Attn: Mods nawasihi hii nyuzi iacheni kama ilivyo ingawa inafanana na ile mliyoitolea ufafanuzi.
Kuna matukio ya ujambazi ambayo yametokea usiku wa saa 8 kuamkia leo 22/ Oktoba/ 2012. Katika matukio haya ambayo yametokea katika jiji la DSM yanahusu uharibifu na wizi wa computer na laptop. Mambo ni hivi:
Wakati kituo na ofisi za ATN (Agape TV) kikivamiwa na majambazi usiku wa saa 8 maeneo ya Mbezi Beach-Jogoo nako huko Mbezi Luis, Kwa Mzungu kituo cha Kulelea watoto wa mitaani " Child in the Sun" ambacho kikochini ya Kanisa katoliki kimevamiwa na majambazi usiku wa saa 8 kuamkia leo.
Mali zilizoporwa katika matukio yote mawili ni computer kadhaa na Laptop kadhaa. Katika matukio hayo yote wahusika hawakumdhuru mtu ye yote kimwili.
Uvamizi wa kituo cha "Child in The Sun" limeripotiwa na padri mlezi wa kituo hicho katika kituo cha Polisi cha Mbezi.
My take: Penye wengi hapa haribiki neno, humu jamvini kuna vichwa hebu tuyaangalie matukio haya mawili tofauti lakini yako kama pacha vile.
Kuna matukio ya ujambazi ambayo yametokea usiku wa saa 8 kuamkia leo 22/ Oktoba/ 2012. Katika matukio haya ambayo yametokea katika jiji la DSM yanahusu uharibifu na wizi wa computer na laptop. Mambo ni hivi:
Wakati kituo na ofisi za ATN (Agape TV) kikivamiwa na majambazi usiku wa saa 8 maeneo ya Mbezi Beach-Jogoo nako huko Mbezi Luis, Kwa Mzungu kituo cha Kulelea watoto wa mitaani " Child in the Sun" ambacho kikochini ya Kanisa katoliki kimevamiwa na majambazi usiku wa saa 8 kuamkia leo.
Mali zilizoporwa katika matukio yote mawili ni computer kadhaa na Laptop kadhaa. Katika matukio hayo yote wahusika hawakumdhuru mtu ye yote kimwili.
Uvamizi wa kituo cha "Child in The Sun" limeripotiwa na padri mlezi wa kituo hicho katika kituo cha Polisi cha Mbezi.
My take: Penye wengi hapa haribiki neno, humu jamvini kuna vichwa hebu tuyaangalie matukio haya mawili tofauti lakini yako kama pacha vile.