ZionTZ
JF-Expert Member
- Oct 6, 2009
- 1,283
- 538
Maiti 150 zimetolewa toka kwenye visima vya maji katika mji wa Jos uliopo ukanda wa kati wa Nigeria.
Jumla ya watu 450 wanahofiwa kufariki kufuatia mashambulizi baina ya waislamu na wakristo katika mji huo.
"Hadi sasa tumefanikiwa kuziopoa maiti 150 toka kwenye visima vya maji lakini watu wengine 60 hawajulikani walipo hadi sasa", alisema Umar Baza, mkuu wa kijiji cha Kuru Karama kilichopo karibu na mji wa Jos.
"Hadi sasa tuna miili ya watu 150 waliopatikana toka kwenye visima kuanzia siku ya alhamisi. Tunaendelea kutafuta miili zaidi ya watu kwenye misitu inayotuzunguka".
Umar alisema kuwa watatafuta miili ya watu kwenye misitu kwa kuwa watu wengi waliuliwa walipokimbilia misituni kukimbia mapambano kwenye kijiji cha Kuru Karama.
"Tunaamini kuna maiti nyingi zaidi kwenye visima lakini kutokana na jinsi zilivyoharibika vibaya tumeamua kuvifukia visima vyote kwa michanga", aliongeza Umar.
Serikali ya Nigeria haijatoa idadi kamili ya watu waliofariki kwenye vurugu hizo za kidini ambazo zilianzia kwenye mji wa Jos na kusambaa kwenye miji ya jirani.
Viongozi wa dini na watoa huduma za afya walisema kwamba hadi kufikia jumatano walikuwa wameishahesabu jumla ya maiti 300.
Jumla ya watu 450 wanahofiwa kufariki kufuatia mashambulizi baina ya waislamu na wakristo katika mji huo.
"Hadi sasa tumefanikiwa kuziopoa maiti 150 toka kwenye visima vya maji lakini watu wengine 60 hawajulikani walipo hadi sasa", alisema Umar Baza, mkuu wa kijiji cha Kuru Karama kilichopo karibu na mji wa Jos.
"Hadi sasa tuna miili ya watu 150 waliopatikana toka kwenye visima kuanzia siku ya alhamisi. Tunaendelea kutafuta miili zaidi ya watu kwenye misitu inayotuzunguka".
Umar alisema kuwa watatafuta miili ya watu kwenye misitu kwa kuwa watu wengi waliuliwa walipokimbilia misituni kukimbia mapambano kwenye kijiji cha Kuru Karama.
"Tunaamini kuna maiti nyingi zaidi kwenye visima lakini kutokana na jinsi zilivyoharibika vibaya tumeamua kuvifukia visima vyote kwa michanga", aliongeza Umar.
Serikali ya Nigeria haijatoa idadi kamili ya watu waliofariki kwenye vurugu hizo za kidini ambazo zilianzia kwenye mji wa Jos na kusambaa kwenye miji ya jirani.
Viongozi wa dini na watoa huduma za afya walisema kwamba hadi kufikia jumatano walikuwa wameishahesabu jumla ya maiti 300.