Mauaji ya Kenya JK na CCM wanaweza kutoa tamko kwa Kibaki?

Lunyungu

JF-Expert Member
Aug 7, 2006
8,873
1,894
Nina wasalimu wote kutokea Eldorest na ndiyo nimetokea eneo ambalo leo watu wameua kinyama na kuleta majonzi zaidi kisa na mkasa ukiwa ni Kibaki kurudi madarakani kwa mabavu.
Ni siku ya 3 sasa tangia matokeo yatangazwe na baadhi ya watu ama viongozi wamekuwa na kauli za haraka za kupongeza na kuondoa kauli kutokana na kitu wazungu wanaita revealation baada ya kura kutangazwa na Kibaki kutamkwa kwamba ni Rais na kukimia kula kiapo akiwa gizani .

Nimeshangaa hadi sasa si Tanzania wala Uganda majirani ambao wamesema neno lolote ama la kupongeza ama la kulaani yaliyo jiri Nchini Kenya . Wala si hata AU ila watu wa mabara mengine kama kawaida wanawasemea ama wanatusemea sisi weusi .

Najua mnataka kujua zaidi ni kitu nimekiona huko Eldoret nami sitasema kwa sasa ila nitasema baadaye kwa sasa nina haya moyoni mwangu kusema nanyi halafu nikimbilie kitandani maana hapa unalala unasikilizia .

Nimekuwa na hamu sana kusikia Rais wangu ndugu JK atasema nini lakini kama kawaida yake na kawaida ya Serikali yake yeye mambo makubwa na magumu huwa wanaamua kuwa bubu hii ndiyo kasi yao . Lakini pia nimejiuliza kama anaamua kutoa tamko atasemaje ? Maana hawezi kusema watu ama polisi waache kuua watu Kenya kwa kuwa Tanzania pia polisi walisha ua watu na hata wakakimbilia Kenya nia afadhali wao Wakenya hawajakimbilia kwetu .

Akisema mzozo juu ya kura Wakenya watawakumbusha ambush yao huko Visiwani na kuwaacha Watanzania wamekufa na wengine hadi leo ni vilema . Maana hata picha ziko online za ukatili wa askari wetu walio ufanya kwa rais kisa wamesimama na kudai haki zao baada ya kupiga kura na kuporwa .

Sana sana JK na CCM wanaweza kuwa wanafurahia kuona watu wanavyo kufa kwa ku resist maana naamini kwamba soon or later CCM watalazimika kutumia njia hii hii kwa kuwa kila mara huwa wanakataa kidogo tu FFU wanamwagwa .

Nimeshangaa kabisa kwamba watu wanaotaka shirikisho wanalitaka liwe la aina gani.Maana kama hawawezi kuelezana ukweli kama sasa kuitana haraka na kusema hapana acheni watu wasife kubalini kufuta utaratibu kweli sisi ni wamoja wa kitu gani ? Umoja huu unanifanya sasa nihitimishe wasi wasi wangu kwamba ulikuwa ni na bado ni umoja wa kujikita madarakani zaidi kuliko umoja wa watu wa Afrika Mashariki na maendeleo yao .

Nasema tena JK unangoja nini kusema kitu ? Au ni kwa vile unajua kwamba aliyo yafanya Kibaki ndiyo CCM wamekuwa wakiyafanyika huko Zenji na hata bara kuiba kura ili kupata wabunge wengi Bungeni? Maana kuna ushahidi wa wazi kuanzia Bukoba hadi Musoma, Arumeru na hata Dar kwamba kura zilitangazwa kwa nguvu baada ya CCM kuwa imepigwa chini .Lakini kwa Tanzania haya yalisha pita na sasa nakuuliza JK utasema lolote na utasema nini ? Kwa usafi upi na nguvu ipi ?

Museveni kusema lolote na nadhani anafurahia kuona watu wanakufa maana yeye hata matembezi ya kawaida Kampala anatumia kifaru. Yeye sawa na CCM wamefanya watu wa Nchi hizi mbili kuwa ni mali yao binafsi na matokeo kama ya Kenya yanatishia usalama wao kesho .

Au mpo .Mpo wapi ? Mnangoja nini ? Mbona juzi Mbeki kapigwa chini na bado mambo yanaendelea kwa nini Kibaki na wengine ya ANC ?

Bado nauliza watu wa Afrika Mashariki viongozi wetu wako wapi ama hadi wazungu waseme ndipo nanyi muweze kusema ?

