choga mkuu
JF-Expert Member
- Apr 11, 2016
- 283
- 110
Wilaya Mpya ya nyang'hwale mkoani Geita kata ya Kharumwa ,kijiji cha Ikangala ,mtaa Wa Rasi,na Nyamp'hela kumetokea tukio la kinyama ambapo mtu mmoja anayejulikana kwa jina la Samweli aliyekuwa mfanyabiashara hapo kijijini juzi alitekwa na kuuawa kinyama na kisha kuzikwa na watu wasiojulikana.
Tukio hilo limetokea usiku wa juzi ambapo marehemu alipokuwa akielekea nyumbani kwake baada ya kufunga kibanda chake,na hapo kutekwa kwake kulitokea.
Aidha watu watatu walishakiwa kutekeleza unyama huo ambapo nao walikamatwa na kupigwa na wananchi wenye hasira kali kisha kuteketezwa kwa moto hapo jana.
Walioteketezwa kwa moto ni Kulwa Misalaba,Abudu na Neema Msaba wote ni wanakijiji wa Ikangala.
Hata hivyo jeshi la polisi linawashikilia watu kadhaa kufuatia kitendo hicho.
Mkoa Wa Geita umekuwa na matukio mengi ya kinyama hali ambayo inapelekea wananchi kuishi kwa hofu .
Tukio hilo limetokea usiku wa juzi ambapo marehemu alipokuwa akielekea nyumbani kwake baada ya kufunga kibanda chake,na hapo kutekwa kwake kulitokea.
Aidha watu watatu walishakiwa kutekeleza unyama huo ambapo nao walikamatwa na kupigwa na wananchi wenye hasira kali kisha kuteketezwa kwa moto hapo jana.
Walioteketezwa kwa moto ni Kulwa Misalaba,Abudu na Neema Msaba wote ni wanakijiji wa Ikangala.
Hata hivyo jeshi la polisi linawashikilia watu kadhaa kufuatia kitendo hicho.
Mkoa Wa Geita umekuwa na matukio mengi ya kinyama hali ambayo inapelekea wananchi kuishi kwa hofu .