Rwamuhuru
Member
- Dec 22, 2010
- 50
- 0
Ni hali ya kusikitisha na isiyoaminika.
Mwanaume mmoja (jina nimeshindwa kulipata sawia) amefanya tukio la kinyama kwa kuua watoto wake wanne, 2 wa kike na 2 wa kiume kwa kuwanywesha sumu na kisha kuwakatakata kwa mapanga kabla ya yeye mwenyewe kujinyonga kwenye tukio hilo lilotokea jana
Jioni hii nilipita kwenye nyumba ambayo tukio hilo limetokea na inasemekana walikuwa na ugomvi na mkewe na siku ya jana kabla ya kufanya mauaji hayo alimpiga mkewe na kumng'ata kidole mpaka kukatika kisha akamkunja shingo kiasi cha mwanamke kupoteza fahamu kabla ya yeye mwanamke kuzinduka na kuaamua kukimbia na kwenda kijijini kwao.
Baada ya tukio hilo, inasemekana mwanaume aliamua kuwa hatataka kumuona tena huyo mwanamke wala uzao wake na aliamua kwa hasira kwenda kuchukua watoto wake (Mmoja mkubwa yuko darasa la 5 na anaefuatia inasemekana yuko darasa la 1 na wadogo wa mwisho ambao ni mapacha wako shule ya awali) na kuwatoa shule na kurudi nao nyumbani ambapo inaonekana mkubwa alishtuka baada ya kumuona baba yake hayuko vizuri na akaacha ujumbe wa maandishi kuwa kama watakufa basi ni baba yao.
Mnamo majira ya jioni jana inasemekana jamaa aliwawekea sumu watoto wake wote wa4 na kama haitoshi aliwaua wote kwa kuwakata na shoka (kama sio panga) na kisha kuwapanga kwa umri. Baada ya kutekeleza mauaji hayo aliamua kujiua na yeye mwenyewe.
Kilichofanya watu kushtuka ni kitendo cha ng'ombe wa baba muuaji kuonekana wakiranda nje usiku na majirani waliamua kwenda kujua ni nini kinaendelea na walipoona kimya waliamua kuvunja mlango na kuuona mwili wa baba muuaji na kuona nyumba nzima imetapakaa damu na walipoendelea kutafuta walikuta watoto wamewekwa kwenye chumba kingine wakiwa wamepangwa kwa umri
Kwa sasa mili wa watoto na baba yao muuaji iko sehemu ya kuhifadhia maiti na kesho ni mazishi ya watoto hawa.
Hakika ni tukio la kusikitisha na unyama wa hali ya juu dhidi ya watoto hawa wasiokuwa na hati ayoyote
Mwanaume mmoja (jina nimeshindwa kulipata sawia) amefanya tukio la kinyama kwa kuua watoto wake wanne, 2 wa kike na 2 wa kiume kwa kuwanywesha sumu na kisha kuwakatakata kwa mapanga kabla ya yeye mwenyewe kujinyonga kwenye tukio hilo lilotokea jana
Jioni hii nilipita kwenye nyumba ambayo tukio hilo limetokea na inasemekana walikuwa na ugomvi na mkewe na siku ya jana kabla ya kufanya mauaji hayo alimpiga mkewe na kumng'ata kidole mpaka kukatika kisha akamkunja shingo kiasi cha mwanamke kupoteza fahamu kabla ya yeye mwanamke kuzinduka na kuaamua kukimbia na kwenda kijijini kwao.
Baada ya tukio hilo, inasemekana mwanaume aliamua kuwa hatataka kumuona tena huyo mwanamke wala uzao wake na aliamua kwa hasira kwenda kuchukua watoto wake (Mmoja mkubwa yuko darasa la 5 na anaefuatia inasemekana yuko darasa la 1 na wadogo wa mwisho ambao ni mapacha wako shule ya awali) na kuwatoa shule na kurudi nao nyumbani ambapo inaonekana mkubwa alishtuka baada ya kumuona baba yake hayuko vizuri na akaacha ujumbe wa maandishi kuwa kama watakufa basi ni baba yao.
Mnamo majira ya jioni jana inasemekana jamaa aliwawekea sumu watoto wake wote wa4 na kama haitoshi aliwaua wote kwa kuwakata na shoka (kama sio panga) na kisha kuwapanga kwa umri. Baada ya kutekeleza mauaji hayo aliamua kujiua na yeye mwenyewe.
Kilichofanya watu kushtuka ni kitendo cha ng'ombe wa baba muuaji kuonekana wakiranda nje usiku na majirani waliamua kwenda kujua ni nini kinaendelea na walipoona kimya waliamua kuvunja mlango na kuuona mwili wa baba muuaji na kuona nyumba nzima imetapakaa damu na walipoendelea kutafuta walikuta watoto wamewekwa kwenye chumba kingine wakiwa wamepangwa kwa umri
Kwa sasa mili wa watoto na baba yao muuaji iko sehemu ya kuhifadhia maiti na kesho ni mazishi ya watoto hawa.
Hakika ni tukio la kusikitisha na unyama wa hali ya juu dhidi ya watoto hawa wasiokuwa na hati ayoyote