Matonya arudi kwenye mziki

likemike

Senior Member
Mar 10, 2016
115
55
Ni vigumu msanii aliyepotea kwenye game kurejea kwa kishindo kile kile. Hii ipo ata kwenye msemo wa kiingeereza – “Golden Chance Never Comes Twice,” – yaani bahati haijirudii mara mbili.

Hata hivyo, kuna wakati bahati inaweza kijirudia, kama ilivyokuwa kwa Jay MoePesa Madafu, na sasa Jay MoeNisaidie Kushare au hata kwa Ray C Unanimaliza.

Na hivyo basi, bahati kujirudia si kwa Jay Moe na Ray C pekee, Matonya emerejea tena kwenye game ya Bongo Flava. Na sasa, ni dhahiri Matonya is here to stay, atakuwepo kwa kipindi kirefu sana. Nyimbo yake ya sasa MatonyaNifungulie ni kiashiria tosha.



Matonya alifanya vizuri sana kwenye Game ya Bongo Flava mwaka 2006 na Album ya Siamini iliyokuwa na nyimbo mashuhuri kama Vaileth, Dunia Mapito na Siamini. Matonya pia alifanya vema mwaka 2008 na Album yake – Safari ya Dunia aliyomshirikisha Prof. Jay, Joslin, Klyinn (Jackline Mengi), TID Mnyama na Lady Jay Dee commando. Nyimbo zilizofanya vizuri kwenye Album hiyo ni pamoja na Matonya x Lady Jay DeeAnitha na Matonya x Lady Jay Dee – Taxi Bubu.

Hivi karibuni, Matonya ametoa nyimbo kadhaa kama MatonyaHakijaeleweka aliyoitoa mapema mwezi January, 2017. Mwaka 2015 Matonya alitoa nyimbo iliyojipatia mashabiki karibu milioni moja Youtube. Katika nyimbo hiyo ya MatonyaMule Mule alimshirikisha Rich Mavoko . Nyingine ni pamoja na MatonyaSugua Bench iliyotoka wiki ya pili ya mwezi October, mwaka 2016.

Matonya anayeonekana kurejea kwa kasi, hasa baada ya nyimbo zake kuanza kutawala kwenye mitandao ya kijamii na vituo vya redio, bado ana kazi kubwa ya kuwaaminisha mashabiki wake atawapa kile wanachokitegemea kutoka kwake, na pengine zaidi.

Matonya kujipatia watazamaji elfu 76 kwa kipindi cha siku nne Youtube akishindana na Nikki wa Pili x G Nako – Quality Time kunapaswa kumuongezea ari Matonya kutengeneza nyimbo bora zaidi, kutengeneza mwili wa kisanii, kutengeneza video nzuri na kutoipoteza nafasi yake tena – Golden Chance Never Comes Thrice.


Chanzo; kibandaumiza.comhttp://www.kibandaumiza.com/matonya-amerudi/
 
Alishapta huyu kurud enz za
Tax bubu,vailet,anita,dunia mapito, n ngumu sana

Kurd kwake n sawa na
Italy kurudisha heshima
Yake ya soccer dunia
Enz za ac milan,international mila
 
Alishapta huyu kurud enz za
Tax bubu,vailet,anita,dunia mapito, n ngumu sana

Kurd kwake n sawa na
Italy kurudisha heshima
Yake ya soccer dunia
Enz za ac milan,international mila

Lolote linawezekana, nadhani umekariri...

AC Milan haifanyi vizuri sasa, lakini sio kweli kwamba mpira umekwisha, haipo tena..Kama mpira bado unaendelea kuchezwa chances are AC Milan na timu nyingine za Italy zinaweza kutake over, kushikilia soka la vilabu kama vinavyofanya vilabu vya Hispania sasa...

Kwenye Muziki vivyo hivyo, nani alijua Jay Moe atarudi kwenye game kama ilivyo sasa na Nisaidie kushare? Ray C na Unanimaliza?

So long as msanii anaendelea kujihusisha na muziki, anything might happen... Anaweza kuirejea nafasi yake au hata zaidi ya ilealiyokuwa nayo, ni plans, hardwork, maandalizi, uwekezaji n.k

Na, Ule msemo Bahati haijurudii mara mbili hauna mashiko sana siku hizi...
 
Mwakajana aliitwa kwenye show nilikuwa bukoba watu waliolipa kuingia hawafiki 30, sijajua walilipanaje na muandaaji, msanii wakati wako ukipita unatia huruma. Anyway niliupenda ule wimbo wake wa 'SUGUA BENCHI', nashangaa haukuwa na promo
 
Alishapta huyu kurud enz za
Tax bubu,vailet,anita,dunia mapito, n ngumu sana

Kurd kwake n sawa na
Italy kurudisha heshima
Yake ya soccer dunia
Enz za ac milan,international mila
Umeisahau UAMINIFU
 
Back
Top Bottom