Matumizi sahihi ya jiko la gesi

Anko Drew

Member
Jun 9, 2021
15
41
MATUMIZI SAHIHI YA JIKO LA GESI

No. 1
Gesi ya kupikia yaweza kuwa ya asili (natural gas), mitungi ya gesi (liquified petroleum gas) na gesi inayotokana na kinyesi (biogas)

No. 2
Gesi hizo ni zile ambazo zina tabia ya kuwaka kama vile butane, propane na methane.

No. 3
Gesi ni nishati nzuri na rahisi kuitumia ila ni hatari kama hautozingatia usalama

No. 4
Unapopika kwa kutumia jiko la gesi hakikisha kuna hewa ya kutosha ili endapo kutakuwa na uvujaji wa gesi yasitokee madhara.

No. 5
Hakikisha mtungi wa gesi haukai Karibu na jiko (cooking place) ikiwezekana mtungi wa gesi ya kupikia uwe nje ya jiko na mpira wa gesi utoke nje kuingia ndani

No. 6
Hakikisha unaweka mtungi wa kupikia ukiwa umesimama (upright) na hakikisha hauwezi kupata misukosuko yeyote ambayo inaweza kuuharibu mtungi huo.

No. 7
Hakikisha unaangalia valve, regulator na pipe kama viko sawa kabla haujaanza kutumia gesi ya kupikia.

No. 8
Unapotumia jiko la gesi usiache kitu Jikoni na wewe ukaondoka vinaweza kuungua na kusababisha moto au tatizo likatokea bila wewe kuona.

No. 9
Hakikisha unakagua mpira unaopitisha gesi mara kwa mara kwa kupaka povu la sabuni ili kuona kama kuna sehemu inavuja. Pia hakikisha unabadilisha mpira kila baada ya miaka miwili na valve baada ya miaka 3-5

No. 10
Ukitaka kujua mtungi wa gesi upo kiasi gani usiutingishe. Chukua kitambaa weka maji kisha paka kwenye huo mtungi kuzungushia kwa pembeni na utaona kiasi kilichobaki, Ni hatari kutingisha mtungi wa gesi ya kupikia.

No. 11
Mambo ya kuzingatia endapo utahisi harufu ya gesi ya kupikia jikoni;
-Hakikisha unafungua milango na madirisha hewa iingie na kutoka.
-hauwashi moto wa aina yeyote.
-hakikisha kama taa zimezimwa usiwashe na kama zimewashwa usizizime. -hakikisha hauwashi tochi au simu.
-Usipige picha kwa simu au camera.
-Toa mtungi nje ya jiko na ukague wapi unavuja.
 
Ebu nisaidie, kwa hii mitungi yetu ya gas inatakiwa mpira wa gesi husizidi urefu gani?

Sababu nilitaka kununua iliyo ndefu ili mtungi niweke nje muuzaji akasema haitakiwi urefu kuzidi nadhani mita 2 kama sijakosea ikabidi ninunue urefu uliopendekezwa.
 
Ebu nisaidie, kwa hii mitungi yetu ya gas inatakiwa mpira wa gesi husizidi urefu gani?

Sababu nilitaka kununua iliyo ndefu ili mtungi niweke nje muuzaji akasema haitakiwi urefu kuzidi nadhani mita 2 kama sijakosea ikabidi ninunue urefu uliopendekezwa.
Inashauliwa urefu 1.5M hadi 2M kwa sababu za Kiusalama, lakini Pia ukizidisha kuweka Pipe ndefu zaidi Flow ya Gas Pressure yake inakuwa ndogo kidogo... Unaweza kuweka Pipe ndefu zaidi ya hiyo 2M ila zingatia sana Usalama
 
Ebu nisaidie, kwa hii mitungi yetu ya gas inatakiwa mpira wa gesi husizidi urefu gani?

Sababu nilitaka kununua iliyo ndefu ili mtungi niweke nje muuzaji akasema haitakiwi urefu kuzidi nadhani mita 2 kama sijakosea ikabidi ninunue urefu uliopendekezwa.
Usalama niuongeleapo hapo ni Watoto wasichezee hiyo Pipe, ila Nje na hapo nakushauri uweke Nje huo Mtungi ndy salama zaidi
 
MATUMIZI SAHIHI YA JIKO LA GESI

No. 1
Gesi ya kupikia yaweza kuwa ya asili (natural gas), mitungi ya gesi (liquified petroleum gas) na gesi inayotokana na kinyesi (biogas)

No. 2
Gesi hizo ni zile ambazo zina tabia ya kuwaka kama vile butane, propane na methane.

No. 3
Gesi ni nishati nzuri na rahisi kuitumia ila ni hatari kama hautozingatia usalama

No. 4
Unapopika kwa kutumia jiko la gesi hakikisha kuna hewa ya kutosha ili endapo kutakuwa na uvujaji wa gesi yasitokee madhara.

