Mauaji ya Daudi Mwangosi: Jaji Mstaafu Ihema Kuongoza Tume Huru ya Uchunguzi!

Tusiingize siasa kwenye kila jambo waachieni wenye fani zao waseme kitaeleweka tu.


Elewa kuwa kila kitukatika maisha yako ni siasa. Ndio maana unakaa Masaki na sisi tunakaa kwa mfuga mbwa, ndio maana unaenda kazini na gari wakati wenzio tunatembea kwa mguu kwenda kazini. Ndio maana unaelimu bora kunizidi mimi, ndio maana ukiugua unaenda Ulaya kutibiwa wakati mimi nikiumwa naenda kwa babu loliondo.

Ndio maana nyumba yako inalindwa na security group, ina fensi ya umeme, ina mbwa wanaokula zaidi yangu na bado unalala na bastola wakati mimi mlango wangu umefunikwa na gunia, na wala siogopi wezi, wataiba nini marapurapu na mitumba?

Ndio maana wewe unafanya mikutano ya kampeni Zanzibar na mwema hasemi kitu, unaenda kulinda kwenye fiesta mwema anakenua lakini mimi nikifanya mikutano unaniua.
 
Mheshimiwa Edward Lowasa alisema ''tatizo la ajira katika nchi hii ni bomu linalo weza kulipuka wakati wote'' na mimi ninachokiona kwa sasa, MUENDELEZO WA UNYANYASAJI WA SERIKALI NA VYOMBO VYA USALAMA KATIKA KULINDA HAKI AMANI NA UTULIVU KWA NCHI YETU NI BOMU LA NYUKLIA LINALOSUBIRI KAMUDA KADOGO TU LILIPUKE NA HII INATOKANA MLUNDIKANO WA MATUKIO MABAYA AMBAYO WATANZANIA WANAFANYIWA DHIDI NA WATU WALIO WAPA RIDHAA YA KUONGOZA, TENA KWA UPENDO NA UPOLE NA HIVI NDIVYO TUNAVYOLIPWA WATANZANIA.

USHAURI KWA UONGOZI, MAMBO YOTE MAOVU YANAYOTOKEA KATIKA TAIFA HILI YANAYOTENDWA NA VIONGOZI NA BAADA YA MUDA WANAYAZIMA KISIASA, WASIJE WAKADHANI YAMEKWISHA BALI WATU WANALIMBIKIZA KATIKA BONGO ZAO NA MWISHO WATANZANIA WOTE WATAKUWA KAMA WAMEPANDWA NA WAZIMU WASIO WEZA KUZUILIKA KATIKA MAAMUZI YAO, YAANI NI KAMA VILE KUSEMA LIWALO NA LIWE BORA MTUUWE TAIFA ZIMA MKABAKI NINYI TULIO WACHAGUA KULIKO KUKANDAMIZWA.

Mungu wangu Wa Mbinguni akupeni adhabu ya siri itakayo wastahili wote watendao mambo yao katika nchi hii kwa hila.

INAUMA NA INASIKITISHA SANA MWENENDO WA HII NCHI.
 
Umekumbuka wakati muafaka.
Wakati wa uuzaji wa Nyumba za Serikali, Nyumba zilizokuwa zikimilikiwa na Serikali za Mitaa hapa Dar es salaam na kwingineko (Halmashauri) ziliundiwa waraka wa kuzisitisha zisiuzwe. Jaji Ihema wakati huo alikuwa akikaa kwenye moja ya nyumba za Halmashauri ya Kinondoni iliyoko Masaki (ingawa hakuwa mtumishi wa Halmashauri). Cha kushangazani kwamba, aliuziwa na serikali hiyo nyumba, kinyume cha sheria na hadi leo anaimiliki. Kwanini Kinondoni hawakuidai hiyo nyumba, haieleweki. JE, UNATEGEMEA JAJI IHEMA KUWA KWENYE TUME HII ATATENDA HAKI? NANI ANAKATA MKONO UNAOMPA CHAKULA?

Mkuu hii ndiyo Tanzania zaidi ya uijuayo. Unanipa chungwa nakupa maji
 
Wanaunda tume wakati wauaji wanaonekana kabisa...
walivyomwua-wangosi.JPG
 
Sisi watanzania kwa kutokuwa serious ndo namba moja.Yani kuna watu kwa nguvu zao zote na kwa imani yao yote wanasubiri matokeo ya tume hata kukubali ujinga wa tume?kwanza ni tume ngapi zimeshaleta matokeo yanayokubaliwa na wananchi?

Kwa wenzetu,kwanza askari wale tayari wangekuwa kwenye likizo ya bila malipo wakisubiri uchunguzi huru,na si wa tume za kifisadi za kuwapa watu ulaji na kubuy taime watu wasahau.Sitaki kuichukia nchi yangu moja kwa moja,nina imani nchi yangu ni nzuri sana tu,except that hatuna uongozi na tuko kama watu wasio na ubongo!Kwanza kulikuwa hakuna haja ya kujadili sijui mambo ya tume na wajumbe wake.Haya mambo yananifanya nipumzike huku kidogo.Kwasababu ni ujinga usiovumilika.
 
