kilitokea, mbele yake aliona giza na kuona maisha yake yakienda kuisha gerezani kama si kuchomwa sindano ya sumu au kunyongwa.
Mdomo wake ulikuwa mzito mno, hakuamini alichokuwa akikiangalia katika karatasi ile, akawaangalia maofisa waliokuwa mbele yake, walionekana kuwa makini na kazi zao, mtazamo waliokuwa wakiutumia kumwangalia Benjamin, ulionyesha walikuwa na uhakika kwamba kijana huyo alikuwa amefanya mauaji waliyokuwa wakimshuku.
“Una lolote la kujitetea kabla hatujakwenda mahakamani?” aliuliza Brett.
“Sikuwahi kufanya mauaji, sijui nini kilitokea...”
“Lakini alama zako zimekutwa kama ushahidi.”
“Najua, ila sijafanya mauaji......ninaanza kukumbuka, ninaweza kuwatajia aliyefanya mauaji haya, ila si mimi. Nakumbuka niliambiwa nifanye mauaji haya, nikakataa, nililazimishwa sana, niliendelea kukataa, nikaambiwa kwamba kama ninakataa, basi kuna mtu atafanya mauaji, baada ya hapo, nitaonekana mimi ndiye nimefanya mauaji. Mungu wangu! Kwanza mchumba wangu Vivian yupo wapi? Walimuua, kwa nini walimuua msichana ninayempenda?” aliuliza Benjamini huku akilia.
Maofisa wale walibaki wakimwangalia, alionekana kukumbuka kitu, kwa jinsi alivyokuwa akijitetea, hata muonekano wake ulionyesha kabisa kwamba hakuwa amefanya mauaji. Kitendo cha kusema kwamba alimfahamu muuaji, kwa maofisa hao kilionekana kuwa nafuu kwao, hicho ndicho kitu walichokuwa wakikihitaji kwani kwa jinsi mauaji yalivyokuwa yamefanyika, ilikuwa ni vigumu kumgundua muuaji.
“Sawa! Sasa muuaji ni nani?” aliuliza Brett huku yeye na mwenzake wakimwangalia Benjamin usoni.
****
Julai 4, 2010
Washington DC
Zaidi ya watu elfu tatu walikuwa wamekusanyika kwa wingi nje ya Ikulu ya Marekani, White House kwa ajili ya kusikiliza hotuba kutoka kwa rais wa nchi hiyo, Barack Obama ambaye ndiye alikuwa akitimiza mwaka wa pili tangu aingie madarakani na kuwa rais wa nchi hiyo.
Watu wote waliokuwa hapo, walikuwa na bendera za nchi yao, waliipenda, waliitukuza na kuiona kuwa na thamani kuliko nchi zote duniani.
Siku hiyo ya kusherehekea Uhuru wa nchi yao tangu mwaka 1776 ambapo George Washington aliuchukua kutoka kwa Waingereza, ndiyo siku ambayo Wamarekani wote duniani huithamini kuliko siku yoyote ile.
Wanafunzi hawakwenda shuleni, wanachuo hawakwenda vyuoni, wafanyakazi hawakwenda kazini, yaani kila mtu alitakiwa kukaa nyumbani kwake, kwa wale waliokuwa mbali na Jiji la Washington, walitakiwa kubaki nyumbani na kuangalia kila kitu kilichokuwa kikiendelea huko kupitia runinga zao ila kwa waliokuwa Washington tena waliokuwa na nafasi, walitakia kufika katika uwanja wa Ikulu ya Marekani, White House.
Miongoni mwa watu wengi waliokuwa katika eneo la uwanja wa Ikulu hiyo alikuwepo kijana msomi kutoka katika Chuo Kikuu cha Harvard, Benjamin Saunders ambaye alibakiza mwaka mmoja kabla ya kuhitimu masomo yake.
Benjamin hakuwa peke yake, alikuwa na mpenzi wake, Vivian ambaye alisafiri kutoka Los Angeles mpaka hapo Washington kwa ajili ya kumsikiliza rais wao mweusi ambaye alitaka kuzungumza na Wamarekani wote duniani.
Kama walivyokuwa wengine, hata na wao walikuwa na bendera za nchi hiyo mikononi mwao. Muda wote walikuwa wakishangilia, walionekana kuwa na furaha mno huku wakati mwingine wakikumbatiana, hakukuwa na kitu kilichowapa furaha kama kuwa wote katika kipindi kama hicho.
