Matumizi sahihi ya Dabo indiketa, gia L,2,3 na O/D katika gari za Automatic

akohi

JF-Expert Member
Jul 13, 2012
788
524
Dabo indiketa inashauriwa itumike wakati una dharula kubwa mf: Ajari au gari Mbovu maana lengo lake ni kuwataarifu madereva wenzako kuwa gari yako inatatizo so wapite kwa uangalifu zaidi lakin utakuta wengi wetu tunatumia visivyo mf; katika kupita njia panda au ukipaki pembezoni mwa barabara. Pia niongezee kuna ambao aki over take gari anawasha indiketa ya kulia (hiyo sawa kabisa ila sasa unapotaka kurudi upande wako wa kushoto hunahaja yak u indiketa tena unless kama kuna gari nyuma yako na iko jirani sana sio
Hata uko pekee yako unawasha indiketa tu.

Katika gari za Automatic kuna gia za L, 2, 3 na O/D.
Kwanza ujue kabisa katika hali ya kawaida gari yako inapaswa kuwa katika D kwa maana ya Drive na hii inategemeana na mazingira ya barabara na hali yali ya hewa kama ni nzuri ila 2, 3 hutumika tu pale unapokuwa either unashuka au unapanda mlima/mteremuko mkali sana na mrefu mf’ sekenke na unataka ushuke au upande kwa speed ile ile ila isizidi 40/60 basi ndo unaruhusiwa kutumia 2, 3. Namba 2, 3 na L inamaana kuwa ina inalock gear box ili gear zisibadilike (-/+) kama ambavyo zinabadika ukiweka D na itambulike kuwa unaweza kubadili toka D kwenda 2 au 3 wakati wowote gari inapokuwa katika mwendo ila hakikisha usiwe speed zaidi ya 40/60 maana kinachofanyika ni kwamba D inasababisha sahani (disks) zilizomo ndani ya gearbox kufanya gazi nah ii upelekea ile hydrolic iliyomo kupata joto linalotoka katika zile sahani ambalo joto lile husababisha gear box kutokuwa na nguvu ile ile (constant velocity) na ndo maana ukiweka 2, 3 au L gear box inakuwa kwenye lock na sahani hazisuguani maana inakuwa inatumika sahani/disk moja tu kwa hiyo inasaidia ile hydrolick kupoa pia na ndo maana gari huongeza nguvu kwa ghafla. L inatumika pale unapokuwa either umekwama au unavuta gari jingine au tera ila inapaswa itumike kwa muda mfupi sana maana inanguvu sana na pia inaongeza ulajo wa mafuta, so kama ukiishatoka katika mkwamo na unaona bado barabara si nzuri labda utelezi au unavuta mzigo kwa mwendo mrefu basi unaweka 2 au 3 na wakati huohuo unaweza kuweka hata D kama hali ya njia na mzigo vinaruhusu na unaweza kuongeza walau speed 40/60 au zaidi kama utaweka D. kwa maana rahisi zaidi kwamba 2,3,na L inafanya kazi kama gari ya Manual nah ii inakuwa rahisi kwa yeyote ambaye anafahamu kuendesha manual.

Over Drive inatumika pale gari inapokuwa speed zaidi ya 60/80 kutegemeana na aina ya gari na hili hutokea bila wewe kujua maana gari yenyewe ndo inafanya nan do maana unashauriwa iwe on muda wote kusudi gari ichague ni wkati gani iweke on au of maana uukiwa chini ya 60/80 hata kama umeweka on bado inakuwa haifanyi kazi.
Cha mwisho ndugu zangu ni kwamba OD unaweza kuitumia kama break/stop engine hasa unapokuwa zaid ya 80 na wakati huo iko ON yaan katika dashboard taa ya OD izime ikiwaka maana yake iko OFF, basi ili upunguze mwenda kwa haraka unachofanya ni kuweka OFF na wakati huo unakanyaga break taratibu utaona mwenyewe gari lako linavyopunguza mwendo tartibu na wakati mwingine si lazima ukanyage break, we iweke OFF tu halafu toa mguu katika pedal ya mafuta gari lazima li slow down na kama lilikuwa ni tuta na umeliisha lipita basii iweke tena ON ongeza mafuta auu unaweza kuweka 2 au 3 ili gari ianze kwa kasi zaidi na ikiisha changanya basi rudi kwenye D na endelea kama kawaida.

Tahadhari: never ever kata kona wakati uko speed kubwa na gear namba tano (Kwa manual) au rpm iko 3000 Kwa automatic hii husababisha kupitiliza maana gari inakuwa nyepesi sana. Hakikisha ume slow down mpaka gia namba nne na break kidogo na Kwa autimatic either uweke 2 au 3 ila lazima weka OD off na break kidogo

Sijui kama ntakuwa nimeeleweka maana Kiswahili na lugha yetu ila mmh …!
 
Nina swali moja mkuu,kuna muda unakuta driver anailazimisha gari kubadili gia bila kugusa gia liva,hasa wkt wa kuovertake,pale inakuaje mkuu?anacheza na pedal ya mafuta au?
 
Nina swali moja mkuu,kuna muda unakuta driver anailazimisha gari kubadili gia bila kugusa gia liva,hasa wkt wa kuovertake,pale inakuaje mkuu?anacheza na pedal ya mafuta au?



Hahaha imebidi nicheke, unajua Vujajungu umeniharibia my next article maana ndo nilitaka mwezi ujao nielezee kuhusu matumizi ya pedal ya mafuta Kwa hizi Automatic Swali zuri sana mkuu!!

Ok iko hivi, hapo juu nilielezea Kuwa unatumia gear kubadili toka D kwenda 2 au 3 ili upate kuanza Kwa Kasi ya kuovertake na ukiisha overtake ten unarudisha katika D bila kuachia pedal ya mafuta, sasa hiyo ni njia ndefu, njia fupi iko namna hii, kwanza lazima uwe kwenye mwendo ambapo OD iko ingaged au ON hapo hata kama uko speed 20 au 40 unachokifanya nikukanyaga Kwa nguvu pedal ya mafuta yaani hakikisha imegota mwisho kabisa maana Kwa kawaida iko Mara 2, ukikanyaga Mara ya kwanza inakuwa imefika nusu na gari inaondoka kawaida na haitovuma ila ukizidi kukanyaga Kwa nguvu mpaka mwisho utashangaa kuona kitu kinataka kama kupaa vile. ONYO: usijaribu kama unajifunza maana unaweza kushindwa kuimudu gari yako Kwa ile nguvu itakayoondoka nayo, endelea kuganyaga huku unaangalia mshale wa revolution usizidi rangi ya njano au namba nne Kwa maana ya 4000rpm (revolution per minute) kama sikosei then legeza pedal yako na endelea kawaida maana hapo nahakika utakuwa tayari unaitafuta 120kph au zaidi. Kumbuka ulaji wa mafuta pia utaongezeka maana kinachokua kimefanyika ni Kwamba ingine inakuwa katika labda gia namba Tatu au nne sasa wewe unaipa mafuta mengi kuliko mahitaji ya hiyo gia Kwa wakati huo na kama ni binadamu agebugia imagine ukinywa maji mengi kuliko uwezo wa koo shart ya kunige au palia ila machine inachofanya inapangua gia mpaka kwenye namba ambayo itayatumia hayo mafuta Kwa haraka zaidi ili yasilete madhari ya kuover flow na hii inawezekana Kwa injini zote sisizo na carburetor hapa naaaanisha Enjection au vvti ndo maana gari inaanza na nguvu kubwa maana imetoka gia namba nne kuja moja au mbili.

Enjoy Driving!

alfredmkohiatgmaildotcom
 
Dabo indiketa inashauriwa itumike wakati una dharula kubwa mf: Ajari au gari Mbovu maana lengo lake ni kuwataarifu madereva wenzako kuwa gari yako inatatizo so wapite kwa uangalifu zaidi lakin utakuta wengi wetu tunatumia visivyo mf; katika kupita njia panda au ukipaki pembezoni mwa barabara. Pia niongezee kuna ambao aki over take gari anawasha indiketa ya kulia (hiyo sawa kabisa ila sasa unapotaka kurudi upande wako wa kushoto hunahaja yak u indiketa tena unless kama kuna gari nyuma yako na iko jirani sana sio
Hata uko pekee yako unawasha indiketa tu.

Katika gari za Automatic kuna gia za L, 2, 3 na O/D.
Kwanza ujue kabisa katika hali ya kawaida gari yako inapaswa kuwa katika D kwa maana ya Drive na hii inategemeana na mazingira ya barabara na hali yali ya hewa kama ni nzuri ila 2, 3 hutumika tu pale unapokuwa either unashuka au unapanda mlima/mteremuko mkali sana na mrefu mf’ sekenke na unataka ushuke au upande kwa speed ile ile ila isizidi 40/60 basi ndo unaruhusiwa kutumia 2, 3. Namba 2, 3 na L inamaana kuwa ina inalock gear box ili gear zisibadilike (-/+) kama ambavyo zinabadika ukiweka D na itambulike kuwa unaweza kubadili toka D kwenda 2 au 3 wakati wowote gari inapokuwa katika mwendo ila hakikisha usiwe speed zaidi ya 40/60 maana kinachofanyika ni kwamba D inasababisha sahani (disks) zilizomo ndani ya gearbox kufanya gazi nah ii upelekea ile hydrolic iliyomo kupata joto linalotoka katika zile sahani ambalo joto lile husababisha gear box kutokuwa na nguvu ile ile (constant velocity) na ndo maana ukiweka 2, 3 au L gear box inakuwa kwenye lock na sahani hazisuguani maana inakuwa inatumika sahani/disk moja tu kwa hiyo inasaidia ile hydrolick kupoa pia na ndo maana gari huongeza nguvu kwa ghafla. L inatumika pale unapokuwa either umekwama au unavuta gari jingine au tera ila inapaswa itumike kwa muda mfupi sana maana inanguvu sana na pia inaongeza ulajo wa mafuta, so kama ukiishatoka katika mkwamo na unaona bado barabara si nzuri labda utelezi au unavuta mzigo kwa mwendo mrefu basi unaweka 2 au 3 na wakati huohuo unaweza kuweka hata D kama hali ya njia na mzigo vinaruhusu na unaweza kuongeza walau speed 40/60 au zaidi kama utaweka D. kwa maana rahisi zaidi kwamba 2,3,na L inafanya kazi kama gari ya Manual nah ii inakuwa rahisi kwa yeyote ambaye anafahamu kuendesha manual.

Over Drive inatumika pale gari inapokuwa speed zaidi ya 60/80 kutegemeana na aina ya gari na hili hutokea bila wewe kujua maana gari yenyewe ndo inafanya nan do maana unashauriwa iwe on muda wote kusudi gari ichague ni wkati gani iweke on au of maana uukiwa chini ya 60/80 hata kama umeweka on bado inakuwa haifanyi kazi.
Cha mwisho ndugu zangu ni kwamba OD unaweza kuitumia kama break/stop engine hasa unapokuwa zaid ya 80 na wakati huo iko ON, basi ili upunguze mwenda kwa haraka unachofanya ni kuweka OFF na wakati huo unakanyaga break taratibu utaona mwenyewe gari lako linavyopunguza mwendo tartibu na wakati mwingine si lazima ukanyage break, we iweke OFF tu halafu toa mguu katika pedal ya mafuta gari lazima li slow down na kama lilikuwa ni tuta na umeliisha lipita basii iweke tena ON ongeza mafuta auu unaweza kuweka 2 au 3 ili gari ianze kwa kasi zaidi na ikiisha changanya basi rudi kwenye D na endelea kama kawaida.

Sijui kama ntakuwa nimeeleweka maana Kiswahili na lugha yetu ila mmh …!

Mkuu naomba unieleweshe kitu kimoja...ni hivi. Mimi gari yangu siku zote naendesha nikiwa nimebonyeza kile kitufe cha OD. Hivyo pale kwenye dashboard inawaka taa ya orange inasoma O/D OFF sasa hapo inamaanisha nini na je ni sawa?
 
Somo zuri mno hongera nakushauri kama ukiweza utoe kwenye magazeti kama makala ili wengine wengi wafaidi elimu hii big up saana!!
 
Mkuu naomba unieleweshe kitu kimoja...ni hivi. Mimi gari yangu siku zote naendesha nikiwa nimebonyeza kile kitufe cha OD. Hivyo pale kwenye dashboard inawaka taa ya orange inasoma O/D OFF sasa hapo inamaanisha nini na je ni sawa?



Hapana enhe si sawa kabisa maana lengo la over drive ni kuongeza ufanisi wa injini na pia kupunguza ulaji wa mafuta Kwa maana kwamba ukiweka OD ON taa inazima na ikiwa OFF taa inawaka inapokuwa ON gia zitawahi kufika namba nne au tano na injini itakuwa nyepesi so ulaji wa mafuta unakuwa mdogo lakin pia hata injini inakuwa na maisha marefu maana rpm haiwezi kuzidi 3000 na labda nishauri Kuwa ili u save mafuta make sure rpm isizi 2000 unless kama uko safarini na unaharaka other wise usiilazimeshe injini kuanza na Kasi zisizo na lazima, weka D then ondoka taratibu huku unaangalia rpm yako isizidi 2000 utaona gari inaongeza mwendo yenyewe mpaka spidi kubwa kabisa hata 140kph na sana sana rpm wakati huo itasoma 3000 ambayo bado ni fuel efficient.

Ukidrive wakat OD iko OFF maana yake ulaji wa mafuta unakuwa Mkubwa sana na pia gari haiwezi kuchanganya haraka lakin pia unaua injini unless huzidi speed 60kph

Here is the trick part, weka OD off kama uko offroad au kuna utelezi na hutaki gari iwe nyepesi ila unataka ikimbie maana inakuwa nzito so ni nzuri Kwa barabara za vumbi lakin make sure huzidi 60kph maana OD inafanyakazi ktk speed kuanzia 60/80kph



alfredmkohiatgmaildotcom
 
Hapana enhe si sawa kabisa maana lengo la over drive ni kuongeza ufanisi wa injini na pia kupunguza ulaji wa mafuta Kwa maana kwamba ukiweka OD ON taa inazima na ikiwa OFF taa inawaka inapokuwa ON gia zitawahi kufika namba nne au tano na injini itakuwa nyepesi so ulaji wa mafuta unakuwa mdogo lakin pia hata injini inakuwa na maisha marefu maana rpm haiwezi kuzidi 3000 na labda nishauri Kuwa ili u save mafuta make sure rpm isizi 2000 unless kama uko safarini na unaharaka other wise usiilazimeshe injini kuanza na Kasi zisizo na lazima, weka D then ondoka taratibu huku unaangalia rpm yako isizidi 2000 utaona gari inaongeza mwendo yenyewe mpaka spidi kubwa kabisa hata 140kph na sana sana rpm wakati huo itasoma 3000 ambayo bado ni fuel efficient.

Ukidrive wakat OD iko OFF maana yake ulaji wa mafuta unakuwa Mkubwa sana na pia gari haiwezi kuchanganya haraka lakin pia unaua injini unless huzidi speed 60kph

Here is the trick part, weka OD off kama uko offroad au kuna utelezi na hutaki gari iwe nyepesi ila unataka ikimbie maana inakuwa nzito so ni nzuri Kwa barabara za vumbi lakin make sure huzidi 60kph maana OD inafanyakazi ktk speed kuanzia 60/80kph



alfredmkohiatgmaildotcom
Hongera sana
MHH SIDHANI KAMA HIYO QUOTE HAPO JUU NIMEKUELEWA. NIJUAVYO UKIBONYEZA OD BASI KWENYE DASHBOARD ITAONYESHA OD OFF, HII NI RETROSPECTIVE ALERT KWAMBA DO YOU WANT TO MAKE IT OFF? GARI YANGU MARA NIKIBONYEZA OD MLIO UNABADILIKA KIDOGO NA KITU KINACHOMOKA. BALAAA. EBU JARIBU KURUDIA KUSOMA SWALI LA MKUU. THANKS
 
Thanks brother ila inabidi wale lena wawe makini sana wasije kuleta adhari kwenye jamii zetu
 
Asante mkuu nimefaidika sana na somo lako Mungu akubariki.

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Hongera sana
MHH SIDHANI KAMA HIYO QUOTE HAPO JUU NIMEKUELEWA. NIJUAVYO UKIBONYEZA OD BASI KWENYE DASHBOARD ITAONYESHA OD OFF, HII NI RETROSPECTIVE ALERT KWAMBA DO YOU WANT TO MAKE IT OFF? GARI YANGU MARA NIKIBONYEZA OD MLIO UNABADILIKA KIDOGO NA KITU KINACHOMOKA. BALAAA. EBU JARIBU KURUDIA KUSOMA SWALI LA MKUU. THANKS

Katika Over Drive switch kuna only two Alternatives, put it own on ur own consent and put it off. Katika dashboard ukiona O/D off, basi ujue iko off, sio kwamba inskualert je wataka kuizima? No, it dont alert you, there is no YES or NO option wakati wa kuieka off
 
Hapana enhe si sawa kabisa maana lengo la over drive ni kuongeza ufanisi wa injini na pia kupunguza ulaji wa mafuta Kwa maana kwamba ukiweka OD ON taa inazima na ikiwa OFF taa inawaka inapokuwa ON gia zitawahi kufika namba nne au tano na injini itakuwa nyepesi so ulaji wa mafuta unakuwa mdogo lakin pia hata injini inakuwa na maisha marefu maana rpm haiwezi kuzidi 3000 na labda nishauri Kuwa ili u save mafuta make sure rpm isizi 2000 unless kama uko safarini na unaharaka other wise usiilazimeshe injini kuanza na Kasi zisizo na lazima, weka D then ondoka taratibu huku unaangalia rpm yako isizidi 2000 utaona gari inaongeza mwendo yenyewe mpaka spidi kubwa kabisa hata 140kph na sana sana rpm wakati huo itasoma 3000 ambayo bado ni fuel efficient.

Ukidrive wakat OD iko OFF maana yake ulaji wa mafuta unakuwa Mkubwa sana na pia gari haiwezi kuchanganya haraka lakin pia unaua injini unless huzidi speed 60kph

Here is the trick part, weka OD off kama uko offroad au kuna utelezi na hutaki gari iwe nyepesi ila unataka ikimbie maana inakuwa nzito so ni nzuri Kwa barabara za vumbi lakin make sure huzidi 60kph maana OD inafanyakazi ktk speed kuanzia 60/80kph



alfredmkohiatgmaildotcom

Somo nzuri lakini mkumbuke kwambahaya mambo ya O/D ni kwa zile Automatic gearbox za zamani. Hizi za sasa kila kitu ni Automatic. Gearbox ina sense kutokana na Engine motion na terrain huna haja ya kubonyeza button ya O/D na tena kwenye gari sa kisasa hazipo kabisa.
 
Somo zuri mno hongera nakushauri kama ukiweza utoe kwenye magazeti kama makala ili wengine wengi wafaidi elimu hii big up saana!!


Asante Mshana Jr Kwa wazo lako na pongezi, ntakifanyia kazi mkuu. Thx!




fesibuku: alfredkohiathotmaildotcom
 
Back
Top Bottom