Matumizi haya ya magari serikali ni sahihi?

JamiiForums

JF Official Account
Nov 9, 2006
6,202
5,012
Hoja hii ilianzishwa wakati JF ikiwa katika matengenezo hivyo tunairejesha kwakuwa haikurejea kikamilifu:
mukama talemwa said:
Jana nilikuwa Shinyanga nikaona VX v8 yenye usajili NW NM (M) kuangakia kwenye gari kaka Stephen Masele ambaye ni juzi tu kaapishwa kuwa naibu Waziri wa madini.

Kitu ambacho sikubaliani nacho siku zote huyu bwana hapa Shinyanga ni Jimbo lake la uchaguzi kwahiyo kuna gari kakopeshwa kwa ajili ya jimbo lake, mafuta anapewa, dereva analipiwa, kwahiyo kuchukua gari la Serikali kwa matumizi ya jimbo lake siyo sahihi hata kidogo. Mbaya zaidi yeye kapanda ndege dereva wake kaendesha hilo gari hadi Shinyanga, kilometer za kutoka Dar hadi Shy ni kama 1000 Dereva analipwa night allowance.

Je, tutegemee jipya gani kwa mabadiliko haya ya uongozi kuapishwa tu, matumizi mabaya ya mali za umma yanaanza kwa kasi mpya. Au ni kuwakoga wananchi wa SHY maana hakuwa chaguo lao.
 
kaka huo ni mfano mdogo tu na nafikiri kwako imekuwa ni jambo geni labda kwenye halmashauri zetu pamoja na taasisi nyingine za serekali mbona ni jambo la kawaida haijulikani mda wa ofisi wala nini na hakuna anayejali hili
 
Hii iko kwa mawaziri wote, wakienda majimboni, wao wanapanda ndege, dereva anachoma mafuta kwenda kumpokea na kumtembeza. Wakati wa kurudi hivyo hivyo, ndege na dereva anachoma mafuta tena kuja Dar. Hii tabia ilianza kidogo kidogo lakini sasa 'its official' na kwa bahati mbaya sana inaanza kushukuka kwenye idara na hata mashirika ya umma. Kwa ufupi matumizi ya serikali ni mabaya sana sana.
 
Hii iko kwa mawaziri wote, wakienda majimboni, wao wanapanda ndege, dereva anachoma mafuta kwenda kumpokea na kumtembeza. Wakati wa kurudi hivyo hivyo, ndege na dereva anachoma mafuta tena kuja Dar. Hii tabia ilianza kidogo kidogo lakini sasa 'its official' na kwa bahati mbaya sana inaanza kushukuka kwenye idara na hata mashirika ya umma. Kwa ufupi matumizi ya serikali ni mabaya sana sana.

Hayo ndiyo matokeo ya utawala unaoanguka. Hata Lowasa anasema kuna ombwe la uongozi lakini Mkama anamkoromea. Kuna rafiki yangu alitoka Japan yeye ni mpenzi sana wa kusafiri kwa treni akaniuliza je Naweza kwenda Nairobi kwa train? Nikamjibu labda apande basi . Akanijibu kwenye ramani aliona reli kutoka Dar Hadi Tororo kule Uganda sasa Ina maana hiyo reli imengolewa ikafanywa chuma chakavu? Hii ni aibu kwa viongozi kuachia miundombinu inakufa halafu wanafanya politiki? How can you talk on effective EA integration but nobody thinks of restoring the rail link glory of the sixties! Sasa Waziri anakwenda Arusha kwa ndege mpaka KIA dereva anaendesha V8 kumpokea Airport ili litimie you have Any Time Cancellation umeipata hiyo? Dou you still think we have a government?
 
Tabia hii ya matumizi mabaya kwa ccm imeota mizizi,sasa hivi Dodoma-Dar ndege.
Badala ya kujenga barabara nzuri hata njia nne,wanapishana angani.
 
Back
Top Bottom