Matukio gani ulihisi yalimaanisha kifo au mwisho wako hapa duniani?

musicarlito

Senior Member
Dec 29, 2020
176
289
Ni kweli ipo siku tutakufa, lakini hali hii haizoeleki.

Mara nyingi yanatokea matukio ambayo karibu yachukue uhai wetu mathalani ajali, magonjwa nk. Huwa tunasema ..."kama Mungu tu" lakini kwa tunaoamini Mungu kweli huwa ni Mungu ameepusha, ashukuriwe.

Yafuatayo ni matukio ambayo siwezi sahau.

Nikiwa mdogo sana kama miaka 8 niliwahi dumbukia kisimani, nikazama mara ya kwanza naibuka bahati nzuri kuna dada alikua anafua nguo jirani akaja kuniokoa.

La pili, ilikua kwenye ajali ya mpira wa miguu...nilipanda mpira ukiwa kwenye 'motion' nilirushwa juu nikaangukia sehemu ya nyuma ya kichwa(kisogo)...nilipoteza fahamu...walioniona wanasema nilitoa povu na damu nashukuru wapo waliojizatiti kunipepea mpaka nikaamka wengine walikimbia siwalaumu mimi pia muoga kuona ajali ila najifunza, nilipoteza fahamu dish lilirudi katika hali yake baada ya muda ila mpaka leo nna matatizo ya kusahau.

Mengine ni ya kukoswa koswa na mgari barabarani

Wewe unakumbuka lipi au yapi?

Tuendelee kumshukuru Mungu...NB kunusurika haimaanishi ambao hawakunusurika wamepewa adhabu
 
Juzi juzi tuu hapa nilikoswa na gari.

Kulikuwa kuna mwendokasi inapakia, sasa nikawa nakatisha pale mbele ya mwendokasi, nakimbia kuwahi daladala.

Kumbe nilisahau kutazama nyuma ya mwendokasi kama kuna gari inakuja.

Ile namaliza tu kuivuka mwendokasi, haice ilipita speed kweli. Yaani kama ningewahi hatua moja, au sekunde moja nilikuwa na gongwa.

Lakini Mwenyezi Mungu ni mwema.
 
Juzi juzi tuu hapa nilikoswa na gari.

Kulikuwa kuna mwendokasi inapakia, sasa nikawa nakatisha pale mbele ya mwendokasi, nakimbia kuwahi daladala.

Kumbe nilisahau kutazama nyuma ya mwendokasi kama kuna gari inakuja.

Ile namaliza tu kuivuka mwendokasi, haice ilipita speed kweli. Yaani kama ningewahi hatua moja, au sekunde moja nilikuwa na gongwa.

Lakini Mwenyezi Mungu ni mwema.
Kabisa Mungu ni mwema
 
Mwaka 2013, eneo la Isimani Iringa nilipata ajali mbaya sana ya gari. Nilikuwa ninaendesha iSt, ikiwa katika mwendo mkali gari lilicheza barabarani nikashindwa kulimudu likatoka nje ya barabara na nikagonga jiwe kubwa lililong'olewa barabarani maana barabara ya Iringa - Dodoma ndio ilikuwa inatengenezwa kiwango cha lami, gari ikabetuliwa na kuruka sarakasi, lilipinduka kama mara 6 hivi likalalia ubavu, garini nipo peke yangu.

Ajabu sikupata hata mchubuko, nilibaki kitini na mkanda wa kiti umenikaa mwilini. Gari lilivyoanza kupinduka nilijua tayari ni kifo changu, nikamwomba Mungu anisamehe na kunipokea kwenye makao yake, nikaona picha ya maisha yangu yote ikipita kama Sinema na muda huohuo nikaona kama kuna mbawa imenikingia na kuniweka kati. Yote haya yalifanyika chini ya dakika 1.

Namshukuru sana Mungu kuniokoa na kifo kile.
 

Attachments

  • 2004 toyota ist 2.jpg
    2004 toyota ist 2.jpg
    33.2 KB · Views: 10
  • 2004 toyota ist 5.jpg
    2004 toyota ist 5.jpg
    45.3 KB · Views: 10
Mwaka 2013, eneo la Isimani Iringa nilipata ajali mbaya sana ya gari. Nilikuwa ninaendesha iSt, ikiwa katika mwendo mkali gari lilicheza barabarani nikashindwa kulimudu likatoka nje ya barabara na nikagonga jiwe kubwa lililong'olewa barabarani maana barabara ya Iringa - Dodoma ndio ilikuwa inatengenezwa kiwango cha lami, gari ikabetuliwa na kuruka sarakasi, lilipinduka kama mara 6 hivi likalalia ubavu, garini nipo peke yangu. Ajabu sikupata hata mchubuko, nilibaki kitini na mkanda wa kiti umenikaa mwilini. Gari lilivyoanza kupinduka nilijua tayari ni kifo changu, nikamwomba Mungu anisamehe na kunipokea kwenye makao yake, nikaona picha ya maisha yangu yote ikipita kama Sinema na muda huohuo nikaona kama kuna mbawa imenikingia na kuniweka kati. Yote haya yalifanyika chini ya dakika 1.
Namshukuru sana Mungu kuniokoa na kife kile.
Ashukuriwe Mungu sana hii ilikua hatari

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna gari lilikuwa linauza sumu za kuuliwa mende, mbu hata panya. Sumu ni za kienyeji ni maji maji hivi. Nikanunua ilikuwa inauzwa buku.
Kesho nikaamka asubuhi, nikamimina chini kwenye kona ya chumba kumbe mkononi nina vidonda kwenye vidole viwili.
Kumbe kipindi namwaga ile sumu inamwagikia kwenye vidole vyenye vidonda. Nikamaliza, nikanawa na sabuni. Nikatoka niende job, ile navuka barabara tu.
Naona km naanza kuona giza halafu mwili unaishiwa nguvu. Nikavuka haraka, nikauliza maziwa nikanywa ikawa pona pona yangu.
N.B
Ukiwa na vidonda au sehemu imechubuka usishike sumu ni hatari sana. Ingekuwa sumu ya Panya nahisi ningeenda na maji.
Tukumbuke kumuomba Mungu
 
Mimi Ajali ya kwanza kunusurika nilikanyaga waya wa umeme ule mkubwa ulianguka barabarani mvua ikinyesha nilirushwa mbali nikalazwa miezi 2 nikapona enzi hizo nipo masomoni Chunya....

Ajali ya pili kunusurika ni ile ya treni Dodoma nilinusurika lakini rafiki yangu alipoteza maisha.

Ajali zingine ni za gari zangu binafsi kwasababu tu ya ulevi lkn kote Mungu kaniokoa.
 
Mi niliishi na mwanamke muathirika akijijua mi bila kujua kwa miaka 2, nilifanya kazi sehemu kuna AC kali sana mapafu yakajaa maji ikabidi nitumie doze ya TB miezi 6 tulipata ajali ya kugongwa na gari moja akafariki moja dish limeyumba hadi leo nilianguka na gari katikati ya mbuga ya wanyama na matukio yote hayo Mungu amenitoa mzima, siju niongee nini ila kuna siri kubwa sana katika maisha ya binadamu
 
Lakini siri kubwa wengi tunaokoka katika matukio hayo huwa tunapata bahati ya mafanikio katika maisha ambayo ukimuhadithia mtu ulivyofanikiwa anaona kama hadithi tu kwahiyo napenda kuweka kwenye kundi la watu wenye bahati
 
Sahihi kabisa Mkuu wakati mwingine ni Mungu ni kujitukuza kupitia wanadamu
Lakini siri kubwa wengi tunaokoka katika matukio hayo huwa tunapata bahati ya mafanikio katika maisha ambayo ukimuhadithia mtu ulivyofanikiwa anaona kama hadithi tu kwahiyo napenda kuweka kwenye kundi la watu wenye bahati
 
Na hapo ndio unapoona thamani ya maisha na uhai. Sio kwamba waliotangulia wamekosea au hawakustahili kuwepo, ni wakati wao umefika.

Hali kadhalika sie tuliobaki Iko siku tutaondoka Kwa namna Moja ama nyingine. Unapopata nafasi ya kuiona siku moja, mshukuru Mungu, ukiweza kuwagusa wengine pia, fanya hivyo. Tuna siku chache sana za kuishi na hakuna mtu anajua ataondoka lini.

Nakumbuka nikiwa na umri wa miaka 6 niliugua ugonjwa usiojulikana lakini unavimba na Hospitali hawaoni kitu. Mzee alichanganyikiwa anawaza kusafiri twende nyumbani Kwa Babu lakini anaona ntafia kwenye gari, kubaki hapo anahisi ntafariki.

Nikiwa O Level nilianguka Bwaloni nikiwa narekebisha taa wanamichezo wapate mwanga, jamaa aliyeshikilia meza akaiachia baada ya taa kuwaka, nilijipigiza kifua macho yakawa mazito, siwezi kuhema, nilikuja kushtuka baadae sana.
 
Mimi Ajali ya kwanza kunusurika nilikanyaga waya wa umeme ule mkubwa ulianguka barabarani mvua ikinyesha nilirushwa mbali nikalazwa miezi 2 nikapona enzi hizo nipo masomoni Chunya....

Ajali ya pili kunusurika ni ile ya treni Dodoma nilinusurika lakini rafiki yangu alipoteza maisha.

Ajali zingine ni za gari zangu binafsi kwasababu tu ya ulevi lkn kote Mungu kaniokoa.
Ooh Mungu anakupenda sana jitahidi upunguze ulevi sasa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mi niliishi na mwanamke muathirika akijijua mi bila kujua kwa miaka 2, nilifanya kazi sehemu kuna AC kali sana mapafu yakajaa maji ikabidi nitumie doze ya TB miezi 6 tulipata ajali ya kugongwa na gari moja akafariki moja dish limeyumba hadi leo nilianguka na gari katikati ya mbuga ya wanyama na matukio yote hayo Mungu amenitoa mzima, siju niongee nini ila kuna siri kubwa sana katika maisha ya binadamu
Kabisa mkuu...Mungu azidi kukulinda

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwaka 2013, eneo la Isimani Iringa nilipata ajali mbaya sana ya gari. Nilikuwa ninaendesha iSt, ikiwa katika mwendo mkali gari lilicheza barabarani nikashindwa kulimudu likatoka nje ya barabara na nikagonga jiwe kubwa lililong'olewa barabarani maana barabara ya Iringa - Dodoma ndio ilikuwa inatengenezwa kiwango cha lami, gari ikabetuliwa na kuruka sarakasi, lilipinduka kama mara 6 hivi likalalia ubavu, garini nipo peke yangu.

Ajabu sikupata hata mchubuko, nilibaki kitini na mkanda wa kiti umenikaa mwilini. Gari lilivyoanza kupinduka nilijua tayari ni kifo changu, nikamwomba Mungu anisamehe na kunipokea kwenye makao yake, nikaona picha ya maisha yangu yote ikipita kama Sinema na muda huohuo nikaona kama kuna mbawa imenikingia na kuniweka kati. Yote haya yalifanyika chini ya dakika 1.

Namshukuru sana Mungu kuniokoa na kifo kile.
Ni MUNGU tu
 
Back
Top Bottom