Matokeo ya Utafiti: Kikwete, Freeman Mbowe, Zitto, Killango, Jerry Silaa na Dr Slaa

Huu ni uchafu ambao CCM imekuwa ikiufanya siku zote, Rais kikwete tangu aingie madarakani hakuna hata alichokifanya zaidi ya kusuluhisha lowasa na sitta. kazi ya pili aliyoifanya ni kuchekacheka tu ikulu kwani huyu ni mtu asiyefahamu wajibu hata kazi yake. Mfano mzuri ni alipokuwa ufaransa , aliuzwa swali kuwa kwa nini tanzania pamoja na kuwa na mali asili nyingi ya kutosha bado ni maskini? kwa nguvu zote yeye alijibu hajui ni kwanini.Mwandishi wa habari alijaribu kumuuliza tena kuwa hata wewe raisi wa nchi hujui? akakili kuwa hajui kabisa .Huyu ni raisi ambaye hajui hata wananchi anawaongoza wana hali gani, na hajui wanchi wake ni maskini au laa, jamani huyu hakutakiwa kuliongoza taifa ila kwa kuwa wanchi bado tumelala basi ccm ndo inapopiga bao .ni noma babu.
 
Leo synovate wamekutana na wanahabari na kutangaza matokeo ya utafiti wao kuhusu hali ya taifa. Wametaja kuwa Kikwete anaongoza kwa kuwa na asilimia 70 akifutiwa na Freeman Mbowe mwenye asilimia 10, akiwa ametangulia kidogo Lipumba. Hii ni katika nafasi ya urais.

Katika bunge utafiti wao unaonyesha kwamba Zitto Kabwe ndiye mbunge bora kuliko wote akifuatiwa na Anna Kilango. Katika matokeo hayo Mbunge mwingine bora anayetajwa ni Jerry Silaa ambaye ni diwani wa ukonga. Utafiti huo unasema kwamba wananchi wapatao elfu mbili waliohojiwa kutoka maeneo mbalimbali ya nchi wamemtaja diwani huyo kuwa anachapa kazi kwa kiwango kikubwa na wakiamini kwamba ni mbunge. Katika utafiti huo Dr Slaa anatajwa kuwa nyuma.

Kwa upande wa vyama matokeo yanaonyesha kwamba CCM iko karibu zaidi na wananchi kwa asilimia 70 ikifuatiwa na CHADEMA yenye asilimia 14.

......ndiyohiyo


Kwangu ni UPUPU MTUPU Hivi hao wananchi 2000 ni wakazi wa Ukonga au Kibondemaji, Gezaulole? Panga la mwingereza? maana nashindwa kuelewa mtu wa Geza ulole atamjua vipi? diwani wa Ukonga? naamini ata hao wa Ukonga wapo wasio mjua diwani wao Jerry.

Tuache jamani kula hela za wahisani na hivi vi NGO's visivyo na Tija.
 
Baba
Unajua waandishi wetu ni kama wanafunzi wanaosemowa insha kisha haooo wanakimbilia newsroom. Hawana maswali yanayojijenga kichwani yenye mantiki. ndo maana tunawaita maripota njaa kali. kwa mwandishi makini hawezi akaitwa kwenye conference kisha akasomewa upuuzi kama huu wa SYNOVATE bila ya kuuliza maswali chechemizi yatakayosisimua ripoti hiyo.

Ni kama waliitwa kwenye hafla fupi wakasomewa risala kisha haooo wakawahi newsroom kupaste walichoambiwa
sasa ndugu yangu waulize maswali kwa elimu gani waliyokuwa nayo??? unafahamu ujinga ni kitu kibaya sanakatika maisha ya binadamu, ukiwa mjinga wa kitu hata unakuwa huna ujasiri wa kusema/ kufanya lolote, 'waandishi' wetu wa habari wakishajua kushika kipaza sauti, notebook na kalamu baaasi, wanawahi kwenye press conf. wapate chai na pengine posho kidogo haooo hata hawaelewi walichoambiwa wanakibwaga kwa wananchi moja kwa moja, hawajifunzi kwa wenzetu angalia kwenye vyombo vya nje waandishi wa habari wanakuwa ni waliobobea kwenye fani fulani kwa hiyo wanahoji kitaalamu na kwa kutumia taaluma zao!
 
