Mauaji yaliyojaa utata

NYEMO CHILONGANI
MAUAJI YALIYOJAA UTATA
Sehemu ya Kumi na Mbili.
David alikuwa akitetemeka, kitu alichokuwa akikiona mbele yake kilikuwa kifo tu, hakuamini kama watu wale wangeweza kumuacha kwani walimtaka kusema ukweli juu ya mahali alipokuwa Benjamin, ila hakutaka kusema, alifanya siri kitu kilichowakasirisha wanaume hao.
Bado walimtaka kuzungumza, kusema ukweli juu ya mahali alipokuwa Benjamin lakini bado msisitizo wa David ulikuwa palepale kwamba hakuwa akimfahamu mtu huyo, ndiyo kwanza alimsikia siku hiyo.
Hawakutaka kusubiri zaidi, David alionekana kuwa jeuri hivyo walichoamua ni kummaliza tu. Huku bastola zikiwa zimekokiwa tayari kwa kufyatuliwa, ghafla wakasikia dirisha la kioo likivunjwa, risasi mfululizo zikaanza kupigwa kuelekea ndani humo, tena kwa ustadi mkubwa kabisa.
Wanaume wawili miongoni mwa wale watatu wakaanguka chini, damu zilikuwa zikiwatoka migongoni mwao, walirusharusha miguu na mikono yao, walihangaika katika hatua za mwisho kabla ya kukata pumzi na kufariki dunia.
Mwanaume mmoja, yeye na David ndiyo waliobaki ndani ya nyumba ile, alikuwa na wasiwasi mkubwa, bastola ilikuwa pembeni yake na hata kuichukua, hakudiriki.
Alikuwa akitetemeka muda wote, macho yake yalipotua kwa wenzake ambao walipigwa risasi na kufa, alizidi kuogopa na kuona kwamba muda wowote ule hata yeye mwenyewe pia angeweza kufa.
Wakati wote wawili wakiwa wamelala chini, ghafla mlango ukafunguliwa na maofisa watatu wa FBI kuingia huku wakiwa na bastola zao mikononi mwao, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kuwaweka wote chini ya ulinzi.
“Sijafanya kitu,” alisema David huku akitetemeka, ndiyo kwanza walikuwa wakimfunga pingu.
“Tutajua...”
“Lakini hawa ndiyo walikuja kunivamia,” alisema.
“Tutajua tu, twendeni!”
Wote wakafungwa pingu na kutolewa ndani ya nyumba ile, muda wote David alikuwa akilia, hakuamini kama kweli alifungwa pingu. Watu walioingia walikuwa ni maofisa wa FBI, walijuaje kama alikuwa amevamiwa? Na wale watu waliokuwa wameingia na kumuweka chini ya ulinzi wao, walijuaje kama yeye alikuwa akimfahamu Benjamin? Kila alilojiuliza, alikosa jibu kabisa.
****
Wote wakachukuliwa, wakaingizwa ndani ya gari na safari ya kuelekea katika kituo cha polisi kuanza mara moja. Njia nzima David alionekana kuchanganyikiwa, hakujua kitu gani kilichokuwa kikiendelea, mawazo mengi, maswali yalimtinga lakini yote hayo hayakuwa na majibu yoyote yale.
Walichukua muda wa dakika ishirini ndipo gari lao likaanza kuingia katika jengo ambalo alikuwa na uhakika halikuwa jengo la polisi. Kwa muonekano wake tu, kwa kuliangalia harakahara lilionekana kujengwa kwa ajili ya kazi maalumu, nje hakukuwa na magari, na sehemu hiyo ilionekana kuwa tofauti kabisa na sehemu nyingine.
Hakukuwa na mtu aliyezungumza kitu chochote kile, wakalipeleka gari katika sehemu ya kuegeshea na kisha kuwataka wote wateremke, wakafanya hivyo. Wakawachukua na kwenda nao ndani, huko, wakatenganishwa vyumba, David alipelekwa katika chumba kingine na yule mwanaume mwingine akapelekwa katika chumba kingine.
Huko, David alikuwa akitetemeka, hakujua ni kitu gani kilichowafanya maofisa hao wa FBI kumchukua na kumuingiza ndani ya chumba hicho badala ya kumuacha nyumbani kwake kwa kuwa alikuwa amevamiwa.
Akawekwa mbele ya meza kubwa, kulikuwa na viti viwili chumba kizima, mbele yake kulikuwa na kioo kikubwa, akajua tu kwamba nyuma ya kioo kile kulikuwa na watu waliokuwa wakimwangalia.
Mbali na hivyo, pia kulikuwa na kamera ndogo mbili za CCTV zilizokuwa zimewekwa katika pembe mbili ndani ya chumba hicho. Alikaa huku akionekana kuwa na hofu, akahisi kwamba kulikuwa na jambo zito mbele yake.
Wakati akiwa kwenye mawazo, mara wanaume wawili wakaingia ndani ya chumba hicho, mmoja akakaa katika kiti kimoja na mwingine kusimama huku bastola ndogo aina ya 45 Automatic ikiwa kiunoni mwake.
“Unamfahamu mtu anaitwa Benjamin?” aliuliza ofisa huyo aliyejitambulisha kwa jina la Gregory.
“Hapana!” alijibu.
