Mauaji ya Albino: Kushindwa kwa serikali?

Nchi ikiongozwa na giza mambo hayo yatatokea. fikiria swala la albino!!!!!!!!!Tunahitai maombi ya kwelikweli.Siku hizi ma askofu namanabii na mitume kibao kama ni waukweli wakemee hayo mambo.
 
Hii ni hatari sana jamani na tena inatisha mno! Naomba waratibu muitoe hii mada kwenye siasa maana hii si siasa hata kidogo. Na tena heading ibadilishwe iendane na habari yenyewe. Weka kwenye "habari za kutisha" au kitu kama hicho!
 
Mods kwa maoni yangu naomba ibakie hapa lakini ipewe appropriate heading maana hiyo heading huwezi kujua kama ni kitu sensitive namna hiyo.
 
Hii nimeipata gazeti la Mwananchi:


Mtoto akamatwa na kichwa cha mtu, akitafuna mbele ya askari
Festo Polea na Kuruthum Ahmed

MTOTO Ramadhani Mussa (12) anashikiliwa na polisi Mkoa wa Ilala kwa kukutwa na kichwa cha mtoto mdogo Salome Yohana (3) alichokuwa amekibeba katika mfuko wa rambo.

Mtoto huyo alikutwa na kichwa hicho jana alfajiri baada ya kutiliwa mashaka na Fulgence Semfukwe ambaye ni mlinzi wa Chuo Kikuu cha Sayansi ya Afya Muhimbili wakati akijaribu kuingia chuoni hapo akiwa na mfuko mkononi.

Baada ya askari hao kumuuliza mtoto huyo hakujibu kitu na badala yake akatoa kichwa cha mtoto kilichokuwa katika mfuko huo na kuanza kuking'ata na kutafuna nyama yake jambo ambalo liliwastua askari hao kumweka chini ya ulinzi huku wakiwasiliana na askari polisi kwa msaada zaidi.

Polisi walipomhoji mtoto huyo alisema anaishi Jeti Lumo na anaishi na bibi yake aliyemtaja kwa jina moja la Andenga na kuongeza kuwa mama yake mzazi anaitwa Khadija na ni mkazi wa Tabata kwa Bibi.

Mtoto huyo alijieleza zaidi kuwa yeye na bibi yake huwa wanaishi kwenye makaburi yaliyopo Jeti Lumo na kazi yao huwa ni kula nyama za watu.

Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Ilala, Charles Mkumbo akizungumzia tukio hilo alisema linahusishwa na tukio lililotokea juzi saa 3.00 usiku ambapo mwili wa mtoto uliokotwa ukiwa umechinjwa kichwa eneo la Segerea.

Alisema katika tukio hilo, wakazi wa Kimara Baruti, Upendo Dastan (27) na mumewe Yohana Mussa Majani (26) aliyekuwa na mtoto wao Salome Yohana (3), juzi walikwenda kumtembelea bibi yao Furaha Majani anayeishi Segerea kwa Bibi kwa lengo la kulala huko.

Mkuu huyo wa upelelezi alisema walipofika kwa bibi yao mtoto wao alianza kucheza na ilipofika saa 3.00 usiku mtoto huyo akapotea katika mazingira ya kutatanisha.

Kamanda Mkombo aliongeza kuwa ilipofika juzi alfajiri, Lukas Kibaya (32) ambaye ni anafanya kazi ya kufyatua matofali katika eneo hilo alipokwenda kujisaidia chooni mita 800 kutoka kwa nyumba waliyofikia alikuta shimo la choo hicho limefunikwa na tofali huku likiwa limegandamizwa na nguo.

Alipolifunua akakuta kiwiliwili cha mtoto mdogo bila kichwa ndipo alipotoa taarifa polisi Sitakishari ambao walifika kuuchukua mwili huo hadi Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa uchunguzi zaidi.

Kamanda Mkumbo aliongeza kuwa baada ya kutukia tukio polisi iliwapeleka wazazi wa mtoto aliyepotea polisi kutambua kichwa cha mtoto kilichokamatwa na kuthibitisha kuwa ni cha mtoto wao.