Yaani huu ni uhuni, wewe huwezi kuhoji watu 2000 kati ya watu milioni 40 halafu unaita ni utafiti. Naona hapa taaluma ya tafiti imemeingiliwa vibaya. Pia unaposema chama kilichopo karibu na wananchi ni kwenye nini? Ufisadi, Majengo pacha ya BOT, EPA, kushuka kwa elimu ya kidato cha nne, usofu wa waalimu, huduma mbovu hospitalini, barabara mbovu? Au ni kwenye kitu gani?
Mkombozi imenibidi nicheke kweli tunatakiwa tujiulize eti chama kilicho karibu zaidi na wananchi watuambie kwenye nini ufisadi ni kama kusema 70% ya watanzania tunajihusisha zaidi na ufisadi kwa namna moja ama nyingine kuliko mambo mengine haa ha ha
 
total knock out
hizi tafiti zitaleta kizaazaa siku moja.
ikifika 2015 hawa waganga njaa watakuja na findings wakisema wamehoji wanachi 2500 kuwakilisha taifa zima kuhusu kubadilisha katiba kumwongezea muungwana another chance kwa kuwa umaarufu wake uko juu na hakuna mwenye uwezo aliyesalia zaidi yake.
 
Kwangu ni UPUPU MTUPU Hivi hao wananchi 2000 ni wakazi wa Ukonga au Kibondemaji, Gezaulole? Panga la mwingereza? maana nashindwa kuelewa mtu wa Geza ulole atamjua vipi? diwani wa Ukonga? naamini ata hao wa Ukonga wapo wasio mjua diwani wao Jerry.

Tuache jamani kula hela za wahisani na hivi vi NGO's visivyo na Tija.
wanadhani watanzania wa leo ni wajinga wa mawazo kama enzi zile za kwanza za mawe!!! hii ni dunia nyingine kabisa watu wanajua mambo meeeengi kuliko wao wanavyofikiri tatizo ni kukosa nafasi ambazo zitawawezesha kutumia kile wanachokijua, wachache walilong'ang'ania nafasi hawana jipya wanalolijua na bado wapo tu? I wish kungetoa mageuzi ya kweli !!! halafu huyo mkuu wa hiyo NGO utasikia kesho kawa mjumbe wa NEC!!!!!! Kabla hajapewa ukuu wa wilaya hizi mpya mpya za kina misungwi etc....
 
Huu ni uchafu ambao CCM imekuwa ikiufanya siku zote, Rais kikwete tangu aingie madarakani hakuna hata alichokifanya zaidi ya kusuluhisha lowasa na sitta. kazi ya pili aliyoifanya ni kuchekacheka tu ikulu kwani huyu ni mtu asiyefahamu wajibu hata kazi yake. Mfano mzuri ni alipokuwa ufaransa , aliuzwa swali kuwa kwa nini tanzania pamoja na kuwa na mali asili nyingi ya kutosha bado ni maskini? kwa nguvu zote yeye alijibu hajui ni kwanini.Mwandishi wa habari alijaribu kumuuliza tena kuwa hata wewe raisi wa nchi hujui? akakili kuwa hajui kabisa .Huyu ni raisi ambaye hajui hata wananchi anawaongoza wana hali gani, na hajui wanchi wake ni maskini au laa, jamani huyu hakutakiwa kuliongoza taifa ila kwa kuwa wanchi bado tumelala basi ccm ndo inapopiga bao .ni noma babu.

Kweli tumeumia pamoja na ma Phd yote aliyonayo anashindwa kujibu hili swali?

si nasikia kasomea uchumi UDSM? sasa alipitapita vipi? au alikuwa anadesa? Kama tuna msomi wa uchumi kutoka UD na awezi kujibu hili swali basi walimu wake ni hasara Tufunge chuo unless mniambie alikuwa anadesa.

Angesingizia wakoloni basi maana si tunasoma Tokea primary kuwa wazungu ndio wametufanya hivi?
 
Leo synovate wamekutana na wanahabari na kutangaza matokeo ya utafiti wao kuhusu hali ya taifa. Wametaja kuwa Kikwete anaongoza kwa kuwa na asilimia 70 akifutiwa na Freeman Mbowe mwenye asilimia 10, akiwa ametangulia kidogo Lipumba. Hii ni katika nafasi ya urais.

Inabidi watu waache kuwalalamikia hawa watafiti na matokeo yao. Uongozi wa CHADEMA ulitakiwa uwe tayari umeshafanya utafiti wao wenyewe na kujaribu kuu-skew kidogo towards CHADEMA, ili kujaribu kurubuni wale wanaofuata upepo.

Lakini kwa kwa vile uongozi ni wa kibinafsi, mawazo yao pia yanakuwa ya kibinafsi. Sasa wamewaachia wapambe wa JK kuendelea kuvutia watu kwake na kuogopesha wengineo wote wenye nia ya kumpinga.
 
