Kudo
JF-Expert Member
- Nov 2, 2017
- 1,809
- 6,081
RIWAYA; MAUAJI YA KIFO
MTUNZI; BAHATI MWAMBA
SIMU;0758573660.
Mwaka 2012
CHAYA-
Kikundi chao kilikuwa na watu wanne. Kikundi hiki kilikuwa na watu wanaopenda kujiongeza, bila kujali matokeo yatakayopatikana baadae. Kwa lugha yao ya utani kambini; kikundi hiki kiliitwa Nanga.
Kikundi hiki kikiwa kimejiondoa kwenye mstari wa mazoezi, kiliingia porini kwa mbwembwe nyingi, kwa nia ya kutafuta maji ya kujipooza koo.
Walikuwa ni vijana waliyokuwa wameamua kutotii amri ya kamanda wa msafara. Amri iliyowataka vijana wote waliyokuwa kozi, kutogawanyika mstarini; wala kutoroka wakiwa katikati ya pori lile kubwa, ambalo walilitumia kufanya mazoezi ya utayari na ulengaji shabaha. Mbali ya kuwa ni pori lenye wanyama wakali,pia lilikuwa ni pori lilioaminika kuwa na jini mla watu.
Wenyeji wa kijiji cha Chaya kilicho wiliyani Manyoni mkoani Singida, walikuwa wametoa tahadhari kwa viongozi wa mafunzo kwa vijana wa jeshi la kujenga taifa, waliyokuwa wamepiga kambi katika pori lile la kutisha, kwa wenyeji wa kijiji cha Chaya.
Kanali Bengo Ndaya aliyekuwa mkuu wa mafunzo rgt 84KJ,aliamua kuwapeleka vijana wa operesheni Nyerere kwenye pori lile, kwa nia ya kuhakikisha vijana wanakuwa na utayari wa kutosha, kukabiliana na aina yoyote ya ugumu, wawapo kwenye uwanja wa vita, au wawapo kwenye maisha ya kawaida wakiwa kama jeshi la akiba.
Vitisho na tahadhari za wenyeji hazikutiliwa mkazo na wakufunzi, wala vitisho vile havikuarifiwa kwa vijana waliokuwa kozi ya wiki sita. Vitisho viliiishia kwa wakufunzi pekee na hawakuonekana kujali.
Wiki mbili ziliisha salama na vijana walionekana kushika vema mafunzo. Wengi walielewa vizuri kile walichofundishwa.
Siku zote palipo na wengi hakukosekani wajanja wajanja. Wajanja ambao hawapendi kushindwa au kuonekana wao ni wa mwisho katika wengi.
Mbali na kutakiwa kuishi pamoja na kufuata amri ya kamanda wa mafunzo, lakini kuliibuka kundi la vijana ambao wao, hawakutaka kufuata amri ya wakufunzi. Vijana hawa waliona ni mateso kukimbia kilomita kumi bila kunywa maji. Waliona ni mateso pale walipozuiwa kunywa maji baada ya kukimbia umbali mrefu.
Vijana hawa walizua tabia ya kutoroka kabla ya kufika kambini, ili wajipatie maji. Siku ya kwanza kutoroka hawakufanikiwa kupata kile walichokitarajia, walirudi kambini wakiwa wamechoka maradufu zaidi, kuliko wale waliotii amri ya kufuata utaratibu wa kanuni za kimazoezi. Lakini wao hawakuona tatizo, badala yake walitamani kurudi tena kwa mara nyingine, kwa lengo la kuhakikisha wanapata chemichemi au kisima cha maji ndani ya pori.
Wahenga walisema ‘mwanakulitafuta, mwanakulipata’. Vijana wanne kati ya kumi wenye nia ya kupata kisima, walijitolea kwenda kukitafuta kisima kwa niaba ya wenzao, huku wakiweka makubaliano ya zamu, endapo wao wangekikosa tena.
