Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 47,013
- 144,371
Japo nina maono fulani,lakini bado,japo kwa muda, nitalazimika kushuhudia nchi hii ikirudi tena mikononi mwa CCM na nikiwaza Bunge lijalo lililotawaliwa na wabunge wa CCM,hakika nakwazika sana maana nikikumbuka waliyoyafanya katiba Bunge lililopita, hakika naweza hata kumkufuru mungu.
Muda si mrefu kabla hata hawajaanza kazi, tunaweza kuwaona wakitumia wingi wao kushinikiza waongezewe mishahara na marupurupu yao ili hali mimi nina miaka 6 kazini bila hata kupata promotion huku mshahara ukiwa kiduchu.
Muda si mrefu tutashududia wakipewa mamilioni kama mikopo(sera ya chama tawala) ili wanunulie magari ya kifahari wakati hospitalini hakuna madawa na wengine wanalilia kulipwa stahiki zao miaka nenda miaka rudi.
Muda si mrefu tutashuhudia wakipitisha ile katiba walioiasisi kwa mbwembwe huku maoni yetu yakipuuzwa!
Muda si mrefu tutashuhudia wale waliokataliwa na wananchi wakiteuliwa kuwa mabalozi,wakuu wa mikoa,wilaya n.k.
Kwa kifupi inauma sana kuendelea kuyashuhudia mambo haya na ndio maana nikasema heri yao waliotangulia mbele ya haki(ingawa inauma) maana maumivi haya wao hawatayasikia.
Muda si mrefu kabla hata hawajaanza kazi, tunaweza kuwaona wakitumia wingi wao kushinikiza waongezewe mishahara na marupurupu yao ili hali mimi nina miaka 6 kazini bila hata kupata promotion huku mshahara ukiwa kiduchu.
Muda si mrefu tutashududia wakipewa mamilioni kama mikopo(sera ya chama tawala) ili wanunulie magari ya kifahari wakati hospitalini hakuna madawa na wengine wanalilia kulipwa stahiki zao miaka nenda miaka rudi.
Muda si mrefu tutashuhudia wakipitisha ile katiba walioiasisi kwa mbwembwe huku maoni yetu yakipuuzwa!
Muda si mrefu tutashuhudia wale waliokataliwa na wananchi wakiteuliwa kuwa mabalozi,wakuu wa mikoa,wilaya n.k.
Kwa kifupi inauma sana kuendelea kuyashuhudia mambo haya na ndio maana nikasema heri yao waliotangulia mbele ya haki(ingawa inauma) maana maumivi haya wao hawatayasikia.