Matusi ya Lema na Matusi ya Lusinde ni Matusi Yetu na Unafiki Wetu!

Nakubaliana na MwanaJF Waberoya, kwamba Matusi ni Matusi, hata kama yanatolewa na supporters na wapenzi wetu. Kama Chama tusipoyakemea, tutaendeleza unafiki na hatimaye tutashindwa kutekeleza yale mema tunayonuia.

Chadema kilipozinduliwa, nakumbuka Mzee Edwin Mtei akisisitiza sana umuhimu wa kuelezea sera na misimamo ya Chama, kwa ufasaha na kwa lugha isiyo na matusi au maneno ya kashfa hadharani. Wakati huo CDM ilieleza utamaduni wa siasa za kisayansi na "kimantiki"! Wengi waliomsikiliza Mzee Mtei walisema huyu hakuwa "mwanasiasa"!

Hata hivyo sasa CDM kimekua na kwa kawaida ni chama kisichosheheni lugha chafu; na umakini na umahiri wa viongozi wake kuchambua matatizo na mustakabali ya taifa unajulikana. Kama ni Dk. Slaa, kama ni Freeman Mbowe au Zitto Kabwe, wote hawa sio tu wanajulikana, bali wanakubalika. Ni utamaduni wa kujivunia.

Kama kutokana na kasi ya CDM kukua na kupanuka, kuna vijana wasiotilia maanani utamaduni wa lugha safi ya Waasisi, huu ni wakati wa kutathmini mikakati ya kuwavunda. Hata hivyo ni vizuri tutambue kuwa wakati wa kampeni ni lazima mapungufu ya wagombea yatatajwa na wapinzani; kama wao wanavyojivunia ubora wao.

Lakini kwa maoni yangu mgombea anayedhani amekashifiwa au kudhalilishwa kwa mapungufu yake kutajwa hadharani, hana budi kujitokeza binafsi na kueleza korti. Kujitokeza kugombea nafasi ktk madaraka ya umma, lazima kutafsiriwe kwamba ni kukubali kuanikwa kwa mapungufu yako. Hii haimaanishi matusi na maneno yasiyotamkwa mbele ya watu wastaarabu e.g yale ya Lusinde yaruhusiwe.

Wakati mwingine, mapungufu yanaweza kutajwa kwa lugha ya kisanii, ili muhadhara ucheke au uelewe zaidi. Kwa mfano wavulana wa "kisasa" waliotoka ng'ambo wametoboa masikio, na wakiwa wagombea wanambiwa watalipiwa nauli kwenda Mombasa kwa shoga wenzao!!. Kama mgombea mvulana aliyetoboa masikio, anaona hilo ni tusi, basi, it is too bad!!

 
Webby,
Tatizo ni Pro-Chadema wanataka tuchukizwe na matusi ya Lusinde halafu tufurahishwe na matusi ya Lema haiwezekani hata kidogo.

Mahakama imesema Lema alithibitika kutenda kosa la kutumia maneno yasiyostahili kwenye kampeni zake.

Ebu tujikumbushe maneno ya Lema "Dr Burian sio mwanamke mwaminifu aliyezaa nje na kupata mimba nje ya ndoa".

Hayo maneno ya Lema ni "Illegal Campaign" inatosha kutengua matokeo ya uchaguzi kwa mujibu wa kifungu 114 cha sheria ya uchaguzi inayozungumzia Illegal.
 
Katika hili ni vema tuwe wazi,mosi,Lema hakuvuliwa ubunge sababu ya matusi bali ni pamoja na kumnyanyasa na kuchochozea dhahiri ubaguzi wa kidini, kijinsia na kieneo dhidi ya aliyekuwa mgombea wa CCM, Pili sheria inawaruhusu wapigakura kufungua kesi ya namna hiyo. Cha msingi tutoe fursa kwa viongozi wa CDM kupitia hukumu dhidi ya Lema na kuja na tamko la chama. Binafsi nina imani kubwa na busara za viongozi wa CDM. Tusubiri!
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
Kuna tatizo kuu la msingi ambalo nisiposema dhamiri yangu itanihukumu na sitakaa kimya kwa sababu wengine wameamua kukaa kimya.

Jamii ya Tanzania iko kwenye ugonjwa mkubwa na tusipoudhibiti huu ugonjwa hakuna wa kutusaidia. Tunaiumiza jamii, tunaharibiu vizazi vijavyo kwa kisingizio cha mabadiliko!

