MAMA POROJO
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 4,974
- 785
Gazeti na Tanzania Daima la Tarehe 30 Aprili, 2012 liliandika kwamba wafuasi wa CHADEMA 15 wameuawa . Habari hii inaungana na kauli ya JOHN Mnyika kwamba wafuasi 15 wa Chadema wameuawa.
Madai haya yanatisha kwa sababu CCM imetawala muda wote tangu uhuru hatujasikia kuwa ni chama cha wauaji, lakini inatisha zaidi kupata majibu kutoka CCM kwamba mauaji hayo yanafanywa na CHADEMA na kusingizia CCM kwa lengo la kujiimarisha kisiasa na kujenga chuki ya wananchi dhidi ya CCM.
Hizi tuhuma ni nzito si vema kuzisambaza bila kuchukua tahadhari ya kutosha. Kutupiana Tuhuma za mauaji au kuua si nyepesi na haziwezi kutangazwa bila ushahidi wa kutosha. Hadi sasa tuhuma hizi zimetugawanya hapa JF wako wanaoona kuwa hii ni mbinu ya CHADEMA kuongeza umaarufu na wapo wanaosema ni mbinu ya CCM kuwatisha wafuasi wa CHADEMA. Hakuna aliyejaribu japo kwa dots mbili tatu kuthibitisha kauli zake.
My take: Ni wapi tunakoelekea?
Madai haya yanatisha kwa sababu CCM imetawala muda wote tangu uhuru hatujasikia kuwa ni chama cha wauaji, lakini inatisha zaidi kupata majibu kutoka CCM kwamba mauaji hayo yanafanywa na CHADEMA na kusingizia CCM kwa lengo la kujiimarisha kisiasa na kujenga chuki ya wananchi dhidi ya CCM.
Hizi tuhuma ni nzito si vema kuzisambaza bila kuchukua tahadhari ya kutosha. Kutupiana Tuhuma za mauaji au kuua si nyepesi na haziwezi kutangazwa bila ushahidi wa kutosha. Hadi sasa tuhuma hizi zimetugawanya hapa JF wako wanaoona kuwa hii ni mbinu ya CHADEMA kuongeza umaarufu na wapo wanaosema ni mbinu ya CCM kuwatisha wafuasi wa CHADEMA. Hakuna aliyejaribu japo kwa dots mbili tatu kuthibitisha kauli zake.
My take: Ni wapi tunakoelekea?