Nashangaa kusiki jina la diwani asiyejulikana kafanya nini hadi kutajw ana wananchi 200 nchi nzima. Nahisi alichangia gharama za utafiti huo ili atajwe naye ajulikane kidogo. Pia haiwezekanai mama Kilango awe maarufu kuliko Slaa hata asitajwe ni uongo uliowazi na inaonyesha walioendesha utafiti huo walielekezwa cha kufanya na matokeo yalipangwa, haiwezekani wananchi 2000 wote wasimjue Dk Slaa wamtaje Zito na Kilango.
Mapungufu ya utafiti huo huenda yalikuwa dhaifi kwa sababu zifuatazo.

1.Maswali yalikuwa yanaelekeza majibu yawe hivyo
2.Walioanya walikusudia yawe hivyo.
3.Waliohojiwa ni wana CCM halisi au watu wa vijijini kule kigoma ambao wanamjua tu Zito na Kikwete.
4.Walifanya utafiti huo kuset agenja za mjadala wakati huu wa kuelekea uchaguzi mkuu ili CCM wanaopinga wajue kuwa wananchi bado wanamkubali Jakaya na chama chao hivyo wasihamie Chadema.

Hayo ni maoni yangu wakuujapo mie mwanasiasa ambaye bado sijaamua chama gani niingie maana zote za kibabaishaji tu labda CCJ kama ni ya kweli.
 
(Habari Leo)
.

Utafiti uliofanywa na kampuni ya Synovate umebainisha kuwa, utendaji wa Kikwete unawaridhisha wananchi kwa asilimia 75.

Wananchi pia wamesema, chama cha siasa ambacho kipo karibu zaidi na wananchi ni Chama Cha Mapinduzi(CCM).

Kwa mujibu wa wananchi hao, CCM ipo karibu na wananchi kwa asilimia 70, Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa asilimia 17, Chama Cha Wananchi(CUF) kwa asilimia 9, NCCR Mageuzi kwa asilimia 2,Tanzania Labour(TLP) na UDP asilimia 1.

Kwa mujibu wa taarifa ya utafiti ya kura ya maoni ya robo ya mwisho Oktoba- Desemba mwaka jana iliyofanywa na kampuni hiyo, lengo lilikuwa ni kupata kura ya maoni ya watanzania katika mambo ya kijamii, kisiasa na kiuchumi katika vipindi tofauti ndani ya mwaka.

Meneja wa Utafiti wa Vyombo vya Habari na Umma wa kampuni hiyo, Abdallah Gunda, amewaeleza waandishi wa habari kuwa, kampuni hiyo ambayo zamani ilijulikana kwa jina la Steadman Group ilikusanya maoni kwa kuwahoji watu 2000.

Amesema, watu hao waligawanywa sawasawa na uwiano wa idadi ya wananchi wa Tanzania na ilikusanya mahojiano ya uso kwa uso katika maeneo tofauti yaliyochaguliwa.


Kumbe ni Kampuni?

Sawa wanataka nini sasa? ardhi au Mgodi?
 
Baba
Unajua waandishi wetu ni kama wanafunzi wanaosemowa insha kisha haooo wanakimbilia newsroom. Hawana maswali yanayojijenga kichwani yenye mantiki. ndo maana tunawaita maripota njaa kali. kwa mwandishi makini hawezi akaitwa kwenye conference kisha akasomewa upuuzi kama huu wa SYNOVATE bila ya kuuliza maswali chechemizi yatakayosisimua ripoti hiyo.

Ni kama waliitwa kwenye hafla fupi wakasomewa risala kisha haooo wakawahi newsroom kupaste walichoambiwa

Sio waandishi, ni maripota. Ndio maana kuna Wasanii na wanamuziki.
Na kwenye redio kuna Presenter na Dj.
 
