Mauaji ya Songea; IGP - Said Mwema aomba radhi

Ludewa

JF-Expert Member
Mar 9, 2009
215
37
Mkuu wa Jeshi la Polisi, Said Mwema, amesema amesikitishwa na kusononeshwa sana na mauaji ya watu wanne yaliyofanywa hivi karibuni katika mji wa songea na vijana wake askari wa jeshi la polisi, ndiyo maana amepeleka kikosi maalum toka makao makuu ili kubaini ukweli wa hali halisi iliyojiri. Said Mwema, ameyasema hayo hivi punde, wakati alipokutana na kamati ya kudumu ya bunge inayoshughulika na maswala ya ukimwi, inayoongozwa na mhe. Lediana Mng'ong'o.

Akiongea kwa upole na unyenyekevu, hata kabla hajaulizwa, IGP, alifafanua kuwa yeye binafsi ameumizwa sana moyoni mwake na mauaji ya raia wasio na hatia. "hivi ninavyozungumza nina kidonda moyoni mwangu," alisema IGP akisisitiza kuwa, "mimi [said mwema] binafsi ninsingependa kuona hali hii inaendelea."

Kufuatia hali hiyo, mbunge wa Ludewa, mhe. Filikunjombe, alimtaka IGP aombe radhi, kuthibitisha kauli yake kwamba ni kweli ana 'kidonda moyoni' kinachosababishwa na mauaji ya watendaji wake wa chini.

Pamoja na kukubali rai ya Mhe. Filikunjombe, IGP Mwema, amesema askari waliofanya yale mauaji, ikibainika wametumia 'nguvu ya ziada', watachakuliwa hatua za kinidhamu. Na hivyo IGP amewataka wabunge wasubiri ripoti ya uchunguzi.

My take: Ni jambo la busara kwa IGP Mwema kuomba radhi kwa makosa yalosababishwa na askari wake. Huu ni uungwana. Hata hivyo, Mawaziri nao wajifunze kuwajibika kwa makosa ya walio chini yao.
 
ya kama ni kweli basi amefanya vyema ila tume tushachoka nazo kwani huwa kinachojiri baada ya tume kuundwa
 
WAMEUA MALA NGAPI NDUGU!! MBONA HAWAKUOMBA MSAMAHA.
but si jambo la kubeza bwana afadhali hata hao polisi wamekamatwa!
 
Inamaana hakupewa taarifa ya machafuko? Na je kwa nini alishindwa kuwazuia askari wake wasiwashambulie raia wasiokuwa na hatia anakuja kuomba radhi ya kinafiki wakati raia wamepoteza maisha yao.
 
mwishowe utaambiwa walifanya hivyo in faith of self-defense. Hili linchi sijuwi lini litakuja pata watu na viongozi wenye akili timamu.
 
Yule RPC wa songea ajiuzuru coz alisema polisi kisheria walikuwa halali.
 
uzuri wa sinema za bongo ni kama zile za hollywood ,utofauti ni kwamba za bongo zinaongozwa na siasa.....
 
wanajamvi sijawahi kona kiongozi mnafiki kama huyu,kwanini asiwaombe radhi wana arusha,mbeya,mwanza,au kwasababu jimbo hilo anatoka gamba mwenzao?
 
Wameshazoea kuua hao, hana lolote ni unafiki tu!!

Kwa nini aliwapa silaha za moto? Polisi pamoja na mkuu wa mkoa waliona shida gani kuwapokea hao waandamanaji na kuwasilikiliza badala ya kumwaga risasi?

Binafsi ili hii apology ya IGP iwe na maana (walau kwa kiasi) ni vema RPC wa mkoa wa Ruvuma akaondolewa haraka. Short of that ni sawa kuwatukana wananchi wa Songea, something which afande Chagonje ameshaanza kwa kuwaita wananchi wa Songea wahuni.
 
Kwa nini aliwapa silaha za moto? Polisi pamoja na mkuu wa mkoa waliona shida gani kuwapokea hao waandamanaji na kuwasilikiliza badala ya kumwaga risasi?

Binafsi ili hii apology ya IGP iwe na maana (walau kwa kiasi) ni vema RPC wa mkoa wa Ruvuma akaondolewa haraka. Short of that ni sawa kuwatukana wananchi wa Songea, something which afande Chagonje ameshaanza kwa kuwaita wananchi wa Songea wahuni.

Askari wanakuwa na silaha za aina zote, all the time, ni wao askari walio kwenye tukio ndo wanaopashwa kutumia busara na kupima uhalali wa matumizi ya silaha husika.
 
Wameshazoea kuua hao, hana lolote ni unafiki tu!!

Kwa nini aliwapa silaha za moto? Polisi pamoja na mkuu wa mkoa waliona shida gani kuwapokea hao waandamanaji na kuwasilikiliza badala ya kumwaga risasi?

Binafsi ili hii apology ya IGP iwe na maana (walau kwa kiasi) ni vema RPC wa mkoa wa Ruvuma akaondolewa haraka. Short of that ni sawa kuwatukana wananchi wa Songea, something which afande Chagonje ameshaanza kwa kuwaita wananchi wa Songea wahuni.
 
Igp ujue umeua watu wenye haki ya kuishi kama ww, je utatubuje hyo dhambi, kuomba msamaha wa aina hyo tu haitoshi
 
Back
Top Bottom