Mara yameonekana maandamano ya kuwapongeza polisi kuuwa wanaosemekana majambazi.
Kwamba maandamano hayo yamekuwa ya amani yakipokelewa na RPC wa huko, ni jambo la kupongezwa kwani haki ya kikatiba imetamalaki.
Hata hivyo kuna tashwishi za kutosha kuwa maandamano haya yameasisiwa na kuratibiwa na polisi wa huko kwa lengo la kuficha maovu yao au kujaribu kujisafisha.
Tuhuma hizi katika hali yoyote ile si za kupuuzwa.
Ikumbukwe kazi ya polisi ni kukamata watuhumiwa na kuwafikisha kunakohusika. Katu si kuwauwa kinyama kama inavyosemekana ilitendeka.
Wakati kunaitishwa uchunguzi kwenye kadhia tata hii, ni vyema polisi wakatarajia kuyapokea maandamano mengine ya amani pia, yenye kuwafikishia ujumbe wa malalamiko.
Ni muhimu wakaliona hilo kuwa ni jambo la kheri kwani wao "kama ma taxi dereva sisi sote ni abiria wao."
Ni vyema wakafahamu wengine tulikaa kwa kutulia wengine walipoandamana kuwaunga wao mkono. Hivyo iwe wakati wao nao wa kukaa kwa kutulia ili kuyapokea malalamiko yetu.
Tunaamini kwa mujibu wa sheria, mkuki hauwezi kuwa mtamu kwa nguruwe tu.
Shime waungwana.
Kwamba maandamano hayo yamekuwa ya amani yakipokelewa na RPC wa huko, ni jambo la kupongezwa kwani haki ya kikatiba imetamalaki.
Hata hivyo kuna tashwishi za kutosha kuwa maandamano haya yameasisiwa na kuratibiwa na polisi wa huko kwa lengo la kuficha maovu yao au kujaribu kujisafisha.
Tuhuma hizi katika hali yoyote ile si za kupuuzwa.
Ikumbukwe kazi ya polisi ni kukamata watuhumiwa na kuwafikisha kunakohusika. Katu si kuwauwa kinyama kama inavyosemekana ilitendeka.
Wakati kunaitishwa uchunguzi kwenye kadhia tata hii, ni vyema polisi wakatarajia kuyapokea maandamano mengine ya amani pia, yenye kuwafikishia ujumbe wa malalamiko.
Ni muhimu wakaliona hilo kuwa ni jambo la kheri kwani wao "kama ma taxi dereva sisi sote ni abiria wao."
Ni vyema wakafahamu wengine tulikaa kwa kutulia wengine walipoandamana kuwaunga wao mkono. Hivyo iwe wakati wao nao wa kukaa kwa kutulia ili kuyapokea malalamiko yetu.
Tunaamini kwa mujibu wa sheria, mkuki hauwezi kuwa mtamu kwa nguruwe tu.
Shime waungwana.