Mauaji yaliyojaa utata

NYEMO CHILONGANI
MAUAJI YALIYOJAA UTATA
Sehemu ya Kumi na Nne.
Benjamin alikuwa akiendesha gari kwa kasi kuwakimbia polisi ambao nao walikuwa wakija nyuma yake, alichanganyikiwa, kitendo cha kukimbizana na polisi barabarani lilikuwa kosa kubwa ambalo lingemfanya kuadhibiwa kwa kupigwa faini au kutumikia kifungo cha miezi sita gerezani.
Ilikuwa ni afadhali kwa kipindi hicho kukimbizwa na polisi hao kuliko kukamatwa na kufikishwa mahakamani. Dunia nzima ilijua kwamba yeye ndiye alikuwa muuaji, hakukuwa na aliyejua lolote kwamba kilichokuwa kimetokea nyuma ni yeye kuyaokoa maisha ya Carter na hata zile alama za vidole vyake, zilikuwa zake ila hakuwahi kuingia ndani ya chumba kile.
Akakanyaga mafuta, gari ile ilikuwa na injini kubwa hivyo aliweza kuwaacha mbali polisi wale, hakutaka kusimama na kujisalimisha, alipoona kwamba inawezekana polisi wale walikuwa wamewasiliana na polisi wengine, akamwambia Vivian kwamba ashikilie usikani.
“NA wewe?” aliuliza msichana huyo.
“Ni lazima niondoke garini, siwezi kuendelea mbele,” alijibu.
“Uondoke?”
“Ndiyo! Vinginevyo nitakamatwa...” alisema Benjamin.
“Unataka kuniacha?”
“Ndiyo! Vivian, unajua ukweli, nataka unisaidie kuiambia dunia ukweli,” alisema Benjamin.
“Sawa! Ila unakwenda wapi?”
“Popote pale, nitajifiicha, sitotaka kuonekana mpaka hapo dunia itakapofahamu ukweli kwamba sikuua,” alisema Benjamin.
Hakukukuwa na muda wa kupoteza, mahali walipokuwa, ilikuwa ni kwenye kijiji cha Hertrown ambacho kilikuwa pembezo mwa Jiji la Boston, barabarani kulizungukwa na miti, sehemu hiyo ilikuwa kama na pori fulani.
Gari likasimamishwa, harakaharaka Benjamin akamsogelea Vivian, akambusu na kisha kuteremka, alichokifanya ni kuingia ndani ya pori lile, Vivian akapiga gia na kuondoka mahali hapo.
Benjamin akaanza kukimbia kwa kasi kubwa, akiwa huko, akasikia king’ora cha polisi, akajua kabisa kwamba tayari gari hilo lilikuwa likipita mahali hapo.
Benjamin akaondoka mpaka katika mlima mmoja mkubwa, huko, kulikuwa na mawe mengi kama milima ya jijini Mwanza, akasimama kwenye kilele na kuanza kuangalia chini, aliliona gari lile alilopanda na Vivian likiwa limesimamishwa na magari matatu ya polisi yaliyokuwa mbele, aliweza kumuona mpenzi wake, Vivian kwa mbali akiwa ameteremka garini na kuongea na polisi waliokuwa wamemsimamisha, hakutaka kusubiri, alichokifanya ni kuanza kushusha mlima ule upande wa pili na kutokomea zake, hakutaka kujua ni kitu gani kilichokuwa kikiendelea huku nyuma.
****
Vivian aliendesha gari lile huku akiwa na maumivu makubwa moyoni mwake, kitendo mcha mpenzi wake, Benjamin kutafutwa kwa kosa la mauaji kilimuumiza sana kwani aliujua ukweli kwamba mpenzi wake hakuhusika katika mauaji hayo bali nyuma ya pazia kulikuwa na watu wengine ambao walihusika.
Hakuendesha gari kwa mwendo wa kasi kama ilivyokuwa kwa Benjamin, aliendelea kusogea mbele mpaka pale alipokutana na magari ya polisi ambapo akapigwa mkono na kuambiwa apaki pembeni, hakubisha, akafanya kama alivyoambiwa.
Polisi wale walipoliangalia gari lile, lilikuwa lilelile waliloambiwa kwamba ndani yake kulikuwa na Benjamin, mwanaume aliyekuwa akitafutwa sana kipindi hicho, wakaingia ndani ya gari na kuanza kupekua kila kona, mtu huyo hakuwepo.
“Benjamin yupo wapi?” aliuliza polisi mmoja.
“Benjamin yupi?”
“Ulikuwa na nani kwenye gari?”
“Peke yangu!”
“Haukuwa na mtu?”
“Hapana!”
Wakati mahojiano yakiendelea, lile gari la polisi lililokuwa likiwakimbiza likafika mahali hapo, moja kwa moja polisi hao wakateremka na kuanza kuelekea kule walipokuwa polisi wenzao na Vivian.
“Alikuwa humu,” alisema mmoja wa polisi waliofika mahali hapo.
“Benjamin alikuwa humu, huyu binti ni lazima atuambie yupo wapi,” alisema polisi mwingine, alikuwa miongoni mwa wale waliofika mahali hapo ambao ndiyo waliokuwa wakiwafukuza.
“Hakukuwa na mtu zaidi yangu!”
“Hapana! Tuambie yupo wapi!”
Japokuwa walimlazimisha Vivian kusema mahali alipokuwa Benjamin lakini msichana huyo hakutaka kuzungumza kitu chochote kile, msimamo wake ulikuwa uleule kwamba hakukuwa na mtu mwingine ndani ya gari lile zaidi yake.