Walipendana mno, hakukuwa na kitu ambacho kingeweza kuwatenganisha. Japokuwa walikuwa kwenye mafarakano ya mara kwa mara lakini muda mwingi walionekana kuwa na furaha kana kwamba hakukuwa na kitu kibaya kilichokuwa kikiendelea.
“Tukitoka hapa?” aliuliza Vivian.
“Twende nyumbani!”
“Kwako?”
“Kwani unaogopa nini?”
“Siogopi chochote, ila naweza kuchelewa masomo,” alijibu Vivian.
“Wala usijali, utawahi tu,” alisema Benjamin.
Benjamin alikuwa akisoma katika Chuo Kikuu cha Harvard kilichokuwa jijini Cambridge ndani ya Jimbo la Boston hapohapo nchini Marekani, mbali na kutoka katika familia iliyokuwa na fedha, Benjamin alikuwa na uwezo mkubwa chuoni. Alikuwa akichukua masomo ya uuguzi, ndoto yake kubwa iliyokuwa mbele yake ni kuwa daktari bingwa wa magonjwa ya moyo nchini Marekani.
Hiyo ilikuwa ndoto yake, hakutaka kuiona ikipotea, katika maisha yake, alimuahidi mama yake kwamba kuna siku angekuwa daktari mkubwa wa magonjwa ya moyo nchini Marekani, baba yake alikufa kwa ugonjwa wa moyo, hakutaka kuona watu wengine wakifa na ndiyo maana alisoma sana kufanikisha ndoto hiyo aliyojiwekea.
Mpenzi wake alikuwa akisomea masomo ya uandishi wa habari katika Chuo cha UCLA (University of California, huko Los Angeles). Kama alivyokuwa Benjamin, hata naye Vivian alikuwa na uwezo mkubwa darasani, aliwaongoza wanachuo wenzake na kuonekana kufanya mambo makubwa hapo baadaye kupitia uandishi aliokuwa akiusomea.
“Ngriii...ngriii...ngriii...” ulisikika mlio wa simu ukiita, mbali na kuita, simu hiyo ilikuwa katika mtetemo.
Mlio wa simu hiyo waliusikia kwa mbali kutoka na kelele zilizokuwa mahali hapo lakini baada ya Benjamin kuhisi mtetemo huo kutoka mfukoni mwake, harakaharaka akaichukua simu hiyo.
Alishangaa, haikuwa simu yake lakini aliikuta katika mfuko wa koti lake, si yeye tu aliyeshangaa, hata msichana wake, Vivian alishangaa pia. Walibaki wakiangaliana kwa sekunde kadhaa, hawakujua ni nani aliiweka simu ile katika koti lake na wala hawakujua lengo la huyo mwekaji lilikuwa nini.
“Hiyo simu umeitoa wapi?” aliuliza Vivian.
“Sijui, ndiyo kwanza nimeikuta mfukoni mwangu!”
“Nani amekuwekea?”
“Sijui pia.”
“Hebu pokea.”
Alichokifanya Benjamin ni kuipokea simu ile na kuita. Japokuwa mtu wa upande wa pili alikuwa akizungumza lakini Benjamin hakuweza kumsikia kutokana na kelele zilizokuwa mahali pale.
Wakati akiwa na simu hiyo sikioni, mara wanaume wawili waliovalia suti wakamsogelea, wakaanza kumwangalia na kumshika mkono huku wakimtaka wamfuate.
“Kuna nini?”
“Wewe twende tu,” alisema mwanaume mmoja, Benjamin hakuwa na wasiwasi, akaanza kuwafuata kama alivyoambiwa, hata Vivian naye hakutaka kubaki mahali hapo, naye akaanza kuwafuata huku akionekana kuwa na hofu kubwa, kichwa chake kikaanza kujiuliza mambo mengi kuhusu watu wale, walikuwa wakina nani? Akakosa jibu.
JE, nini kitaendelea?
Nilivoona notification ya hii post nkajua mzigo umeingia, kumbe holaAsanteni jaman karibuni kwenye arosto
tulia tu siku ikiwekwa ntaeka kwa kweli na sisi tuko na foleni kama mlivo hapaNilivoona notification ya hii post nkajua mzigo umeingia, kumbe hola
Ha ha haaaa aya mamatulia tu siku ikiwekwa ntaeka kwa kweli na sisi tuko na foleni kama mlivo hapa
Hili arosto sio la Ulimwengu huu aiseeAsanteni jaman karibuni kwenye arosto
NYEMO CHILONGANI