No. 5
Hakikisha mtungi wa gesi haukai Karibu na jiko (cooking place) ikiwezekana mtungi wa gesi ya kupikia uwe nje ya jiko na mpira wa gesi utoke nje kuingia ndani

No. 6
Hakikisha unaweka mtungi wa kupikia ukiwa umesimama (upright) na hakikisha hauwezi kupata misukosuko yeyote ambayo inaweza kuuharibu mtungi huo.

No. 7
Hakikisha unaangalia valve, regulator na pipe kama viko sawa kabla haujaanza kutumia gesi ya kupikia.

No. 8
Unapotumia jiko la gesi usiache kitu Jikoni na wewe ukaondoka vinaweza kuungua na kusababisha moto au tatizo likatokea bila wewe kuona.

No. 9
Hakikisha unakagua mpira unaopitisha gesi mara kwa mara kwa kupaka povu la sabuni ili kuona kama kuna sehemu inavuja. Pia hakikisha unabadilisha mpira kila baada ya miaka miwili na valve baada ya miaka 3-5

No. 10
Ukitaka kujua mtungi wa gesi upo kiasi gani usiutingishe. Chukua kitambaa weka maji kisha paka kwenye huo mtungi kuzungushia kwa pembeni na utaona kiasi kilichobaki, Ni hatari kutingisha mtungi wa gesi ya kupikia.

No. 11
Mambo ya kuzingatia endapo utahisi harufu ya gesi ya kupikia jikoni;
-Hakikisha unafungua milango na madirisha hewa iingie na kutoka.
-hauwashi moto wa aina yeyote.
-hakikisha kama taa zimezimwa usiwashe na kama zimewashwa usizizime. -hakikisha hauwashi tochi au simu.
-Usipige picha kwa simu au camera.
-Toa mtungi nje ya jiko na ukague wapi unavuja.

Hiyo namba 10 nimejifunza kitu kipya.

Asante
 
MATUMIZI SAHIHI YA JIKO LA GESI

No. 1
Gesi ya kupikia yaweza kuwa ya asili (natural gas), mitungi ya gesi (liquified petroleum gas) na gesi inayotokana na kinyesi (biogas)

No. 2
Gesi hizo ni zile ambazo zina tabia ya kuwaka kama vile butane, propane na methane.

No. 3
Gesi ni nishati nzuri na rahisi kuitumia ila ni hatari kama hautozingatia usalama

No. 4
Unapopika kwa kutumia jiko la gesi hakikisha kuna hewa ya kutosha ili endapo kutakuwa na uvujaji wa gesi yasitokee madhara.

No. 5
Hakikisha mtungi wa gesi haukai Karibu na jiko (cooking place) ikiwezekana mtungi wa gesi ya kupikia uwe nje ya jiko na mpira wa gesi utoke nje kuingia ndani

No. 6
Hakikisha unaweka mtungi wa kupikia ukiwa umesimama (upright) na hakikisha hauwezi kupata misukosuko yeyote ambayo inaweza kuuharibu mtungi huo.

No. 7
Hakikisha unaangalia valve, regulator na pipe kama viko sawa kabla haujaanza kutumia gesi ya kupikia.

No. 8
Unapotumia jiko la gesi usiache kitu Jikoni na wewe ukaondoka vinaweza kuungua na kusababisha moto au tatizo likatokea bila wewe kuona.

No. 9
Hakikisha unakagua mpira unaopitisha gesi mara kwa mara kwa kupaka povu la sabuni ili kuona kama kuna sehemu inavuja. Pia hakikisha unabadilisha mpira kila baada ya miaka miwili na valve baada ya miaka 3-5

No. 10
Ukitaka kujua mtungi wa gesi upo kiasi gani usiutingishe. Chukua kitambaa weka maji kisha paka kwenye huo mtungi kuzungushia kwa pembeni na utaona kiasi kilichobaki, Ni hatari kutingisha mtungi wa gesi ya kupikia.

No. 11
Mambo ya kuzingatia endapo utahisi harufu ya gesi ya kupikia jikoni;
-Hakikisha unafungua milango na madirisha hewa iingie na kutoka.
-hauwashi moto wa aina yeyote.
-hakikisha kama taa zimezimwa usiwashe na kama zimewashwa usizizime. -hakikisha hauwashi tochi au simu.
-Usipige picha kwa simu au camera.
-Toa mtungi nje ya jiko na ukague wapi unavuja.
Nakupongeza sana kwa ufafanuzi mzuri sana.
Ila, kwa sisi Waswahili, namba 11 ndiyo ya kusisitiziwa sana. Asilimia yetu kubwa (95%) tuko bize sana kuweza kuzingatia hayo mengine kwa ufasaha.
Asante
 
Nakupongeza sana kwa ufafanuzi mzuri sana.
Ila, kwa sisi Waswahili, namba 11 ndiyo ya kusisitiziwa sana. Asilimia yetu kubwa (95%) tuko bize sana kuweza kuzingatia hayo mengine kwa ufasaha.
Asante
Shukrani sana Mkuu.. Kweli hilo la 11 ni changamoto kubwa sana kwa watu wengi
 
Back
Top Bottom