nguzo1
JF-Expert Member
- Jul 30, 2015
- 347
- 530
Wakuu heshima kwenu,
Kwa mara ya kwanza nimeweza kujicontroll na kuacha kufanya mapenzi na kunywa pombe kwa muda wa miezi mitatu (kuanzia January hadi Aprill mwanzoni)
Nikiri kwamba nimepata nguvu za ajabu mno na uwezo wa ubongo kuchanganua mambo umeongezeka mara dufu. Nilipokuwa meza moja na jamaa zangu nilikuwa nawapa ushauri na wanaosolve mambo yao 95%
Kubwa katika yote ni kwamba hivi karibuni (Mwezi May 2021) kila nikilala usiku ninakuwa usingizini lakini bado akili yangu inakuwa macho na ninaweza kupanga mipango yangu ya kesho au kuvuta kumbukumbu ya nini nimekifanya kwa siku ya leo Na ninakuwa na feelings za mazingira ya hapa duniani na dunia ingine mpya( Yani tuseme Sebuleni = hapa duniani na Chumbani= Dunia ingine mpya) Sasa ndani ya ubongo wangu ndiyo na switch either Chumbani Au sebuleni na mazingira yanabadilika muda huohuo.
Usiku mida ya kulala Nikifunga macho na kutuliza sehemu zote za mwili na bila kukaza msuli wa aina yoyote ninakuwa sioni tena giza badala yake naona screen mbele ya paji la uso wangu na kuna maandishi yanapita na ninakuwa na uwezo wa kuyasoma na yanakuwa ni kama maelekezo fulani juu ya vitu ambavyo sijawahi kabisa kuona au kusikia popote hata google.
Inafikia mahali najisahau nachezesha kope za macho na hiyo hali inaondoka narudi kwenye ulimwengu huu wa nyama na damu lakini nikitulia baada ya nusu saa naingia tena kwenye ile hali na muda huo ninakuwa najua kabisa kwamba hapa nikichezesha kope za macho au nikijitingisha popote mwilini au kukaza msuli wowote iyo hali itapotea na nikifanya hivyo inakuwa kweli.
Nina mengi ya kusimulia ila nahisi sitaeleweka.
Hapa kati kati nilikuja kujihusisha na mapenzi na pombe kidogo na ile hali ikapotea kabisa. Mwili ukawa mzito, nikiamka asubuhi najiona nimechoka sana, akili inakuwa nzito nashindwa kufikiri kwa haraka na confidence ya kuongea na watu ikapungua.
Sina hakika kama mapenzi na pombe ndiyo chanzo cha kupoteza uwezo wangu ila nimeamua tena kuviacha kwa muda wa miezi mitatu nione kama hii hali itajirudia tena.
Mara ya kwanza niliweza kufikisha miezi 3 kutokana na kwamba niligombana na mpenzi wangu na nikapata safari ya huko maporini kwa muda wotehuo ndiyo maana sikupata chance ya kufanya mapenzi kwa muda huo.
Chakula nilichokuwa natumia ni Mihogo, karanga, Ugali mboga za majani, matunda , maziwa tangawizi ya kutafuna kila siku asubuhi na jioni, hakika mwili ulibadilika na nikawa mwepesi sana na nilijiamini kupita kiasi. Pia nilikuwa na uwezo wa kufikiria mambo magumu na kuyatolea ufafanuzi japo sikuwaji kujifunza kabla. Nilikuwa na uwezo wa kusikiliza watu wawili wakiongea kwa wakati mmoja mfululizo hata kwa dakika kumi na nikawaelewa wote kwa mkupuo.
Yani sijui nisemeje wakuu ila yote haya yameondoka baada ya kulala na mwanamke mwezi huu wa sita huku nikiwa na k-vant kichwani
Itaendelea.....
Kwa mara ya kwanza nimeweza kujicontroll na kuacha kufanya mapenzi na kunywa pombe kwa muda wa miezi mitatu (kuanzia January hadi Aprill mwanzoni)
Nikiri kwamba nimepata nguvu za ajabu mno na uwezo wa ubongo kuchanganua mambo umeongezeka mara dufu. Nilipokuwa meza moja na jamaa zangu nilikuwa nawapa ushauri na wanaosolve mambo yao 95%
Kubwa katika yote ni kwamba hivi karibuni (Mwezi May 2021) kila nikilala usiku ninakuwa usingizini lakini bado akili yangu inakuwa macho na ninaweza kupanga mipango yangu ya kesho au kuvuta kumbukumbu ya nini nimekifanya kwa siku ya leo Na ninakuwa na feelings za mazingira ya hapa duniani na dunia ingine mpya( Yani tuseme Sebuleni = hapa duniani na Chumbani= Dunia ingine mpya) Sasa ndani ya ubongo wangu ndiyo na switch either Chumbani Au sebuleni na mazingira yanabadilika muda huohuo.
Usiku mida ya kulala Nikifunga macho na kutuliza sehemu zote za mwili na bila kukaza msuli wa aina yoyote ninakuwa sioni tena giza badala yake naona screen mbele ya paji la uso wangu na kuna maandishi yanapita na ninakuwa na uwezo wa kuyasoma na yanakuwa ni kama maelekezo fulani juu ya vitu ambavyo sijawahi kabisa kuona au kusikia popote hata google.
Inafikia mahali najisahau nachezesha kope za macho na hiyo hali inaondoka narudi kwenye ulimwengu huu wa nyama na damu lakini nikitulia baada ya nusu saa naingia tena kwenye ile hali na muda huo ninakuwa najua kabisa kwamba hapa nikichezesha kope za macho au nikijitingisha popote mwilini au kukaza msuli wowote iyo hali itapotea na nikifanya hivyo inakuwa kweli.
Nina mengi ya kusimulia ila nahisi sitaeleweka.
Hapa kati kati nilikuja kujihusisha na mapenzi na pombe kidogo na ile hali ikapotea kabisa. Mwili ukawa mzito, nikiamka asubuhi najiona nimechoka sana, akili inakuwa nzito nashindwa kufikiri kwa haraka na confidence ya kuongea na watu ikapungua.
Sina hakika kama mapenzi na pombe ndiyo chanzo cha kupoteza uwezo wangu ila nimeamua tena kuviacha kwa muda wa miezi mitatu nione kama hii hali itajirudia tena.
Mara ya kwanza niliweza kufikisha miezi 3 kutokana na kwamba niligombana na mpenzi wangu na nikapata safari ya huko maporini kwa muda wotehuo ndiyo maana sikupata chance ya kufanya mapenzi kwa muda huo.
Chakula nilichokuwa natumia ni Mihogo, karanga, Ugali mboga za majani, matunda , maziwa tangawizi ya kutafuna kila siku asubuhi na jioni, hakika mwili ulibadilika na nikawa mwepesi sana na nilijiamini kupita kiasi. Pia nilikuwa na uwezo wa kufikiria mambo magumu na kuyatolea ufafanuzi japo sikuwaji kujifunza kabla. Nilikuwa na uwezo wa kusikiliza watu wawili wakiongea kwa wakati mmoja mfululizo hata kwa dakika kumi na nikawaelewa wote kwa mkupuo.
Yani sijui nisemeje wakuu ila yote haya yameondoka baada ya kulala na mwanamke mwezi huu wa sita huku nikiwa na k-vant kichwani
Itaendelea.....