Siku hiyo ilikuwa ni siku maalumu kwa zoezi la ulengaji shabaha. Kila mmoja alipewa silaha yake na risasi zake bandia. Kule walikoelekea kwa ajili ya ulengaji, ndiko walitarajia kutorokea baada ya zamu zao za ulengaji kuisha.
Kama walivyopanga, baada ya kumaliza ulengaji shabaha, ilitakiwa waanze safari ya kurudi kambini.
Nao hawakuwa mbali na lengo lao, nafasi ilipopatikana waliishia porini, wakiwa na silaha zao begani, huku vibuyu vya maji vikining’inia kiuononi.
Vijana hawa maarufu kama Nanga, waliongozwa na William Kondo. Wenzake walipenda kumuita Willy Kondo.
Alikuwa ni kijana mrefu na mweusi tii, huku akiwa na kichwa kidogo kilichonyolewa kwa wembe, bila kuacha salia hata kidogo.
Kijana huyu alikuwa na mikono imara huku akiwa na kifua kipana. Alipendwa na watu wengi kwa kuwa mthubutu kila wakati, huku mara chache akigeuka msanii na kuwaburudisha wenzake, wakati wa mapumziko.
Willy alipendwa na wengi kwa ucheshi wake na pia wengi walimpenda kwa kuwa walitamani kuona kichwa kidogo, kikiwa kwenye mwili mpana huku sauti ikiwa nzito kupindukia. Licha ya sauti yake kuwa nzito; aliweza kuimba vizuri na kuigeuza kuwa burudani tosha kwa wenzake.
Kifupi Willy alikuwa ni burudani tosha, wakati u mtazamapo au wakati umsikilizapo.
Lakini mbali na hayo yote; Willy alikuwa ni miongoni mwa vijana wanaopenda kujiongeza, bila kuwaza matokeo ya baadae.
*****
Walitembea umbali wa kilomita nne bila kufanikiwa kukutana na kisima au chemichemi ya maji. Waliona muda unazidi kwenda bila mafanikio, hapo ndipo walipoamua kubadilisha mbinu, mbinu ambayo ilileta kizaazaa kwa vijana wale.
Baada ya kukubaliana kugawanyika, walikubaliana sehemu ya kukutana ndani ya nusu saa baadae.
Willy Kondo alikuwa na bunduki yake mkononi na, ilikuwa na risasi tatu za bandia(blanko). Risasi hizi zilibaki baada ya kuwa amelenga kwa usahihi risasi saba, kati ya kumi alizokuwa amepewa. Baada ya hapo alichezesha kidogo mgongo wa bunduki na risasi hazikutoka tena. Kwa kuwa alilenga kwa usahihi alipewa alama zake na kuruhusiwa kutoka eneo la ulengaji, huku akiingia kwenye orodha ya wapigaji wazuri, watakao jaribiwa tena wakati mwingine, ili kuupima uwezo wao.
Alikuwa anatembea kwa hatua ndefu, huku akijaribu kufuata nyasi fupi zilizonawiri. Kichwani mwake aliamini nyasi zile zilipokea maji karibu, au kuna mto unaopita kwenye mazingira yale.
Alikuwa anatembea kwa kufuata njia za wachunga ng’ombe. Aliamua kufuata njia hizo akiwa na lengo la kukutana na wachungaji, au sehemu ambayo wachungaji walinywesha mifugo yao. Aliendelea kujipa tumaini hilo kwa sababu ya nyasi fupi alizoziona kwenye njia alizopita.
Akiwa ametembea zaidi ya nusu kilomita, alikutana na njia nyingine kutoonekana kutumika mara kwa mara. Njia ile halikuonesha kuwa fupi na haikuonekana kususwa, bali ilipitisha viumbe hai kila wakati.
Alisimama kwa dakika mbili huku akijaribu kutafari ukubwa wa njia ile. Alitizama alikotoka na alitizama aendako.
Kote kulikuwa ni pori na ni ndege pekee walisikika wakiimba kwa furaha, huku wengine wakirukaruka na kumshukuru Mungu kwa uhai aliowapa.
Alijikuta akianza kuwa na wasiwasi bila kutarajia, huku nafsi ikimtuma aifuate njia ile.
