Paul Alex
JF-Expert Member
- Jul 14, 2012
- 4,240
- 9,527
Sehemu ya Kwanza.
John Fitzgerald Kennedy, aliyekuwa maarufu kama JFK au Bobby, alikuwa mwanasiasa wa Marekani aliyehudumu kama rais wa 35 wa USA kutoka mwaka 1961 hadi alipouawa mwishoni mwa mwaka wake wa tatu katika ofisi hiyo.
Aliuawa huko Dallas, Texas, US na kifo hicho kilitangazwa rasmi katika hospitali ya Parkland.
Alizaliwa: May 29,1917, Brookline, Massachusetts, huko Marekani.
Mke wake wa ndoa aliitwa Jacqueline Kennedy Onassis na walioana mwaka 1953 hadi 1963 JFK alipouawa..
Makamu wake wa rais alikuwa Lyndon B. Johnson kutoka mwaka 1961 hadi 1963.
Kuna nadharia nyingi sana za njama za jinsi JFK alivyouawa (conspiracy theories), mtu aliyemuua na sababu ya yeye kuuawa. Lakini ukipitia nadharia zote hizo utaona mapungufu makubwa. Na hata msimamo wa Serikali ya Marekani na vyombo vya usalama mpaka sasa kuwa Lee Harvey Oswald ndiye muuaji wa JFK pia una mapungufu makubwa.
Ni mpaka mwaka 2003 ambapo utata uliondolewa na mahojiano aliyofanya bwana James Files ambae kwa hakika ndiye muuaji wa JFK.
Kwenye mahojiano hayo ambayo yatafuata hapa utajionea mipangilio na matukio hatua kwa hatua jinsi JFK alivyouawa.
Mahojiano haya yalifanyika November 19, 2003 ndani ya magereza ya Stateville huko Joliet, Illinois.
Wahusika katika mahojiano haya ni;
1. James Files - muuaji aliyekiri kumpiga JFK risasi ya kichwa.
2. Pamela Ray - mtunzi wa vitabu na rafiki wa karibu wa James Files tangu mwaka 1999 - alipaswa kuwa katika mahojiano na James Files.
3. Jim Marrs - mtunzi wa vitabu na mtu ambaye Pamela Ray alikubali amuhoji James Files badala yake mwaka 2003.
4. Gary Beebe - mchukua video.
5. Mrs. French - mtu wa utawala katika magereza ya Stateville.
6. Wim Dankbaar - afsa mauzo mwenye asili ya Dutch.
Kuna kipande kidogo cha mwanzo cha mahojiano ambapo sintofahamu ilitokea baada ya timu ya mahojiano kufika kwenye mahojiano bila Pamela Ray.
Pamela Ray alikuwa mtu muhimu sana kwa Files maana kwanza alimwamini na pili yeye asingeweza kukubaliana mkataba wowote kisheria akiwa mfungwa hivyo alimtegemea sana Pamela kwenye mambo ya mikataba.
Ila baada ya Files kueleweshwa na kuona maandishi kutoka kwa Pamela yakimtaka amwamini Jim Marrs basi mahojiano yakaendelea kama ifuatavyo;
Jim Marrs - swali : kumbukumbu zako juu ya jinsi Joe West alivyowasiliana na wewe na ulichofikiria juu yake, zikoje?
James Files - jibu : Mara ya kwanza Joe West aliwasiliana na mimi hapa magereza nikiwa nimetembelewa na mgeni. Mshauri nasaha wa magereza akaja kwenye chumba cha wageni nilipokua na akasema anataka nitoke na nipige simu. Nikamwambia," Haiwezekani, niko hapa siku 365 za mwaka. Siwezi kumuacha mgeni wangu ili nikapige simu. Nikauliza,"nani anapiga simu?" . Akajibu,"Kuna mtu kutoka Texas anaitwa Joe West".
Nikamwambia," simjui huyo mtu. Mwambie, nitampigia kwa muda wangu, sio muda wake. Niko na ugeni. Usinisumbue nikiwa kwenye ugeni".
Siku iliyofuata walikuja wakanitoa kwenye sero yangu, wakaniteremsha chini kwenye ngazi; walikua wamening'iniza simu ikinisubiri. Nikampigia Joe West na kuongea nae. Nikamwambia : una dakika tatu (3) za kunishawishi kwanini niongee na wewe. Joe alipoanza kuongea, nikamwambia : Woo, usiendelee! Umegusa sehemu nyingi nyeti; hizi simu zote zinarekodiwa. Kila simu inayoingia na kutoka inarekodiwa. Kama una nia kiasi hicho ya kuongea na mimi, basi napendekeza uje unitembelee. Joe West akanitaka nimuweke kwenye orodha ya wageni. Na akaja kunitembelea.
Alitumia siku mbili kuongea na mimi. Siku ya kwanza wala sikutaka kuongelea suala la Kennedy. Tuliongelea michezo; hali ya hewa, kwa ujumla kuhusu jela, na vitu vya kawaida mpaka nikawa na amani na yeye.
Siku iliyofuata, baada ya kuwa nimetafakari hilo jambo usiku mzima, Joe alionekana kuwa mtu mzuri tu, nilimpenda Joe. Alikuwa na mvuto fulani juu yake. Siku iliyofuata tulikaa chini na tukawa 'serious' na kisha tukaanza kuongea.
Nikiwa kwenye chumba cha wageni na Joe. Wakanipa penseli na karatasi. Nikaichora Dealey Plaza yote, bila kunakili kwenye ramani, bila picha, bila chochote kuwepo, na nikamuelezea Joe wakati ule, kwasababu Joe alitaka kujua nilikuwa sehemu gani katika huo mchoro. Na nikasema: Nitaweka alama ya 'X' katika karatasi, kunitambulisha mimi, ila hii 'X' haitakuwa sehemu sahihi. Nikasema: muda sahihi ukifika, hapo nitaiweka 'X' pale inapopaswa kuwa
Itaendelea....
John Fitzgerald Kennedy, aliyekuwa maarufu kama JFK au Bobby, alikuwa mwanasiasa wa Marekani aliyehudumu kama rais wa 35 wa USA kutoka mwaka 1961 hadi alipouawa mwishoni mwa mwaka wake wa tatu katika ofisi hiyo.
Aliuawa huko Dallas, Texas, US na kifo hicho kilitangazwa rasmi katika hospitali ya Parkland.
Alizaliwa: May 29,1917, Brookline, Massachusetts, huko Marekani.
Mke wake wa ndoa aliitwa Jacqueline Kennedy Onassis na walioana mwaka 1953 hadi 1963 JFK alipouawa..
Makamu wake wa rais alikuwa Lyndon B. Johnson kutoka mwaka 1961 hadi 1963.
Kuna nadharia nyingi sana za njama za jinsi JFK alivyouawa (conspiracy theories), mtu aliyemuua na sababu ya yeye kuuawa. Lakini ukipitia nadharia zote hizo utaona mapungufu makubwa. Na hata msimamo wa Serikali ya Marekani na vyombo vya usalama mpaka sasa kuwa Lee Harvey Oswald ndiye muuaji wa JFK pia una mapungufu makubwa.
Ni mpaka mwaka 2003 ambapo utata uliondolewa na mahojiano aliyofanya bwana James Files ambae kwa hakika ndiye muuaji wa JFK.
Kwenye mahojiano hayo ambayo yatafuata hapa utajionea mipangilio na matukio hatua kwa hatua jinsi JFK alivyouawa.
Mahojiano haya yalifanyika November 19, 2003 ndani ya magereza ya Stateville huko Joliet, Illinois.
Wahusika katika mahojiano haya ni;
1. James Files - muuaji aliyekiri kumpiga JFK risasi ya kichwa.
2. Pamela Ray - mtunzi wa vitabu na rafiki wa karibu wa James Files tangu mwaka 1999 - alipaswa kuwa katika mahojiano na James Files.
3. Jim Marrs - mtunzi wa vitabu na mtu ambaye Pamela Ray alikubali amuhoji James Files badala yake mwaka 2003.
4. Gary Beebe - mchukua video.
5. Mrs. French - mtu wa utawala katika magereza ya Stateville.
6. Wim Dankbaar - afsa mauzo mwenye asili ya Dutch.
Kuna kipande kidogo cha mwanzo cha mahojiano ambapo sintofahamu ilitokea baada ya timu ya mahojiano kufika kwenye mahojiano bila Pamela Ray.
Pamela Ray alikuwa mtu muhimu sana kwa Files maana kwanza alimwamini na pili yeye asingeweza kukubaliana mkataba wowote kisheria akiwa mfungwa hivyo alimtegemea sana Pamela kwenye mambo ya mikataba.
Ila baada ya Files kueleweshwa na kuona maandishi kutoka kwa Pamela yakimtaka amwamini Jim Marrs basi mahojiano yakaendelea kama ifuatavyo;
Jim Marrs - swali : kumbukumbu zako juu ya jinsi Joe West alivyowasiliana na wewe na ulichofikiria juu yake, zikoje?
James Files - jibu : Mara ya kwanza Joe West aliwasiliana na mimi hapa magereza nikiwa nimetembelewa na mgeni. Mshauri nasaha wa magereza akaja kwenye chumba cha wageni nilipokua na akasema anataka nitoke na nipige simu. Nikamwambia," Haiwezekani, niko hapa siku 365 za mwaka. Siwezi kumuacha mgeni wangu ili nikapige simu. Nikauliza,"nani anapiga simu?" . Akajibu,"Kuna mtu kutoka Texas anaitwa Joe West".
Nikamwambia," simjui huyo mtu. Mwambie, nitampigia kwa muda wangu, sio muda wake. Niko na ugeni. Usinisumbue nikiwa kwenye ugeni".
Siku iliyofuata walikuja wakanitoa kwenye sero yangu, wakaniteremsha chini kwenye ngazi; walikua wamening'iniza simu ikinisubiri. Nikampigia Joe West na kuongea nae. Nikamwambia : una dakika tatu (3) za kunishawishi kwanini niongee na wewe. Joe alipoanza kuongea, nikamwambia : Woo, usiendelee! Umegusa sehemu nyingi nyeti; hizi simu zote zinarekodiwa. Kila simu inayoingia na kutoka inarekodiwa. Kama una nia kiasi hicho ya kuongea na mimi, basi napendekeza uje unitembelee. Joe West akanitaka nimuweke kwenye orodha ya wageni. Na akaja kunitembelea.
Alitumia siku mbili kuongea na mimi. Siku ya kwanza wala sikutaka kuongelea suala la Kennedy. Tuliongelea michezo; hali ya hewa, kwa ujumla kuhusu jela, na vitu vya kawaida mpaka nikawa na amani na yeye.
Siku iliyofuata, baada ya kuwa nimetafakari hilo jambo usiku mzima, Joe alionekana kuwa mtu mzuri tu, nilimpenda Joe. Alikuwa na mvuto fulani juu yake. Siku iliyofuata tulikaa chini na tukawa 'serious' na kisha tukaanza kuongea.
Nikiwa kwenye chumba cha wageni na Joe. Wakanipa penseli na karatasi. Nikaichora Dealey Plaza yote, bila kunakili kwenye ramani, bila picha, bila chochote kuwepo, na nikamuelezea Joe wakati ule, kwasababu Joe alitaka kujua nilikuwa sehemu gani katika huo mchoro. Na nikasema: Nitaweka alama ya 'X' katika karatasi, kunitambulisha mimi, ila hii 'X' haitakuwa sehemu sahihi. Nikasema: muda sahihi ukifika, hapo nitaiweka 'X' pale inapopaswa kuwa
Itaendelea....