Angepata vidonda walipouwawa watu wasio na hatia Arusha na Tarime labda tungekuwa na IGP mwingine bora kuliko huyu 'bora IGP'. Amechelewa sana kupata kidonda moyoni."hivi ninavyozungumza nina kidonda moyoni mwangu,"
Mkuu wa Jeshi la Polisi, Said Mwema, amesema amesikitishwa na kusononeshwa sana na mauaji ya watu wanne yaliyofanywa hivi karibuni katika mji wa songea na vijana wake askari wa jeshi la polisi, ndiyo maana amepeleka kikosi maalum toka makao makuu ili kubaini ukweli wa hali halisi iliyojiri. Said Mwema, ameyasema hayo hivi punde, wakati alipokutana na kamati ya kudumu ya bunge inayoshughulika na maswala ya ukimwi, inayoongozwa na mhe. Lediana Mng'ong'o.
Akiongea kwa upole na unyenyekevu, hata kabla hajaulizwa, IGP, alifafanua kuwa yeye binafsi ameumizwa sana moyoni mwake na mauaji ya raia wasio na hatia. "hivi ninavyozungumza nina kidonda moyoni mwangu," alisema IGP akisisitiza kuwa, "mimi [said mwema] binafsi ninsingependa kuona hali hii inaendelea."
Kufuatia hali hiyo, mbunge wa Ludewa, mhe. Filikunjombe, alimtaka IGP aombe radhi, kuthibitisha kauli yake kwamba ni kweli ana 'kidonda moyoni' kinachosababishwa na mauaji ya watendaji wake wa chini.
Pamoja na kukubali rai ya Mhe. Filikunjombe, IGP Mwema, amesema askari waliofanya yale mauaji, ikibainika wametumia 'nguvu ya ziada', watachakuliwa hatua za kinidhamu. Na hivyo IGP amewataka wabunge wasubiri ripoti ya uchunguzi.
My take: Ni jambo la busara kwa IGP Mwema kuomba radhi kwa makosa yalosababishwa na askari wake. Huu ni uungwana. Hata hivyo, Mawaziri nao wajifunze kuwajibika kwa makosa ya walio chini yao.
assa von micky said:uzuri wa sinema za bongo ni kama zile za hollywood ,utofauti ni kwamba za bongo zinaongozwa na siasa.....
mkuu wangu Limbani ni kweli wamezoea kuua na huwa hawaombi msamaha lakini juzi wameua ktk jimbo linaloongozwa na mbunge wa CCM na waziri ktk serikali ya JMT. Bila shaka umenipata mkuu wangu.Wameshazoea kuua hao, hana lolote ni unafiki tu!!
ya kama ni kweli basi amefanya vyema ila tume tushachoka nazo kwani huwa kinachojiri baada ya tume kuundwa
Sasa aombe radhi au awajibike kwa kujiuzulu?
Sasa aombe radhi au awajibike kwa kujiuzulu?