Hakujua ni kwa nini aliingiwa na wasiwasi, lakini aliamini kuna kitu hakikuwa sawa kuhusu njia ile.
Kwa nini?
Kwa sababu njia ile ilianzia pale alipokuwa na haikuonekana kuwa na mwanzo upande mwingine, uliyoiunganisha.
Wazo la kuendelea kuifuatilia njia ile ya wachunga ng’ombe liliishia pale. Na likaibuka wazo jipya la kuifuatilia njia ile iliyopitika mara kwa mara.
Aliifuata taratibu huku akijikuta anaongeza umakini bila kupenda. Kadiri alivyoendelea kwenda, ndivyo mapigo yake ya moyo yalivyozidi kudunda kwa kasi, huku miguu yake nayo ikianza kuwa mizito.
Alisimama!.
Alivuta pumzi nyingi na kuziachia taratibu. Alirudia tena mara mbili, kisha alitulia na kusikiliza udundaji wa mapigo yake ya moyo.
Yalidunda kawaida na hata alipojaribu kusogeza mguu, ulienda bila uzito wowote.
Licha ya mwili wake kukubali kuendelea, lakini akili yake ilikuwa inapigana na mambo mawili.
Jambo la kwanza akili yake ilikuwa inakubaliana na mwili wake, kuendelea mbele; lakini wakati huohuo akili yake ilikuwa inapingana na uamuzi wa mwili kukubali kwenda na ilitaka arudi alikotoka mara moja.
Sasa ilibidi akubali kufuata moja kati ya hayo mawili.
Alijikuta akipiga mluzi usio na maana huku mikono yake ikichomoa magazini na kuziangalia zile risasi tatu alizosalia nazo.
Ujasiri ukamvaa na alipiga hatua kusonga mbele, bila kujali matokeo ya mgongano wa nafsi yake.
Lakini siku zote ninge huja yakishatokea. Na endapo Willy angelijua nini maana ya mgongano wa nafsi, asingeliendelea na safari yake, kwenye ile njia ya ajabu.
****
Ungana nami kesho!
MTUNZI; BAHATI MWAMBA
SIMU;0758573660.
Mwaka 2012
CHAYA-
Kikundi chao kilikuwa na watu wanne. Kikundi hiki kilikuwa na watu wanaopenda kujiongeza, bila kujali matokeo yatakayopatikana baadae. Kwa lugha yao ya utani kambini; kikundi hiki kiliitwa Nanga.
Kikundi hiki kikiwa kimejiondoa kwenye mstari wa mazoezi, kiliingia porini kwa mbwembwe nyingi, kwa nia ya kutafuta maji ya kujipooza koo.
Walikuwa ni vijana waliyokuwa wameamua kutotii amri ya kamanda wa msafara. Amri iliyowataka vijana wote waliyokuwa kozi, kutogawanyika mstarini; wala kutoroka wakiwa katikati ya pori lile kubwa, ambalo walilitumia kufanya mazoezi ya utayari na ulengaji shabaha. Mbali ya kuwa ni pori lenye wanyama wakali,pia lilikuwa ni pori lilioaminika kuwa na jini mla watu.
Wenyeji wa kijiji cha Chaya kilicho wiliyani Manyoni mkoani Singida, walikuwa wametoa tahadhari kwa viongozi wa mafunzo kwa vijana wa jeshi la kujenga taifa, waliyokuwa wamepiga kambi katika pori lile la kutisha, kwa wenyeji wa kijiji cha Chaya.
Kanali Bengo Ndaya aliyekuwa mkuu wa mafunzo rgt 84KJ,aliamua kuwapeleka vijana wa operesheni Nyerere kwenye pori lile, kwa nia ya kuhakikisha vijana wanakuwa na utayari wa kutosha, kukabiliana na aina yoyote ya ugumu, wawapo kwenye uwanja wa vita, au wawapo kwenye maisha ya kawaida wakiwa kama jeshi la akiba.
Vitisho na tahadhari za wenyeji hazikutiliwa mkazo na wakufunzi, wala vitisho vile havikuarifiwa kwa vijana waliokuwa kozi ya wiki sita. Vitisho viliiishia kwa wakufunzi pekee na hawakuonekana kujali.
Wiki mbili ziliisha salama na vijana walionekana kushika vema mafunzo. Wengi walielewa vizuri kile walichofundishwa.
Siku zote palipo na wengi hakukosekani wajanja wajanja. Wajanja ambao hawapendi kushindwa au kuonekana wao ni wa mwisho katika wengi.
Mbali na kutakiwa kuishi pamoja na kufuata amri ya kamanda wa mafunzo, lakini kuliibuka kundi la vijana ambao wao, hawakutaka kufuata amri ya wakufunzi. Vijana hawa waliona ni mateso kukimbia kilomita kumi bila kunywa maji. Waliona ni mateso pale walipozuiwa kunywa maji baada ya kukimbia umbali mrefu.
Vijana hawa walizua tabia ya kutoroka kabla ya kufika kambini, ili wajipatie maji. Siku ya kwanza kutoroka hawakufanikiwa kupata kile walichokitarajia, walirudi kambini wakiwa wamechoka maradufu zaidi, kuliko wale waliotii amri ya kufuata utaratibu wa kanuni za kimazoezi. Lakini wao hawakuona tatizo, badala yake walitamani kurudi tena kwa mara nyingine, kwa lengo la kuhakikisha wanapata chemichemi au kisima cha maji ndani ya pori.
Wahenga walisema ‘mwanakulitafuta, mwanakulipata’. Vijana wanne kati ya kumi wenye nia ya kupata kisima, walijitolea kwenda kukitafuta kisima kwa niaba ya wenzao, huku wakiweka makubaliano ya zamu, endapo wao wangekikosa tena.
Siku hiyo ilikuwa ni siku maalumu kwa zoezi la ulengaji shabaha. Kila mmoja alipewa silaha yake na risasi zake bandia. Kule walikoelekea kwa ajili ya ulengaji, ndiko walitarajia kutorokea baada ya zamu zao za ulengaji kuisha.
Kama walivyopanga, baada ya kumaliza ulengaji shabaha, ilitakiwa waanze safari ya kurudi kambini.
Nao hawakuwa mbali na lengo lao, nafasi ilipopatikana waliishia porini, wakiwa na silaha zao begani, huku vibuyu vya maji vikining’inia kiuononi.
Vijana hawa maarufu kama Nanga, waliongozwa na William Kondo. Wenzake walipenda kumuita Willy Kondo.
Alikuwa ni kijana mrefu na mweusi tii, huku akiwa na kichwa kidogo kilichonyolewa kwa wembe, bila kuacha salia hata kidogo.
Kijana huyu alikuwa na mikono imara huku akiwa na kifua kipana. Alipendwa na watu wengi kwa kuwa mthubutu kila wakati, huku mara chache akigeuka msanii na kuwaburudisha wenzake, wakati wa mapumziko.
Willy alipendwa na wengi kwa ucheshi wake na pia wengi walimpenda kwa kuwa walitamani kuona kichwa kidogo, kikiwa kwenye mwili mpana huku sauti ikiwa nzito kupindukia. Licha ya sauti yake kuwa nzito; aliweza kuimba vizuri na kuigeuza kuwa burudani tosha kwa wenzake.
Kifupi Willy alikuwa ni burudani tosha, wakati u mtazamapo au wakati umsikilizapo.
Lakini mbali na hayo yote; Willy alikuwa ni miongoni mwa vijana wanaopenda kujiongeza, bila kuwaza matokeo ya baadae.
*****
Walitembea umbali wa kilomita nne bila kufanikiwa kukutana na kisima au chemichemi ya maji. Waliona muda unazidi kwenda bila mafanikio, hapo ndipo walipoamua kubadilisha mbinu, mbinu ambayo ilileta kizaazaa kwa vijana wale.
Baada ya kukubaliana kugawanyika, walikubaliana sehemu ya kukutana ndani ya nusu saa baadae.
Willy Kondo alikuwa na bunduki yake mkononi na, ilikuwa na risasi tatu za bandia(blanko). Risasi hizi zilibaki baada ya kuwa amelenga kwa usahihi risasi saba, kati ya kumi alizokuwa amepewa. Baada ya hapo alichezesha kidogo mgongo wa bunduki na risasi hazikutoka tena. Kwa kuwa alilenga kwa usahihi alipewa alama zake na kuruhusiwa kutoka eneo la ulengaji, huku akiingia kwenye orodha ya wapigaji wazuri, watakao jaribiwa tena wakati mwingine, ili kuupima uwezo wao.
Alikuwa anatembea kwa hatua ndefu, huku akijaribu kufuata nyasi fupi zilizonawiri. Kichwani mwake aliamini nyasi zile zilipokea maji karibu, au kuna mto unaopita kwenye mazingira yale.
Alikuwa anatembea kwa kufuata njia za wachunga ng’ombe. Aliamua kufuata njia hizo akiwa na lengo la kukutana na wachungaji, au sehemu ambayo wachungaji walinywesha mifugo yao. Aliendelea kujipa tumaini hilo kwa sababu ya nyasi fupi alizoziona kwenye njia alizopita.
Akiwa ametembea zaidi ya nusu kilomita, alikutana na njia nyingine kutoonekana kutumika mara kwa mara. Njia ile halikuonesha kuwa fupi na haikuonekana kususwa, bali ilipitisha viumbe hai kila wakati.
Alisimama kwa dakika mbili huku akijaribu kutafari ukubwa wa njia ile. Alitizama alikotoka na alitizama aendako.
Kote kulikuwa ni pori na ni ndege pekee walisikika wakiimba kwa furaha, huku wengine wakirukaruka na kumshukuru Mungu kwa uhai aliowapa.
Alijikuta akianza kuwa na wasiwasi bila kutarajia, huku nafsi ikimtuma aifuate njia ile.
Hakujua ni kwa nini aliingiwa na wasiwasi, lakini aliamini kuna kitu hakikuwa sawa kuhusu njia ile.
Kwa nini?
Kwa sababu njia ile ilianzia pale alipokuwa na haikuonekana kuwa na mwanzo upande mwingine, uliyoiunganisha.
Wazo la kuendelea kuifuatilia njia ile ya wachunga ng’ombe liliishia pale. Na likaibuka wazo jipya la kuifuatilia njia ile iliyopitika mara kwa mara.
Aliifuata taratibu huku akijikuta anaongeza umakini bila kupenda. Kadiri alivyoendelea kwenda, ndivyo mapigo yake ya moyo yalivyozidi kudunda kwa kasi, huku miguu yake nayo ikianza kuwa mizito.
Alisimama!.
Alivuta pumzi nyingi na kuziachia taratibu. Alirudia tena mara mbili, kisha alitulia na kusikiliza udundaji wa mapigo yake ya moyo.
Yalidunda kawaida na hata alipojaribu kusogeza mguu, ulienda bila uzito wowote.
Licha ya mwili wake kukubali kuendelea, lakini akili yake ilikuwa inapigana na mambo mawili.
Jambo la kwanza akili yake ilikuwa inakubaliana na mwili wake, kuendelea mbele; lakini wakati huohuo akili yake ilikuwa inapingana na uamuzi wa mwili kukubali kwenda na ilitaka arudi alikotoka mara moja.
Sasa ilibidi akubali kufuata moja kati ya hayo mawili.
Alijikuta akipiga mluzi usio na maana huku mikono yake ikichomoa magazini na kuziangalia zile risasi tatu alizosalia nazo.
Ujasiri ukamvaa na alipiga hatua kusonga mbele, bila kujali matokeo ya mgongano wa nafsi yake.
Lakini siku zote ninge huja yakishatokea. Na endapo Willy angelijua nini maana ya mgongano wa nafsi, asingeliendelea na safari yake, kwenye ile njia ya ajabu.
****
Ungana nami kesho!