Wewe ni mzoefu sana wa siasa za Bongo lakini huzielewi kila siku unakuwa kama mgeni.Anabadilika taratibu baada ya watu kumsemea hovyo mitandaoni hasa kule Twitter wakiwemo wanafunzi wake wa UDSM ambao wanamzodoa sana kuhusu kubadilika sana baada ya kuula uKM.
Huyu jamaa hapendi kushindwa ndo maana anapenda igi na askofu.nimeirudia sana clip yake huyu jamaa kuna siku Kwa mfano wa mbwa ataongia msikitini na jiwe hapo ndo itakua mtafaruku.lakini nadhani jiwe haoni kasoro yoyoye Kwa mbwa wake na mapenzi kwake yamezidi.so kuna siku atam-adhirisha mbele ya wenye heshma na itakua too late.Dk Bashiru amuombea msamaha Makonda
Thursday May 9 2019
Kwa ufupi
Katibu mkuu wa CCm, Dk Bashiru Ally amesema kutokana na kutofanyika kwa kazi ya kuandaa viongozi bora matunda ya kutoandaa vijana yameanza kuonekana.
By Aurea Simtowe, Mwananchi asimtowe@mwananchi.co.tz
Dar es Salaam. Katibu Mkuu wa CCM, Dk Bashiru Ally amesema kutokana na kutofanyika kwa kazi ya kuandaa viongozi bora matunda ya kutoandaa vijana yameanza kuonekana.
Ameyasema hayo leo Alhamisi ya Mei 9, 2019 katika ibada ya mazishi ya Mwenyekiti wa kampuni za IPP, Reginald Mengi inayofanyika katika kanisa la KKKT Usharika wa Moshi mjini.
“Kuwa viongozi bora, watiifu, wanyenyekevu na wenye heshima, naomba nitumie fursa hii kumuombe msamaha kijana wangu Makonda mimi namfahamu na hii ni mara yangu ya pili namsema hadharani,”
“Mara yangu ya kwanza nilimsema Simiyu akaja analia ofisini nikasema ubadilike na kwa kweli ameanza kubadilika, bado ni kijana mzuri, shupavu lakini tunahitaji kuwasaidia vijana wetu,” amesema Dk Ally
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema kitendo cha Dk Bashiru kuomba radhi kwa niaba yake ni upendo wa hali ya juu lakini alibainisha kuwa huenda trafsiri ya maneno aliyoyatoa hayakueleweka vizuri.
“Mimi niombe radhi kwa tafsiri hiyo kwa sababu nimemsifia mchaga katikati ya wachanga siyo mchaga katikati ya kabila lingine, mapokeo na nitaendelea kumuenzi mzee Mengi kwa mema yote aliyoyafanya kwa walemavu hasa katika mkoa wetu yatabaki kuwa alama,” amesema Makonda
Kumbe hata Raisi hatukumuandakutokana na kutofanyika kwa kazi ya kuandaa viongozi bora matunda ya kutoandaa vijana yameanza kuonekana,"
Wahuni hawa, uhuni ndio unao wapa hivyo vyeo sasa hawawezi uache uhuni wao.
Exactly, UVCCM ni sehemu sahihi ya mafunzo ya uhuni wa siasa. Kwani mmesahau huyu alipanda ghafla baada ya kumlipikia Lowassa wakati akiwa sijui mlezi sijui kitu gani cha UVCCM kuhusu majengo ya UVCCM na mikataba yake?
Hapo ndipo Kikwete akampa ukuu wa wilaya ghafla.
Unapoonjesha uhuni uliotukuka ndani ya UVCCM ndipo unapewa ulaji zaidi.
Hivi hawa wote anaowasema Bushiru si wamepitia UCCM? Nilidhani UVCCM ni jumuiya ya vijana wa CCM na huko ndiko palitakiwa kama kuna maandalizi yoyote yafanyike huko. Sasa Leo Bushiru anaposema na nanukuu, " kutokana na kutofanyika kwa kazi ya kuandaa viongozi bora matunda ya kutoandaa vijana yameanza kuonekana," anataka kutuambia nini? Kwamba huko UVCCM wanaandaa tu vijana wahuni tu kama tunavyoshuhudia kila leo?
Kama ni hivyo tatizo linalolikabili taifa si dogo kwani hawa hawa wahuni ndio huteuliwa kuwa viongozi serikalini, katika vyombo vya Ulinzi na Usalama, taasisi mbali mbali na katika vyombo vya umma. Polisi kugeuka kuwa maadui wa wananchi badala ya kuwalinda, TISS kugeuka watekaji, watesaji na wauwaji, JW kuanza kutembeza vipigo mitaani na kuvunja makazi ya watu, Ma RC na ma DC kugeuka miungu watu wilayani na mikoani n.k...tatizo juu ya tatizo!
Watanzania tunahitaji maobi, tujiombee...
Na asingeanza kuongea mbowe kuhusu Dogo, wala bashiru asingesema yote hayo. Ile ilikuwa kusawazisha uwanja. 1-1.Wewe ni mzoefu sana wa siasa za Bongo lakini huzielewi kila siku unakuwa kama mgeni.
Anachokifanya Bashiru kilifanywa na Kinana kila unapokaribia wakati wa uchaguzi mkuu - kukosoa chama na kujisahihisha (kurudisha imani).
Mfundisheni Mashinji sayansi ya siasa!