�Tuliwasiliana na wazazi na wakathibitisha kuwa ndiye mtoto," alisema na kuongeza kuwa Ramadhani aliyekamatwa na kichwa hicho anashikiliwa na polisi SitakiShari kwa uchunguzi zaidi na kichwa hicho kimehifadhiwa katika katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Akizungumza na Mwananchi jana mama wa mtoto huyo, Upendo Dustani alisema mtoto wao Salome alishinda nyumbani kutwa nzima ilipofika saa 3:45 usiku baada ya kumlisha chakula cha usiku ndipo alipotoroka na kukutwa alfajiri akiwa amekufa.

Mama wa mtoto huyo alisema walikuja kwa ajili ya kumsalimia shangazi yake anayeishi Tabata Segerea ambaye hawakuonana kwa muda mrefu.

"Kifo cha mwanangu kimetokea katika mazingira ya kutatanisha na nina imani Mungu atatulipia kwa waliofanya kitendo hicho cha unyama", alisema mama huyo kwa uchungu.

Naye Mjumbe wa Shina wa eneo hilo, Salum Pembe alisema amepata taarifa hiyo alfajiri kutoka kwa majirani na kumueleza kuwa Salome alikutwa akiwa amekufa kwenye shimo la choo akiwa maiti yake ameviringishwa matambara na akiwa amekatwa kichwa.

hii nayo kali sasa duh nashindwa kushangaa sasaaa!
 
maendeleo ya sakata hili ni kuwa kichwa cha huyo mtoto kimeshatambuliwa na kijana alokamatwa nacho ameshikwa yeye na mama yake
 
Huyu mtoto Ramadhani ni wa kwenda kumpima akili! Si uchawi, ni matatizo ya kisaikolojia. Hii inachangiwa kwa kiasi kikubwa na kukithiri kwa imani za ulozi katika jamii yetu. Watoto wanakuwa na kuamini kuwa kweli nao wanaweza kuingia huko. Hayo yote ya makaburini, kusafiri kwa ungo ni vitu alivyosikia na kuja kuamini ingawa sidhani kama kweli alikuwa akivitenda.

Mungu ailaze mahali pema roho ya marehemu Salome.
 
(Sick)!!!!

sheria za Tanzania zinasemaje kuhusu hili? huyu kijana anastahili kifungo cha maisha bila parole, iwe katika juvenile prisons, au jela za wagonjwa wa vichaa, kama sio Kunyongwa!, (kumradhi Human right activists!)

' "hakuna dhambi kama kula nyama ya mtu, ukianza kula huachi"- JK Nyerere.'

Mbaya zaidi sasa inaonekana yeye kama 'wenzake' wana prey on young victims, imagine kabinti ka miaka mitatu maskini!?,

Imefika wakati serikali ipitishe sheria ili makosa haya ya kishirikina vifungo viwe ni maisha, kwani hata watoto mazeruzeru nao mashakani siku hizi!
 
Two Morogoro albino siblings under death threat

2008-04-27 10:57:00
By Peter Mwangu


The lives of Amina Abdul (11) and her brother Sadiki (13) are literally on the firing line. The youngsters, pupils at Mtibwa Primary School in Turiani, Morogoro, are being hunted by unknown people because they are albinos.

This has instilled fear and panic in the kids, as well as the school and Kidudwe village where they live.

This reporter has established that some strangers have been making enquiries on the siblings, who form part of the broader albino community in Tanzania who are targeted for murder, as a preamble for superstitious rituals linked to perceived fast wealth-generation.

Their schoolmate, Asteria Pascha, says: ``On Monday this week at around 4pm two short, tough-looking middle-aged men approached me while returning home after school. They asked me if I was studying alongside two albinos, to which I answered in the affirmative.

``I was very shocked when they offered to reward me handsomely with cash if I helped them get the pupils, who they said they wanted for a reason they did not disclose.

They explained that the exercise would be easy because they had established that the parents of the children had been away from the village on a paddy farming mission.``

Asteria said she was alarmed because she had heard news on the radio about albinos being kidnapped, killed, and some of their body parts being used for superstitious motives.

To play it safe, however, she faked co-operation by jotting down on a palm of her hand, a mobile phone number they gave her to facilitate follow-up contacts.

She explained, however, that the number was subsequently erased. She had not memorized it, and wasn`t keen to, because she wouldn`t contact them.

The girl reported the matter to the school administration which consolidated security around Amina and Sadiki, to protect them against abduction, particularly considering that they cover an eight-kilometre round trip to school and home, through a dense sugarcane plantation.

Sadiki was personally contacted by an unknown person who he feared was after him and her sister.

Sadiki said: ``One day two men (different from those who spoke to Asteria) came home with a box full of white garments like our school shirts and my sister Malizia Abdul was cooking in the house.

They told me that they had brought us some clothes but I declined the offer. They left, promising to bring more pleasant gifts on their return visit.``

Sadiki and his sister Amina have to walk the distance to and from school through the sugarcane plantations alone starting at 6am and late in the evening back home.

The school has reported the matter to respective authorities for further action on the security of the innocent kids. ``As teachers we are concerned.

We are taking necessary precautions to protect these kids and we have reported the issue to appropriate authorities,`` remarked a teacher who sought anonymity.

Abdul Said and Fatuma John, parents of the two albinos, have five children, Said, Idi and Malizia.

They lead a poor life and the health of Sadiki and Amina is not very good, due to their skins being too sensitive to ultra-violet radiation from the sun.

They have wounds almost all over their bodies due to poor shelter and medication.

More than 20 albinos have been killed in several parts of the country for purposes of getting rich.

SOURCE: Sunday Observer

Comment on this article
 
(Sick)!!!!

sheria za Tanzania zinasemaje kuhusu hili? huyu kijana anastahili kifungo cha maisha bila parole, iwe katika juvenile prisons, au jela za wagonjwa wa vichaa, kama sio Kunyongwa!, (kumradhi Human right activists!)



Mbaya zaidi sasa inaonekana yeye kama 'wenzake' wana prey on young victims, imagine kabinti ka miaka mitatu maskini!?,

Imefika wakati serikali ipitishe sheria ili makosa haya ya kishirikina vifungo viwe ni maisha, kwani hata watoto mazeruzeru nao mashakani siku hizi!


Mchongoma,

I get this feeling huyu mtoto alikua na wazimu na sio eti ni
ushirikina.He must have some psyche issues going on inside him!
 
Well mi nafikiri hapa pia chanzo ni lazima kijulikane maana hata akifungwa maisha huyu dogo, the person behind all this bado ataendelea kufanya mambo haya!!!
Huyo anayewatumia ni lazima awe tracked down na apewe adhabu kali... afungwe maisha na viboko 20kila siku!!!!
 
Huyu mtoto ni kioo cha jamii yetu. Imani za ushirikina zikishikamana si ajabu watoto nao wakiona wachangamkie dili! Ikiwa kila siku anawasikia wale anaowaheshimu wakizungumzia kwa imani masuala ya usafiri wa ungo, wanga, kuchuna ngozi na upuuzi mwingine kama huo ataacha kuamini? Ni sisi tuliowafikisha wote wawili, Salome na Ramadhani, hapo walipo. Sitashangaa kama sasa watashikwa wazazi wake, shangazi zake na bibi zake kwa tuhuma kama hizi ingawa pengine hawana hata hatia!
 
Kwa aibu nakumbuka wakati nikiwa mdogo nilifundishwa kutema mate kifuani nikikutana na albino (unaona sijui hata wenyewe wangependa kuitwa vipi!)ama sivyo balaa gani sijui itanikumba. Na sidhani kuwa ni peke yangu niliyefundishwa hivi. Ni hatua ndogo kutoka hapo hadi kujenga dharau ambayo nayo itafuatwa na kuwaona kuwa ni expendables! Kwenye hili la hawa ndugu zetu, wote tumo kama jamii. Ni wajibu wetu kama jamii kupiga vita imani na vitendo vyote viovu dhidi yao. Inabidi viongozi wetu wa imani zetu nao wainue sauti zao. Inabidi mashuleni watoto wote wafundishwe athari za aina yeyote ya discrimination. Serikali peke yake haitaweza ingawa hii isiwe kisingizio cha kutokufanya kitu. Bado wanawajibika kuwalinda kwa kadri ya uwezo wao na kuwasaka wale wote wanaowatendea maovu.
 
Mchongoma,

I get this feeling huyu mtoto alikua na wazimu na sio eti ni
ushirikina.He must have some psyche issues going on inside him!

...kuna mtoa mada mmoja hapo nyuma aligusia huyu mtoto 'Ramadhan', anahusiana na article iliyotoka kabla ya 31st March 2008 kwenye www.freemedia.co.tz na www.bongo5.com watoto wamtia 'changa la macho' Dr Rwakatare,
ni kweli???
au mkanganyiko wa majina tu?

Watoto wawili wanaojulikana kwa majina ya Yusufu na Ramadhani wamelidanganya kanisa la Mikocheni B la Assemblies Of God lililo chini ya Mchungaji Dk Getrude Rwakatare, wakijifanya wamedondoka kutoka angani walikokuwa wakiwanga baada ya kuchukuliwa na wachawi lakini kutokana na maombi ya waumini wa kanisa hilo ndiyo yaliyowaoko na ndizo sababu zilizowapelekea wao kuwasili kanisani hapo.

Habari kuhusiana na utapeli wa watoto hao uliwahi kutangazwa na kituo maarufu cha runinga hapa nchini cha ITV ambapo ulithibitishwa na kamanda wa polisi wilaya ya kinondoni bwana Jamal Rwambow na kudai kuwa kabla ya kujifanya wameangukia katika kanisa hilo, siku chache zilizopita wamewahi kufanya tukio kama hilo huko maeneo ya mbezi tangi bovu mnamo januari 6 mwaka huu.

"baada ya polisi kupokea taarifa hizo za watoto hao, vijana wangu walifika katika eneo la tukio huko mbezi na kuwachukua mpaka katika kituo kidogo kilichoko maeneo ya kawe na kuwahoji kasha kuwapeleka hospitalini kwa ajili ya uchunguzi wa afya zao ambapo wauguzi waliwacheki na kugundua hawana maradhi yoyote na baada ya muda tulipokea taarifa kutoka kwa raia wanaowafahamu vijana hao zikidai kuwa hawana lolote ni matapeli kwani mwanzoni mwa Februari waliwahi kujifanya wameangukia huko maeneo ya Manzese kwenye noja ya makanisa ya maeneo ambapo walichukuliwa na kupelekwa katika moja ya vituo vya kulelea watoto yatima huko maeneo ya kurasini" alisema Kamanda Rwambow.

...haya basi, kama ni wazimu, je wale wanaoua watoto maalbino?
 
Mchongoma,

Asante kwa kunipa taarifa.
Hao wanaoua mazeruzeru ni wahuni tu.
Wanalao jambo!
 
Huyu mtoto ndiyo yule aliyeanguka na mwenzie pale kanisani mikocheni b kwa mama rwakatare, kwa wale waliomuona siku ile watamtambua, ni yule yule. Pia kuna habari zinazagaa mtaani kuwa hii ni system at work kuhamisha fikra za wananchi kwenye discussion ya ufisadi????????????????
 
Ebwana hiyo inatisha inabidi sasa serikali iandae sheria mahsusi ya kudhibiti hivi vitu. Nadhani serikali imelifumbia macho limekuwa ni kama wimbo wa bongo flava utapigwa wee mwishowe watu wanachoka na kusahau. Haitofautiani sana na mauaji ya albino na uchunaji wa ngozi.
 
Asalamu alaykum.

Kama hana wazimu hupo na akili timamu basi ana udogo wa kufanya jambo bila ya kujua lazima anafahamu vyema kutokana na umri wake na kama anafahamu lazima angekataa kutumwa mambo mabaya kama hayo lakini amefanya kwa kujua kabisa.

lakini mimi nahisi wapo wakubwa wanaomtuma kufnaya vitendo hivyo na hao ndio wa kukamatwa kwa sababu wanaweza kusababisha watoto wnegi kuingia katika mchezo huo mbaya ambapo hivi sasa jamii yetu imekosa maadili mema vijana wengi wamekuwa na tamaa ya maisha na kukosa mafunzo mema kw ahivyo ni rahisi sana kuingia katika michezo michafu ya aina hiyo wakiwa na lengo la kupata fedha za kukimu maisha yao tu.
Mungu atusaidie lakini ni balaa kubwa sana ikiwa imani inamfanya mtu athubutu kumkata kichwa mwenzake? ni hatari kubwa sana.
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom