Matokeo ya udiwani kata 23 (Oktoba 2, 2011)

Kwa taarifa nilizozipata hivi punde kutoka kwa mtu wangu wa karibu sana.Katika uchaguzi uliokuwa unafanyika wa udiwani wa kata ya stendi kuu Chama cha bemokrasia na maendeleo chadema kimeibuka kidedea baada ya kuwabwaga chini wagombea wenzake wa chama cha Mapinduzi CCM na CUF

upo juu kama Chadema
 
Wakuu...wakati tukisubiri dakika tu ili CHADEMA itangazwe rasmi kama washindi wa ubunge IGUNGA tayari mgombea wa udiwani wa chadema kata ya masekelo manispaa ya shinyanga bw.MFUKO ametangazwa mshindi wa kata hiyo iliyoachwa wazi na marehemu shelembi magadula kwa kujinyakulia kura 1501 dhidi ya 587 za mgombea wa CCm bi rashida rajamu..
Kwa matokeo hayo ya zaidi ya 72% chadema imefanikiwa kutetea kiti chake kwa ushindi wa kimbunga..
Kazi kwenu magamba..
Nawasilisha
 
Naambiwa hata wamama na wabibi wako mtaani wanasherehekea wakiimba PEOPLES POWER!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Baada ya kumtangaza mshidi
 
DOCTOR wa Ukweli Mwenyewe Mwenyewe,

Freeman Mbowe, Mzee wa Jeshi la Anga, Kamanda Regia, Kamanda Zitto Kabwe ... Mzee Ndesamburo, Mr II; chonde tunaomba muelewe ya kwamba Wa-Tanzania kote nchini tumedhamiria kuwakabidhini DOLA kuongoza nchi hii wakati wowote ule.

Kama hamuamini bado basi angalieni tulivyoanza kwa kuwapeni idadi ya MADIWANI wa kumwaga kote nchini. Ndio kama hivyo tumeanza kuwakunjisha jamvi CCM taratibu tukianza na upande wa serikali za mitaa na kuja kumalizia kabisa kwenye kuchekecha Bunge zima na kufukuzilia mbali wala-rushwa wote na wale wachapa usingizi.

Pipozzzzzzzzzzzz Pawaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
hii ni mvua ya vuli, bado kimbunga 2015, labda ccm wajitoe kwenye kinyang'anyiro kwa kutambua kutokubalika na wananchi
 
Kwa taarifa nilizozipata hivi punde kutoka kwa mtu wangu wa karibu sana.Katika uchaguzi uliokuwa unafanyika wa udiwani wa kata ya stendi kuu Chama cha bemokrasia na maendeleo chadema kimeibuka kidedea baada ya kuwabwaga chini wagombea wenzake wa chama cha Mapinduzi CCM na CUF

Datz good people needz changes nw
 
safi sana ila kuna mtu kanijulisha kuwa chadema tumepoteza huko Engototo..
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom