Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 301
Limeibuka wimbi la mauaji ya makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika mazingira yanayoacha shaka kwamba huenda kuna mikono ya kisiasa katika vitendo hivyo.
Wakati wakazi wa Jiji la Mwanza wapo katika simanzi kubwa ya kumpoteza Katibu wa CCM Kata ya Isamilo, Bahati Stephano (49), aliyeuawa kikatili kwa kuchomwa kisu ofisini kwake na mtuhumiwa aliyetambuliwa kwa jina la Jummane Oscar (30),
na baadaye kifo cha mwanamke aliyekuwa ametangaza nia ya kuomba uteuzi wa kugombea ubunge katika jimbo la Busega kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Magu, Mkoa wa Mwanza katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 31, mwaka huu, Nsega Aloyce Ntobi kufariki katika mazingira ya kutatanisha.
Mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Salama A, kata ya Salama wilayani Bunda, Messo Kubuka (46), kupitia CCM naye ameuawa kinyama baada ya kukatwakatwa kwa mapanga na watu wasiojulikana.
Imedaiwa kuwa Mwenyekiti huyo alikutwa na mauti hayo baada ya kutoka katika mkutano wa hadhara wa Mbunge wa Bunda ambaye pia ni Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wasira.
Wakati wakazi wa Jiji la Mwanza wapo katika simanzi kubwa ya kumpoteza Katibu wa CCM Kata ya Isamilo, Bahati Stephano (49), aliyeuawa kikatili kwa kuchomwa kisu ofisini kwake na mtuhumiwa aliyetambuliwa kwa jina la Jummane Oscar (30),
na baadaye kifo cha mwanamke aliyekuwa ametangaza nia ya kuomba uteuzi wa kugombea ubunge katika jimbo la Busega kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Magu, Mkoa wa Mwanza katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 31, mwaka huu, Nsega Aloyce Ntobi kufariki katika mazingira ya kutatanisha.
Mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Salama A, kata ya Salama wilayani Bunda, Messo Kubuka (46), kupitia CCM naye ameuawa kinyama baada ya kukatwakatwa kwa mapanga na watu wasiojulikana.
Imedaiwa kuwa Mwenyekiti huyo alikutwa na mauti hayo baada ya kutoka katika mkutano wa hadhara wa Mbunge wa Bunda ambaye pia ni Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wasira.