Nyota Njema
Senior Member
- Nov 18, 2010
- 148
- 16
Toka kampeni za uchaguzi mkuu wa 2010 zilipoanza, CCM wamekuwa na wakati mgumu wa kuwaaminisha watanzania kuwa bado wana uwezo wa kuendelea kuliongoza Taifa hili kutoka kwenye lindi la umaskini ambao sehemu kubwa ya umaskini huo umesababishwa na sera na uongozi wao mbovu ulioandamana na rushwa, uwezo mdogo wa kiuongozi, wizi, tamaa pamoja na ajira za kufahamiana na kulindana.
Pamoja na udanganyifu mkubwa kwenye uchaguzi huo, CCM imejikuta ikipoteza maeneo mengi muhimu katika nchi kama majiji makubwa na hata baadhi ya sehemu za vijijini. Inafahamika kuwa watu wengi wenye upeo na uelewa mkubwa wa mambo ya kisiasa wanaishi sasa sehemu za mijini, hivyo jambo hili linawasumbua sana viongozi wa chama hiki kinachopoteza mwelekeo na mvuto kwa watanzania.
Katika kujaribu kunusuru kupoteza ushawishi kwenye miji mikubwa, wamejaribu kwa kila njia kuhakikisha wanapata uongozi sehemu hizo ikiwa ni kwa kutumia rushwa kama ilivyo kawaida yao, na pia matumizi ya nguvu kama ilivyotokea Arusha. Lawama za mauaji ya Arusha kwanza zilianza kutupiwa kwa CHADEMA, walipoona jambo hilo halina mshiko kwa watanzania, sasa hivi kosa limerudishwa kwa polisi waliohusika kama alivyonukuliwa Membe. Ukweli bado unafichwa kuhusiana na nani hasa ni kiini cha uhalifu huu mkubwa kwa Taifa.
Ninajojiuliza mara kwa mara kuhusiana na chanzo cha uhalifu huu ni kuwa, kama kamanda wa polisi wa mkoa wa Arusha aliyaruhusu maandamano hayo, na huku akijua kuwa viongozi wa kitaifa wa CHADEMA watayaongoza, je hakumshirikisha IGP na kupata baraka zake kweli? Na kama ni hivyo, ni nini kichosababisha IGP abadili mawazo katika hatua za mwisho kabla ya kuanza maandamano hayo?
Jibu ninalolipata ni kuwa, kwa upande wa polisi makao makuu, jambo hili halikuwa na tatizo lolote, na maandamano waliamini (na ndivyo ingekuwa kama ilivyo tokea wakati wa mazishi jana) yatakuwa ya amani bila uhalifu wowote kutokea, lakini amri ya mwisho ya kuyazuia ilikuwa ya kisiasa na ilitolewa na mwanasiasa mwenye nafasi kubwa serikalini. Mwanasiasa pekee mwenye nguvu hiyo kisheria ni rais wa jamhuri ya muungano ambaye ndiye amri jeshi mkuu wa majeshi yote ya Tanzania. IGP hawezi kupewa amri na Makamba, bali Kikwete mwenyewe hata kama alishauriwa na Makamba!
Wana JF, kinachonishangaza ni kuwa, sisikii mtu yeyote akimzungumzia Kikwete kuhusika na hili, na hii ni hatari sana katika kutafuta chanzo cha suala hili ambalo limeleta kilio kisicho na sababu kwa watanzania wapenda haki, pamoja na wapenda haki wote duniani. Rai yangu ni kuwa Kikwete awajibike kwa tukio hili maana ndiye mhusika wa jambo hili kimantiki, na kama IGP ndiye aliyehusika, basi amwajibishe haraka iwezekanavyo, vinginevyo awajibike mwenyewe! Asipofanya hivyo, umma utawawajibisha wote.
Naomba kuwakilisha.
Pamoja na udanganyifu mkubwa kwenye uchaguzi huo, CCM imejikuta ikipoteza maeneo mengi muhimu katika nchi kama majiji makubwa na hata baadhi ya sehemu za vijijini. Inafahamika kuwa watu wengi wenye upeo na uelewa mkubwa wa mambo ya kisiasa wanaishi sasa sehemu za mijini, hivyo jambo hili linawasumbua sana viongozi wa chama hiki kinachopoteza mwelekeo na mvuto kwa watanzania.
Katika kujaribu kunusuru kupoteza ushawishi kwenye miji mikubwa, wamejaribu kwa kila njia kuhakikisha wanapata uongozi sehemu hizo ikiwa ni kwa kutumia rushwa kama ilivyo kawaida yao, na pia matumizi ya nguvu kama ilivyotokea Arusha. Lawama za mauaji ya Arusha kwanza zilianza kutupiwa kwa CHADEMA, walipoona jambo hilo halina mshiko kwa watanzania, sasa hivi kosa limerudishwa kwa polisi waliohusika kama alivyonukuliwa Membe. Ukweli bado unafichwa kuhusiana na nani hasa ni kiini cha uhalifu huu mkubwa kwa Taifa.
Ninajojiuliza mara kwa mara kuhusiana na chanzo cha uhalifu huu ni kuwa, kama kamanda wa polisi wa mkoa wa Arusha aliyaruhusu maandamano hayo, na huku akijua kuwa viongozi wa kitaifa wa CHADEMA watayaongoza, je hakumshirikisha IGP na kupata baraka zake kweli? Na kama ni hivyo, ni nini kichosababisha IGP abadili mawazo katika hatua za mwisho kabla ya kuanza maandamano hayo?
Jibu ninalolipata ni kuwa, kwa upande wa polisi makao makuu, jambo hili halikuwa na tatizo lolote, na maandamano waliamini (na ndivyo ingekuwa kama ilivyo tokea wakati wa mazishi jana) yatakuwa ya amani bila uhalifu wowote kutokea, lakini amri ya mwisho ya kuyazuia ilikuwa ya kisiasa na ilitolewa na mwanasiasa mwenye nafasi kubwa serikalini. Mwanasiasa pekee mwenye nguvu hiyo kisheria ni rais wa jamhuri ya muungano ambaye ndiye amri jeshi mkuu wa majeshi yote ya Tanzania. IGP hawezi kupewa amri na Makamba, bali Kikwete mwenyewe hata kama alishauriwa na Makamba!
Wana JF, kinachonishangaza ni kuwa, sisikii mtu yeyote akimzungumzia Kikwete kuhusika na hili, na hii ni hatari sana katika kutafuta chanzo cha suala hili ambalo limeleta kilio kisicho na sababu kwa watanzania wapenda haki, pamoja na wapenda haki wote duniani. Rai yangu ni kuwa Kikwete awajibike kwa tukio hili maana ndiye mhusika wa jambo hili kimantiki, na kama IGP ndiye aliyehusika, basi amwajibishe haraka iwezekanavyo, vinginevyo awajibike mwenyewe! Asipofanya hivyo, umma utawawajibisha wote.
Naomba kuwakilisha.