Matumaini yote ya siku 100 aliyowapa Wananchi yazikwa na kauli ya dk 1

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,377
217,438
Tulifahamu tangu awali kwamba ccm ni ile ile , ila kuna tofauti kidogo kati ya viongozi wanaopewa Mamlaka na Chama hicho , kiongozi mwenye exposure hutofautiana kidogo uungwana na kiongozi wa kutoka porini , tofauti ipo ya namna ya kuhandle issues , kujua wapi aongee nini na wapi atishie watu, badala labda ya kukamata mwingine aweza kuonya tu na mambo yakasonga.

Lakini kwa kiasi kikubwa kwenye masuala ya haki za kikatiba ccm bado ni moja , hawataki usawa hata chembe , viongozi wote wa ccm hawataki katiba itakayoleta usawa ndani ya nchi wala hawataki Tume huru ya uchaguzi , pamoja na mama kuondoa baadhi ya uchafu uliofanywa na awamu iliyopita , ambao kwa kiasi kikubwa uliidhalilisha nchi na kuitia aibu duniani , lakini kimsingi hana tofauti kubwa na viongozi wengine wa ccm waliomtangulia.

Labda kwa kuwakumbusha tu ni kwamba Mama ni miongoni mwa watu wasiopenda kusikia habari ya serikali 3 , huyu alikuwa makamu Mwenyekiti wa bunge la Katiba , aliyesaidia sana kuinyofoa katiba yote ya Warioba na kupachika madudu waliyoyataka , Mwenyekiti alikuwa Samuel Sitta , kwahiyo huyu hakuwahi kuwa mwema kwa Taifa , bali ni mtu anayeuma na kupuliza , inawezekana katika uongozi wake akawa ana nafuu kuliko yule mkomoa watu , lakini kuhusu Katiba mpya tuendelee tu kupambana naye kama tulivyopambana na wengine.

Huwezi kushawishi wawekezaji wakubwa ikiwa hauna mifumo imara ya kisheria , mifumo hii inawekwa ndani ya Katiba , Katiba ya sasa ya Tanzania inamwezesha rais wake kufanya chochote bila kuhojiwa , ni mwekezaji gani mwenye akili timamu awezaye kuja kwenye nchi ya hivyo?

Inasikitisha tu kwamba imani ndogo aliyowapa Watanzania kwa siku 100 za mwanzo ameiteketeza kwa kauli ya dakika 1 tu ya KUENDELEA KUVUNJA KATIBA ALIYOAPA KUILINDA , huku akiwa kashika quran Tukufu mkono wa kulia .
 
Hapo feri kigamboni kuna mtu kanzisha biashara yake ya barakoa kwa kulazimisha watu kutoingia kwenye feri kama huna barakoa. Cha ajabu baada ya kushuka kwenye feri huko kwenye daladala kila mmoja anavua barakoa na maisha yanaendelea.

Maamuzi haya dhaifu wengeni wanayachukulia kama fursa. Hapa atakuambia anamsaidia Rais kazi ya kuwavisha wananchi barakoa.

CCM kuweni macho mambo yote yaliyokuwa yanawafanya mshindwe kuvaa sare zenu hadharani na mitaani yanarudishwa taratibu moja baada ya jengine. Kemeeni hii hali vinginevyo salfeti zinawahusu kitambo si kirefu kijacho.
 
Tatizo nchi inaongozwa kutoka Msoga!🚶🚶🚶
An8NV.jpg
 
Jinsia yake na umri viliwafanya wengi waweke matumaini makubwa kwake, "Mama" wengine wakasahau kumbe wao ni "watoto wa kambo" kwa huyu "mama", waliamini nao atawalea kama anavyowalea watoto wa nyumbani kwake, sasa ndio imekuja kudhihirika kumbe damu ni nzito kuliko maji, sasa vilio na majuto ndio vimeanza kusikika toka kwa "watoto wa kambo".
 
Jinsia yake na umri viliwafanya wengi waweke matumaini makubwa kwake, "Mama" wengine wakasahau kumbe wao ni "watoto wa kambo" kwa huyu "mama", waliamini nao atawalea kama anavyowalea watoto wa nyumbani kwake, sasa ndio imekuja kudhihirika kumbe damu ni nzito kuliko maji, sasa vilio na majuto ndio vimeanza kusikika toka kwa "watoto wa kambo".
Nakuhakikishia kwamba Mama amechochea mno mapambano ya Katiba mpya
 
Mkuu Erythrocyte heshima kwako. Nisiache kukwambia, ninachelea kukubaliana na hoja yako.

Kwani Mama yeye hapaswi kuwa na maoni yake?


Msingi wa kutofautiana nawe ni huo.

Cc: BAK
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Back
Top Bottom