Matokeo ya Law school of Tanzania, kati ya wanafunzi 500+ walio-clear masomo yote ni 22 tuu!

Daah! na sisi tuliosomea PHARMACIST, ushapata degree yako hapo ya miaka 4, ili upate cheti(register) sasa inabidi ufanye mtihani wa phc,concl, huo huwa wanafanya wanafunzi 1000, wanaofaulu hawafiki 100, ndio unapata cheti sasa na muhuri, unaokuruhusu kuweka kwenye Pharmacy.. waliofeli wanapaswa kurudia, na unalipia mkwanja mrefu si bure... namshukuru mungu nilipita kati ya 98 tuliofaulu. LLB sijui LST, poleni kwa kudisco, komaeni mtapata tu muhuri.

Kweli Mfamasia, Hawa watanzania wengi wanaojambajamba hapa ni watoto wa wakubwa waliosoma shule za inglishi midiam, na Pia wana penda kubebwa, Wengi ni watoto wa majaji na nitakuja siju kuleta majina yao hapa na sehemu walipochomekwa:
Hawa hamna kitu kichwani na ni mzigo kwa taifa;Hiyo law school ya Tanzania unaambiwa ni moja ya shule ya Sheria duniani ambayo ni nyepesi.Ukija UK ama Us Asikwambie mtu, kwanza ukitaka kuwa wakili unaanza na digrii labda ya Economics, then unasoma Llb, then ndio unaingia law school kwa mwaka tena so unatumia miaka nane kuwa wakili.
 
Upo darasa la ngapi kwnz?!
Dalili ya kutokuwa na hoja ya msingi
Pale Law school lazima usome...ni Programme nzuri sana na mhimu inaivisha watu hasa wanasheria ukitaka uive vzr baada ya Degree soma pale..lakini usome kweli kweli sio ujanja ujanja wa kibongo mkipigwa mnakimbia mitandaoni kulia lia...hawa watoto wa leo hawasomi wanachat tu na misimu yao sasa wakipigwa wanawahi mtandaoni ...Hata hao Law school wakikufaulisha ujue kabisa ukiingia mahakamani Bila ujuzi utalia mchozi utapigwa PO mpaka wakili wa upande wa pili akuhurumie..Sheria lazima usome ujue procedure its a science no short cut
 
Matendo ya leo ndio matoleo ya kesho, hao walibweteka walikotoka wakidhani mambo ni rahisi waendapo
 
Jamani matokeo yametoka, kati ya wanafunzi 500+ walio clear masomo yote ni 22!
Hapa kuna tatizo na si weak students kama mtu anavyoweza kudhani. Kuna tatizo katika teaching and examining/exam set up!.
hii inatusaidia nini si watarudia inakuhusu nini umbea tuuu
 
Kweli Mfamasia, Hawa watanzania wengi wanaojambajamba hapa ni watoto wa wakubwa waliosoma shule za inglishi midiam, na Pia wana penda kubebwa, Wengi ni watoto wa majaji na nitakuja siju kuleta majina yao hapa na sehemu walipochomekwa:
Hawa hamna kitu kichwani na ni mzigo kwa taifa;Hiyo law school ya Tanzania unaambiwa ni moja ya shule ya Sheria duniani ambayo ni nyepesi.Ukija UK ama Us Asikwambie mtu, kwanza ukitaka kuwa wakili unaanza na digrii labda ya Economics, then unasoma Llb, then ndio unaingia law school kwa mwaka tena so unatumia miaka nane kuwa wakili.
Mkuu nimechunguza sana nimegundua Law School hakuna tatizo tatizo lipo huko vyuoni ndo kumeoza...

sasa law school inapokea takataka zote za vyuoni ndo mana wanalaumiwa wao wakianza kuchuja lakini ukweli ni kua vyuoni kumeoza..
 
Ni ukweli mkuu ni kama vile kipindi fulani wanafunzi wa kiislamu walikua wanamlaumu ndalichako kwa kuwafelisha necta wakawa wanataka ajiuzulu ila kiukweli shule za kiislamu kipindi kile kulikua hakuna kitu kabisa yani hawafundishi masomo ya necta zaidi mambo ya dini na kiarabu na kuswali swala tano na hadithi za mtume.....
sasa unategemea ukimletea mtoto mtihani wa biology wakati amekariri kiarabu na hadithi za mtume ataacha kuona nyota na kutaga ndo mana kikwete kipindi kile na yeye ni muislam akaona hawana mashiko na wala hakumtoa ndalichako..

Mfano sasa hivi unaona watoto wanafeli sana Form 4 halafu mtu analaumu necta wakati mfumo wa elimu bure huko chini umeoza..ndo kama ilivo kwa law school..

Kuna jamaa tulisoma naye undergraduate kiukweli jamaa alikua mtupu sana yani..ile fani haikua size yake ila mwisho wa siku akapata degree yake

Basi tukaingia nae law school cohort moja inasikitisha sana maana jamaa alikua anatamani sana muhuri wa uwakili yani ukikaa naye anakuambia muhuri ndo kila kitu muhuri ni hela muhjri ni dili mjini hapa hapo mimi nilikua simuelewi mana sikujua kuna mawakili wana mihuri so nikajifunza kitu kwake...

ila Jamaa yule aliDISCO straight away na ndoto zake muhuri zikaishia pale...na yule jamaa nilikua namjua toka first year undergraduate na LST amedisco lile disco lenyewe kabisa...
mi sikushangaa ila nikaamini kua pale haonewi mtu kwakweli mana kadisco mtu ambaye nilikua namjua vizuri....

Inasikitisha lakini who knows je angepata huo muhuri halafu akapata kesi ya mteja wa murder akashindwa kumtetea vizuri mtu akafungwa...ingesikitisha zaidi unafungwa kwa uzembe wa mtu uliyemlipa akutetee
 
don't change the topic, that is just a minor mistake(typing error) hata computer zinakosea
Computer is error free unless kuna human error
Pale Law school lazima usome...ni Programme nzuri sana na mhimu inaivisha watu hasa wanasheria ukitaka uive vzr baada ya Degree soma pale..lakini usome kweli kweli sio ujanja ujanja wa kibongo mkipigwa mnakimbia mitandaoni kulia lia...hawa watoto wa leo hawasomi wanachat tu na misimu yao sasa wakipigwa wanawahi mtandaoni ...Hata hao Law school wakikufaulisha ujue kabisa ukiingia mahakamani Bila ujuzi utalia mchozi utapigwa PO mpaka wakili wa upande wa pili akuhurumie..Sheria lazima usome ujue procedure its a science no short cut
 
Mkuu vipi chuo Tumaini kwa Degree ya sheria wako vipi??
Tumaini ya Dar?
Kama ndio, walikua vizuri kwa sasa sijui kwakweli mana sijapata data za decently ila kipindi icho walimu wengi wa law school walikua wanatokea Tumaini Dar so yeah wako vizuri....

Utakua na bahati ukimkuta Masumbuko Lamwai yupo vizuri SANA kwenye Criminal na Civil Law na Procedure....
 
Tumaini ya Dar?
Kama ndio, walikua vizuri kwa sasa sijui kwakweli mana sijapata data za decently ila kipindi icho walimu wengi wa law school walikua wanatokea Tumaini Dar so yeah wako vizuri....

Utakua na bahati ukimkuta Masumbuko Lamwai yupo vizuri SANA kwenye Criminal na Civil Law na Procedure....
Tumaini ya Iringa mkuu vipi??
 
me huwa sielewi
hivi law huwa ni ngumu sana au wanafunzi ndio Vilaza?
Law ni kati ya kozi nyepesi sana! Wahadhiri ndo wanalazimisha ionekane ngumu kwa sababu wanazozijua wenyewe!! Miaka ile ya themanini (1983-1986) nilipokuwa nasoma hapo mlimani, kitivo cha sheria ndo kilikuwa kitivo pekee ambacho hakikuwa kina-disco wanafunzi!!! Disco pale sheria zilikuwa adimu sana!! Disco nyingi zilikuwa sayansi ikifuatiwa na engineering!!!!
Hakuna sababu ya sheria kuwa ngumu! Ndio maana MTU yeyote anaweza kusoma sheria kutoka kombinesheni yoyote aliyofaulu, ili mradi awe na credit za historia na English huko O-level!!
Sheria ni taarifa na mfumo!! Hakuna ugumu wowote wa kuielewa taarifa na mfumo!!!!!
 
14 Reactions
Reply
Back
Top Bottom