Sera ya chadema si matusi!! Sera ya chadema ni mabadiliko, sijawahi kuona Slaa akitoa matusi ya nguoni, sijawahi kuona Mbowe akitoa matusi ya nguoni, wala sijawahi kuona Zito akitukana, these people they are still high in their positions na popular kwenye siasa na wanaaminika kwenye jamii kwa kuleta mabadiliko

Ila nimemsikia Mdee akitukana( personally nilimkataza) , nilimsikia Lema akitukana, tumeona Sugu akitukana mpaka kujirekodi!! Hawa ndio wabunge wetu, ndio tuliowapa dhamana ya kuongoza taifa letu kwa nafasi zao…ila wanatukana, wakitukana hawa ni sawa??

Nani kasema?

Kuna uwezekano mkubwa akina Mbowe, slaa hawawezi kuwadhibiti akina Lema, kwa sababu ya kuwaonea aibu!! Unapopagawa na siasa na kuona kila unachotukana kinashangiliwa, basi jamii nzima inakuwa imeoza! Msikilize Lusinde utaamini!

ILA; Ukiwa mpinzani lazima uangalie zile nafasi/chances/ opportunities ambazo adui yako anaweza kuzitumia kukuangamiza!

Kama CCM wametumia mahakama kumuondoa adui yao Lema, it is okay na wametumia karata yao vizuri sana.

Lakini kama si CCM na mahakama, je matusi yanakubaliwa katika jamii yetu??

Hivi Mdee, sugu, Lema na Lusinde tofauti yao ni nini??

Na sisi wataka mabadiliko , ukweli wa mioyo yetu na matusi uko wapi? Kuwa tutukane tu kwa sababu kwa kufanya hivyo ndio tunahimiza moto wa mabadiliko??

Matusi mangapi yanatukanwa humu ndani? Wanaotukana ni akina nani? Je wakipewa uongozi hawatatukana kwa sababu ni viongozi? Yaani uongozi una mechanism ya kuzuia matusi biologically? Matusi tumeyakubali, tunaishi nayo, tunalala nayo kila kona ya nchi yetu si kwa hao niliowataja, yako kila kona, kwenye madaladala, kwenye michezo name it!

Lema ameadhibiwa na mahakama, Lusinde ameadhibiwa na wananchi-ambao wengi wao wanatukana, mwisho wa siku wote ni watukanaji! Ikifika hatua tukaona Lema ni shujaa tunakuwa tumevua akili zetu na utu wetu na kuuweka kando na sisi……..tunaishi kinafiki , tuna post kinafiki kwani usafi na intergirty is not part of our life!!


In this case mahama iko clean..tena wanapongezana, hivi..juzi tu tumelia Lusinde anatukana-tukasema kila kona na kulaani, leo hii Lema anavuliwa ubunge kwa kutukana tunaona ubaya?? Kweli??

Hivi mwanamke kuambiwa ana mimba na mtu kusema kuwa mila za kiarusha au kimasai haziruhusu mwanamke kuwa kiongozi ni matusi.
Naomba wenye majibu sahihi atupie hapa.
 
Wakuu mimi napata shida na sheria/mahakama,eg matusi ya Lusinde yamesemwa sana,na yamejiidhirisha kwa wengi naamini hata Rais,Pm na baadhi ya mahakimu.Hata yeye Lusinde amekiri kwenye baadhi ya vyombo vya hbr pia kaomba msamaha wa kulazimishwa. Lakini leo hii mimi kama mwananchi wa kawaida nisiyejua vizuri taratibu za mahakama,nikifungua kesi kumshitaki Lusinde na kesi kuendeshwa na hakimu/jaji aliyesikia clip ya matusi ya Lusinde naweza kushindwa hiyo kesi.Hapa ndio napata shida na haya m
 
kwa hiyo kutukana kidogo is okay, ila kutukana sana si sawa?? mnataka ushahidi wa matusi ya lema ili hali amevuliwa ubunge na mahakama kwa kutukana matusi!!! what a joke
Mahakama ipi?
Mahakama hii hii iliyomfunga dereva wa wangwe miaka 3 kwa kuendesha gari bila leseni na kusababisha kifo?
Mahakama hii hii iliyompiga faini chenge ya laki 7 kwa kugonga watu 2 na kusababisha vifo pamoja na kupatikana na hatia ya kuendesha gari yenye bima ya kughushi?
Au mahakama ipi unayosema ww?
 
Hivi mwanamke kuambiwa ana mimba na mtu kusema kuwa mila za kiarusha au kimasai haziruhusu mwanamke kuwa kiongozi ni matusi.
Naomba wenye majibu sahihi atupie hapa.