  1. Judge...........Mwenyekiti
  2. Theophile Makunga-Tanzania Editors Forum (TEF)
  3. Pili Mtambalike-MCT
  4. Jeshi la Polisi
  5. Mtaalamu wa Mabomu
ameipa mwezi mmoja ilete taarifa, anasema kuna maswali mengi yamegubika kifo cha Mwangosi mojawapo ikiwa ni mahusiano kati ya mwandishi na jeshi la polisi na amesema hivi karibuni atachukua hatua kali dhili ya polisi wazembe

Huo ni ***** -TORS
 
Nchimbi-right-addresses-journalists.jpg


Minister for Home Affairs, Mr Emmanuel Nchimbi (right) addresses journalists

Hadidu Rejea sita ambazo tume ya uchunguzi imepewa na Waziri Nchimbi ni hoja nzuri za msingi. Katika kumbukumbu zangu, ni miezi michache tu kulikuwa na hali ya mtifuano wa kutoelewana kati ya polisi na waandishi wa habari hali kadhalika Mkuu wa Mkoa Iringa. Upatanishi uliowakutanisha huenda ulikuwa wa kisiasa zaidi kuliko hali halisi. Hoja ya kuhusu vyama vya siasa kama haviridhishwi na uamuzi wa posili kama kuna rufaa, kwani mara kadhaa kumekuwepo hali ya kubadilika makubaliano ya awali kitu ambacho kimeleta dosara na hali ya kutoelewana kati ya polisi na mikutano ya Chadema.

Hadidu Rejea ambazo Waziri Nchimbi ameagiza tume ya uchunguzi kutumia katika kazi hiyo ni kama ifuatavyo:


  1. Nini chanzo cha mauaji ya Daud Mwangosi.
  2. Uhasama kati ya polisi na waandishi Iringa.
  3. Kuna waandishi watatu mkoa wa Iringa wapo kwenye orodha ya kuuawa na polisi.
  4. Kama nguvu iliyotumika Nyororo Iringa kumwua Daud Mwangosi ilikuwa sahihi.
  5. Kama kuna utaratibu wa vyama vya siasa kukata rufaa kama haviridhishwi na uamuzi wa polisi.
  6. Kama kuna uhusiano mbaya kati ya polisi na vyama vya siasa.
Hoja hizo kama zinafanyiwa kazi vizuri zinaweza kusaidia kuweka msingi ambao unaweza kusaidia kuziba nyufa zilizokuwa zinazidi kuongezeka na kusababisha maafa yasiyokubalika. Kwani polisi wamekuwa na tabia ya kuzidi kuonyesha ubabe badala ya weledi wa kazi yao dhidi ya wananchi na vyama vya siasa vya upinzani nchini.
 
Nchimbi-right-addresses-journalists.jpg


Minister for Home Affairs, Mr Emmanuel Nchimbi (right) addresses journalists

Hadidu Rejea sita ambazo tume ya uchunguzi imepewa na Waziri Nchimbi ni hoja nzuri za msingi. Katika kumbukumbu zangu, ni miezi michache tu kulikuwa na hali ya mtifuano wa kutoelewana kati ya polisi na waandishi wa habari hali kadhalika Mkuu wa Mkoa Iringa. Upatanishi uliowakutanisha huenda ulikuwa wa kisiasa zaidi kuliko hali halisi. Hoja ya kuhusu vyama vya siasa kama haviridhishwi na uamuzi wa posili kama kuna rufaa, kwani mara kadhaa kumekuwepo hali ya kubadilika makubaliano ya awali kitu ambacho kimeleta dosara na hali ya kutoelewana kati ya polisi na mikutano ya Chadema.

Hadidu Rejea ambazo Waziri Nchimbi ameagiza tume ya uchunguzi kutumia katika kazi hiyo ni kama ifuatavyo:


  1. Nini chanzo cha mauaji ya Daud Mwangosi
  2. Uhasama kati ya polisi na waandishi Iringa.
  3. Kuna waandishi watatu mkoa wa Iringa wapo kwenye orodha ya kuuawa na polisi.
  4. Kama nguvu iliyotumika Nyororo Iringa kumwua Daud Mwangosi ilikuwa sahihi.
  5. Kama kuna utaratibu wa vyama vya siasa kukata rufaa kama haviridhishwi na uamuzi wa polisi.
  6. Kama kuna uhusiano mbaya kati ya polisi na vyama vya siasa.
..............................................................................
7
. Nani anahusika na kifo cha DM
8. Je kulikuwa na ulazima wa mauaji hayo
9. hatua gani stahiki zichukuliwe kwa wahusika wa mauaji
10.Je nini kifanyike kuzuia mauaji haya ya polisi kwenye mikutano ya kisiasa

Namba 7-10 najaribu kumsaidia bwana Nchimbi katika TORs alizowapa tume aliyounda japo kisheria hana mamlaka ya kuunda tume. By the way tume hii lengo lake ni kulisafisha jeshi la polisi na mauaji hayo ambayo yako wazi kabisa, na hayo ni matokeo ya ukondoo tulionao wanannchi. Ni wakati sasa wananchi tunatakiwa tudai haki kwa gharama yoyote maana wanazidi kutuonea.
 