Walichokifanya ni kumchukua na kumpeleka kituoni, walidhani kwamba angebadilisha msimamo wa majibu yake lakini aliendelea kusisitiza kwamba hakukuwa na mtu yeyote ndani ya gari zaidi yake kitu kilichowaweka polisi katika wakati mgumu wa kumpata Benjamin.
****
David hakutaka kutulia, bado mbele yake kulikuwa na kazi kubwa ya kujua yule mtumiaji wa namba iliyokuwa ikitumika kuwasiliana na Benjamin ilikuwa ni ya nani na ilitoka wapi.
Japokuwa simu yake ilichukuliwa lakini data zote za simu ile alikuwa amekwishazituma katika email yake hivyo akaingia na kuanza kuangalia. Alipoipata namba ile, akachukua programu aliyoitengeneza mwenyewe iliyoitwa Davy Hack kisha kuanza kuipekua simu iliyotoka namba ile.
Hukondipo alipopata majibu ya maswali yote aliyokuwa akijiuliza, akakutana na namba nyingi zilizokuwa zikiingia na kutoka ila kitu kilichompa uhakika kwamba mtu aliyekuwa akihusika zaidi alikuwa ni mtu ambaye namba yake inaishia na 69 kwani ndiye mtu aliyekuwa akipiga mara kwa mara.
“Huyu ni nani?” alijiuliza.
Hakutaka kuchelewa, kila swali alilokuwa nalo kichwani mwake ilikuwa ni lazima kupata majibu yake hivyo alichokifanya ni kuanza kuangalia usajili wa namba ile.
Kazi wala haikuwa kubwa, japokuwa watu pekee ambao wangeweza kuangalia namba ya usajili kwa undani zaidi walikuwa ni wale wenye mtandao husika lakini yeye akafanikiwa kwa asilimia mia moja, mtumiaji wa namba hiyo iliyokuwa ikipigwa mara kwa mara katika namba ya simu ya huyo aliyekuwa akimsumbua Benjamin aliitwa David Seppy.
Taarifa hizo hazikuishia hapo, ziliendelea kutoa zaidi taarifa na kuonyesha mahali alipokuwa akiishi, kila kitu kuhusu yeye ambacho hakikuwa na siri yoyote vilionekana.
David akashusha pumzi ndefu, hakuamini kwamba matukio mengi yaliyokuwa yakitokea yalipangwa na mzee huyo. Hakujua tatizo lilikuwa nini, alimfahamu rafiki yake, hakuwa mtu mwenye ugomvi na mtu yeyote, na hakujua kama kulikuwa na ulazima wa Benjamin kufahamiana na mzee huyo kwani walikuwa watu tofauti kabisa, sasa kwa nini kulikuwa kama na ukaribu fulani?
Alichokifanya cha zaidi ni kuangalia meseji zilizokuwa zikiingia na kutoka katika namba hizo mbili. Alipoziona, akashtuka kwani meseji hizo ndizo zilizoonyesha kila kitu kilichokuwa kikiendelea, David akashusha pumzi ndefu, akachoka, hakuamini kama mzee aliyekuwa akiheshimika, David Seppy ndiye aliyekuwa akihusika kwenye mauaji ya Carter, pia, mbali na hivyo, alijipanga kumuua Todd baada ya mwezi mmoja.
****
“Benjamin, niambie ukweli kuhusu hili linaloendelea,” alisema Harry, rafiki mkubwa wa Benjamin.
“Hakuna jipya, sikuhusika kumuua Carter.”
“Una uhakika?”
“Ndiyo!”
“Mbona alama zako za vidole zimeonekana katika mwili wa Carter?” aliuliza Harry.
“Huwezi kuamini Harry, ila jua kwamba sikuhusika na chochote kile,” alisema Benjamin.
“Una uhakika?”
“Ndiyo!”
Benjamin aliamua kufunga safari kuelekea katika Mtaa wa Augestberg uliokuwa hapohapo Boston nchini Marekani. Hakuwa na sehemu nyingine ya kwenda zaidi ya hapo.
Alimwamini sana Harry, alikuwa rafiki yake mkubwa, walikuwa pamoja kila kona katika kipindi walichokuwa chuo. Hakuwa na sehemu nyingine ambayo aliona kustahili kukimbilia zaidi ya hapo, kwa Harry ndipo kulikuwa kila kitu kwa kipindi hicho.
Maneno aliyosema Benjamin bado yalimuweka Harry katika wakati mgumu, hakujua kama alitakiwa kumwamini Benjamin kama kweli hajaua au la, kila alipojiuliza swali hilo, alikosa jibu.
“Kwa hiyo tufanye nini?” aliuliza Harry.
“Nahitaji unisaidie.”
“Nikusaidie nini?”
“Nataka niwe na nawasiliana na David mara kwa mara, kuna kazi nimemwambia anisaidie. Harry, nimechanganyikiwa, sina hatia, sijui ni kwa nini muuaji aliamua kumuua Carter,” alisema Benjamin huku akionekana kuvurugwa kabisa.
Hakuwa na jinsi, kwa sababu alikuwa rafiki yake na alikuwa akikumbana na matatizo mengi, akaamua kuishi naye kwa kumficha, humo alipokuwa, hakutaka hata marafiki zake wengine wafahamu kama Benjamin alikuwa ndani kwake, si hao tu, bali hata mpenzi wake, Shakira naye hakutakiwa ufahamu kitu chochote kile.
Siku ziliendelea kukatika, Benjamin akaamua kuwasiliana na David juu ya mahali alipofikia hasa baada ya kumpa namba ile ambayo alitakiwa kuifuatilia, majibu aliyopewa, hakuyaamini kwamba nyuma ya kila kitu, alikuwepo mzee mwenye utajiri mkubwa nchini Marekani, Bwana David Seppy.
“Unasemaje?” aliuliza Benjamin huku akionekana kushtuka, Harry alikuwa pembeni yake.