Naishia hapa nimechoka na majonzi mengi . Niliyo yaona nitayasema kesho lakini naomba msaada wa majibu yangu kama kweli manadhani JK anaweza kusema lolote na atasema nini na kw ausafi upi wa CCM yake .
 
CCM itoe tamko au serikali? nimeona ile habari ya kanisa kuhomwa moto imenisikitisha sana.
 
CCM itoe tamko au serikali? nimeona ile habari ya kanisa kuhomwa moto imenisikitisha sana.

Thats one mkuu, issue nyingine ni kuwa hii inadhihirisha kwa nini waTZ walikataa shirikisho la kisiasa (walau uharakishwaji wake) maana kama aina ya watawala tulio nao ndio wa aina hii, basi kuna kazi huko mbeleni!
 
Thats one mkuu, issue nyingine ni kuwa hii inadhihirisha kwa nini waTZ walikataa shirikisho la kisiasa (walau uharakishwaji wake) maana kama aina ya watawala tulio nao ndio wa aina hii, basi kuna kazi huko mbeleni!

Tatizo watu wengie tunaangalia hawa majirani zetu kibiashara na kiuchumi mno, lakini ukiangalia wana matatizo ya ukabila mengi sana kuliko sisi.
 
Tatizo watu wengie tunaangalia hawa majirani zetu kibiashara na kiuchumi mno, lakini ukiangalia wana matatizo ya ukabila mengi sana kuliko sisi.

na tena basi, ndo kwanza najifunza kuwa kumbe uchumi wa kenya upo mikononi wa wakikuyu wachache ambao wameapa kutokubali mtu mwingine atawale ili kulinda maslahi yao

bora sisi hapa wezi wetu ni individual na wanatoka makabila mbalimbali...(list of shame)

uchumi unaweza kukua sawa kwa garama ya walio wengi na kwa faida ya walio wachache!
 
angalau ikulu ingetoa tamko la "kusikitishwa na upotevu wa maisha ya binadamu huko kenya na kuomba wananchi wa kenya wavute subira wakati viongozi wa pande zinazohusika wakitafuta suluhu. aidha iwaombe viongozi wa pande zinazohusika watatue tatizo na kuweka maisha na maslahi taifa mbele"

sidhani kwa wakati huu ni vyema kwa serikali yetu kuanza kulani/kulaumu upande moja au mwengine kwamba ndio chanzo cha matatizo. ni vyema tukumbuke kwamba jirani zetu watatuuliza tulikuwa wapi wakati wako kwenye dhuruba inayowapata sasa? naamini jibu halitakuwa "nao walikuwa wapi wakati zanzibar walipopata kichapo"

mola ibariki afrika
 
What you want JK to do? Think before you opened your mouth. To this point JK needs to maintain silence. You have to avoid taking sides, you don't have any factors either to condemn Mwai Kibaki, or congratulate him. Leadership does not means to wake up and yap yap about everything going on around the world, you need facts before of saying anything.
 
Mtanganyika good Point,

our government need to take steps which will ensure that democracy is prevailing in eastafrica. whether we work in underground manner or publicly,but the whole stratergy should be to do something.

for the kenya case at the moment it is not wise to increase rhehotorics with Kibaki regime, instead it is wise to work with an international community to exert pressure on the regime.

at the moment so far, any unilateral action by Our government to issue a statement to support or condemn the Kibaki and the rigging of the votes can not be productive.

sometimes to do something is better than to say something
 
JK is in Kenya trying to reconcile the parties in conflict.He is playing his cards silently with patiency and wisdom.
In his leardership he has not killed anyone or use the military against his opponents.He has the trust of CUF as the talks on muafaka continue.Thre is no way you can compare JK to Ben Mkapa whose hands are still smelling blood for the killings in Zanzibaris.
The turmoil in Kenya has been brought up by the PNU Kikuyu hardliners through Kibaki by hijacking the election.The whole world knows it and Jk knows it too,so for him to address the Kenya problem at the moment is very crucial.Gordon Brown has come forward and asked both Raila and Kibaki to meet and resolve the problem.We have to give everyone a chance to try make peace in Kenya.
 