“Kweli?”
“Ndiyo!”
“David Belshaaz, hatupo hapa kama watu wabaya, unajua dhahiri kwamba tunamtafuta mtu huyo, kwa nini unatuficha, kuna nini? Hutuamini?” aliuliza Gregory.
“Simfahamu! Watu wale walionivamia, walikuja na kuniuliza kuhusu Benjamin, mmewaua, na nyie mnakuja na kuniuliza kuhusu Benjamin, huyu Benjamin ni nani na amefanya nini?’ aliuliza David huku akimkazia macho Gregory.
“Ina maana haumfahamu Benjamin?”
“Ndiyo! Au naweza nikawa namfahamu kwa kumwangalia, ila jina, ni geni kwangu,” alijibu David.
“Una uhakika?”
“Ndiyo ofisa...”
Alijua fika hakuwa na kosa lolote lile, hata kama angekataa kusema mahali alipokuwa Benjamin, asingepigwa wala kuuawa, au hata kutishiwa. Alizungumza kwa kujiamini kwani alijipa uhakika kwamba mahali alipokuwa palikuwa salama kabisa.
“Unamfahamu marehemu Carter?” aliuliza Gregory.
“Ndiyo! Kuna mtu asiyemfahamu mtaalamu wa Pop?”
“Unajua nini kuhusu yeye?”
“Kwamba alikuwa mwanamuziki mkali, labda kingine, alipenda sana kucheza chess,” alijibu David.
“Na kuhusu kifo chake?”
“Nitajua nini kuhusu hilo? Nafuatilia vyombo vya habari, nadhani waandishi watakuwa wanajua zaidi kuliko mimi,” alijibu David.
“Sawa. Naomba simu yako!”
“Ya nini?”
“Hakuna ubaya. Naweza kuipata?”
“Unaweza ukaipata kama ukiniambia ya kazi gani, ila vinginevyo, hautoweza kuipata,” alijibu David.
Gregory akabaki akimwangalia David, kwa namna alivyokuwa akizungumza, alionekana kuwa mtu makini, hakuingiza utani, kila alichokiongea, uso wake ulimaanisha kila sentensi kwamba hakuwa akileta utani hata mara moja.
Gregory akabaki akimshangaa, katika kufanya naye kazi hakuwahi kukutana na mtu aliyekuwa akijiamini kama ilivyokuwa kwa David. Si yeye tu aliyeshangaa bali hata wale waliokuwa wakifuatilia nyuma ya kioo, walishangaa, huyu David alikuwa mtu mwingine kabisa.
“Si kwa lengo baya!”
“Najua ofisa. Naweza kuondoka?”
Gregory akashusha pumzi nzito, akayapeleka macho yake kwa mwenzake aliyekuwa amesimama pembeni, wakapeana ishara fulani, David aliiona ila hakutaka kujali kwani bado akili yake ilimwambia kwamba alikuwa katika mikono salama kabisa.
“Oooh! Samahani ofisa, mlisema kwamba mnaitaka simu yangu, si ndiyo?’ aliuliza David.
“Ndiyo!”
“Mtaweza kuitumia?”
“Ndiyo!”
“Sawa! Naombeni niwape kwa masharti.”
“Yapi?”
“Nikiwapa niondoke zangu, mtaniletea mkishamaliza kazi nayo,” alisema David, maofisa hao wakaangaliana.
“Sawa!”
Alichokifanya David ni kuichukua simu hiyo kutoka mfukoni na kisha kumgawia Gregory ambaye akaipokea huku macho yake yakiwa usoni mwa David.
Maswali mengi yakaanza kumiminika kichwani mwake, kwamba ilikuwaje David atake kumpa simu baada ya kujifikiria kwa muda mrefu lakini pia kumuuliza kama angeweza kuitumia?
Hakupata jibu ila alijua kwamba kwenye kutumia simu hakukuwa na tatizo lolote lile na ndio maana akakubaliana naye. Alipopewa, hakuwa na jinsi, alitakiwa kutekeleza ahadi yake hivyo wakamruhusu kuondoka na kuahidi kumrudishia simu ile pindi watakapomaliza kuitumia.
Kitu cha kwanza kabisa walichotaka kukifanya ni kuipekua simu ile. Haikuwa rahisi kama walivyofikiria, kwanza sehemu ya simu zilizopigwa na kuingia hazikuwa zikionekana. Walishangaa, haikuwa simu ya kawaida, ilionekana kuingizwa programu ambayo hawakuwa wakiifahamu.
Wakaipeleka kwa watu wao wa masuala ya kompyuta (IT), walipowapa ile simu na kuanza kuichezea ili kujua ni simu zipi zilikuwa zimepigwa na kutoka, hawakuweza kuona chochote kile.
Walihitaji muda wa saa moja huku wakiishughulikia simu ile, maofisa wengine wa FBI waliwasubiri zaidi lakini mpaka saa moja linafika, hakukuwa na kilichowezekana, bado majibu yalikuwa yaleyale kwamba simu haikuweza kufunguka sehemu ya simu zilizoingia na kutoka.
Je, nini kitaendelea?
 
NYEMO CHILONGANI
MAUAJI YALIYOJAA UTATA
Sehemu ya Kumi na Tatu.
Ilikuwa ni usiku sana, walikuwa safarini kuondoka walipokuwa wakiishi na kuelekea sehemu ambayo hawakuifahamu. Walembea kwa mwendo wa harakaharaka, hawakutaka kusimama, kila walipoangalia nyuma, walihisi kwamba kulikuwa na watu walikuwa wakiwafuata hivyo ilikuwa ni lazima kukimbia.
Walikwenda mpaka walipofika sehemu iliyokuwa na kituo cha mafuta, kitu walichokihitaji ni chakula, kilipita kipindi fulani hawakuwa wamekula chakula chochote kile, walihisi njaa hivyo ilikuwa ni lazima kununua chakula.
Wakaingia katika supamaketi iliyokuwa katika kituo hicho cha mafuta na kuanza kuzunguka huku na kule kutafuta chakula. Hakukuwa na mteja yeyote, walikuwa wao na muuzaji mwanamke ambaye kila wakati alibaki akimwangalia Benjamin kama mtu aliyekuwa akimfahamu.
Benjamin hakujua hilo, alikuwa bize kuangalia huku na kule, walipomaliza kuchagua vyakula walivyovitaka, wakaenda mpaka katikasehemu ya kulipia tayari kwa kumlipa mwanamke huyo.
“Kuna nini?” aliuliza Benjamin kwa sauti ya chini, alikuwa akimuuliza Vivian.
“Kivipi?”
“Huoni jinsi anavyotuangalia huyu mwanamke?”
“Mmh!”
“Nahisi kuna kitu!”
Wakati wamesimama hapo, mwanamke huyo hakuonekana kuwa na haraka, alikuwa akiwahudumia taratibu huku chini ya meza yake kukiwa na kitufe ambacho kama ungekibonyeza, kilipeleka taarifa katika kituo kidogo cha polisi kilichokuwa karibu na supamaketi hiyo kwamba kulikuwa na kitu kilichokuwa kikiendelea.
Alimfahamu Benjamin, picha yake ilikuwa maarufu hata zaidi ya Gazeti la New York Times na zilibandikwa kona nyingi hapo Marekani. Alikuwa akimchelewa mahali hapo kwa kuwa alijua kwamba tayari polisi walipokea taarifa hivyo wangefika mahali hapo muda wowote ule.
“Tunaweza kuondoka?” aliuliza Benjamin, alimshangaa namna mwanamke huyo alivyokuwa akijichelewsha.
“Subirini kwanza...”
“Tusubiri nini?” aliuliza Vivian, mwanamke huyo hakujibu, aliendelea kujifanya anapanga baadhi ya bidhaa zake, hivyo Benjamin na Vivian wakasubiri pasipo kujua kwamba polisi walikuwa njiani kufika mahali hapo.
Walionekana kukasirika lakini hawakutaka kuondoka, kwa jinsi mwanamke huyo alivyoonekana bize, ilionyesha kuwa hakuwa akifanya kusudi, kweli alikuwa bize.
Huku wakiendelea kuwa mahali hapo, ghafla wakaanza kusikia ving’ora vya gari la polisi likija kule walipokuwa. Kwanza wakashtuka, walipoyapeleka macho yao kwa mwanamke yule, alionekana kabisa kushtuka.
“Umeita polisi?” aliuliza Benjamin.
“Nani?”
“Umeita polisi...umeita polisi wewe...” alisema Benjamin huku akimshika mkono Vivian na kuanza kuondoka naye mahali hapo.
Tayari gari la polisi lilikaribia kabisa karibu na kituo hicho cha mafuta, waliona kabisa kama wangepita kwa kutumia mlango wa mbele ingekuwa rahisi sana kuonekana, hivyo ilikuwa ni lazima waondoke kwa kupitia mlango wa nyuma.
Hakukuwa na muda wa kujifikiria mahali hapo, wakaanza kuondoka kupitia mlango wa nyuma, mwanamke yule akatoka nje, alionekana kuwa na haraka, akaanza kuwahimiza polisi wale wafike haraka mahali hapo kwani mtu waliyekuwa wakimtaka, alikuwa akikimbia.
Baada ya polisi kufika mahali hapo, wakasimamisha gari lao na kisha kuteremka, hawakutaka kuzungumza na mwanamke yule, walichokifanya ni kuingia ndani moja kwa moja, bastola ndogo zilikuwa mikononi mwao, wakaanza kuangalia huku na kule wakimtafuta.
“Yupo wapi?’ aliuliza polisi mmoja huku akiwa makini kuangalia huku na kule.
“Aliondoka kupitia mlango ule,” alisema mwanamke yule, polisi wakaanza kuelekea huko.
Sehemu walipotokea ilikuwa ni stoo, kulikuwa na bidhaa nyingi, hawakutaka kusimama mahali hapo, ilikuwa ni lazima wakimbie, mbele yao kulikuwa na mlango mkubwa wa chuma, wakaufuata na kisha kuufungua.
Sehemu waliyotokea ilikuwa na mifuko mingi iliyokuwa imefungwa, wakapita katikati mpaka walipokutana na mlango mwingine ambapo baada ya kuufungua, wakakutana na gari aina ya Jeep.
“Tuingie garini,” alisema Benjamin huku akilifuata gari hilo.
“Hatuna ufunguo...”
“Wakati mwingine si lazima uwe na ufunguo...” alisema Benjamin huku akikivunja kioo cha gari lile.
Akaingia ndani, akamfungulia mlango Vivian na kuingia ndani. Alichokifanya ni kuifungua sehemu iliyokuwa chini ya usukani na kisha kuanza kuziunganisha nyaya zilizokuwa mahali hapo, tena kwa kasi ya ajabu.
“Fanya haraka....wanakuja...”
“Najitahidi...nipe sekunde tano...” alisema Benjamin huku akizichuna zile nyaya kwa meno yake na kisha kuanza kuziunganisha, yote hiyo ilikuwa ni harakati za kuwasha gari hilo.
Wakati akiendelea kuliwasha lile gari kwa kutumia nyaya kadhaa, polisi wale walikuwa wakikaribia, muda huo nao walikuwa stoo, walikimbia kuelekea kule walipoelekea Benjamin na mpenzi wake, Vivian.
Wakati wameufikia mlango, ghafla wakasikia mlio wa gari likiwa limewashwa, wakati wameufungua mlango huo, wakaliona gari hilo likiondoka kwa kasi mahali hapo, hata mlango mkubwa wa nyuma haukufunguliwa, Benjamin akaufunja mlango huo kwa gari lile na kuanza kuondoka.
“Tuwakimbize, twende garini,” alisema polisi mmoja.
Wakatoka nje, wakalifuata gari lao, wakaingia na kuanza kuondoka kulifuata gari lile ambalo lilikuwa mbali kama mita mia moja na hamsini kwani injini yake ilikuwa na nguvu kubwa.
“Tunahitaji msaada Barabara ya St. Joseph 45W, tumemuona mtuhumiwa wa mauaji, Benjamin, tunahitaji msaada....ova..” alisema polisi mmoja, alikuwa ameshika redio call, mwenzake alikuwa akiendesha gari hilo kwa kasi kubwa.
****
Bwana David Seppy alichanganyikiwa, hakuamini zile taarifa alizokuwa amepewa kwamba vijana wake waliokuwa jijini Washington DC waliuawa huku mmoja akikamatwa na kupelekwa katika kituo cha polisi chini ya maofisa wa FBI.
Hakutaka kuona hilo likitokea, alijua vilivyo jinsi maofisa hao walivyojua kuzungumza na mtu, kumuuliza maswali ya mitego na hatimaye kuwaambia mtu aliyekuwa amewatuma.
Kwa kijana huyo kushikiliwa na FBI lilionekana kuwa jambo bata sana, hakutaka kuona akigundulika kwamba yeye ndiye aliyekuwa akihusika na mauaji yaliyokuwa yakitokea, hivyo ilikuwa ni lazima ahakikishe kijana huyo anauawa.
Akawasiliana na Dracula ambaye naye tayari alifika huko, akampa amri kwamba iwe isiwe ilikuwa ni lazima kijana huyo auawe kwa kuwatumia baadhi ya maofisa waliokuwa ndani ya jengo hilo kumuua kijana huyo kwa kumchoma sindano.
Hilo likachukuliwa na Dracula, akawasiliana na maofisa wawili wa FBI ambao walikuwa upande wao na kuwalipa kiasi kikubwa cha fedha, akawaambia kwamba kijana huyo alitakiwa kuuawa haraka iwezekanavyo, hivyo mishemishe zikaanza.
“Imekuwaje?” aliuliza Bwana Seppy.
“Vijana wanafuatilia, bila shaka watafanikiwa,” alijibu Dracula.
Alikaa na kusubiri, alitaka kujua kama maofisa hao walifanikiwa au la, baada ya saa nne, akapigiwa simu na kupewa taarifa kwamba kijana yule aliyenusurika kuuawa, aliuawa katika chumba kimojawapo katika kituo cha polisi baada ya kuchomwa sindano.
“Safi sana,” alisema Bwana Seppy huku akionekana kuwa na furaha kubwa.
Baada ya wiki moja, akaamua kumuita kijana wake, Dracula na kumpa mpango kabambe uliokuwa mbele yake, alimwambia wazi kwamba alitaka kuzitangaza biashara zake kupitia watu maarufu hivyo mtu ambaye kwa kipindi hicho alikuwa juu ambaye ilikuwa ni lazima kuonana naye, alikuwa muigizaji, kijana mdogo, mwenye uwezo mkubwa, Lewis Todd.
Kumpata Todd halikuwa tatizo hata kidogo kwani kwa sababu mambo ambayo walitakiwa kuzungumza naye yalikuwa ni biashara, wakawasiliana na meneja wake na kumwambia kila kitu kilichokuwa kikiendelea hivyo aliakiwa kuzungumza mtu wake.
“Hakuna tatizo, nitazungumza naye,” alisema meneja huyo, Bwana Oswald Genz.
Genz alikuwa mtu wa fedha, kila alipokaa, kitu alichokifikiria kilikuwa fedha tu. Kulikuwa na madili mengi yaliyokuwa yakija mezani kwake kwa ajili ya mtu wake, hivyo kupewa taarifa kwamba Bwana Seppy alitaka kuingia mkataba wa kufanyiwa matangazo na mwanamuziki aliyekuwa akimsimamia, kwake ilikuwa dili nzuri.
Kitu cha kwanza akawasiliana na Todd na kumwambia kila kitu kilichokuwa kikiendelea, akampa mchakato mzima kuhusu dili hilo ambapo kwa upande wa Todd, hakukuwa na tatizo lolote lile, alitakiwa kurudi kutoka nchini Ukraine na ndipo angesaini mkataba huo.
“Ila walikwambia ni kiasi gani?” aliuliza Todd kwenye simu.
“Hapana!”
“Ni lazima tujue. Bila dola milioni ishirini, hakuna biashara hapo,” alisema Todd.
“Nadhani inaweza kuwa zaidi ya hapo, si unajua jinsi Seppy alivyokuwa na fedha?”
“Ndiyo! Najua hilo! Kama itakuwa ni zaidi, basi hilo ni bonge la dili,” alisema Todd na simu kukatwa.
Baada ya wiki tatu, Todd akafika nchini Marekani, kitu cha kwanza kabisa kukifanya ni kupanga mikakati ya kuonana na Bwana Seppy, mikakati hiyo ikafanyika na ndani ya siku mbili, walikuwa katika hoteli ya kifahari ya Leopard Vile iliyokuwa ikimilikiwa na mzee huyo kwa ajili ya kuingia mkataba.
“Nitakulipa dola milioni tano,” alisema Bwana Seppy.
“Unasemaje?” aliuliza Todd huku akionekana kutokuamini kile alichokisikia.
“Dola milioni tano! Unaonaje?” aliuliza.
Todd akaangaliana na meneja wake, hawakuamini walichokuwa wamekisikia kutoka kwa mzee huyo. Walitegemea kwamba wangepata zaidi ya dola milioni ishirini kutokana na jina kubwa alilokuwa nalo kipindi hicho, sasa iweje apewe milioni tano na wakati nyuma yake kulikuwa na watu wengi, waliofanya alichokifanya?
“Haiwezekani,” alisema Todd.
“Kivipi?”
“Bila milioni thelathini, hakuna kinachofanyika,” alisema Todd, alionekana kumaanisha haswa.
“Nisikilize Todd.....”
“Hakuna suala la kusikiliza. Kiasi hicho nilikuwa nikipokea miaka miwili iliyopita, si sasa, kuna watu wengi mno nyuma yangu, kiasi hicho kidogo,” alisema Todd.
Bwana Seppy akakasirika kama kawaida yake, kwake, mtu kukataa kuingia mkataba na yeye, tena kwa fedha alizozitaka yeye ilionekana kuwa dharau kubwa, akabaki akimwangalia kijana huyo, hasira kali iliyomkaba kooni ikamwambia kwamba ilikuwa ni lazima amuue kijana huyo, yaani kama ilivyotokea kwa Carter.
Bwana Seppy alitumia muda huo kumbembeleza Todd akubaliane naye lakini kijana huyo akakataa kabisa kwa kusema kwamba kiasi kilichotolewa, kisingeweza kumfikisha kokote kule kwani mbali na yeye, kulikuwa na watu wengi nyuma yake.
Bwana Seppy hakutaka kuzungumza tena, moyo wake ulimuuma sana kwa kuona kama akilazimishwa kumuua kijana huyo, hivyo alichokifanya ni kuondoka kuelekea nyumbani kwake.
Alikuwa na mawazo mengi, hata mkewe alipomuona, aligundua kwamba mume wake hakuwa sawa kichwani hivyo akamlazimisha kumwambia ukweli lakini akasema kwamba kulikuwa na vitu vidogo vya kibiashara vilivyokuwa vikimsumbua.
“Kweli?” aliuliza mkewe.
“Ndiyo mke wangu! Kichwa changu hakipo saa, biashara zangu zinasumbua sana,” alisema mzee huyo.
Hakutaka kupoteza muda, alichokifanya ni kumwambia Dracula kwamba Todd alitakiwa kuuawa kama kawaida, hakutaka kumuona mtu huyo akiendelea kuishi, alimpa muda wa mwezi mmoja kijana huyo afe.
“Tumuue kwa risasi?” aliuliza Dracula.
“Itagundulika kama ameuawa...” alijibu.
“Au ajali?”
“Napo itagundulika kama ilivyokuwa kwa Princess Diana...”
“Sasa tumuue vipi?”
“Kama ilivyokuwa kwa Carter. Mfanyeni aonekane kama amejidunga madawa ya kulevya, tena iwe ndani ya nyumba yake,” alisema Bwana Seppy.
“Sawa! Tutafanya hivyo mkuu!”
“Tena ni vizuri ikiwa ndani ya gari lake,” alisema Bwana Seppy.
“Ila....”
“Ila nini bosi?”
“Isiwe mwezi huu, acheni mpaka mwezi ujao,” alisema.
“Sawa!”
“Natumaini mtaifanya kazi yangu ipasavyo!”
“Ndiyo mkuu! Hela zitahitajika kuwekwa?”
“Kama kawaida. Kama ilivyokuwa kwa Carter, acha iwe kwa Todd pia, na msisahau kuweka na alama za vidole vya Benjamin,” alisema Bwana Seppy.
“Hakuna tatizo!”
Je, nini kitaendelea?
 
NYEMO CHILONGANI
MAUAJI YALIYOJAA UTATA
Sehemu ya Kumi na Tatu.
Ilikuwa ni usiku sana, walikuwa safarini kuondoka walipokuwa wakiishi na kuelekea sehemu ambayo hawakuifahamu. Walembea kwa mwendo wa harakaharaka, hawakutaka kusimama, kila walipoangalia nyuma, walihisi kwamba kulikuwa na watu walikuwa wakiwafuata hivyo ilikuwa ni lazima kukimbia.
Walikwenda mpaka walipofika sehemu iliyokuwa na kituo cha mafuta, kitu walichokihitaji ni chakula, kilipita kipindi fulani hawakuwa wamekula chakula chochote kile, walihisi njaa hivyo ilikuwa ni lazima kununua chakula.
Wakaingia katika supamaketi iliyokuwa katika kituo hicho cha mafuta na kuanza kuzunguka huku na kule kutafuta chakula. Hakukuwa na mteja yeyote, walikuwa wao na muuzaji mwanamke ambaye kila wakati alibaki akimwangalia Benjamin kama mtu aliyekuwa akimfahamu.
Benjamin hakujua hilo, alikuwa bize kuangalia huku na kule, walipomaliza kuchagua vyakula walivyovitaka, wakaenda mpaka katikasehemu ya kulipia tayari kwa kumlipa mwanamke huyo.
“Kuna nini?” aliuliza Benjamin kwa sauti ya chini, alikuwa akimuuliza Vivian.
“Kivipi?”
“Huoni jinsi anavyotuangalia huyu mwanamke?”
“Mmh!”
“Nahisi kuna kitu!”
Wakati wamesimama hapo, mwanamke huyo hakuonekana kuwa na haraka, alikuwa akiwahudumia taratibu huku chini ya meza yake kukiwa na kitufe ambacho kama ungekibonyeza, kilipeleka taarifa katika kituo kidogo cha polisi kilichokuwa karibu na supamaketi hiyo kwamba kulikuwa na kitu kilichokuwa kikiendelea.
Alimfahamu Benjamin, picha yake ilikuwa maarufu hata zaidi ya Gazeti la New York Times na zilibandikwa kona nyingi hapo Marekani. Alikuwa akimchelewa mahali hapo kwa kuwa alijua kwamba tayari polisi walipokea taarifa hivyo wangefika mahali hapo muda wowote ule.
“Tunaweza kuondoka?” aliuliza Benjamin, alimshangaa namna mwanamke huyo alivyokuwa akijichelewsha.
“Subirini kwanza...”
“Tusubiri nini?” aliuliza Vivian, mwanamke huyo hakujibu, aliendelea kujifanya anapanga baadhi ya bidhaa zake, hivyo Benjamin na Vivian wakasubiri pasipo kujua kwamba polisi walikuwa njiani kufika mahali hapo.
Walionekana kukasirika lakini hawakutaka kuondoka, kwa jinsi mwanamke huyo alivyoonekana bize, ilionyesha kuwa hakuwa akifanya kusudi, kweli alikuwa bize.
Huku wakiendelea kuwa mahali hapo, ghafla wakaanza kusikia ving’ora vya gari la polisi likija kule walipokuwa. Kwanza wakashtuka, walipoyapeleka macho yao kwa mwanamke yule, alionekana kabisa kushtuka.
“Umeita polisi?” aliuliza Benjamin.
“Nani?”
“Umeita polisi...umeita polisi wewe...” alisema Benjamin huku akimshika mkono Vivian na kuanza kuondoka naye mahali hapo.
Tayari gari la polisi lilikaribia kabisa karibu na kituo hicho cha mafuta, waliona kabisa kama wangepita kwa kutumia mlango wa mbele ingekuwa rahisi sana kuonekana, hivyo ilikuwa ni lazima waondoke kwa kupitia mlango wa nyuma.
Hakukuwa na muda wa kujifikiria mahali hapo, wakaanza kuondoka kupitia mlango wa nyuma, mwanamke yule akatoka nje, alionekana kuwa na haraka, akaanza kuwahimiza polisi wale wafike haraka mahali hapo kwani mtu waliyekuwa wakimtaka, alikuwa akikimbia.
Baada ya polisi kufika mahali hapo, wakasimamisha gari lao na kisha kuteremka, hawakutaka kuzungumza na mwanamke yule, walichokifanya ni kuingia ndani moja kwa moja, bastola ndogo zilikuwa mikononi mwao, wakaanza kuangalia huku na kule wakimtafuta.
“Yupo wapi?’ aliuliza polisi mmoja huku akiwa makini kuangalia huku na kule.
“Aliondoka kupitia mlango ule,” alisema mwanamke yule, polisi wakaanza kuelekea huko.
Sehemu walipotokea ilikuwa ni stoo, kulikuwa na bidhaa nyingi, hawakutaka kusimama mahali hapo, ilikuwa ni lazima wakimbie, mbele yao kulikuwa na mlango mkubwa wa chuma, wakaufuata na kisha kuufungua.
Sehemu waliyotokea ilikuwa na mifuko mingi iliyokuwa imefungwa, wakapita katikati mpaka walipokutana na mlango mwingine ambapo baada ya kuufungua, wakakutana na gari aina ya Jeep.
“Tuingie garini,” alisema Benjamin huku akilifuata gari hilo.
“Hatuna ufunguo...”
“Wakati mwingine si lazima uwe na ufunguo...” alisema Benjamin huku akikivunja kioo cha gari lile.
Akaingia ndani, akamfungulia mlango Vivian na kuingia ndani. Alichokifanya ni kuifungua sehemu iliyokuwa chini ya usukani na kisha kuanza kuziunganisha nyaya zilizokuwa mahali hapo, tena kwa kasi ya ajabu.
“Fanya haraka....wanakuja...”
“Najitahidi...nipe sekunde tano...” alisema Benjamin huku akizichuna zile nyaya kwa meno yake na kisha kuanza kuziunganisha, yote hiyo ilikuwa ni harakati za kuwasha gari hilo.
Wakati akiendelea kuliwasha lile gari kwa kutumia nyaya kadhaa, polisi wale walikuwa wakikaribia, muda huo nao walikuwa stoo, walikimbia kuelekea kule walipoelekea Benjamin na mpenzi wake, Vivian.
Wakati wameufikia mlango, ghafla wakasikia mlio wa gari likiwa limewashwa, wakati wameufungua mlango huo, wakaliona gari hilo likiondoka kwa kasi mahali hapo, hata mlango mkubwa wa nyuma haukufunguliwa, Benjamin akaufunja mlango huo kwa gari lile na kuanza kuondoka.
“Tuwakimbize, twende garini,” alisema polisi mmoja.
Wakatoka nje, wakalifuata gari lao, wakaingia na kuanza kuondoka kulifuata gari lile ambalo lilikuwa mbali kama mita mia moja na hamsini kwani injini yake ilikuwa na nguvu kubwa.
“Tunahitaji msaada Barabara ya St. Joseph 45W, tumemuona mtuhumiwa wa mauaji, Benjamin, tunahitaji msaada....ova..” alisema polisi mmoja, alikuwa ameshika redio call, mwenzake alikuwa akiendesha gari hilo kwa kasi kubwa.
****
Bwana David Seppy alichanganyikiwa, hakuamini zile taarifa alizokuwa amepewa kwamba vijana wake waliokuwa jijini Washington DC waliuawa huku mmoja akikamatwa na kupelekwa katika kituo cha polisi chini ya maofisa wa FBI.
Hakutaka kuona hilo likitokea, alijua vilivyo jinsi maofisa hao walivyojua kuzungumza na mtu, kumuuliza maswali ya mitego na hatimaye kuwaambia mtu aliyekuwa amewatuma.
Kwa kijana huyo kushikiliwa na FBI lilionekana kuwa jambo bata sana, hakutaka kuona akigundulika kwamba yeye ndiye aliyekuwa akihusika na mauaji yaliyokuwa yakitokea, hivyo ilikuwa ni lazima ahakikishe kijana huyo anauawa.
Akawasiliana na Dracula ambaye naye tayari alifika huko, akampa amri kwamba iwe isiwe ilikuwa ni lazima kijana huyo auawe kwa kuwatumia baadhi ya maofisa waliokuwa ndani ya jengo hilo kumuua kijana huyo kwa kumchoma sindano.
Hilo likachukuliwa na Dracula, akawasiliana na maofisa wawili wa FBI ambao walikuwa upande wao na kuwalipa kiasi kikubwa cha fedha, akawaambia kwamba kijana huyo alitakiwa kuuawa haraka iwezekanavyo, hivyo mishemishe zikaanza.
“Imekuwaje?” aliuliza Bwana Seppy.
“Vijana wanafuatilia, bila shaka watafanikiwa,” alijibu Dracula.
Alikaa na kusubiri, alitaka kujua kama maofisa hao walifanikiwa au la, baada ya saa nne, akapigiwa simu na kupewa taarifa kwamba kijana yule aliyenusurika kuuawa, aliuawa katika chumba kimojawapo katika kituo cha polisi baada ya kuchomwa sindano.
“Safi sana,” alisema Bwana Seppy huku akionekana kuwa na furaha kubwa.
Baada ya wiki moja, akaamua kumuita kijana wake, Dracula na kumpa mpango kabambe uliokuwa mbele yake, alimwambia wazi kwamba alitaka kuzitangaza biashara zake kupitia watu maarufu hivyo mtu ambaye kwa kipindi hicho alikuwa juu ambaye ilikuwa ni lazima kuonana naye, alikuwa muigizaji, kijana mdogo, mwenye uwezo mkubwa, Lewis Todd.
Kumpata Todd halikuwa tatizo hata kidogo kwani kwa sababu mambo ambayo walitakiwa kuzungumza naye yalikuwa ni biashara, wakawasiliana na meneja wake na kumwambia kila kitu kilichokuwa kikiendelea hivyo aliakiwa kuzungumza mtu wake.
“Hakuna tatizo, nitazungumza naye,” alisema meneja huyo, Bwana Oswald Genz.
Genz alikuwa mtu wa fedha, kila alipokaa, kitu alichokifikiria kilikuwa fedha tu. Kulikuwa na madili mengi yaliyokuwa yakija mezani kwake kwa ajili ya mtu wake, hivyo kupewa taarifa kwamba Bwana Seppy alitaka kuingia mkataba wa kufanyiwa matangazo na mwanamuziki aliyekuwa akimsimamia, kwake ilikuwa dili nzuri.