Sasa labda waje na vitu vingine kufanya utafiti wao, Hotel, vyuo, Warembo, Magari, kila aina ya huduma na hospital
 
Yaani huu ni uhuni, wewe huwezi kuhoji watu 2000 kati ya watu milioni 40 halafu unaita ni utafiti. Naona hapa taaluma ya tafiti imemeingiliwa vibaya. Pia unaposema chama kilichopo karibu na wananchi ni kwenye nini? Ufisadi, Majengo pacha ya BOT, EPA, kushuka kwa elimu ya kidato cha nne, usofu wa waalimu, huduma mbovu hospitalini, barabara mbovu? Au ni kwenye kitu gani?
Pili mbunge kuongea kwa ukali haimfanyi kua bora, kuna waliofanya mambo mazito na wafuatiliaji wazuri wa kazi zao Mfano DR Magufuli, Dr. Mwakiyembe, Dr. Slaa, mbona hawa hamkuweka kwenye tafiti zenu mlizoandika?
Ili utafiti ukamilike na uweze kuutumia kufanyia maamuzi ni lazima huhoji watu wa kutosha na wenye uelewa wa hayo mbambo. Mtu ameishila la sana ni lazima atakwambia Rais anaongoza akimaanisha anaongoza nchi au safari za nje, wewe unaweka kama anaongoza kwa kufanya vizuri.
Huu utafit warudie na watuhoji tulioenda shule ili tutoke maoni. Hili taifa bwana, yaani hata wafaya tafit zimefisadiwa?

Utafit wao warudie kwani Hauna TBS, haujapitiwa na wasomi ili kujua kama kanuni za tafiti zilifuatwa. Pia ikumbukwe tafiti kama hizi wanatakiwa waseme walitumia Shs ngapi kukusanya data

Yaani mpaka wachina wametuingilia kwenye tafiti, Eee Mola tuepushe na balaa hili.
Mkombozi umenena. Hawa jamaa walipata fedha za wafadhili sasa wamejitahidi ku-"justify" matumizi ya hizo fedha. Huu ni uhuni na ufisadi mtupu. Kama mtu anaamua kufanya utafiti basi uwe utafiti wa maana na siyo kuchezea watu.
 
Watanzania walitaka kuibadilikia CCM mwaka 1995. Mwalimu akaokoa jahazi. Ni lazima sasa apatikane mtu mwingine mwenye haiba na ushawishi kama aliokuwa nao Mrema wakati ule. Vinginevyo tafiti hizi zitabaki hivyo zilivyo.

Ah, wakati ule wala si kwa sababu walitaka kuigeuzia kibao CCM, ni ile excitement ya uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi.

Sasa hivi hamna tena hiyo, labda mtu achomoke CCM aweke mambo wazi kwa wananchi kwenye grass roots.

Bila hivyo kitadumu chama cha mapinduzi!
 
Inabidi watu waache kuwalalamikia hawa watafiti na matokeo yao. Uongozi wa CHADEMA ulitakiwa uwe tayari umeshafanya utafiti wao wenyewe na kujaribu kuu-skew kidogo towards CHADEMA, ili kujaribu kurubuni wale wanaofuata upepo.

Lakini kwa kwa vile uongozi ni wa kibinafsi, mawazo yao pia yanakuwa ya kibinafsi. Sasa wamewaachia wapambe wa JK kuendelea kuvutia watu kwake na kuogopesha wengineo wote wenye nia ya kumpinga.

umenena mtu wangu,

Ushauri uliousema hapa wakiupata baadhi ya wanachadema damu lakini wenye ubongo wa kutokufikiri wataona kama unawatukana.

who is synovate? hivi vyama vya upinzani should conduct their own studies, that will be another way of evaluating themselves!

Hii kusubiri ulipwe deni lako , halafu uchikichie sio vizuri, ni vyema hivi vyama vikajua mapigano ya sasa yako too scientificaly. kukaa ofisini kusubiri kudra za mwenyezi sio vizuri.

Hao waliofanya study, wanaweza wakawa wamepika data, kesho wanaweza kusema Mbowe anaongoza! wakati sio. Hivi siku za hivi karibuni mwananchi wa kawaida huko vijijini anajua Mbowe anafanya nini? isn't this alone questionable? angalau Slaa watu wanasikia mara huku mara huku, Mbowe kwenye hiyo list kapandikizwa, halafu watabweteka. CCM hao....
 
Kumbe ni Kampuni?

Sawa wanataka nini sasa? ardhi au Mgodi?

Nafikiri kuna haja ya kuwafikishia hilo swali:

Synovate Tanzania
Aggrey Oriwo — Country Manager
Regent Estate
Mikocheni Street
Plot 161 P.O. Box 106253
Dar-Es Salaam
Tanzania
Telephone: +255 22 277 5851 / 2037
Fax: +255 22 270 1606
Send an email


SYNOVATE: REINVENTING RESEARCH
We help our clients meet the commercial challenges of the information age by constantly creating innovative ways of gathering facts, and turning that data into strategic business insights. If there's no existing method of finding out what you need to know, we'll invent it.
Nimeuzimia huo mkakati wao kwenye nyekundu hapo.
icon10.gif
 
Back
Top Bottom