KOMBARJR,
Lema kasema Dr Burian kapewa mimba nje ya ndoa aliyempa mimba sio mume wake usitake kupotosha.
 
Katika hili ni vema tuwe wazi,mosi,Lema hakuvuliwa ubunge sababu ya matusi bali ni pamoja na kumnyanyasa na kuchochozea dhahiri ubaguzi wa kidini, kijinsia na kieneo dhidi ya aliyekuwa mgombea wa CCM, Pili sheria inawaruhusu wapigakura kufungua kesi ya namna hiyo. Cha msingi tutoe fursa kwa viongozi wa CDM kupitia hukumu dhidi ya Lema na kuja na tamko la chama. Binafsi nina imani kubwa na busara za viongozi wa CDM. Tusubiri!
Na mm najiandaa kwenda kumshtaki lusinde kwa niaba ya Slaa, Mbowe, Nassari, na Lema!
 
Webby,
Tatizo ni Pro-Chadema wanataka tuchukizwe na matusi ya Lusinde halafu tufurahishwe na matusi ya Lema haiwezekani hata kidogo.

Mahakama imesema Lema alithibitika kutenda kosa la kutumia maneno yasiyostahili kwenye kampeni zake.

Ebu tujikumbushe maneno ya Lema "Dr Burian sio mwanamke mwaminifu aliyezaa nje na kupata mimba nje ya ndoa".

Hayo maneno ya Lema ni "Illegal Campaign" inatosha kutengua matokeo ya uchaguzi kwa mujibu wa kifungu 114 cha sheria ya uchaguzi inayozungumzia Illegal.
Tuwekee hiyo Clip ya Lema akitukana tuione..ya lusinde iko madukani inauzwa sh 1000
 
Ninaikumbuka sana kauli ya Mwl Nyerere aliyoitoa 1995 ktk mkutano na waandishi wa habari juu ya Nyufa za taifa.Wakati akizungumzia suala la rushwa na mahakama zetu alisema,"SHERIA NA HAKI NI VITU TOFAUTI".Ni kweli jaji ametumia sheria kutengua ubunge wa Lema lkn je,HAKI IMETENDEKA??
 
WanaJF,

Nimerudia kusikiliza rekodi ya hotuba ya Livingstone Lusinde, Mbunge wa Mtera (CCM) wakati akimwaga MATUSI katika kampeni za uchaguzi mdogo wa jimbo la Arumeru Mashariki, mkutano wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya Ngarasero. Nimeandika zaidi ya sentensi 15, ambazo ni matusi au zina viashiria vya lugha ya matusi.

Karibuni, Katibu Mkuu wa CCM, Mh. Mkama amesikika akitetea kwamba Lusinde alikuwa anajibu hoja za wapinzani wake, CDM.

Aidha jana, tarehe 5/4/12, ubunge wa Mh. Godbless Lema (Arusha Mjini, CDM), umetenguliwa kwa kile kinasemwa kufanya kampeni bila kuzingatia maadili ya kampeni, ikiwepo matumizi ya lugha inayotafasiriwa kwamba ni matusi. Jambo zuri tu, kama kweli tunataka kulenga kampeni za kistaarabu!

Katika dk 16:06 zilizorekodi hotuba ya Lusinde kama ilivyo katika mtandao, nimetambua mambo haya kama matusi au lugha ya matusi, wastani wa karibu sentinsi/tusi moja katika kila dk moja aliyotumia kuongea Lusinde:-

  1. Kuda-dada-deki (amerudia karibu mara sita).
  2. Wewe umekuwa ukiwachanja chale mpaka matakoni (akimlaumu Prof. Majimarefu).
  3. Hata wao ni mashoga basi, (akihusisha kutoga masikio na suala la ushoga).
  4. Nani hafahamu kwamba mbunge wa Arusha mjini aliolewa kule mahabusu/amepata bwana, (akihusisha Lema kuwa mahabusu na kwamba aliolewa), (ikiwa ni sodomization kwa tafsiri yangu).
  5. Dk. Slaa alitimuliwa uPadri baada ya kuwatia mimba wanakwaya. (akimtukana Dk. Slaa moja kwa moja)
  6. ***** huyu - Vicent Nyerere, ana akili mbovu. (akimtukana Mh. Vicenti Nyerere)
  7. Ameliwa -------- siye hatusemi. (ikimaanisha kuwa sodomized, iwapo sikujua anamtukana Vicent Nyerere au Godbless Lema).
  8. Acheni ushamba nyie. (akiwatukana wananchi, ambao wanaonyesha kuwa wafuasi wa CDM)
  9. Washamba wakubwa nyie x 2. (akiwatukana wananchi)
  10. Washamba wakubwa ----, Dk. Slaa mshamba mkubwa, akivaa kombati, anakuwa kama kajinyea. (akimtukana Dk. Slaa)
  11. Viongozi wa CDM vichaa wa kulogwa. (akiwatukana viongozi wa CDM)
  12. Dk. Slaa anatishia kujamba wakati anaharisha. (akimtukana Dk. Slaa)
  13. Sera ya CDM ni sera ya jogoo, jogoo linamuahidi kuku gauni, huku lenyewe hata chupi halina. (akikitukana chama kwa ujumla wake).
  14. Mbowe anasema ana uchungu, kwani ana mimba? (akimtukana Mbowe)
  15. Mbowe pigwa mimba! Slaa pigwa mimba! Nasari pigwa mimba! (akiwatukana Mbowe, Slaa na Nasari).

Sasa, nimeambiwa kupitia vyombo vya habari kwamba watu 3 ndiyo waliomfungulia mashtaka Mh. Godbless Lema, kufanya illegal practices katika kampeni wala siyo aliyeshindana naye katika ubunge Batilda Burian, vema. NANI WATAMFUNGULIA MASHTAKA LUSINDE KWA KUFANYA ILLEGAL PRACTICES katika kampeni za Arumeru Mashariki kama kweli tunatendeana haki?

Sentensi na maneno ya viashiria vya matusi niliyotaja mnaweza kuyafanyia uchambuzi zaidi, na kurudia kuisikiliza hotuba ile ili kujenga hoja vizuri. Najua kuna mdau alikwisha uliza hoja kama hii humu mtandaoni, lakini sijui hatua gani zimeendelea kuchukuliwa.

Nasisitiza wanasiasa kujenga hoja za msingi wakati wa kampeni. Ushahidi unajionyesha wengi wamekuwa wanajikita zaidi katika kumshambulia mgombea kuliko kushambulia-kwa uchambuzi na mikakati mambo ambayo ni matatizo na changamoto katika maendeleo ya wananchi. Lusinde alitumia zaidi ya dk 15, kushambulia watu, sio kushambulia kwa uchambuzi na mikakati matatizo ya wanaArumeru Mashariki.

Kwa mzaha kabisa, Katibu Mkuu wake anaunga mkono kwamba huko ilikuwa kujibu hoja za wapinzani wake. Hapa unajua unashindwa kutafsiri hekima na busara ya kiongozi mkuu wa chama, katika kukiwezesha chama chake kupaa na kuaminiwa. Sijui bwana, SIKIO LA KUFA HALISIKII DAWA!


Perecy Ugula
MwanaJF Mchanga,
Email: ugulapp@yahoo.co.uk
Simu: +255 766 082388


Surely!! sijasikia watu wakimjia juu Mkama kama walivyofanya kwa Lusinde...next time M-CCM mwingine atatukana akijua atatetewa na Mkama

Tukiibariki hii tabia tutatukana mpaka makanisani na misikitini

kwani hivi sasa matusi yanatukanwa kila kona nchi hii...kwa DSM wanaoongoza kwa matusi ni wazee!! acha kabisa wazee wengi wanatoa maneno machafu huwezi kuamini

kuna wakati unasikia tusi linapigwa sehemu fulani wakati uko na mkeo, mtoto, hata wazazi!!! tunacheka, tunafurahi tunapiga ,makofi...askari nimeshuhudia nao wanatukana kabisa
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
Hivi mwanamke kuambiwa ana mimba na mtu kusema kuwa mila za kiarusha au kimasai haziruhusu mwanamke kuwa kiongozi ni matusi.
Naomba wenye majibu sahihi atupie hapa.

Mimba inatamkwa jukwaani?? grow up man,.....usifikiri wengine sio CDM humu. acha kutetea uovu!! mila siyo jamhuri...sawa???
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
Mahakama ipi?
Mahakama hii hii iliyomfunga dereva wa wangwe miaka 3 kwa kuendesha gari bila leseni na kusababisha kifo?
Mahakama hii hii iliyompiga faini chenge ya laki 7 kwa kugonga watu 2 na kusababisha vifo pamoja na kupatikana na hatia ya kuendesha gari yenye bima ya kughushi?
Au mahakama ipi unayosema ww?

unasema mahakama ipi wewe,

nazungumzia mahakama ambayo Lema alikuwa anaenda kila siku kusikiliza kesi

kama ulion mahakama haiko fair ulitakiwa kumshauri Lema kutopoteza muda kwenda kusikiliza

hivi wapinzani hawajahi hata siku moja kushinda kesi yeyote ile?? ilikuwa mahakama gani??
 
Batilda kuambiwa kazaa nje ya ndo si tusi...privided hajaahi kuja court kukanusha....ila kumwabia mtu ...KAMA KAJ..EA nitus dhahari hata mtoto anajua....usitake kulinganisha manano ya LEMA na matusi ya LUSINDE

hizi ndio sera za chadema...kuwa fulani kazaa nje ya ndoa...hivi tukianza kutajana waliozaa nje ya ndoa mbona wako wengi?? slaa na josefine wamefunga ndoa? mtoto wa slaa akisikia unasema wazazi wake hawajafunga ndoa kwa hiyo ni mtoto wa nje ya ndoa atajisikiaje?? guys grow up stand for the truth..matusi ni matusi haijalishi nani katoa na katoa wapi, wakiwa na lengo gani
 
Waberoya unafikiri sana na hujawa addicted na politics za Bongo.Siasa zetu huwa za kulewa na chongo turns to Kengeza.Binafsi wote wenye matatizo ya kufanana wawajibishwe tu yaani Mkapa(kama kuhoji uhalali wa Vicent ni tusi),Vicent Nyerere (kama kumuhusisha mkapa na kifo cha Kambarage ni tusi),Mndee,Sugu,Lema, Lusinde wote ni ''manzi ga nyanza''

kweli kabisa mkuu wote ni 'manzi ga nyanza'
 
Waberoya umesema vizuri, lakini ushahidi wa matusi ya Lema uko wapi? Hebu tuwekeeni hapa ushahidi wa Matusi ya Lema.

nikuwekee ushahidi wakati amevuliwa ubunge?? usinichekeshe
 
Kamanda naona umeweka nyama za kutosha kwenye makala yako.Unaweza toa angalau clip moja ya ushahidi wa matusi ya Lema na Mdee kama ilivyofanyika kwa Lusinde?. Umenifunua kumbe Mdee na Lema nao ni watukanaji ! !

unauliza mdee wakati juzi tuliongozana na slaa kwenda kuomba msamaha kwa mbatia kesi ifutwe??

unauliza Lema ili hali yeye hajabisha?? duh upenzi huu jamani hatari
 
Mkuu Apolycaripto,

Ulishasikia matusi ya Sugu kwenye jukwaa la Siasa?

Hapa anachosema Waberoya ni zile nyimbo aliimba kuwashambulia Redio ya Wafu. Hizo hazikuimbwa kwenye Jukwaa la Siasa. Sijui kama unafuatilia sawasawa kila kinachoendelea hapa na huko tulikotoka.

Kumbuka kuwa kuna maneno hutamkwa, kila mtu anajua fulani katukanwa ila huwezi kuthibitisha kuwa ni tusi. Obama alivyomwambia Sarah Pallin kuwa "Nguruwe atabaki nguruwe hata kama akipakwa Lipstick" watu walielewa ni nani anapewa habari zake ila huwezi kuthibitisha kwa asilimia mia 100 kuwa alimaanishwa fulani.

Mdee anafanya kosa kutaja jina la mtu. Ingelitosha tu kusema kutumia lugha ya picha na kuacha watu wafikiri kidogo na kukumbuka kuwa hapo alimaanishwa fulani.

Anyway, tunashukuru kuwa kuanzia sasa, itabidi viongozi kwenye kampeni wawe makini na si kutumia matusi. Ila kwa hali ya Tanzania ilivyo, nilifikiri tutaanzia na waliotoa RUSHWA na kuchakachua na ndiyo tuje kwenye matusi. Ila Watanzania kama kawaida yetu, tunaanzia na kununua matairi na kesho ndiyo tufikiri kununua gari. TUTAFIKA TU.
Sikonge

Napata shida kidogo kukupata kwa kile unachojaribu kuharalisha hapa.Tambua siasa ni disciplinary code of conduct na players wake ni waomba kura na wapiga kura.Huwezi kusema eti wasanii wanahurumiwa kutumia lugha zao za kitaa katika jukwaa la siasa.

Tusi ni tusi tu na adhabu yake ni pale anayetukanwa ama jamii ikilichukulia kama tusi na si utani.Tujenge heshima tunapokuwa majukwaani kwani wanaotusikiliza ni (wazee,vijana,watoto,baba,mama,wakwe n.k).Siasa za kihuni hazikubaliki kwa namna yeyote.
 
Back
Top Bottom