Gosbertgoodluck
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 2,855
- 401
Ni jambo lisiloingia akilini eti kikwete amemzidi Dr. Slaa hata kwenye majimbo ambayo wagombea ubunge wa Chadema wameshinda. Wananchi wengi mitaani wanashangaa na wanashindwa cha kufanya zaidi ya kusikitika. Wanaoweza kuwasaidia wananchi ni Chadema yenyewe na wanaharakati. Lazima hatua stahili zichukuliwe ili ikiwezekana zoezi la kuhakiki na kuhesabu kura lifanyike upya ili haki itendeke. Inawezekana ni kweli kwamba kikwete ameshinda lakini siamini kama amemshinda Dr. Slaa kwa tofauti kubwa kiasi hicho. Chonde chonde viongozi wa Chadema chukueni hatua wananchi tupate amani.