kimanu
Senior Member
- May 31, 2013
- 196
- 64
Mimi si mwanasiasa na wala sina chama. Lakini imenipasa kutoa maoni yangu leo hii nikiamini ukimya wangu, ilhali nina cha kusema, utakuwa ni chukizo kwa Mungu aliyenipa maono haya.
Haya matukio yanayotokea, mauaji hasa ya kigaidi ni ishara mbaya sana. Tunapokwenda sipo!
nachelea kusema kuwa, Watanzania wenyewe ndo tunajiwekea hali hizi wakati mwingine.
mfano, kwa miaka 50 chama tawala hakijatusaidia kitu. Ukiongea na kila unayekutana naye, analaumu na kuilaani CCM. Na wote wanajua kuwa, kura zao ndo zitaiondoa madarakani. Bt mwisho wa siku, utawaona kwenye kampeni na mikutano yao.
hii inawapa matumaini hata ya huko "kuchakachua" matokeo ya kura, na kusingizia halaiki ya watu kwenye kampeni kama ishara ya kukubalika. Kwanini msiwasusie hiyo mikutano yao? cuz hata sera zao for decades tushazikariri.
huu ni unafiki wetu. km kweli tumechoka utawala huu, moja ya viashiria ni kuwaacha majukwaani na kuongea kwa kura.
Pia, sidhani kwamba , just because CCM haifanyi vizuri, basi automatically chama pinzani ndo kinafaa. sio kila suluhisho la matatizo yetu CDM itatatua. Jino la pembe si dawa ya pengo.
cha msingi, yeyote mwenye dhamira ya dhati anaweza kuleta mabadiliko popote alipo na si viongozi pekee.
Kwa hali ilivyo, ningependa idadi ya wabunge wa upinzani iwe sawa na ya CCM ili yale makofi na zile "ndiyooo" zipate upinzani , hatimaye mambo ya kipuuzi yakose support kutoka kwa wabunge wa upinzani pamoja na CCM wachache wenye mapenzi mema.
Mungu ibariki Tanzania!
I dont see CCM madarakani 2015 km watanzania watajua wanachokitaka , h.o.n.e.s.t.l.y
Haya matukio yanayotokea, mauaji hasa ya kigaidi ni ishara mbaya sana. Tunapokwenda sipo!
nachelea kusema kuwa, Watanzania wenyewe ndo tunajiwekea hali hizi wakati mwingine.
mfano, kwa miaka 50 chama tawala hakijatusaidia kitu. Ukiongea na kila unayekutana naye, analaumu na kuilaani CCM. Na wote wanajua kuwa, kura zao ndo zitaiondoa madarakani. Bt mwisho wa siku, utawaona kwenye kampeni na mikutano yao.
hii inawapa matumaini hata ya huko "kuchakachua" matokeo ya kura, na kusingizia halaiki ya watu kwenye kampeni kama ishara ya kukubalika. Kwanini msiwasusie hiyo mikutano yao? cuz hata sera zao for decades tushazikariri.
huu ni unafiki wetu. km kweli tumechoka utawala huu, moja ya viashiria ni kuwaacha majukwaani na kuongea kwa kura.
Pia, sidhani kwamba , just because CCM haifanyi vizuri, basi automatically chama pinzani ndo kinafaa. sio kila suluhisho la matatizo yetu CDM itatatua. Jino la pembe si dawa ya pengo.
cha msingi, yeyote mwenye dhamira ya dhati anaweza kuleta mabadiliko popote alipo na si viongozi pekee.
Kwa hali ilivyo, ningependa idadi ya wabunge wa upinzani iwe sawa na ya CCM ili yale makofi na zile "ndiyooo" zipate upinzani , hatimaye mambo ya kipuuzi yakose support kutoka kwa wabunge wa upinzani pamoja na CCM wachache wenye mapenzi mema.
Mungu ibariki Tanzania!
I dont see CCM madarakani 2015 km watanzania watajua wanachokitaka , h.o.n.e.s.t.l.y