Kama waziri ya mambo ya ndani moja kwa moja ndiwe mwenye dhamana ya mwenendo mzima wa Jeshi la Polisi. Ni kweli kule Iringa kumetokea jambo baya sana lisilokubalika - maisha ya mtanzania yamepotea mikononi mwa polisi. Kama kawaida Polisi ambao ni watuhumiwa wakuu wanajitokeza na tume ya kuchunguza (na kufunika) nasema hivyo kwa sababu huku nyuma tumeshuhudia matukio mengi ya watanzania kupoteza maisha wakiwa mikononi mwa polisi na tumeona kilichofuata- kuundwa kwa tume za kuchunguza(na kufunika). Juzi tu tumeyaona Morogoro. Sasa tunajiuliza imekuaje Iringa unakuja na mkakati tofauti na mauji ya Arusha, Ruvuma, Nyamongo, na Morogoro na kwingineko? Je, ya Iringa yana tofauti gani? Jibu ni wazi yamehusu wenye mdomo wa kusemea na hiyo inawatisha. Kama ulivyounda tume yako juu ya ile ya polisi sitashangaa kama kesho bosi wako naye atakuja na tume yake juu ya hii yako. Swali ni je, lengo la kuunda tume husika ni nini? Je, una nia ya dhati ya kusafisha Jeshi hili? Sina uhakika kama unaona umuhimu wa kufanya hivyo. Kumbuka tumechoshwa na tuhuma za kila siku dhidi ya jeshi la polisi. Orodha ya tuhuma hizi ni nyingi mno (rejea mhariri wa Nipashe jana). Japo hata yeye alichoka na orodha ya tuhuma akaacha nyingi mfano zile za rushwa barabarani, mauaji wa raia migodini, kubambikia raia kesi na lile baya zaidi la kuwepo genge la polisi linalojihusisha na ujambazi ambalo lilitolewa bungeni na mbunge kudai ana ushahidi. Cha kushangaza ni kwamba bunge lilifunika hili japo tumeshuhudia spika na wenyeviti wakidai ushahidi wa mambo mengine madogo ukilinganisha na hili. Ndiyo umeiunda tume lakini kumbuka matatizo ya Jeshi la polisi ni makubwa zaiadi na hatutegemei litakate kwa kufunika funika tuhuma juu yao. Wananchi ni waelewa kuliko mnavyotuchukulia. Hivi kama tunawahimiza raia washiriki ulinzi shiriki itakuaje kama tumeanza mauaji nayo yawe shirikishi? Kwako nikukumbushe yaliyomkuta kada mwenzako Mapuri. Labda uanze kuchagua nchi sivyo jiulize unataka nini kutoka tume uliyounda na je, baada ya hapo jeshi la polisi litakuwa limetakata?:A S 465:
 
Nchimbi sijasikia analizungumzia na kulaani kile kilichofanywa na polisi zaidi amajikita kumshambulia dokta slaa na chadema....haoni mikutanpo ya ccm na matamasha ya fiesta yalifanywa na clouds siku ya tukio la mauji kama yalikuwa hayaathiri sensa.....huyu ni kiongozi mbaya sana hana dhamira ya kulisafisha jeshi la polisi bali ni kulitumia kwa maslai yake.....ikumbukwe pale songea mjini nchimbi alichakachua matokea ya ubunge 2010 ambapo washindi walikuwa ni chadema,kwa vyovyote kiongozi kama huyu mwenye mgongano w maslai hawezi kutafuta suluhisho la ufumbuzi wa tatizo hilo...rais wetu dhaifu yaani amakaa kimya kimsingi kwenye swala zito na nyeti kama ili rais ndiye aliyetakiwa kuunda tume kisheria nchimbi amekurupuka gafla kwani anajua yeye ni mtuhumiwa na alipaswa kujiuzulu mbaya ameanza kutumi tbc kueneza propaganda hii kuwa chadema ndio wahusika wa mauaji hayo shame on him.....katika ili nchimbi hana budi kukaa pembeni
 
Kucheleweshwa kesi kunachangiwa na mambo mengi huwezi kumlaumu jaji moja kwa moja.

Unaonekana humfahamu huyu Jaji, ni bora kukaa kimya. Nani asiyejua kuchelewa kesi kunasababishwa na mambo mengi, tunachosema ni kwamba yeye ni Bingwa wa kuchelewesha kesi bila sababu za msingi.
 
Back
Top Bottom