Kitu cha kwanza akawasiliana na Todd na kumwambia kila kitu kilichokuwa kikiendelea, akampa mchakato mzima kuhusu dili hilo ambapo kwa upande wa Todd, hakukuwa na tatizo lolote lile, alitakiwa kurudi kutoka nchini Ukraine na ndipo angesaini mkataba huo.
“Ila walikwambia ni kiasi gani?” aliuliza Todd kwenye simu.
“Hapana!”
“Ni lazima tujue. Bila dola milioni ishirini, hakuna biashara hapo,” alisema Todd.
“Nadhani inaweza kuwa zaidi ya hapo, si unajua jinsi Seppy alivyokuwa na fedha?”
“Ndiyo! Najua hilo! Kama itakuwa ni zaidi, basi hilo ni bonge la dili,” alisema Todd na simu kukatwa.
Baada ya wiki tatu, Todd akafika nchini Marekani, kitu cha kwanza kabisa kukifanya ni kupanga mikakati ya kuonana na Bwana Seppy, mikakati hiyo ikafanyika na ndani ya siku mbili, walikuwa katika hoteli ya kifahari ya Leopard Vile iliyokuwa ikimilikiwa na mzee huyo kwa ajili ya kuingia mkataba.
“Nitakulipa dola milioni tano,” alisema Bwana Seppy.
“Unasemaje?” aliuliza Todd huku akionekana kutokuamini kile alichokisikia.
“Dola milioni tano! Unaonaje?” aliuliza.
Todd akaangaliana na meneja wake, hawakuamini walichokuwa wamekisikia kutoka kwa mzee huyo. Walitegemea kwamba wangepata zaidi ya dola milioni ishirini kutokana na jina kubwa alilokuwa nalo kipindi hicho, sasa iweje apewe milioni tano na wakati nyuma yake kulikuwa na watu wengi, waliofanya alichokifanya?
“Haiwezekani,” alisema Todd.
“Kivipi?”
“Bila milioni thelathini, hakuna kinachofanyika,” alisema Todd, alionekana kumaanisha haswa.
“Nisikilize Todd.....”
“Hakuna suala la kusikiliza. Kiasi hicho nilikuwa nikipokea miaka miwili iliyopita, si sasa, kuna watu wengi mno nyuma yangu, kiasi hicho kidogo,” alisema Todd.
Bwana Seppy akakasirika kama kawaida yake, kwake, mtu kukataa kuingia mkataba na yeye, tena kwa fedha alizozitaka yeye ilionekana kuwa dharau kubwa, akabaki akimwangalia kijana huyo, hasira kali iliyomkaba kooni ikamwambia kwamba ilikuwa ni lazima amuue kijana huyo, yaani kama ilivyotokea kwa Carter.
Bwana Seppy alitumia muda huo kumbembeleza Todd akubaliane naye lakini kijana huyo akakataa kabisa kwa kusema kwamba kiasi kilichotolewa, kisingeweza kumfikisha kokote kule kwani mbali na yeye, kulikuwa na watu wengi nyuma yake.
Bwana Seppy hakutaka kuzungumza tena, moyo wake ulimuuma sana kwa kuona kama akilazimishwa kumuua kijana huyo, hivyo alichokifanya ni kuondoka kuelekea nyumbani kwake.
Alikuwa na mawazo mengi, hata mkewe alipomuona, aligundua kwamba mume wake hakuwa sawa kichwani hivyo akamlazimisha kumwambia ukweli lakini akasema kwamba kulikuwa na vitu vidogo vya kibiashara vilivyokuwa vikimsumbua.
“Kweli?” aliuliza mkewe.
“Ndiyo mke wangu! Kichwa changu hakipo saa, biashara zangu zinasumbua sana,” alisema mzee huyo.
Hakutaka kupoteza muda, alichokifanya ni kumwambia Dracula kwamba Todd alitakiwa kuuawa kama kawaida, hakutaka kumuona mtu huyo akiendelea kuishi, alimpa muda wa mwezi mmoja kijana huyo afe.
“Tumuue kwa risasi?” aliuliza Dracula.
“Itagundulika kama ameuawa...” alijibu.
“Au ajali?”
“Napo itagundulika kama ilivyokuwa kwa Princess Diana...”
“Sasa tumuue vipi?”
“Kama ilivyokuwa kwa Carter. Mfanyeni aonekane kama amejidunga madawa ya kulevya, tena iwe ndani ya nyumba yake,” alisema Bwana Seppy.
“Sawa! Tutafanya hivyo mkuu!”
“Tena ni vizuri ikiwa ndani ya gari lake,” alisema Bwana Seppy.
“Ila....”
“Ila nini bosi?”
“Isiwe mwezi huu, acheni mpaka mwezi ujao,” alisema.
“Sawa!”
“Natumaini mtaifanya kazi yangu ipasavyo!”
“Ndiyo mkuu! Hela zitahitajika kuwekwa?”
“Kama kawaida. Kama ilivyokuwa kwa Carter, acha iwe kwa Todd pia, na msisahau kuweka na alama za vidole vya Benjamin,” alisema Bwana Seppy.
“Hakuna tatizo!”
Je, nini kitaendelea?
Madame santeeee
 
Back
Top Bottom