Ccm Jk Na Wenzake Wote Wasaani Bandugu Waacheni Kenya Wataafute Raisi Watakaemtaka Hata Kwa Adam Hamkumbuki Madagascar Jamani Mwisho Wakakubali,,,mungiki Mpo Jamani Tunataka Amani Msiwaache Wahuni Wachkue Nchi Kihunihuni Kama Kibaki,,ccm Mnajua Mlichochangia Kuleta Yaliotokea Kenya Kaeni Kimya Muone Kitakachotokea
 
Waingereza wanapenda kuiita Kenya 'the most stable nation in eastern Africa'. I'm sue they are eating their words now.Maana hata tv zimefungiwa kutangaza yanayojiri.mimi kwangu i get KBC na NTV zote sasa hivi zinaoyesha news za CNN,the same thing happened in Pakistan and the whole world condemmened it.Kama haya yangetokea Tanzania,ungeona hizo kelele.Yanayotokea Kenya huwezi kulinganisha na yaliyotokea Zanzibar.Watu wamechomwa moto kanisani,tena watoto wadogo!200 plus have died.

Lakini on the whole,labda kuna kitu tunaki overlook hapa.Huyu Kibaki kwenye uchaguzi kabla ya huu,alikuwa ni mpinzani,na alipigiwa debe na wapinzani hata huku.Baada ya kushinda sasa tunaona yanatokea yaleyale,nae anaiba kura!Kwa hio huu ni ugonjwa inaelekea upo once mtu akiwa madarakani.Is there a lesson to be learnt here? Hao CCM,rafiki zao Kenya ni KANU,hata kule Dodoma waliwaalika,pamoja na kwamba ni chama cha upinzani,je wapinzani hapa Kibaki ni mwenzao aliyewatangulia kushika madaraka au urafiki ni lazima wawe wapinzani pia?
Ni mtazamo wangu tu
 
Kama uongozi wenyewe wa namna hii siutaki milele!!! Namuomba Mungu aniepushe nao....

Mshairi mkongwe Shaaban Robert alipata kusema 'Kiongozi anaefaa/muadilifu ni yule anaetawala mioyo ya watu na sio viwiliwili vyao'.

Yanayotekea Kenya yanahuzunisha na kusikitisha sio tu kwa Afrika bali kwa wapenda amani duniani kote.

Hivi ni lini viongozi uchwara wataheshimu 'will of the people'.

Kwa mujibu wa mtazamaji mmoja wa EU, uchaguzi wa Kenya haujafikia viwango vya demokrasia ya kimataifa na hata ile Kenya yenyewe; there were discrepancies between the results anounced in Nairobi and other parts of Kenya. This rises a big question mark (?).

Nimesoma humu Mkuu JK yupo Kenya kuwaweka sawa Odinga na Kibaki, if thas is the case then it is an Excellent actions by our Prez.

Lakini pia sikubaliani na ukimya wetu Watz bila hata kulaani mauaji ya Civilians hapo Kenya. Nimeshuhudia ktk TV askari akimwaga risasi za moto kwa kundi la raia wa kawaida, hii inapaswa kulaaniwa na serikali zote zinazopenda amani duniani.

Cha kuhuzunisha zaidi ni kitendo cha wahuni/maharamia (call them any bad name they still won't fill the category) walipoenda kuchoma moto kanisa, mahali ambapo watu waliamini wamekwenda kusalimisha maisha yao. Haiingii akilini kwa nini wakachome moto mahali pale pa ibada?

Nakubaliana na muandishi aliepita Mh. Kikwete bado anayo mikono misafi na rekodi nzuri ukilinganisha na M7 na Kibaki, ya kuwa na uthubutu wa kuwakabili na kuwapa ukweli wa ubaya wa wanayoyafanya kwa wananchi wao.

Lakini pamoja na hilo haituzii kutoka hadharani na kutoa kauli kali kulaani mauaji yanayoendelea ambayo yanaathiri watoto, wanawake, wazee na makundi mengine yasiyoweza kujihami.
Nieleweka wazi hapa sizungumzii kutetea either Kibak's or Odinga's side bali kulaani mauaji yale yanayofanywa 'dhahir shair' kwa kutumia silaha za moto dhidi halaiki za watu.

Mungu ibariki Afrika
Mungu ibariki Afrika Mashariki
 
Hakuna kipya ambacho kinachotekea Kenya, zaidi ya kusema siasa halisi za kiafrika na walioshika hatamu kuendelea kung'ang'ania madaraka kwa gharama za maisha ya watu wengine.

