Maua kupandwa barabarani

Power to the People

JF-Expert Member
Jul 11, 2007
1,198
892
Weekend hii nilikuwa Arusha, nilishangaa sana baada ya kuona maua yanapandwa sehemu za parking ya magari along sokoine au auhuru road.

Nilishangaa kwa sababu ukiangalia ufinyu wa sehemu ya kuegesha magari katika mji wa Arusha jambo linalokujia akilini ni jinsi ya kuongeza sehemu za parking hasa hasa katikati ya mji na sio kuzipunguza.

Sijui nani anawashauri hawa wanaopanda miti na kuizungushia matofali ambayo yameshagongwa na kubomoka. Hizo fedha haziwezi kutumika katika shughuli muhimu zaidi kama vile uzoaji wa taka zilizozagaa kila mahala?
 
Je, kwa sababu parking hazitoshi basi tungoe miti na maua ili kupisha magari? Maua/miti yana faida zake pia kwa wakazi wa mji. Imagine Co2 zinakuwa emitted na magari halafu hakuna mimia ya kuabsorb angalau sehemu ya Co2 hiyo!
 
Je, kwa sababu parking hazitoshi basi tungoe miti na maua ili kupisha magari? Maua/miti yana faida zake pia kwa wakazi wa mji. Imagine Co2 zinakuwa emitted na magari halafu hakuna mimia ya kuabsorb angalau sehemu ya Co2 hiyo!

Hujaelewa. Sio kama miti ilikuwepo ikwatwe kuongeza parking. Ni kwamba wameamua kuchimba barabara sehemu za parking ili kupanda miti.

Hao municipal fathers hawatumii hata chembe ya akili. Kwanza wanapunguza parking, pili , naturally hizo kingo zitagongwa na kagari kwa sababu hazikupangwa .(planned before) Mimi naona kama ni miti wangepanda zaidi zile sehemu ambazo ni za wazi na haziingilii shughuli nyingine. Kuotesha miti barabarani kwenye lami ni upuuzi mtupu.

CO2 sio lazima iwe absorbed barabarani. Na kama wanafikiri hivyo leo ,walikuwa wapi miaka yote hii? Wizi tu
 
Je, kwa sababu parking hazitoshi basi tungoe miti na maua ili kupisha magari? Maua/miti yana faida zake pia kwa wakazi wa mji. Imagine Co2 zinakuwa emitted na magari halafu hakuna mimia ya kuabsorb angalau sehemu ya Co2 hiyo!

We ushawahi kuona miti inapadwa mpaka kwenye zebra crossing in the middle of the road. I should have taken a photo halafu niipost hapa.

Yaani imekuwa kero madereva wanakosa parking na ole wako uegeshe gari kombokombo watu wa parking system wanakutokea na kukutaka ulipe fine kwa kuegesha vibaya. Nasema haya kwa sababu kwa muda mfupi niliokuwepo Arusha nimepata usumbufu mkubwa.
 
Poleni sana na usumbufu mnaoupata wana arusha lakini hata hayo maua ni aina ya kivutio labda muwasiliane na uongozi wa jiji mshauriane na ikibidi basi watenge sehemu maalum za parking
 
sikiliza mkubwa moja kati ya vivutio vikubwa vya sehemu husika ni pamoja na mandhari iliyopo
uwekwaji wa maua huko arusha ni moja kati ya mipango ya kupendezesha mji huo hususani ukiwa ni financial center inayokuwa kwa haraka
hivyo basi maua ni bora ya wepo na magari si lazima mkubwa!!!
 
kaka/dada uliyopost mada hii unaonekana huna elimu ya darasani na hata ikaundwa wizara ya mazingira,wizara ya maliasili bodi mbalimbali,Nemc,hata waandishi wa habari wa mazingira na hata ujenzi pia kabla haujafanyika unatakiwa utafiti wa kutosha kuhusu mazingira-enviroment impact assessment, na mtu au mkandarasi mbora ni yule anayejenga na kujali au kufata mazingira yalivyo.
tatizo lako kila kitu wanavyofanya aidha halimashauri au manispaa wakifany autajua ufisadi ondoa zana hiyo. hata hiyo global warming japo huku nchi zetu za afrika effect yake siyo kubwa sana ndiyo maana huoni umuhimu wake. kumbuka kuna siku ya mazingira na upandaji miti.
soma sana au angalia mtandao na siyo kulaumu kila kitu kwa serikali.
 
kaka/dada uliyopost mada hii unaonekana huna elimu ya darasani na hata ikaundwa wizara ya mazingira,wizara ya maliasili bodi mbalimbali,Nemc,hata waandishi wa habari wa mazingira na hata ujenzi pia kabla haujafanyika unatakiwa utafiti wa kutosha kuhusu mazingira-enviroment impact assessment, na mtu au mkandarasi mbora ni yule anayejenga na kujali au kufata mazingira yalivyo.
tatizo lako kila kitu wanavyofanya aidha halimashauri au manispaa wakifany autajua ufisadi ondoa zana hiyo. hata hiyo global warming japo huku nchi zetu za afrika effect yake siyo kubwa sana ndiyo maana huoni umuhimu wake. kumbuka kuna siku ya mazingira na upandaji miti.
soma sana au angalia mtandao na siyo kulaumu kila kitu kwa serikali.

jamani hakuna mtu anasema halmashauri zisipande miti tena miti ipandwe kwa wingi pale inapotakiwa na sio halmashauri tu yeyote yule mwenye uwezo wa kupanda miti na apande. let us be serious kwa kweli hili la kupanda mti barabarani haliniingi akilini, I mean hauhutaji hata elimu ya darasani kutambua kwamba you cannot plant trees or plants for that matter barabarani tena wakati sehemu yenyewe ni finyu you just need to use your common sense. Muda sio mrefu matofali yaliyojengewa kuzunguka mimea hii yataboka yote kama hayajabomoka by now. this is wastage of money

Mbona kuna maeneo mengine ya barabarani ambayo yamepandwa miti na hakuna anayesema chochote. hata hivyo kuna sehemu nyingi sana ambazo wanaweza kupanda miti na ikastawi vizuri bila kutumia gharama ambayo inatumika sasa.

if you had any idea of what Environmental Impact Assesment entails usingesema kwamba ilifanyika kabla ya maamuzi ya kupanda hii miti or plants hayajachukuliwa, au ilifanyika katika ile stayle ya Zima Moto??
 
yeyote anayesupport wanachofanya Municipals kule arusha nadhani hajafika akaona mwenyewe. hata mtoto wa shule ya msingi hawezi kutoa ushauri wa vile. Ile ni upotevu tu wa mali za nchi hii. hata wangekuwa wanafanya evaluations matofali ambayo yameshakanyagwa na magari ni mengi kuliko ambayo bado mazima. Hii pekee yake inaprove kuwa ule mradi wao siyo endelevu!
 
yeyote anayesupport wanachofanya Municipals kule arusha nadhani hajafika akaona mwenyewe. hata mtoto wa shule ya msingi hawezi kutoa ushauri wa vile. Ile ni upotevu tu wa mali za nchi hii. hata wangekuwa wanafanya evaluations matofali ambayo yameshakanyagwa na magari ni mengi kuliko ambayo bado mazima. Hii pekee yake inaprove kuwa ule mradi wao siyo endelevu!

Tuma picha ya hiyo mandhari ya upandaji miti hapo Arusha ili kama tunachangia mawazo basi tujue tatizo ni lipo wapi na pengine tunaweza kuwashauri jinsi ya kufanya kwa baadaye.
 
yeyote anayesupport wanachofanya municipals kule arusha nadhani hajafika akaona mwenyewe. Hata mtoto wa shule ya msingi hawezi kutoa ushauri wa vile. Ile ni upotevu tu wa mali za nchi hii. Hata wangekuwa wanafanya evaluations matofali ambayo yameshakanyagwa na magari ni mengi kuliko ambayo bado mazima. Hii pekee yake inaprove kuwa ule mradi wao siyo endelevu!

it is unbelieveable and if seeing is believing then you have to see the actual location of the plantings to believe how the muncipality can get away with such blantant stupidity or more correctly ufisadi.
i hope there is somebody who can provide the actual cost of this project and then we will all say --- aaahhh kumbe.
 
Back
Top Bottom