“Nimefuatilia mawasiliano, nimegundua hilo, ushahidi upo, tena nikwambie kitu?’ aliuliza David.
“Niambie!”
“Anayefuata ni muigizaji Todd!”
“Unasemaje?”
“Hiyo ndiyo taarifa, kila kitu kinachoendelea kinajionyesha hapa, wanatumiana meseji pasipo kugundua kwamba ninafuatilia kila kitu,” alisema David kwenye simu.
Maneno aliyoyaongea yalikuwa mazito mno, yaliwachanganya wote wawili lakini pia walitaka kufuatilia kama kweli walivyokuwa wamewasiliana kwenye simu, Todd angeuawa kweli au la.
Wote wakabaki kimya, wakaenda pembeni ya chumba hicho na kubaki kimya kabisa. Vichwa vyao vikaanza kuwafikiria watu wawili, Bwana Seppy na Todd.
Kulikuwa na maswali mawili yaliyokuwa yakivitesa vichwa vyao, sababu ya Bwana Seppy kufanya mauaji hayo kwa watu waliopendwa na watu wengi, hawakujua kitu chochote kile.
“Kwa nini?” aliuliza Benjamin.
“Hata mimi najiuliza hilohilo! Kwa nini?”
“Ni lazima tukatoe taarifa polisi,” alisema Benjamin.
“Hapana! Ukifanya hivyo tutakuwa tunakosea,” alisema Harry.
“Kwa nini? La sivyo Todd atakufa, huoni kama itanisaidia hata mimi mwenyewe kuwa huru?” aliuliza Benjamin.
“Una ushahidi kama Bwana Seppy ndiye muuaji?” aliuliza Harry.
“Si David anao!”
“Sawa! Wewe unao?”
“Sina, mpaka David atakaponipa!”
“Nisikilize Ben, hatutakiwi kufanya mambo kwa kukurupuka, ni lazima twende kama wasomi, tukusanye ushahidi wa kutosha, hata kama Todd atauawa, si tatizo kwani kupitia kifo chake tutazidi kujikusanyia ushahidi wa kutosha, tukicheza, hatutoweza kumtia hatihani huyu mtu, tuwe na subira,” alisema Harry.
“Mpaka lini?”
“Sijui! Ila tuwe na subira!”
“Kwa hiyo tuache Todd auawe?”
“Kama inawezekana, tuache, haina jinsi,” alisema Harry, Benjamin akashusha pumzi ndefu.
Kuanzia siku hiyo, hakukuwa na mtu mwenye furaha, wlaimchukia sana Bwana Seppy ambaye mara kwa mara alikuwa mtu wa kuwasaidia watoto yatima na kufungua taasisi zake za kuwasaidia masikini huku nyuma ya pazia akiwa mtu wa matukio ya kikatili.
Hakukuwa na mtu aliyemshtukia, ilikuwa ngumu kugundua kwa sababu muda wote alijifanya kuwa mtu wa watu. Matendo yake maovu aliyaficha kwa kutumia kivuli cha misaada kwa watu masikini na wengine ambao hawakujiweza.
Serikali iliendelea kumwamini huku ikimpa tenda nyingi. Kwa watu watatu, Bwana Seppy alionekana kuwa mtu katili ambaye iliwabidi wamfikishe mahakamani haraka iwezekanavyo.
“Ni lazima huyu mtu ahukumiwe,” alisema Benjamin.
Kuanzia siku hiyo, wala hawakukaa sana, wakapata taarifa ambayo waliitegemea kuisikia siku za karibuni kwamba muigizaji chipukizi aliyekuwa na kipaji cha hali ya juu katika mapigano, Todd Lewis alikutwa akiwa amejiua ndani ya gari lake baada ya kujidunga dawa za kulevya aina ya Cocaine.
Taarifa ziliendelea kusema kwamba mara baada ya polisi kuingia ndani ya gari hilo, pembeni ya mwili wa Todd kulikuwa na fedha za noti, dola, yeni, euro napaundi.
Hawakujua sababu ya Todd kujidunga sindano hiyo, mwili wake ulichukuliwa na kupelekwa katika Hospitali ya Calvary ambapo huko ndipo madaktari pamoja na polisi wangejua ni kitu gani kilichokuwa kimemuua, kama ni madawa ya kulevya peke yake au kulikuwa na kingine.
Je, nini kitaendelea?
 
NYEMO CHILONGANI
MAUAJI YALIYOJAA UTATA

Sehemu ya Pili.

“You are a killer,” (Wewe ni muuaji)
“No! I am not a killer officer, I am not,” (Hapana! Mimi si muuaji ofisa, mimi si muuaji)
“You killed them, why? Why did you kill them? Why?” (Umewaua, kwa nini? Kwa nini umewaua? Kwa nini?)
“I killed nobody officer,” (sijamuua yeyote ofisa)
Yalikuwa ni mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea ndani ya chumba kimoja katika Kituo Kikuu cha Polisi jijini New York. Ndani ya chumba kile, kulikuwa na kijana mmoja, kwa kumwangalia, alikuwa na miaka isiyozidi ishirini na tano, alikuwa mtu mwenye mchanganyiko wa rangi, mama yake alikuwa Mzungu na baba yake alikuwa mtu mweusi.
Polisi wanne waliovalia makoti makubwa ambayo nyuma yaliandikwa NYPD yaani New York Police Department walikuwa wakifanya naye mahojiano kwa sauti kubwa, walimuuliza maswali na kumwambia kwamba yeye alikuwa muuaji lakini alikataa, alikataa katakata lakini polisi hawakuacha, waliendelea kumwambia kwamba alifanya mauaji.
Polisi hao walizungumza naye kwa zaidi ya dakika arobaini, neno lao lilikuwa lilelile kwamba mtu huyo alikuwa muuaji. Kijana huyo aliyeitwa Benjamin Saunders hakukubali, aliwaambia wazi kwamba hakuwa amemuua mtu yeyote na katika maisha yake hakuwahi kuua hata siku moja.
Polisi hawakuridhika, waliendelea kumwambia hivyohivyo mpaka baada ya dakika kadhaa walipotoka ndani ya chumba hicho. Benjamin alikuwa kimya, pingu zilikuwa mikononi mwake, alilia, kila alipokiangalia kile chumba, moyo wake ulimuuma mno, hakuwahi kufikiria kwamba kuna siku angeitwa ndani ya jumba hilo kubwa la polisi na kuambiwa kwamba aliua.
Wakati akiwa humo huku akilia, mara mlango ukafunguliwa, wanaume wawili waliovalia suti nyeusi wakaingia ndani, mmoja alikuwa na begi dogo, wakachukua viti na kukaa mbele yake.
Hawakuzungumza kitu kwanza, walibaki wakimwangalia kwa muda, waliporidhika, wakachukua vitambulisho vyao na kumuonyeshea Benjamini, walikuwa ni maofisa kutoka katika Shirika la Kijasusi la FBI(Federal Bureau of Investigation).
“Naitwa Brett Phillip,” alisema mwanaume mmoja.
“Naitwa Ryan Cashman,” alisema mwingine na kunyamaza.
Benjamin akawaangalia wanaume hao usoni, walionekana kuwa makini na kazi yao. Walipoona kijana huyo ameangalia vitambulisho vyao na kujiridhisha kwamba wao walikuwa maofisa kutoka FBI, wakavirudisha vitambulisho vyao mifukoni.
“Tunajua kwamba hukuua, tunajua hilo Benjamin,” alisema Brett huku akimwangalia Benjamin usoni.
“Ndiyo! Sijaua, sijawahi kuua, na kamwe sitoua,” alisema Benjamin kwa sauti ya chini huku akijifuta machozi.
“Ila alama zote zinaonyesha kwamba uliua,” alisema Brett.
“Sijajua nini kilitokea ila sijamuua mtu yeyote,” alisema Benjamin.
“Kweli?”
“Ndiyo! Sijamuua yeyote yule.”
Alichokifanya Brett ni kuchukua begi lake aliloingia nalo humo ndani, akalifungua na kutoa karatasi fulani kisha kuiweka mezani huku akimtaka Benjamin aichukue na iangalie.
“Mungu wangu!” alisema Benjamin huku akianza kulia.
“Kweli mpaka hapo unasema hujaua?”
Benjamin akabaki kimya, kile alichokiona kwenye karatasi ile hakuamini, hakujua kitu gani kilitokea, mbele yake aliona giza na kuona maisha yake yakienda kuisha gerezani kama si kuchomwa sindano ya sumu au kunyongwa.
Mdomo wake ulikuwa mzito mno, hakuamini alichokuwa akikiangalia katika karatasi ile, akawaangalia maofisa waliokuwa mbele yake, walionekana kuwa makini na kazi zao, mtazamo waliokuwa wakiutumia kumwangalia Benjamin, ulionyesha walikuwa na uhakika kwamba kijana huyo alikuwa amefanya mauaji waliyokuwa wakimshuku.
“Una lolote la kujitetea kabla hatujakwenda mahakamani?” aliuliza Brett.
“Sikuwahi kufanya mauaji, sijui nini kilitokea...”
“Lakini alama zako zimekutwa kama ushahidi.”
“Najua, ila sijafanya mauaji......ninaanza kukumbuka, ninaweza kuwatajia aliyefanya mauaji haya, ila si mimi. Nakumbuka niliambiwa nifanye mauaji haya, nikakataa, nililazimishwa sana, niliendelea kukataa, nikaambiwa kwamba kama ninakataa, basi kuna mtu atafanya mauaji, baada ya hapo, nitaonekana mimi ndiye nimefanya mauaji. Mungu wangu! Kwanza mchumba wangu Vivian yupo wapi? Walimuua, kwa nini walimuua msichana ninayempenda?” aliuliza Benjamini huku akilia.
Maofisa wale walibaki wakimwangalia, alionekana kukumbuka kitu, kwa jinsi alivyokuwa akijitetea, hata muonekano wake ulionyesha kabisa kwamba hakuwa amefanya mauaji. Kitendo cha kusema kwamba alimfahamu muuaji, kwa maofisa hao kilionekana kuwa nafuu kwao, hicho ndicho kitu walichokuwa wakikihitaji kwani kwa jinsi mauaji yalivyokuwa yamefanyika, ilikuwa ni vigumu kumgundua muuaji.
“Sawa! Sasa muuaji ni nani?” aliuliza Brett huku yeye na mwenzake wakimwangalia Benjamin usoni.
****
Julai 4, 2010
Washington DC
Zaidi ya watu elfu tatu walikuwa wamekusanyika kwa wingi nje ya Ikulu ya Marekani, White House kwa ajili ya kusikiliza hotuba kutoka kwa rais wa nchi hiyo, Barack Obama ambaye ndiye alikuwa akitimiza mwaka wa pili tangu aingie madarakani na kuwa rais wa nchi hiyo.
Watu wote waliokuwa hapo, walikuwa na bendera za nchi yao, waliipenda, waliitukuza na kuiona kuwa na thamani kuliko nchi zote duniani.
Siku hiyo ya kusherehekea Uhuru wa nchi yao tangu mwaka 1776 ambapo George Washington aliuchukua kutoka kwa Waingereza, ndiyo siku ambayo Wamarekani wote duniani huithamini kuliko siku yoyote ile.
Wanafunzi hawakwenda shuleni, wanachuo hawakwenda vyuoni, wafanyakazi hawakwenda kazini, yaani kila mtu alitakiwa kukaa nyumbani kwake, kwa wale waliokuwa mbali na Jiji la Washington, walitakiwa kubaki nyumbani na kuangalia kila kitu kilichokuwa kikiendelea huko kupitia runinga zao ila kwa waliokuwa Washington tena waliokuwa na nafasi, walitakia kufika katika uwanja wa Ikulu ya Marekani, White House.
Miongoni mwa watu wengi waliokuwa katika eneo la uwanja wa Ikulu hiyo alikuwepo kijana msomi kutoka katika Chuo Kikuu cha Harvard, Benjamin Saunders ambaye alibakiza mwaka mmoja kabla ya kuhitimu masomo yake.
Benjamin hakuwa peke yake, alikuwa na mpenzi wake, Vivian ambaye alisafiri kutoka Los Angeles mpaka hapo Washington kwa ajili ya kumsikiliza rais wao mweusi ambaye alitaka kuzungumza na Wamarekani wote duniani.
Kama walivyokuwa wengine, hata na wao walikuwa na bendera za nchi hiyo mikononi mwao. Muda wote walikuwa wakishangilia, walionekana kuwa na furaha mno huku wakati mwingine wakikumbatiana, hakukuwa na kitu kilichowapa furaha kama kuwa wote katika kipindi kama hicho.
Walipendana mno, hakukuwa na kitu ambacho kingeweza kuwatenganisha. Japokuwa walikuwa kwenye mafarakano ya mara kwa mara lakini muda mwingi walionekana kuwa na furaha kana kwamba hakukuwa na kitu kibaya kilichokuwa kikiendelea.
“Tukitoka hapa?” aliuliza Vivian.
“Twende nyumbani!”
“Kwako?”
“Kwani unaogopa nini?”
“Siogopi chochote, ila naweza kuchelewa masomo,” alijibu Vivian.
“Wala usijali, utawahi tu,” alisema Benjamin.
Benjamin alikuwa akisoma katika Chuo Kikuu cha Harvard kilichokuwa jijini Cambridge ndani ya Jimbo la Boston hapohapo nchini Marekani, mbali na kutoka katika familia iliyokuwa na fedha, Benjamin alikuwa na uwezo mkubwa chuoni. Alikuwa akichukua masomo ya uuguzi, ndoto yake kubwa iliyokuwa mbele yake ni kuwa daktari bingwa wa magonjwa ya moyo nchini Marekani.
Hiyo ilikuwa ndoto yake, hakutaka kuiona ikipotea, katika maisha yake, alimuahidi mama yake kwamba kuna siku angekuwa daktari mkubwa wa magonjwa ya moyo nchini Marekani, baba yake alikufa kwa ugonjwa wa moyo, hakutaka kuona watu wengine wakifa na ndiyo maana alisoma sana kufanikisha ndoto hiyo aliyojiwekea.
Mpenzi wake alikuwa akisomea masomo ya uandishi wa habari katika Chuo cha UCLA (University of California, huko Los Angeles). Kama alivyokuwa Benjamin, hata naye Vivian alikuwa na uwezo mkubwa darasani, aliwaongoza wanachuo wenzake na kuonekana kufanya mambo makubwa hapo baadaye kupitia uandishi aliokuwa akiusomea.
“Ngriii...ngriii...ngriii...” ulisikika mlio wa simu ukiita, mbali na kuita, simu hiyo ilikuwa katika mtetemo.
Mlio wa simu hiyo waliusikia kwa mbali kutoka na kelele zilizokuwa mahali hapo lakini baada ya Benjamin kuhisi mtetemo huo kutoka mfukoni mwake, harakaharaka akaichukua simu hiyo.
Alishangaa, haikuwa simu yake lakini aliikuta katika mfuko wa koti lake, si yeye tu aliyeshangaa, hata msichana wake, Vivian alishangaa pia. Walibaki wakiangaliana kwa sekunde kadhaa, hawakujua ni nani aliiweka simu ile katika koti lake na wala hawakujua lengo la huyo mwekaji lilikuwa nini.
“Hiyo simu umeitoa wapi?” aliuliza Vivian.
“Sijui, ndiyo kwanza nimeikuta mfukoni mwangu!”
“Nani amekuwekea?”
“Sijui pia.”
“Hebu pokea.”
Alichokifanya Benjamin ni kuipokea simu ile na kuita. Japokuwa mtu wa upande wa pili alikuwa akizungumza lakini Benjamin hakuweza kumsikia kutokana na kelele zilizokuwa mahali pale.
Wakati akiwa na simu hiyo sikioni, mara wanaume wawili waliovalia suti wakamsogelea, wakaanza kumwangalia na kumshika mkono huku wakimtaka wamfuate.
“Kuna nini?”
“Wewe twende tu,” alisema mwanaume mmoja, Benjamin hakuwa na wasiwasi, akaanza kuwafuata kama alivyoambiwa, hata Vivian naye hakutaka kubaki mahali hapo, naye akaanza kuwafuata huku akionekana kuwa na hofu kubwa, kichwa chake kikaanza kujiuliza mambo mengi kuhusu watu wale, walikuwa wakina nani? Akakosa jibu.

JE, nini kitaendelea?
n nzuri
 
Hili arosto sio la Ulimwengu huu aisee

Sent using Jamii Forums mobile app
NYEMO CHILONGANI
MAUAJI YALIYOJAA UTATA
Sehemu ya Kumi na Tano.
Todd Lewis, muigizaji aliyekuwa na jina kubwa duniani alikuwa akitoka katika Uwanja wa Kikapu wa Stapple Center kuangalia mechi ambayo iliwakutanisha wenyewe, La Lakers ikiongozwa na Shaq O’ Neil ambayo ilikuwa ikipambana na Chicago Bulls.
Alikuwa ameamua kusafiri kutoka jijini New York mpaka Los Angeles kwa ajili ya kuangalia mechi hiyo. Alipenda mchezo wa kikapu na hakutaka kabisa kukosa mchezo huo ambao ulikuwa ukizikutanisha timu kongwe, kali ambazo zilikuwa na nguvu mno katika kipindi hicho.
Nje ya uwanja huo, watu wengi walikuwa wakimsubiri, alikuwa na jina kubwa, ukiachana na mastaa wengi wa mchezo wa kikapu, pia siku hiyo Todd alikuwa gumzo kubwa, ndani ya uwanja huo, watu wengi walitaka kupiga naye picha, pale alipokuwa amekaa, watu walimsogelea na kuanza kujifotoa picha kadhaa na mpaka mchezo huo unamalizika, kulikuwa na watu wengi waliopata nafasi ya kupiga naye picha.
Wengine hawakuridhika, hata walipokuwa wakitoka, bado mashabiki walikmfuata Todd, walitaka kupiga naye picha huku wengine wakitaka kusainiwa vitabu vyao.
Hayo yalikuwa maisha ya usupastaa, walimheshimu kwa kuwa aliifanya kazi yake ipasavyo, wengi walipenda kutazama filamu zake, kwa kifupi, Todd aliwavutia watu wengi mno.
Alipomaliza kuwasainia watu vitabu vyao na hata kupiga nao picha, kama kawaida akaifuata gari yake ya kifahari, Ferrari nyekundu na kisha kuingia, kilichofuata ni kuanza safari ya kuelekea hotelini kabla ya kurudi New York alipokuwa akiishi siku inayofuata.
Akaliwasha gari hilo na kuondoka mahali hapo. Moyo wake ulijisikia faraja, hakuamini kwamba mwisho wa siku angekuwa na umaarufu mkubwa kama aliokuwa nao katika kipindi hicho.
Katika kipindi cha nyuma alipokuwa akianza, mambo yalikuwa magumu mno, alipambana usiku na mchana lakini mwisho wa siku, alifanikiwa kuwa kama alivyokuwa, hakukuwa na kitu kingine kilichokuwa kikiendelea zaidi ya kukusanya fedha na kuwa nazo zaidi ya zile alizokuwa nazo.
Wakati safari ikiendelea na kuyakuta makutano ya Barabara za St. Barnaba na Morovian ambayo ilikuwa ikienda mpaka katika Mtaa wa Butterfly uliokuwa umbali kama wa kilometa tatu, akashtuka baada ya kuona gari moja likija kwa kasi nyumba yake, lilikwenda mbele yake kwa mwendo wa kasi na kisha kusimama kwa katikati ya barabara, tena kiubavuubavu.
Kama haukuwa umakini wake mkubwa, basi angeweza kuligonga gari hilo. Kwa ustadi mkubwa, Todd akafunga breki na kisha kusimama, alibaki akihema kwa nguvu, mbele yake ilionekana ajali kubwa ambayo pasipo kutumia uwezo wake basi angeweza kuligonga gari hilo.
Huku akijiuliza ni kitu gani kinaendelea, wanaume wawili wakateremka kutoka kwenye ile gari na kuanza kuelekea kule alipokuwa. Hakujua watu hao walikuwa wakina nani na walihitaji nini kutoka kwake.
Mahali hapohakukuwa na magari, ilikuwa usiku sana na magari hayakuwa yakipita mara kwa mara, hasa katika barabara hiyo ya magari yaendayo kasi. Akashindwa kuliwasha gari lake, watu wale walikwenda kwa kasi mpaka pale lilipokuwa gari lake, wakamwambia afungue mlango vinginevyo wangempiga risasi humohumo.
Hakuwa na jinsi, hakutaka kupinga, kitu cha kwanza kabisa, akashusha kioo cha mbele cha mlango wa upande mwingine, mwanaume mmoja akaingia na kumwamuru aendeshe mpaka sehemu waliyotaka wao waelekee.
“Naomba uniache, kama unataka gari chukua,” alisema Todd huku akitetemeka.
“Unadhani sisi tunataka gari?” aliuliza mwanaume huyo huku akiwa na bastola mkononi mwake.
“Hata kama unataka kiasi chochote cha fedha, nitakupa, naomba uniache...” alisema Todd, tayari machozi yakaanza kububujika mashavuni mwake.
Mwanaume yule mwingine akapita upande wa pili, akaufungua mlango na kumshusha Todd kisha kumpeleka katika gari lao walilokuja nalo huku yule mwingine akiachwa katika gari lile kwa ajili ya kuondoka nalo.
Kila kitu kilichokuwa kikifanyika mahali hapo, kilifanyika kwa haraka sana, tukio zima lilichukua sekunde arobaini na tano tu, tayari wakaondoka huku wakiwa na Todd ndani ya gari.
“Naombeni mniacheee...” alisema Todd.
“Hutakiwi kupiga kelele...” alisema mwanaume mmoja huku akimnyooshea bastola.
“Nimefanya nini? Naombeni msiniue..” alisema Todd.
“Kwani kila anayeuawa kuna baya amelifanya? Hakuna kitu kama hicho, kuwa mpole,” alisema mwanaume huyo.
Baada ya hapo, hawakutaka kuongea kitu chochote kile, wakaondoka naye huku garini wakiwa kimya, kwani hata Todd naye aliyetaka kuzungumza maneno mengi aeleweke na hivyo kuachwa, aliambiwa akae kimya kwani suala la kumuua lisingeweza kuzuilika hata kidogo.
Walikwenda mpaka katika barabara nyingine ya Queen Elizabeth I ambayo ilikuwa ikienda moja kwa moja mpaka kwenye jumba la makumbusho ya Lincoln, hawakufika huko, wakakata kulia na kisha kuchukua barabara nyingine ambayo iliwapeleka mpaka katika sehemu ambayo haikuwa na watu, giza lilitawala, gari likasimamishwa mahali hapo.
“Naomba mnisamehe....”
“Halafu?”
“Niondoke, nitawalipa kiasi cha fedha chochote mnacholkitaka....”
“Halafu?”
“Naomba mnisamehe...”
Hawakutaka kupoteza muda, saa zao zilionyeshwa kwamba tayari ilikuwa ni saa nane za usiku hivyo walitakiwa wafanye haraka, wamuue na kisha kuendelea na mambo yao.
Walichokifanya ni kumkaba kooni, tena kwa nguvu kuhakikisha anakufa na kisha kufanya kile walichoambiwa kukifanya. Mwanaume mmoja mwenye nguvu ndiye aliyetumika kumuua Todd ndani ya gari hilo.
Dracula hakutaka kwenda katika lile gari kwani aliamini kwamba vijana wale wangefanya kama jinsi alivyowapa maagizo, kweli wakafanya. Kilichofuata baada ya kuhakikisha kwamba Todd amekufa ni kumchoma sindano iliyokuwa na madawa aina ya cocaine, walipomaliza, wakachukua nailo zenye unyevuunyevu ambazo kwa kutumia utaalamu wao waliweza kuweka alama za vidole za Benjamin na kisha kuziweka katika shingo ya Todd na sehemu nyingine za mwili.
“Vipi?”
“Tayari!”
“Mbebeni mkamuweke ndani ya gari lake, pia wekeni na hizi fedha,” aliagiza Dracula huku akiwapa noti ambazo zilitakiwa kuwekwa ndani ya gari hilo, vijana wale wakafanya kama walivyoagizwa, wakaubeba mwili wa Todd na kisha kuupeleka garini mwake na kuziweka noti zile.
“Tuondokeni!” alisema Dracula baada ya kumaliza kila kitu. Wakaondoka mahali hapo huku kila mmoja akiwa na furaha ya kukamilisha kazi waliyokuwa wamepewa.
****
Hakukuwa na mtu aliyeamini mara baada ya taarifa juu ya kifo cha Todd zilipotolewa katika vyombo mbalimbali vya habari nchini Marekani. Wengi walipigwa na bumbuwazi, kile walichokisikia, hakikuaminika kwao kwamba yule muigizaji, mwenye jina aliyekuwa akivuma sana kipindi hicho, Todd Lewis alikutwa amejidunga madawa ya kulevya kwakujiovadozi.
Watu wakapigiana simu, kila aliyesikia, hakutaka kukubaliana na habari hiyo kwani miongoni mwa watu waliokuwa wakifanya vizuri kipindi hicho, alikuwa huyo Todd, sasa kwa nini afe mapema hivyo? Tena mbaya zaidi alikutwa akiwa amejiovadozi madawa ya kulevya kitu ambacho kiliwachanganya watu wote kwani Todd hakuwa mtumiaji wa madawa hayo hata mara moja.
Wengi wakaenda katika Hospitali ya Calvary kujionea, huko, watu walikuwa wakilia kwani ndipo walipopata taarifa kamili kwamba muigizaji huyo alikutwa ndani ya gari yake ya kifahari ya Ferrari akiwa amejiovadozi madawa ya kulevya.
“Haiwezekani Bwana! Huyu jamaa hakuwa mlevi kabisa,” alisema jamaa mmoja.
“Ndiyo! Hata mimi nimeshangaa sana, yaani Todd awe mlevi wa madawa ya kulevya! Haiwezekani hata kidogo,” alisikika jamaa mwingine.
Kila mmoja alikuwa sahihi kabisa, hakukuwa na mtu yeyote aliyekuwa na shaka na Todd kwamba alikuwa mtumiaji wa madawa hayo, taarifa hizo zikaendelea kusambaa kila kona mpaka ndani ya saa moja tu, dunia nzima ilijua nini kilitokea nchini Marekani.
Hofu zikaanza kutanda, taarifa zilizosema kwamba ndani ya gari la marehemu kulikutwa noti za fedha kutoka nchi mbalimbali ziliwashtua sana kwani hata siku ambayo Carter alikutwa akiwa amekufa ndani ya chumba cha hoteli, fedha kama hizo zilikutwa kitu kilichowafanya watu kuona cha kawaida ila baada ya fedha hizo kukutwa ndani ya gari hilo, wakagundua kwamba inawezekana hizo fedha zilibeba ujumbe fulani.
“Kama huyu Benjamin ndiye aliyemuua Carter, basi inawezekana akawa amemuua na Todd pia,” alisema jamaa mmoja wakati alipokuwa supamaketi, katika sehemu ya kuuzia magazeti na majarida mbalimbali.
“Inawezekana kabisa...hebu tuwasikilizie polisi tuone watasemaje,” alisema jamaa mwingine.
Hilo ndilo lililokuwa vichwani mwa watu wengi, kila aliyesikia namna gari hilo lilivyokutwa, alikuwa na uhakika kwamba muuaji alikuwa yuleyule, kijana wa chuo mwenye akili nyingi, Benjamin Saunders.
Hilo ndilo lililotokea, baada ya siku mbili, taarifa zikatolewa kwamba alama za vidole vya Benjamin vilikuta katika mwili wa Todd, yaani kabla ya kumchoma sindano, alimkaba kooni na kumuua na ndipo alipofanya mambo mengine likiwepo lile la kumchoma sindano ya madawa ya kulevya ili ionekane kwamba alikuwa amejiovadozi.
Hakukuwa na mtu aliyejua sababu ya Benjamin kuwaua watu maarufu, wengi waliuliza, kwenye mitandao wakatoa maoni yao lakini hakukuwa na mtu aliyefahamu lolote lile juu ya sababu ya Benjamin kuwaua watu maarufu na kisha kuacha noti za fedha mbalimbali karibu na miili yao.
“Ila kwa nini anawaua watu maarufu?’ aliuliza mwanamke mmoja.
“Hata mimi sifahamu! Kwanza nashangaa...”
“Halafu nasikia huyu Benjamin mwenyewe ana akili sana darasani.”
“Hata mimi nimesikia hivyohivyo na watu walipokwenda, wakakuta kweli ana akili sana, inawezekana ndiyo ikawa sababu ya kuwasumbua polisi na wananchi kumtia nguvuni,” alisema jamaa mmoja.
Bado watu walitakiwa kumtafuta Benjamin lakini hakukuwa na yeyote aliyempata, kiasi kikubwa cha fedha zaidi ya dola milioni ishirini na tano ambazo zilikuwa ni zaidi ya bilioni hamsini kilitolewa lakini bado majibu yalikuwa yaleyale kwamba mitaani hakuonekana kabisa.
Maofisa wa FBI walikuwa na kazi kubwa, hakukuwa na aliyeamini kwamba mpaka muda huo Benjamin hakuwa amepatikana. Taarifa zilizopelekwa katika meza ya mkuu wa kitengo chao zilisema kwamba walitakiwa kupewa muda zaidi kwani inawezekana kulikuwa na mtu hatari ambaye alikuwa akimlinda Benjamin ili asiingie katika mikono yao.
“Kwa hiyo tumeshindwa?” aliuliza mkuu wa FBI, Bwana Connery Gibson.
“Hapana!”
“Sasa mbona hapatikani?”
“Ngoja tuendelee nadhani kuna kipindi tutampata tu.”
Hakukuwa na muda mwingine wa kupoteza, kama kusubiri, walisubiri kwa kipindi kirefu lakini hakukuwa na mafanikio yoyote yale, kuna kipindi walijiona kama kushindwa hivyo walitakiwa kuwasiliana na Shirika la Kijasusi la FBI ili wawasaidie kwani huyu Benjamin, japokuwa walijua kwamba hakuwa polisi au mtu yeyote mwenye uwezo wowote wa kijeshi lakini alikuwa mgumu mno kupatikana.
Walichokifanya ni kujiongeza tu, wakawagawa vijana wao katika miji mingine kama Los Angeles, Miami, Texas na sehemu nyingine ili kuhakikisha Benjamin anapatikana haraka iwezekanavyo.
“Nadhani hatotushinda tena, si ndiyo?”
“Tutegemee hilo mkuu!”
****
Harry alichanganyikiwa, hakuamini kile alichokuwa amekiona kwamba muigizaji maarufu duniani kwa kipindi hicho, Todd Lewis aliuawa ndani ya gari lake huku wauaji hao wakitaka kuionyeshea dunia kwamba alijiovadozi madawa ya kulevya kitu ambacho hakikuwa kweli kabisa.
Kilichomchanganya zaidi ni alama za vidole zilizopatikana ndani ya gari lile na hata katika mwili wa Todd ambazo zilionyesha kwamba ni Benjamin ndiye aliyefanya mauaji hayo.
Hapo ndipo alipoamini kwamba Benjamin hakuhusika katika mauaji, kulikuwa na watu wengine waliokuwa wakiyafanya huku wakiweka alama za vidole vyake katika kila tukio walilolifanya.
Alimwangalia Benjamin mara mbilimbili, hakuamini kilichokuwa kimetokea, alimuonea huruma sana kwamba inawezekana vipi mtu auwe na kisha kuweka alama za vidole vyake? Alimuuliza Benjamin lakini mwanaume huyo alimwambia ukweli kwamba hakujua kitu chochote kile.
“Sifahamu!” alisema Benjamin.
“Kuna kitu unajua!”
“Harry! Sifahamu chochote, huyu mzee Seppy ndiye anahusika, yaani ni lazima dunia ijue kwamba yeye ndiye anahusika, vinginevyo, nitahukumiwa kwa mauaji ambayo sikuyafanya,” alisema Benjamin.
“Tutatoa vipi taarifa polisi? Watakukamata!”
Huo ndiyo ulikuwa mtihani mwingine, hawakujua ni kitu gani walitakiwa kufanya, hawakuwa na ushahidi wa kutosha hivyo kama wangekosea sehemu moja basi lingekuwa tatizo kubwa kwao, walitakiwa kujipanga ili hata kama watakwenda kutoa taarifa polisi basi kusiwe na tatizo lolote lile.
David ndiye alikuwa na ushahidi kamili lakini bado kulikuwa na kitu kimoja kilichokuwa kikiwatatiza, kila mauaji yalipotokea, kulikuwa na fedha zilizokuwa zikiachwa, zile fedha zilimaanisha nini? Kila walichojiuliza, walikosa jibu.
“Sijui zinamaanisha nini, ila kama nikipewa muda, nitaweza kufahamu tu, kuna kitu,” alisema Benjamin huku akionekana kama mtu aliyekuwa akijifikiria sana.
“Hili ndilo la msingi, sidhani kama hata FBI watakuwa wanajua maana, huu utakuwa ni ujumbe, ujumbe gani sasa? Hebu tuhangaike mpaka tufahamu,” alisema Harry.
Wote wakakubaliana na kuingia kazini kuhakikisha wanajua kwanza maana ya zile fedha za noti zilizokuwa zikiwekwa katika mauaji yaliyokuwa yakitokea.
Je, nini kitaendelea?
Tukutane Jumamosi
 
19 Reactions
Reply
Back
Top Bottom