Usitegemee kusikia chochote tofauti kutoka TZ au Uganda, sababu ya utamaduni wa viongozi wetu ni wakuigiza na si wakutoa hali halisi. Hawako tayari kuonyesha misimamo yao zaidi wanasoma upepo na kuangukia palipo na nguvu.
Usitegemee kauli yoyote ya kuwatetea wanyonge au wanaoathirika kutokana na mauaji yanayotokea Kenya, kwani si katika tamaduni zetu, wanataka kusikia wakubwa wanataka nini ili nao wasijiaribie.
Namna yalivyo tangazwa matokea na kuapishwa rais tayari ilitoa picha ya nini kitafuata.Chakufanya ni kutoa fursa kwa wana forum kama kwaida yao wajadili mawazo mbadala kuliko kusubiri kauli za marais wa kiafrika. Hata ya Rwanda waliyakalia kimya mpaka yakafika yalipo fika.

Maoni yangu kwa wakenya wote, ni kuwataka wawe na subira katika kutafuta njia mbadala ya kudai haki.Walio chelewesha ama kudhulumu wapo na wanafahamika, mapambano yote ya kudai haki yawalenge wahusika na si raia wasio na hatia
 
Few guys seems to miss my point na maandiko yangu . Nime hoji kama kweli CCM na JK ama M7 wanaweza kusimama na kusema lolote lile . What is international community ? Yaani kwako international community lazima Bush na Brown then EU ?Kwa uovu wa vyama na namna viongozi wetu wanavyo ingia madarakani ndiyo maana watasita na kulindana kwa Africa .Wanangoja International Community ipi yaanin hadi yatokee kama yale ya Rwanda na Burundi ?

Nimesema JK hatakuwa na nguvu kusema kwa kuwa yeye na CCM yake walishiriki katika kupora uchaguzi Zanzibar . Yeye alikuwa waziri wa mambo ya Nje na hata kusema nje alishindwa .Yeye alikuwa anajiandaa na kugombea Urais pia lakini aliona uchafu ule na akwa kimya . Leo unaongelea Muafaka ? Upi ? Wanavuta time hadi 2010 na ndipo watasema wata endelea baada ya hapo . Muafaka kama wana nia ungalikuwa umeisha lakini wako akina Kingunge wanachezea akili za watu . Nimesema mifano michache ambako CCM walipora ushindi . Nilikuwa Moshi ambakio walichukua siku zaidi ya 3 kutangaza matokeo wakitaka kubadili ili Mama Minde ashinde lakini wakashindwa . Je watu waliopata ushindi ama madaraka kwa njia hii wanaweza kusema lolote kwa Kibaki ?

AU iko wapi ? Observe silence hadi wafe watu wangapi ?

Kweli Waafrika ndiyo hivyo tulivyo .
 
Naamini JK mswahili safi, anajua ukimuonyeshea mwenzio kimoja, basi vinne vinakungalia wewe. Huyo Jk anajua gari lake limeuwa wangapi, tokea kuwakolimba hadi kwenye maandamano ya amani, sasa unategemea amwambie nini Kibaka (sorry Kibaki)? Anauchuna tu.
Kasheshe zake 2010!
 
Sidhani kama sisiemu ama sirikali yao watatoa tamko la kulaani vurugu za jirani zetu Wakenya kwa kudai haki yao inayopokonywa kwa mtutu, ilhali na wao waliyafanya hayo hayo aliyoyafanya Kibaki. Mara hii tushasahau kadhia za chaguzi za Zanzibar? Hatukumbuki majeshi yeto yote kujaa visiwani na kuwakandamiza Wapemba?
Nani wa kumnyooshea kidole Kibaki hapa Afrika?
 
Ndiyo maana nikaleta makala hii kutaka kujua wewe utasemaje .Lakini I have been attacked without the attackers knowing my point. Uharamia ule wa Kibaki ndiyo uko Tanzania . Naona watu wameanza kujenga hoja kwamba Kenya kuna ukabila nasema hapana .Kenya kuna wizi wa kura .Kama si wizi haya yasingalikuwepo. Najua wapenzi wa mafisadi Tanzania mtasema kwamba this is more than uchaguzi I might say yes but what has triggered all this ni wizi wa kura . Je JK anaonanana M7 watasema nini wakati wao hata Katiba TZ wanasema si muda kuafaka wa kuijadili watasema nini juu ya Kibaki ?
 
Kuna Tofauti gani kati ya Askari wa kenya na Tanzania.
Wote wametumwa kwa Jina la Mafisadi ili Kuangamiza Roho za wananchi kudumisha ndoto zao za kutawala milele.
 

Attachments

  • Uchaguzi_na_Kibano_Zanzibar[1].ppt
    353 KB · Views: 75
Nimesoma sehemu kuwa Kikwete anajaribu kuwapatanisha hawa waungwana.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom